Wednesday, December 25, 2013

SINDI... NA LAURA PETTIE (50)

50

Alisimama mbele ya Sindi Nalela kama binadamu aliyevukwa na fahamu, aliyekosa utashi na kupigwa bumbuwazi. Nadina akarudi kinyume nyume kwa hatua hafifu zilizokosa uelekeo wa maana. Macho yako yalimwemweseka katika namna ya kuzidiwa na ile hali ya bumbuwazi, midomo yake iliyokuwa wazi ilitulia vile vile mithili ya mtoto asubiriaye tonge la ugali. Akarudi nyuma mpaka alipogota ukutani, mikono ikiwa kifuani pake.

Friday, December 20, 2013

SINDI...NA LAURA PETTIE (49)

49

Gari aina ya Acadia iliserereka barabarani ikiwa katika mwendo wa kasi kiasi, dereva aliyekuwa ameukamata usukani kwa mikono yote miwili alikuwa akibubujikwa na machozi kiasi cha kushindwa kuona mbele vizuri. Akauondoa mkono wa kushoto toka kwenye usukani na kuutumia kupangusa machozi yaliyoonekana kuuelemea uso wake.

Thursday, December 5, 2013

PERUZI YA ENZI... YESU KRISTU BY KANDA BONGOMAN



 
Yesu kristu yaleee yakilangai mawaaa yoooo heheheheheee....

what a masterpiece!.... inanikumbusha mbaaali sana aiseee, mambo ya inde monie inde monie eeeh

lets enjoy our Thursday this way!
ya kale dhahabu ati....

Enjoy!

SINDI....na LAURA PETTIE (48)

48

Casino la Madam Adella lilikuwa na utulivu ulioambatana na muziki wa taratibu uliokuwa ukiporomoshwa na Dj aliyekuwa zamu, taa za rangi ya bluu na nyekundu zilimulika ndani ya Casino hilo na kuleta mchanganyiko wa rangi uliohamasisha mahaba. Watu wengi walionekana kutulia sehemu zao huku wahudumu waliovalia nguo fupi za kuacha sehemu kubwa ya miili yao wakihudumia kwa kupita pita huku na kule kwa madaha.

Monday, November 18, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE(47)

47


Ni sauti za vijiko kugonga sahani ndiyo hasa iliyokuwa inasikika katikati ya mlo huu wa usiku. Jerry alitua kijiko chini na kunyanyua glasi ya maji iliyokuwa kando ya sahani. Akapiga funda moja la kutosha na kurudisha glasi mezani.

Sunday, November 17, 2013

PERUZI YA ENZI.... MUZIKI ASILI YAKE WAPI BY REMMY ONGALA NA LYRICS ZAKE.




NI MOJA KATI YA NYIMBO ZA REMMY ONGALA NINAZOZIPENDA SANA....


Muziki asili yake wapi eeeeee,Muziki ni wa nani eeeeeeeeeeeee,
Muziki hakuna mwenyewe,Muziki ni mwito,
Muziki ni fundisho,Muzi maombolezo kilio
Usinione nikiimba,ukadhani ninayo furaha,kumbe ninayo huzuni moyoni.

SINDI....NA LAURA PETTIE(46)

46


Jua la adhuhuri lilishachomoza na makali yake yalichoma mara mbili ya jua la utosi. Hali ya hewa ilikuwa ya joto kali lisilovumilika kusimama juani pasi ulazima. Muda huu wa saa tatu asubuhi Mzee Okello alikuwa na pilika pilika za kujiandaa kutoka nyumbani kwake kuelekea kaika mihangaiko yake.

Wednesday, November 6, 2013

PERUZI YA ENZI.... NALIA KWA FURAHA BY JACQUE ft. BUSHOKE





NI WIMBO WA KITAMBO TU ILA EVERY TIME NINAPOUSIKILIZA NI KAMA MPYA TU
LEO NIMEAMKA NAO KICHWANI....


Mbona wanitazama kisha waanza kulia 
kama nimekukosea,naomba unisamehe. 
Hapana hujanikosea,ninalia kwafuraha 
Mapenzi unayo nipa sijawahi kupata.(2 times) 

SINDI.... na LAURA PETTIE (45)

45
Sindi Nalela alikuwa sakafuni ndani ya chumba kile kile alicholazwa usiku uliopita, uso wake uliovilia damu hapa na pale ulilalia shavu la kushoto sababu ya kule kulala kiubavu huku mikono yake ikiwa imefungwa nyuma kwa kamba. Miguu yake ilikuwa imeunganishwa kwa kamba nzito ambayo haikumruhusu kutanua miguu yake hata kwa sentimeta moja. Alilala vile akimtazama Nadina aliyekuwa amelala mbele yake!

Sunday, October 27, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (44)

44
Pamoja na usiku huu kuwa wenye mvua na upepo wa kuleta usingizi mnono, kwa Sindi Nalela, usiku huu ulikuwa kama kitanzi shingoni. Matone ya mvua yaliyofanya michirizi kwenye dirisha la kioo lililokuwa limejengewa mita chache toka lilipo dari yalipita machoni mwa Sindi pasipo kutambulika akilini.

Sunday, October 20, 2013

BARAZANI... TUNAPASWA KUSHUKURU KWA DHATI



Katika safu yetu ya leo ya barazani… ninayo machache tu ya kusema na wewe ndugu msomaji…

Yawezekana wewe ni mwanamke…. una kazi nzuri yenye kukuingizia kipato… una afya njema tu inayokupa nafasi ya kuzunguka huku na kule…. una marafiki wanaoifanya siku yako iishe katika namna ya kupendeza…. lakini huna mume pengine huna hata boyfriend ama unaye lakini maumivu anayokupatia katika uhusiano uliopo unajihisi kama mtu mpweke sana. Pengine unavyo vyote hivi lakini huna mtoto na unaona kama dunia inakuonea, Mungu amekutupa!

Friday, October 18, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (43)

43


Siku hii ilijaaliwa mawingu mazito yaliyofifisha ukali wa jua na kuleta  hali ya ubaridi iliyokuja na kutoweka. Ndani ya saluni kubwa ya kisasa ya wanawake iitwayo Marino kulikuwa na pilika pilika za hapa na pale. Huyu akioshwa nywele, yule akisuguliwa kucha hapa wakiwekana rolazi na kule wakitindana nyusi, mradi kulikuwa na hekaheka za hapa na pale.

Tuesday, October 8, 2013

SINDI.... NA LAURA PETTIE (42)

42

....Fiona Agapella aliendesha gari lake mpaka nyumbani kwa rafiki yake Iloma. akaingia ndani kwa mbwembwe akicheka kwa furaha na chupa ya mvinyo mkononi. Akaitua mezani na kukimbilia jikoni. Akarudi na glasi mbili na kuziweka mezani karibu na chupa ya ule mvinyo. Iloma, rafiki yake akiwa bado na butwaa lililomfanya shindwe hata kuufunga mlango itakiwavyo.

Monday, September 30, 2013

PERUZI YA ENZI:.... NA WEWE MILELE BY RAY C




nataka niwe na wewe milele... nataka tuwe na watoto baby... nataka tuishi wote pamoja

siku nilipokuona...macho yangu alishtuka... nilijua roho yangu mimi kwako imefika... na sasa tupo pamoja uwe wangu niwe wako... kwa shida na raha zooote moyo wangu uko kwako na raha zako mimi kwako kuzikosa...

RAY C rocks all the time... !
 nimekumbuka sana huu wimbo leo

ENJOY!

SINDI...NA LAURA PETTIE (41)

41

‘yaani hatutalewana humu ndani leo… kamtoe umrudishe uko uko ulikomtoa’ sauti ya mwanamke mtu mzima ilimfikia vema Sindi Nalela pale sebuleni alikokuwa ameketi. Sauti ilitokea chumba cha pili alichohisi kilikuwa chumba cha kulala.

Monday, September 23, 2013

SINDI.... NA LAURA PETTIE (40)

40

Pale alipokuwa amesimama, Sindi alinesa nesa mwili mzima, ilikuwa zaidi ya kutetemeka, zaidi ya hofu na kuchanganyikiwa kulikochanganyikana na hali ya kutoamini alichokiona. Mlango ulipogongwa mara ya pili, Sindi alifumba macho kwa nguvu zote na kujaribu kujikakamaza asianguke ila mwili uligoma kutulia, uligoma kutii amri ya kukakamaa na kinyume chake kila sehemu ya mwili ilimcheza mpaka utumbo!

WIMBO HUU UWAFARIJI WOTE WANAOPITIA KIPINDI KIGUMU....




  1. Nearer, my God, to thee,
    Nearer, my God, to thee,
    Nearer to thee!

    MUNGU AWAPE FARAJA, TUMAINI NA NGUVU ZA KUHIMILI MAUMIVU, HUZUNI NA WAKATI MGUMU AMBAO NDUGU ZETU WALIOATHIRIKA NA TUKIO LILILOTOKEA WESTGATE MALL, NAIROBI

    Najaribu tu kuvaa viatu vya hawa ndugu zangu... nashindwa kuhisi hata punje ndogo tu ya maumivu waliyonayo waliopoteza ndugu na waliokwama katika mikono ya magaidi hawa

    POLENI SANA WAPENDWA!

Monday, September 16, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (39)

39
‘Karibu..’ Sindi Nalela alitaka kuiondoa ile hali ya kuzubaa iliyomkuta Patrick Mazimbwe pale mlangoni. Hakujibiwa!


Sindi akautanua mlango kwa mapana kidogo na kujirudisha nyuma hatua moja akiwa ameuegemea mlango na Patrick akanyanyua mguu kwa kutaka kukivuka kizingiti cha mlango lakini akajikwaa kwenye lile jenereta lililokuwa miguuni pake, kujikwaa kule ndiko kulikomrejeshea akili yake sawia.

Tuesday, September 10, 2013

SINDI.... na LAURA PETTIE (38)

38

Jua la saa nne asubuhi lilishachomoza kwa makali ya kiasi chake. Utulivu mkubwa ulikuwa umetanda eneo kubwa la jumba la Mzee Okello… sauti chache zilizosikika zilikuwa za watumishi waliokuwa wakifyeka nje na kupunguza michongoma iliyoizunguka nyumba hiyo. Kwa mbali zilisikika ngurumo za magari toka barabara kuu ya lami iliyokuwa mita kadhaa toka lilipo jumba hilo.

Friday, September 6, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (37)

37

Wale vijana aliokuja nao kusomba vyombo ndio waliomtoa katika lindi la simanzi. Akajikuta tu akiwalipa pesa walizokubaliana pasipo kuhamisha hata kijiko. Wakaondoka wakimuacha na wapangaji wawili watatu waliokuwepo muda huo. Kila mmoja akisema lake lakini hakuna kati yao aliyemuona Sindi wakati akiondoka!

PERUZI YA ENZI:.....ESWI YO WAPI BY MBILIA BEL




This is one of my favorite Congolese music.....
 i have been singing this today mpaka basi
nimekutafutia na lyrics  na maana yake kabisaaaa

yaani unaimba kama Mbilia Bel mwenyewe hahahahaha
twende kazi sasa......

Tika ngai na vanda na ngai
tika ngai na benda nzoto
obandi kopanza na basango bipayi biso likambo o ngai na nani eh
Let me be on my own
let me break the relationship
before you start spreading news of our issues

Wednesday, September 4, 2013

SINDI.....NA LAURA PETTIE (36)

36

Jenifa Agapella na Clarita Gabson marafiki wa tangu utoto walikuwa nyumbani kwa Mzee Agapella wakipeana michapo mbalimbali huku wakiandaa chakula chepesi cha kupata jioni ya siku hiyo. Clarita alikuwa na kikopo chake cha ice cream, akiikwangua hiyo ice cream kwa kijiko na kuila taratibu kana kwamba hakutaka iishe haraka, wakati huo akiwa amesimama kwa kuigemea friji kubwa iliyokuwa jikoni hapo.

Tuesday, August 13, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (35)

35


Fiona Agapella alimeza mate kwa juhudi zote wakati akijaribu kujiweka sawa kumpokea Mzee Okello. Macho yake yalicheza kulia na kushoto katika namna ya kutafuta utulivu wa nafsi. Akameza tena mate kwa juhudi kiasi cha kufanya koo lake lididimie ndani kwa nguvu kidogo. Alihamanika!

Sunday, August 11, 2013

SINDI.....NA LAURA PETTIE (34)

34

Jua la saa nne asubuhi lilikuwa kali kiasi cha kufanya waliokuwa juani kukunja nyuso zao na  wengine kutafuta vivuli. Pilika pilika za hapa na pale zilishaanza na vurumai za jumatatu zilishika kasi kila kona. Sindi alikuwa uani akifua nguo zake na za Jerry.

Kulikuwa na ukimya mkubwa uani hapo kutokana na wapangaji wengi kutokuwepo asubuhi hiyo. Akiwa ameketi kwenye stuli yake aliendelea kufua taratibu  shati alilokuwa nalo mkononi huku akiimba wimbo alioutoa kwa sauti ya miguno tu na kutikisa kichwa.

Monday, August 5, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (33)

33


mke wa Mzee Okello, mama wa Pamella alikata simu na kusimama akiwa kama mtu aliyetaka kupayuka kitu kwa sauti ya juu na asiweze. Mdomo ulikuwa aukiwayawaya huku macho yakipepesuka na kutembea huku na kule. Mchecheto!

Akalazimika kujiweka sawa pamoja na mchecheto ule ili binti yake aliyekuwa anaingia pale dukani asigundue hali aliyokuwa nayo.

Thursday, August 1, 2013

MGENI WANGU:....MHADHIRI WA SAUT BW. ROBERT MKOSAMALI

Leo mgeni wangu ni Mhadhiri wa chuo kikuu cha St. Augustine University of Tanzania, bwana Robert Mkosamali. Pasi kupoteza muda karibu utiririke na mtiririko wa maswali  toka kwa Blogger wako Laura Pettie…. Karibu sana!
MHADHIRI WA SAUT
BW. ROBERT MKOSAMALI

Laura Pettie Blog: Kwa maneno matatu tu, unamwelezeaje Robert Mkosamali?
Robert Mkosamali:     Haahaaa! Ninaweza kumwelezea Robert J. Mkosamali kama mtu simple, straight forward na hardworking!

Laura Pettie Blog:  Kitu gani kilikuvutia kujiunga na tasnia ya habari? Is there any motivational story behind?
Robert Mkosamali:      Kitu kilichonivutia kuingia katika tasnia ya habari ni umaskini uliokithiri wa watanzania hasa wale wanaoishi katika mikoa ya pembezoni. Mikoa hii mbali ya kuwa katika hali ngumu ya maisha ilikosa waandishi wa habari ambao wangeweza kuelezea matatizo ya watu walio ndani ya mikoa hiyo na hivyo kuifanya serikali iweze kuchukua hatua.

Nakumbuka miaka ya 1993 kulikuwa na mfumko wa wakimbizi mkoani Kigoma lakini kwa bahati mbaya maisha ya watu wa Kigoma yalionekana kuwa duni kuliko hata yale ya wakimbizi kutokana na mashirika mengi ya kimataifa ........



PERUZI YA ENZI....LORD'S PRAYER SONG IN SARAFINA MOVIE




I LOOOOVE THE DANCE UWIIII..... 
Our father
Which art in heavenHallowed be thy nameThy kingdom comeThy will be done on earthAs it is in heaven
And forgive us our trespassesAs we forgive those who trespass against usAnd lead us not into temptation
But deliver us from evilFor thine is the kingdomAnd the powerAnd the glory, forever, amen

ENJOY!

Tuesday, July 30, 2013

MAMBO YA FLEXY COLLECTION..... VITU JUU YA VITU MPAKA RAHA!

TUMERUDI..... NI FLEXY COLLECTION..... WALE WALE WATAALAMU WA FASHION
Wanakwambia Don't do Fashion...just be Fashion itself

WAAAPI?... KIJITONYAMA KARIBU NA PALE ILIPOKUWA CHAGGA BITE
SIMU: .....0718 - 378384
BB:.... 296e08c6

MADAME GRACE....MAMAA WA FLEXY

MAMBO KAMA HAYA...KWA BEI POA TU



UBAHILI PEMBENI...VAA UPENDEZE JAMANI



KUNA ZAIDI YA HAYA UNAYOYAONA HUMU
NENDA NENDA HIMAAA
USIJEKOMBA MPAKA NAULI TU HEHEHEEE MAANA BEI SAWA NA BURE



WALE WA MAOFISINI....PANAKUHUSU HAPA!
JAMANI KUPENDEZA HAKUBAGUI MTU

MITOKO YAKO SIMPLE SIMPLE UNAPIGA VITU KAMA HIVI


MAMAA FLEXY NIWEKEE HII LOL

MAMBO KAMA HAYA MTU ANAKUSHANGAA
MPAKA ANAPARAMIA MEZA YA MATUNDA MJINI
MAMBO YA FLEEEEEXY!



ZAIDI YA NGUO KUNA VIKOROMBWEZO CHUNGU NZIMAAAA
YAANI UKIINGIA HUMU UKATOKA BILA KITU HUMU BASI TENA MWAYA



 .... KWA MAMBO MATAMU MATAMU ZAIDI HEBU WATEMBELEE 

www.flexycollection.blogspot.com


SINDI.....NA LAURA PETTIE (32)

32

Alikirudisha kile kifaa cha kupimia ujauzito katika kile kibahasha kidogo cheupe na kukiweka pembeni yake. Kichwa kilikuwa na matundu ghafla. Ufahamu ulimtoka na kukimbilia kusikojulikana. Akashusha pumzi ndefu, akihisi pia tumbo likimcheza. Akanyanyuka na na asijue kilichomnyanyua. Akalikodolea macho kochi lililokuwa mbele yake pasipo kuelewa kwanini alilitumbulia macho.

Sunday, July 28, 2013

HII NDIO BARUA INAYODAIWA KUTOKA KWA WAFUNGWA HONGKONG



SOURCE: MITANDAO YA KIJAMII

SINDI....NA LAURA PETTIE (31)

31
Sindi Nalela aliiona wazi hali ya kubabaika aliyokuwa nayo Jerry pale juu yake. Akatumia mkono wake wa kushoto kumsukumia kando Jerry na kuanza kuikusanya khanga yake iliyokuwa imeshatolewamaungoni. Muziki wa simu wa simu ukakatika na Jerry aliyekuwa ameangukia chali kando ya Sindi hakutamani hata kunyanyuka pale kwenda kumjua mpigaji. alimshamhisi!

Saturday, July 27, 2013

10 MINUTES WITH GOD:.... SHUKA BWANA BY ABIUDI MISHOLI


.......Yawezekana mpendwa rafiki mihangaiko ya kidunia imekushika kiasi kwamba kile kitabu kitakatifu kiitwacho biblia… umekisahau…kimejaa vumbi… unakiona lakini uvivu wa kukifungua unakupata…. Yawezekana lipo jambo unalomlilia Mungu akutimizie Lakini…. siku, wiki mwezi, miaka inakatika na huoni lolote linalotokea… unamatazama Mungu kwa wasiwasi…. unajiuliza umekosa nini?...kwanini wewe… kwanini hili…kwanini sasa… na hupati majibu. Mungu anaonekana yuko mbali sana na wewe. 


katika kitabu cha ZABURI 145: 17 – 19….. anasema “Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote…..Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote…….Bwana yu karibu na wote wamwitao…..wote wamuitao kwa uaminifu…. atafanyia wamchao matakwa yao….Naye atasikia kilio chao na kuwaokoa” MPENDWA RAFIKI MUITE MUNGU KWA UAMINIFU….KWA UVUMILIVU NAYE ATAKUITIKIA…MUNGU HACHELEWI ….YUPO KWA AJILI YAKO KWA AJILI YANGU KWA AJILI YETU SOTE…. BARIKIWA NA WIMBO HUU…. NIMEKUANDIKIA MAISHA YAKE HAPO CHINI

Nakuhitaji bwana… Nakuhitaji Jehova… wewe ndiwe msaada wangu…. niende wapi
ila kwako…tazama shida zangu…tazama kwanza…Bwana nitazame… sina wa kunisaidia…ila ni wewe… hima bwana shuka…uniokoe

Thursday, July 25, 2013

SINDI.....NA LAURA PETTIE (30)

30


Jenifa akamuachia kaka yake na kumtazama kuanzia utosini hadi unyayoni. akajikuta akicheka
‘Na huyu ndio Jerry sio yule wa jana usiku…’ Jenifa akamtania kaka yake ambaye akili yake haikuonekana kuyazingatia maneno ya Jenifa. Alikuwa anatazamana na Fiona huku wote wawili wakitabasamu. Chuki ilisomeka mioyoni huku upendo ukionekana usoni!

Tuesday, July 23, 2013

SINDI.....na LAURA PETTIE (29)

29


Jerry Agapela alishindwa kuendelea kuzisikiliza kwikwi za baba yake, aliiteremsha simu chini na kuitua mezani, akiiacha hapo na kufuta machozi kwanza. Taratibu akijaribu  kuhema na kujituliza nafsi.

Monday, July 22, 2013

MATUKIO: CHRISTINA'S KITCHEN PARTY...PART ONE!

Ms. Christine Minja
 ....the bride to be....
Cute....Elegant....Classy...Beautiful...you name it
Christine just made it...!!

                                         Everything on point 
The pose.... the dress....the make up...the hair do
watu wana wanavishwa wanavalishika...
hawadumbukii dumbwi
i can see the curve lol
 
 I zooomed the shoe...
 Tina i want i want i want to see it....lol!


 Tina with her beautiful  mom
"hongera mwanangu wee..hongeraa'


 
I can hear HIM saying HALELUYAH!...Where is Abra? lol


The smile says it all....
....with friends

Cutie ladies

  21st July, 2013 was Tina's kitchen Party... ilifanyika ukumbi wa Abnois...Sinza Shekilango.....
 NILIKUWA NA MACHACHE YA KUMUULIZA CHRISTINA
ALIJISIKIAJE:...
I was nervous...a lil bit nervous kabla ya shughuli...but i was so happy kuona mambo yalienda kama nilivyotaka

SHUKRANI...
the Almighty God, my sweet mom, Aunt Esther Mafole... my siblings...Grace na Happy....my best friends... kina....Janeth....Natasha...Mado....Pendo....Halima...Agnes... nisimasahau my darling Abraham kwa sapoi yake ya maombi....

Pia nawashukuru wote waliojumuika nami katika siku hii.... na wote walioshirikiana nami kwa namna moja ama nyingine ila wakashindwa kufika...ASANTENI SANA SANA SANA...

TUKIO LA KUKUMBUKWA...
wakati mama anatuzwa...it was so emotional...oh dear am short of words sijui niseme nini

....KUNA MEEEENGI YAJA...PICHA ZENYEWE ZILEEEEE .....SIO ZA KUKOSA AISEE
HAPA TUNAONJA ONJA TU KAMA CHUMVI IMEKOLEA HAHAHAHAHAAA

BEST OF LUCK TINA.... MUCH LOVE DEAR!!!











Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger