Friday, July 24, 2015

UREMBO NA LAURA:.....MATUMIZI YA NAPKINS MEZANI..

NAPKIN

 Baada ya kuwa kimya muda mrefu kwenye kona hii sasa nimerejea! Twende kazi

Wengi wetu nadhani tunajua ni kitu gani. Kwa maelezo ya juu juu ni karatasi au kitambaa kinachokaa mezani kwa ajili ya kufutia pembe za  mdomo na vidole wakati wa kula au baada ya kumaliza kula. 

Kinaweza kuwa kitambaa cha material yoyote ile ila cotton  inapendeza zaidi kwa kuwa ni rahisi kuikunja kwa staili mbalimbali za kupendeza kuliko kitambaa laini.

Kitambaa hiki unaweza ukakikuta mezani hotelini, nyumbani kwa mtu au kwenye sherehe.  Hata wewe unaweza kuandaa msosi wako mzuri nyumbani na kualika wageni wako  kisha ukakitumia kuongeza umaridadi mezani pako. Si unakumbuka charger plates!!

Kuwa Classic ndio habari ya mjini my dear!.... mumeo kaalika watu wa kazini kwake, hebu fanya kitu cha kuwafanya wakitoka hapo waone mwenzao ana mtu anayependa vitu vizuri. Simple table setting ya uhakika!! Hakuna kuomba omba tishu heheheeee!

Zipo staili mbali mbali za namna ya kuiweka napkin mezani. Kuna wengine hufunga kama kipepeo, kuna wengine huikunja pembe tatu na kuiweka juu ya sahani yaani staili za kuifunga ni nyingi sana,  ni wewe tu na uamuzi wako.

NAPKIN HUKAA WAPI?

Kama ni mlo wa kawaida na si ule rasmi wa shughuli maalumu Napkin inakaa popote kulingana na nafasi kwenye meza yako. Ila kwenye shughuli kubwa utaikuta napkin mezani juu ya sahani.

UMEIKUTA NAPKIN KWENYE MTOKO WAKO…UFANYEJE?

Umealikwa mahali mwenzangu, sehemu yenye mchanganyiko wa watu. Nadhani hutotaka kuonekana mshamba saaana au kushindwa kujua ustaarabu wa matumizi ya Napkins au sio? Hahahahaaaa!!

1. Ukifika mezani usikimbilie kuchukua napkin haraka haraka…ngoja watu wawili watatu wakae…na kama mko wawili ngoja mwenzio naye akae!

2. Chukua napkin yako iweke mapajani. Napkin inakaa mapajani kamwe usiweke napkin shingoni. That is not a bib jamani. Bib ni kile kidude tunafungiaga watoto shingoni wakati wa kula, kwa Kiswahili sijui kinaitwaje. Bibs are for babies not adults!! Labda kama unafanya comedy.


3. Ukishaiweka mapajani anza kupata mlo wako kama kawaida. Unapofuta midomo ikunje upate ncha hivi na kufuta kando ya midomo yako. Usitumie napkins kufuta lips za midomo yako. Hahahahahaa na utafutaje mdomo mzima mwenzangu kwani unakulaje kwa mfano?


Saturday, July 18, 2015

10 MINUTES WITH GOD!....AMETENDA MAAJABU BY FANUEL SEDEKIA



I'M IN LOVE WITH THIS SONG!

Nimejikuta nausikiliza mara mbili tatu nne tano.... and i was like mmmh kwanini nisishee na nyie 
Ninapofanya shughuli zangu mara nyingi tu huwa nasikiliza muziki
na nyimbo za dini ni sehemu ya muziki ninaosikiliza sana!

R.I.P Fanuel .... 

Friday, July 17, 2015

EID MUBARAK


 KWA WASOMAJI WANGU WOOOOOTE POPOTE MLIPO DUNIANI!!

NAWAPENDA!!


Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger