Wednesday, December 24, 2014

MERRY CHRISTMAS WADAU....

Nachukua nafasi hii kuwatakia sikukuu njema ya Christmas. Let us celebrate responsibly!

Nimekuwa kimya kidogo sababu ya majukumu fulani, ila yote ni kukusanya nguvu ili kuleta mabadiliko kwenye blog yetu pendwa ili mwaka ujao tuanze kuwa more serious.

Katika siku hii ya leo, wewe mdau nakuombea furaha, amani, utulivu na usherehekeaji mwema.

Nawapenda sana!

LAURA PETTIE
BLOGGER!

Thursday, December 18, 2014

UREMBO NA LAURA:... KUONDOA MAKUNYANZI USONI KWA TANGO NA NYANYA.


Tumeshukuru Mungu!

Kwa mara nyingine tena  tunakutana hapa kusoma makala hii ya UREMBO na Laura. Ni jambo la kipekee kwa kweli. Mwaka umekuwa mgumu sana huu!

Haya siku ya leo nakuletea tiba ya kuondoa makunyanzi usoni. Kuna vijana, ni vijana tu wala uzee haupo karibu leo wala kesho lakini wana mikuno usoni Ashakum si matusi utasema ngozi  ya goti! 
kuna makunyanzi ya paji la uso, ya pembeni ya macho, chini ya macho, kwenye mistari ya tabasamu na hata kidevuni.

Makunyanzi, kuna umri unafika hayaepukiki, ndio vile umri umeenda. Ulaya uko wanafanya mpaka upasuaji wa kunyoosha ngozi. Ila kwako wewe kijana tu hapana!....narudia hapana huna haki ya kuwa na makunyanzi kabisaaaaa!!

Makunyanzi yanaletwa na mambo mengi mno. Seli zilizochoka usoni na hazijaondolewa, Mwili hauna maji ya kutosha, lishe yako ni duni, una stress, na kuna makunyanzi mengine wanasema ni ya kigenetic tu au namna unavyoukunja uso wako… lakini hii haimaanishi usipambane nayo. Mwenzangu uso mchovu mwisho ukooo mjini kila mtu softi tachi hahahahaa! sasa wewe wa wapi hapa mjini?

Tunaishi mara moja katika maisha haya ya duniani, kwanini usijipende tu, ukajihudumia na ukajifurahia kujiona ukipendeza, ukiwa na ngozi ya kuvutia tena kwa kutumia mambo ambayo hayana gharama kabisa. 

Wakati mwingine tunakosa umaridadi na mvuto si kwa kuwa hatuna pesa za kumudu gharama za mahitaji ila hatujipendi au tunaendekeza uvivu tu wa kuandaa hiki na kile ili kuuleta umaridadi. na wakati mwingine nyuso zinakosa mvuto kwa kuwa tunatumia vipodozi visivyo sahihi vyenye kemikali.

NJIA ZA KUONDOA MAKUNYANZI USONI

Zipo njia nyingi sana. Kuha mafuta, krimu, vidonge, upasuaji na kadhalika. Ila mimi nitakupa njia moja ya kiasili ya kuondoa makunyanzi.
MAHITAJI….
1. TANGO

2. NYANYA


JINSI YA KUFANYA….

1. Osha yango lako, kata kipande likiwa na ganda lake. Usimenye!

2. Hicho kipande kitwange kwenye vile vinu vidogo ya jikoni au saga

3. Osha nyanya yako na ukate nusu , yale maji maji ya ndani ya nyanya yakamulie kwenye Tango ulilosaga AU wakati unatwanga tango au kusaga tupia kipande cha nyanya, kidogo tu

4. Osha uso na kausha kwa taulo safi…nasisitiza sana kutumia vitu visafi kukausha uso. Maana kuna wakati rashes zako zinatokana na taulo tu unalotumia. Labda limepigwa sana vumbi hapo unapolining’iniza au hujalifua siku mbili tatu. Taulo la uso ni kitu cha muhimu sana kufuliwa mara kwa mara jamani.
Ukishaosha. Paka mchanganyiko wako kuzunguka uso mzima

5. Kaa kwa nusu saa hadi saa nzima. Ukipata sehemu yenye upepo itakauka haraka sana


6. Ikishakauka, wakati wa kuondoa. Chovya vidole kwenye maji na usugue ule mkauko polepole. Nasisitiza polepole jamani…. Hasa sehemu zile zenye mikunjo.

7. osha uso wako na maji safi, na sabuni unayotumia kisha kausha uso na uuache upigwe na upepo kidogo kabla hujapaka chochote

Fanya hivi kadiri unavyoweza iwe kila siku, iwe mara  mbili au tatu kwa wiki. Ni wewe tu na juhudi zako ila lazima makunyanzi yataondoka ama kupungua saaaaana. Utapata ngozi f’lani ng’aavu maana nyanya inang’arisha uso.


TUKUTANE TENA PANAPO MAJAALIWA….

Thursday, December 4, 2014

UREMBO NA LAURA:.... BIDHAA NA BEI ZAKE NA NAMNA YA KUVIPATA



Nikiwa sina kipodozi chochote usoni.... hapa ni baada ya 
kufanya facial treatment yangu mwenyewe nyumbani.

Watu wengi wamekuwa wakiuliza wapi watapata hiki na kile katika zile bidhaa za asili ninazohimiza kutumia katika makala za urembo na Laura. Leo nakuwekea hapa baadhi ya vitu, bei zake na namna ya kuvipata.

Nimekuwa nikisisitiza sana matumizi ya vitu asilia kwa kuwa kwanza havina madhara kabisaaa! labda uwe na allergy na kitu, vinginevyo sijawahi kuwa disappointed.  

Pili vinapotibu tatizo hutibu taratibu ila kwa ufasaha na  matokeo ya matibabu yako hudumu kwa muda mrefu. Gharama zake ni nafuu sana  na utaweza kuzimudu  hata kipato kikiyumba ati! Lol!

Hivi kwanini usijivunie rangi yako, kwanini usiiboreshe rangi yako tu pasipo kuibadili?... kwanini usitafute muonekano wako wa kipekee!... hizi kemikali tunazo hangaika nazo mwisho wa siku tunapata chunusi za ajabu ajabu na kuungua uso zinapokukataa halafu unaanza kuhangaika tena kutatua tatizo kwa kemikali zaidi...Pheeew! Haya tusikilizane mwenzangu!

TUANZE NA BAADHI YA VITU VYA  FACIAL TREATMENT

1. CHUMVI BODY SCRUB



Hii ni scrub yenye mchanganyiko wa chumvi na manjano…. Ni nzuri sana, nakuhakikishia ubora wake kwa vile ninaitumia pia. Ni laini na unapomaliza kuitumia unasikia kabisa mwili unabaki na hali ya ulaini wa kuvutia na unapoitumia kila mara kuna mng’ao fulani unaupata. Namaanisha unatakata sio kuchubuka!

Kuna wakati uso unakuwa na weusi ambao sio wa asili, weusi uliofifia au kufubaa, au weupe uliochujuka. Chumvi Body Scrub  inakuondolea hali ya kufubaa. Ni uitumie tu kila baada ya siku mbili kusafishia uso wako. Kwa wale wavivu wa kuosha uso after make up au kupaka paka facial kila mara…nafasi ya facial hadi weekend hii  ni booonge la msaada!

Au kichunusi kikianza tu wakati wa kuoga chukua kidogo  sugulia hapo, baaasi kesho ukiamka unaona kinaanza kupotea siku inayoafuata hakipo! na hubaki na doa hata!

MATUMIZI: unaweza kuitumia kila siku mwilini kama utapenda kuitumia mwilini, au  ukaitumia kila baada ya siku mbili usoni.  Unachovya kidogo unalowesha uso kisha unamassage kwa mtindo wa kuzungusha maduara usoni. Inaua chembechembe  hafifu za uso na kuuweka uso wako fresh kabisa. Unaosha uso wako na sabuni yako baaaaasi umemaliza!
Inafaa wanaume na wanawake.

BEI: ni Tsh. 15,000 tu! 
Utakaa nayo sana tu

2. UNGA WA LIWA

Kuna liwa hii nyeupe...tunaita liwa ya Comoro

Kuna Liwa hii ya Brown

Liwa hukausha chunusi, liwa hutibu chunusi…

Ipo liwa ya kawaida nyeupe na ipo liwa ya kahawia. pia ipo nyekundu ambayo kwa sasa imeniishia...
hii nyekundu huwa naichanganya na poda ya kawaida. 
Aisee! inakupa poda yenye rangi nzuriiiii sana hasa kwetu weusi!

MATUMIZI:  unachukua unga wa liwa kidogo unachanganya na maji ya Liwa au maji ya Rose unapata uji mzito kidogo. Unapaka usoni unaacha ikaukie kwa nusu saa hadi saa nzima. Kisha taratibu unachovya vidole kwenye maji na kumassage uso ili kulainisha ile liwa iliyokauka. Fanya taratibu tu usiwe n haraka ya kuindoa kwa kusugua kwanguuuuuvu. Hapana!

Ukimaliza osha uso wako vizuri na sabuni yako uache uso upumue kidogo hata dakika 10 hivi  kabla ya kuanza purukushani za make up!
BEI: ni Tsh. 5,000 tu!


3. UNGA WA DENGU


Unga wa Dengu kwa kiingereza unaitwa Gram flour au Besan yaani una majina lukuki…hebu google uone faida zake kama huniamini.
Kwa wale wenye chunisi ngumu, hii ni kiboko yao na mbali na kuondoa chunusi kali, pia hung’arisha uso sana tu!

MATUMIZI: Chukua unga wa dengu changanya na manjano na maji ya liwa kama huna maji ya liwa basi weka maji ya limao fresh… pata uji mzito kisha paka usoni. Kaa nao nusu saa hadi saa nzima. Kisha taratibu unachovya vidole kwenye maji na kumassage uso ili kulainisha ule mchanganyiko uliokauka. usiparuze mchanganyiko kwa nguvu

BEI: Tsh. 5000 tu


4. SINGO WAKAWAKA

Monday, December 1, 2014

PERUZI YA ENZI.... HABIBI YA NOUR EL AIN BY AMR DIAB NA LYRICS ZAKE!!



Mambo ya kiarabu!..... unaambiwa viuno viuno... mapigo mapigo sasa pata na maana yake
unaachaje kuupenda huu wimbo ati!

Niliupenda hata kabla ya kujua maana yake...
nangojea tu pale habibiii habibiii habibiii hahahahahaaaa
Hebu twende sambamba na Amr kwanza...
tupunguze uchovu wa kazi

Habibi ya nour el-ain
Ya sakin khayali
Aashek bakali sneen wala ghayrak bibali

Habibi, Habibi, Habibi ya nour el-ain, aah
Habibi, Habibi, Habibi ya nour el-ain
Ya sakin khayali


Agmal aouyoun filkone ana shiftaha ...
Allah aalake allah ala sihraha
Aoyonak maaaya ...
Aoyonak kifaya ...
Tinawar layali


Habibi, Habibi, Habibi ya nour el-ain, aah
Habibi, Habibi, Habibi ya nour el-ain
Ya sakin khayali

Kalbak nadani wkal bithibini
Allah aalake allah
Tamentini

Maaak elbidaya ...
Wkoul elhikaya ...
Maaak lilnihaya

Habibi, Habibi, Habibi ya nour el-ain, aah
Habibi, Habibi, Habibi ya nour el-ain, aah
Aah ... Habibi ... Habibi ... aah



ENJOY!!


Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger