Saturday, March 30, 2013

SINDI.......NA LAURA PETTIE (4)

4
Sehemu ya nne
Njia nzima Sindi na Jerry walibishana hiki na kile, wakaelezana haya na yale. Kwa muda mfupi tu waliozungumza njiani Jerry aligundua Sindi Nalela alikuwa na upeo mkubwa tofauti na elimu yake ya shule ya msingi aliyokuwa nayo.

Pasipo kujua Nyanza alikuwa akiwafuatilia nyuma, walisimama na kubishana, wakisontana kwa vidole na mara kadhaa Jerry akikwepa vibao vya Sindi pale alipomtania na kumcheka. Nyanza aliyaona yote haya na aliyafuatilia kwa umakini mkubwa mpaka pale alipohisi asingeweza kuwafuatilia tena baada ya Sindi na Jerry kuagana na kila mmoja kushika njia yake. 

Thursday, March 21, 2013

SINDI....na LAURA PETTIE (3)

3

SEHEMU YA TATU....

Nyanza alikimbilia bondeni kidogo kulikokuwa na vijana wakivua samaki, akawapigia mbija na kuwapa ishara ya kumfuata. Sindi alikimbilia kijijini na kukusanya watu waliokuwa karibu na baada ya dakika kumi na tano Jerry alishazungukwa na wanakijiji, wengine wakimtazama kwa mbali, wengine wakijaribu kumuinua na wengine wakishauriana cha kufanya.

Wakiwa bado katika hekaheka ya kumhoji yeye ni nani na imekuwaje, Jerry akapoteza tena fahamu palepale na taharuki ikazuka kwa hofu kuwa pengine amekufa.

Sunday, March 17, 2013

SINDI....na LAURA PETTIE (2)

2
SINDI......NA LAURA PETTIE (2)

Asubuhi ya siku hii ilikuwa siku ya ibada kwa wakristo walioishi kijiji cha mzimbuni, Ndani ya kanisa lililoezekwa kwa mabati chakavu, ibada ilikuwa inaendelea na waumini walikuwa wamesimama wakiimba wimbo kwa kutumia vitabu cha nyimbo ambavyo vilionekana kumilikiwa na waumini wachache huku waliobaki wakiwa wamekariri beti za wimbo huo.

Mbele ya moja ya mabenchi ya mbao yaliyosimikwa ardhini alisimama mama yake Sindi, akifuatiwa na Peter kisha Sindi, Maria na Alma, marafiki wa Sindi pamoja na  bibi yake Sindi. Wakati waumini wengine wakikazana kuimba Sindi na marafiki zake walikuwa wakiimba huku nyuso zako zikionyesha wazi akili zao hazikuwa eneo lile.

Friday, March 15, 2013

SINDI.....NA LAURA PETTIE (1)

1


 Giza jepesi lilikuwa limegubika sehemu kubwa ya kijiji cha Mzimbuni, miale ya moto, taa za kandili, mishumaa pamoja na vibatari ilikuwa ikionekana hapana pale huku ikichagizwa na mwanga hafifu wa mbalamwezi. Hali hii iliashiria kuwepo kwa pilika pilika huku na kule.

Watoto walikimbizana na kupigizana kelele za kimichezo, Wanaume wa kila rika wakiwa wamejikusanya mahali wakizungumza na wengine wakipata pombe za kienyeji huku wanawake na mabinti wakiwa makini na shughuli za upishi katika nyumba zao. Ndege wa usiku hawakuacha kupiga miluzi na kuleta hali ya kuvutia, hali ya kijiji, hali ya maisha ya ujamaa.

Monday, March 11, 2013

IT IS MY BIRTHDAY.... 11TH MARCH, 2013

Nimshukuru Mungu kwa majaaliwa aliyonijaalia.....
Niwashukuru wazazi wangu kwa mapenzi na malezi mema waliyonipatia
Niwashukuru ndugu zangu na familia yangu kwa upendo na ushirikiano wanaonipatia
Niwashukuru Marafiki zangu wakiongozwa na Pascalina na Zuhura kwa urafiki mwema walionizawadia
Niwashukuru nyie wasomaji wangu, msiochoka kuingia humu kujua lipi limejiri!


Friday, March 1, 2013

PERUZI Y ENZI: ONE MORE TIME ...BY JAMES INGRAM








NAUPENDA HUU WIMBO MNO......
Nyakati zote ninapotaka kuondoka ndani ya huzuni na kujipa nafsi ya kutabasamu
huwa nauimba huu wimbo kwa fujo zote
Nauimba kana kwamba uliimbwa special kwa ajili yangu

Maneno yake, midundo yake na sauti tamu ya James Ingram
Sadakta! sijawahi choka kuusikiliza!
Chini ni maneno ya huu wimbo ulioimbwa na Michael Bolton na kurudiwa
na James ingram katika Filamu ya sarafina

 Don't look back 
Don't be scared 
We've got dreams and we're still young Just think about how far we've come
 Think of all We have shared It's a wonder we survive But here we are and we're alive! 
Can we hold on, hold on? Take a moment to celebrate 
Now before we are gone Take a moment to celebrate 
There's music in the wind Let's dance one more time 
There's a rhythm deep within 
Let's dance one more time One more time Sing the song 
There's a power in our voices Hopeful and strong 
 Years from now Somewhere down the line 
We'll remember and we'll all sing One more time

ENJOY!!


Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger