Thursday, January 10, 2013

PERUZI YA ENZI.......REMEMBER ME BY LUCKY DUBE


....


...I just love this song.... ninamengi ya kuelelzea kwanini naupenda ila kwa leo acha niutume kwa binadamu wote duniani waliokos amapenzi ya baba zao....waliokosa kuwajua baba zao na zaidi ambao wanatamani kukutana nao!...

HUWA WANAANZA NA KIITIKIO

 Daddy where ever you are remember me......In what ever you do I love you
 Daddy where ever you are remember me......In what ever you do I love you

HAPA SASA NDIPO HUWA PANANIGUUUUSA
You left for the city many years ago,.....Promised to come back.......And take care of us
Many years have gone by now.......Still no sign of you Daddy........Mother died of a heart attack
Many years ago when she heard........That you were married again.......Now, I'm the only one left In the family

WANATANDIKA KIITIKIO KWA HISIIIIIA
KISHA ANANUNG'UNIKA BALAA
Wandering up and down......The streets of Soweto......No place to call my home
I tried to find you....... Many years ago......But the women you' re married to was no good at all


ENJOY!!




 Daddy yo!

BARAZANI: ......MAMBO HAYAENDI??



Habari zenu wadau…..nafarijiiika sana ninapoona mnazidi kuongezeka taratibu! na ni matumaini yangu Mungu anawajaalia kwa kadiri ya kila mja na  gawio lake.

Nisizunguke tu kama tiara….niseme lililonileta hapa!....kweli kuishi ni kujifunza na unajifunza uyaongoze maisha yaliyo bora. Ukiwa unaishi tu bila kujifunza mwenzangu kaa chini kwanza urudie alphabet za maisha yako pengine kuna mahali umeruka alphabet muhimu!

KOREAN DRAMA..... SONG II GOOK a.k.a JUMONG!!


Nazipenda sana tamthiliya za kikorea ambazo nyingi zimeonyeshwa na kituo cha ITV....enzi za Anologia.... nimeshaziona nyingi sana na nimejikuta niwa na my favorite Korean drama hadi favorite korean actors na kwa leo nimzungumdie kwa ufupi tu huyu jamaa wenyewe tunamuita jumong....ila kwao uko wanamtambua kama  SONG II GOOK
Song II Gook .......a.k.a Jumong
Aaaww he is Damn haaawt!

Ni muigizaji mashuhuri toka korea ya kusini. Akiwa ameigiza tamthilia kadhaa za kihistoria kama Jumong ambayo imempatia umaarufu mkubwa nchini, Emperor of the Sea na nyingine nyingi. 

Saturday, January 5, 2013

PERUZI YA ENZI....SOLEMBA BY JUWATA JAZZ BAND




Naupenda huu wimbo sana.... sauti ya mwanamuziki mwenye ulemavu wa macho  Zengakala ni burudani ya aina yake. kuna stori nyingi kuhusu huyu jamaa....ila tisa kumi Mungu alimjaaliwa kipaji cha aina yake.

hapa chini mashairi ya huu wimbo...kama kuna vijimakosa mtaniwia radhi wadau

Ulinipa ahadi tukutane kwenu.........Nikitumaini nimewahi
Nilichopata kwako ni matusi oo, oo na dharau tele
Ungenieleza ukweli solemba......Kuliko kunidanganya oo
Najuta kuitimiza ahadi oo ambayo si ya kweli.

 KORASI SASA....
Nilikupenda kimapenzi Solemba ee...... ila dharau uliweka mbele solemba.

ZENGAKALA SASA.....
Nilichomwa na jua toka asubuhi....... mpaka saa nane Solemba sababu ya kukungoja wewe
Kumbe ulikua ndani ukichungulia dirishani
Nimeshituka Solemba , Nimeshituka Solemba

 KORASI....

ZENGAKALA ANARUDI.....
Sikutaki tenaaa...... sina haja nawe......nimeshapata mwingine atakaye nipenda kwa roho moja, Tafuta bwana mwingine utakae mbabaisha kama mimi Huna huruma Solemba.......Aloi I love you baby

KORASI INARUDIWA HAPA



ENJOY!!



MAMBO 10 NINAYOKUOMBA UJARIBU 2013!!!


Habari zenu wadau....

Mwaka ndio umeanza hivi, wiki ya kwanza kwanza, kama hujatoa sadaka ya shukrani nenda ndugu yangu upendeleo aliokupa Mungu kuuona mwaka mwingine si mdogo. Ni zaidi ya mibaraka elfu moja. Uhai kitu kingine jamani.

Sasa  mdau hebu ngoja tuzungumze kitu.... katika maisha nimegundua kuna vitu huwa tunajiwekea mipaka wenyewe pasipo kushurutishwa wala kutishwa. Tunajinyanyapaa, tunajitenga tunajohofisha, tunajishusha mno kabla ya kutendewa haya yote na mtu yoyote na mwisho wa siku tunawalaumu wengine kwa mambo tuliyoyajenga wenyewe.....

Umenielewa?....bado?...hebu rudia tena kusoma hapo juu basi....tulioelewana twende kazi....
Umewahi kujiuliza kwanini unaweza kukwepa kuingia mahali kwa vile unahisi huna hadhi ya kuingia mle ndani?....hujakatazwa na mtu....wewe tu na hofu zako unajiwekea mipaka...
'aah pale kuna wenyewe bwana' hao wenyewe na wewe mna tofauti gani?....kuna mwenye mkataba na Mungu? au kuna mwenye kufa na kufufuka? jibu ni hakuna wako sawa tu na wewe, ukiacha mbali kupishana kimatabaka hususani kwenye kumiliki pesa na vitu vya mpito tu!

Sasa hebu tuangalia mambo ambayo binafsi nahisi unaweza kujaribu kuyafanya na pengine yakaongeza kujiamini kwako, yakakufanya ukajifunza zaidi, ama ukajikuta ukipata njia ya kutokea kimaisha bila kutarajia.


1. JARIBU ENEO/ HUDUMA MPYA ......



.......Umekuwa ukizipita hoteli mbalimbali kwa kigezo tu kuwa huna hadhi ya kuingia pale, ama kwa kigezo tu gharama zao ni kubwa sana. Hebu weka choyo ya nafsi kando na uingie uagize japo maji tu ya 1,500 utulie na glasi yako uburudike na kuyasoma mazingira...sio kila siku kwenye vigrosari na vibanda vya chini ya mti hahahahaaaaa.....nenda sehemu mpya ujifunze hata kufungua milango ya kisasa!!....



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger