Friday, November 28, 2014

UREMBO NA LAURA:.... DETOX WATER NA FAIDA ZAKE MWILINI....


Kwa rehema za Mwenyezi Mungu. Natumaini wasomaji wangu mu  wazima… kuwa tu na ule uzima ni jambo la kushukuru Mungu.

Leo nawaletea hiki kitu kinaitwa kuondoa sumu mwilini… ninaposema sumu simaanishi sumu kama ile ya panya… La hasha! Nazungumzia sumu, hizi takataka za mwilini.

Unajua na hii milo yetu tunayokula si ajabu tu kujisikia ovyo ovyo kila siku na ukapanga foleni kumuona dokta na ukaambiwa huna hata malaria. Lakini ndio mwili haueshi uchovu na maradhi yasoeleweka! 

Na hospitali hizi za siku hizi hawawezi kukuacha ukatoka bila kupewa dawa!...
Sasa hii kudetox mwili kwa maji , ndio kama kuupunguzia mwili kadhia na kuuimarisha. Nyumba inakarabatiwa seuze mwili, tena mwili wa binadamu! Hii si yakukosa ndugu yangu!

Zipo aina nyingi za detoxification…. Zipo dawa za vidonge, zipo dawa za hali ya kimiminika hasa kwenye bidhaa za Forever living na GNLD… zipo detox diet, na detox  ya maji ambayo mimi ndio nitaizungumzia maana ni nafuu mnooooo na rahisi sana kutengeneza!

Kwanza tujue DETOX WATER NI NINI?


Huu ni mchanganyiko wa maji na virutubisho kadhaa (matunda etc) vyenye nia ya kuusafisha mwili na mifumo yake. Ni kinywaji murua kabisa, chenye ladha  fulani tulivu na chenye manufaa makubwa mwilini mwako kuliko unavyofikiria.

FAIDA ZA DETOX WATER

1. Hukupa nguvu (energy)… ile hali ya kuhisi kuchoka choka bila sababu  hupotea kabisaaaa

2. Huondoa ‘sumu’ mwilini. Tunajua mwili hujisafisha kwa kutoa taka kupitia jasho n.k lakini unapodetox mwili unaondoa hata zile taka ambazo kwa namna moja ama nyingine hazikutoka ipasavyo. Yaani kama ni usafi basi ndio umeamua kuchukua brashi sabuni na maji… full kutakata!!

Tuesday, November 25, 2014

HAPPY BIRTHDAY MAMA YANGU!!.





Dear Mom,
Sijui hata nianzie wapi jamani...
Now i know there’s no bond quite like that between mother and child. 
You know me in ways no one else ever will. You also see in me all the things I can still become and continue having faith that I can do and be whatever I want, no matter what my age.
You are my biggest fan, my mentor, my confidant, my hero, my turn-to person when my world comes crashing down and the first person I call to tell when things are going great.
The comfort that comes from our friendship, the confidence that your faith in me instills, and your unquestioning support of whatever I do, is irreplaceable. The kind of there-for-me that you are is the very essence of what makes a great mother. I wear your unconditional love and support around me like a big hug every single day.
I am so blessed to have you in my life. I’ve probably said it before …. you are my angel on earth. Thank you for always, always being at my side and having my back. No one is in my corner quite the way you are. I treasure you, mother, and love you more than life itself.
You are an amazing soul ever ready to learn something new, always open to differing opinions, and so compassionate and kind. You have always taught by example.
I hope you break 100 with good health and a strong mind. There’ll never be a day in my life when I won’t need you. I’m here for you too. Please remember that.
Happy, Happy, Happy Birthday, mom. You make the world a better place.
Love you always, I mean alwaaaaays mom!!
your daughter
LAURA PETTIE
NB. ni siku kama ya leo mwaka jana nilivunjika mguu!... from there life was never the same again... but i'm still thankful to God!!

Saturday, November 22, 2014

10 MINUTES WITH GOD!...WATEULE WA BWANA





Wateule wa Bwana karibuni mezani pake, njoni, Bwana awaalika enyi wenye moyo safi x 2

Amewaandalia, leo, karamu takatifu, njoni mwili na damu yake chakula safi cha roho x 2
  1. Kwanza tujitakase, nafsi zetu wenyewe, tukishakutakata, tujongee meza yake.
     
  2. Karibuni mezani, Bwana awaalika, kwenye karamu yake, enyi wenye moyo safi.
     
  3. Na tule mwili wake, na tunywe damu yake, ndicho chakula bora, cha roho zetu karibu.
     
  4. Tusipokula mwili, na kunywa damu yake, tunazinyima roho zetu neema zake Bwana.




ENJOY!!

Friday, November 14, 2014

UREMBO NA LAURA:.....JE WAZIJUA CHARGER PLATES??


hiyo sahani ya chini, rangi ya pink ndio inaitwa Charger Plate!

Kuna vitu ambavyo wengi wetu tunaviona tu katika sherehe au mialiko majumbani mwa watu lakini hatuvijui vizuri, si kwa majina wala kazi zake. Moja ya vitu hivi ni hizi sahani paaaana zinazoitwa ‘Charger Plates’

 Unazijua? au unaziona tu kwenye picha?.... hahahahaaaa!!...
Najua mnazijua bwana ila kwa wale wenzangu na mimi ambao kuna mambo ya kisasa na nini na nini yanapita kushoto kwa kasi wakati sisi tuko kulia…ndio hivi tunaelezana ili mwisho wa siku usije ukabeba Charger  Plate ukaenda kupakulia  chakula ohooo!!

MATUMIZI YA CHARGER PLATES
1. MAPAMBO

Sahani hizi pana mara nyingi huwa mapambo. kuna umaridadi fulani unaletwa na hizi sahani unapotumia kupambia meza yako wakati wa mlo. Yes! unaweza kuzitumia hata nyumbani
Mfano unawageni wako, basi unazitumia kupamba meza na hakika
utajizolea maksi tele za umaridadi.

Katika sherehe Charger Plates zinaweza kuendana na rangi ya Party. Hebu angalia hiyo picha hapo juu uone rangi nyekundu ilivyoendana na rangi nyekundu kwenye viti!
classy!....

Thursday, November 6, 2014

UREMBO NA LAURA:.....JINSI YA KUKABILIANA NA WEUSI KWAPANI!!

K


Habari zenu wasomaji wangu!
Kama kawaida leo tunakutana tena ulingoni…. Katika kuwekana sawa hapa na pale kwenye masuala ya urembo masuala ya usafi na kadhalika! Mradi kwa gharama ndogo tu unabaki msaaafi kabisa na mwenye furaha tele! Team kubana matumizi hahahaha!

Leo nataka kugusia suala la makwapa kuwa meusi. 
Inakera sana!... hasaaa linapokuja suala la kuvaa nguo ya kukata mikono. Yaani unakosa kujiamini. Tena  basi uwe kwenye kadamnasi ambapo unatakiwa kupunga mikono hivi…ni zaidi ya shughuli!... unashindwa hata kujimwayamwaya mwenzangu aiiii kisa tukwapa tweusi!

Kuwa na kwapa jeusi sio ugonjwa, sio dhambi lakini mwenzangu linapunguza maksi kiasi fulani…. Halafu kwanini uwe na lami makwapani wakati njia tele za kuondoa na kuzuia zimejaaaa!!

Kwanza tuangalie sababu za makwapa kuwa meusi!
1. Unyoaji…. Wembe unachangia sana kuwa na makwapa meusi…ile puruuu puruuuu aaah mwenzangu lazima kwapa lidate hahahahaaa…. Hapo umetia vijisabuni kidogo unashave kwa nguuuuvu ili kwapa libaki jeupe mpaka mtu nje anaweza uliza jamani kuna usalama uko? anhaaaa!!

2. Deodorant:… unaroll deodorant  wiki ya kwanza…ya pili..ya tatu…unaona mabadiliko kwapani we umo tu!.... kipodozi chochote kikionyesha hali ya kukukataa hata kama ni siku mbili tatu…KIACHE!! Ukijitia una uchungu na hela yako utagharamamika zaidi ya hizo ulizotoa kwenye kutibu matokeo, unapaka deodorant unasikia  kwapa linawaka moto jamani bado umo tu! yahusu!

3. Magonjwa… hapa sitaingia sana maana sina utaalamu huo ila ndio hivyo kuna wakati hali hiyo inaletwa na ugonjwa ulionao na utagundua hili kama njia zingine zote zikidunda.
Haya sasa ndio tushapata kwapa jeusi...tufanyeje?

NAMNA YA KUKABILIANA NA  KWAPA JEUSI
1. LIMAO NA SUKARI


Hii njia ya kwanza iliyo bora kabisa na nyepesiiii
Kata kipande cha limao kichovye kwenye sukari, tena ile ya brown ndio nzuri zaidi.
Sugua kwapa lako kwa mtindo wa kuzunguka. Taratibu tu ila hakikisha unasugua eneo zima. Usikamue limao wewe sugua tu…majimaji  yatatoka yenyewe.
Acha kwa dakika 10-15 kisha osha makwapa yako vizuri kwa sabuni yako ya kila siku.
Fanya hivi asubuhi na jioni mpaka uone weusi umeondoka na lazima uondoke.
Faida yake ni kuwa Limao litaondoa pia harufu ya kwapa, na katika kipindi hiki usipake deodorant yoyote.

Monday, November 3, 2014

PERUNZI YA ENZI....AZALAKI AWA BY GATHO BEEVANS WITH LYRICS!



Sijui hata nilichokumbuka...basi tu nimejikuta naimba huu wimbo leo saaana!
Halafu naimba kiitikio tu tena ninavyojua mwenyewe hahahahaaa
chezea kilingala!
ila nimekumbuka mbaaaali kweli dah!...twende kazi sasa!

Azalaki awa
Pembeni na nga
Esika akeyi ekaboli nga na yé

Ye na bembo na ndako mosika
Distance na kati ye ngambo ngai na ngambo

Tango mususu soki na kanisi ndengué oyo tozalaki epesi nga kobanga
Moto na lingi akoma mosika
Natondi na ba souvenirs na motema
Na lela na nani ?, na salako nini ?, na kende ko wapi ?
Nakomi se ko banza ngai moko

Azalaki se awa
Se awa
Cherie a keyi nayé
Alobaki na ngai akozonga
Se awa
Ngako na zelaka yé


Azalaki se awa
Se awa
Cherie a keyi mosika
Alobaki na ngai akozonga
Se awa
Suka se okoya



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger