Sunday, October 27, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (44)

44
Pamoja na usiku huu kuwa wenye mvua na upepo wa kuleta usingizi mnono, kwa Sindi Nalela, usiku huu ulikuwa kama kitanzi shingoni. Matone ya mvua yaliyofanya michirizi kwenye dirisha la kioo lililokuwa limejengewa mita chache toka lilipo dari yalipita machoni mwa Sindi pasipo kutambulika akilini.

Sunday, October 20, 2013

BARAZANI... TUNAPASWA KUSHUKURU KWA DHATI



Katika safu yetu ya leo ya barazani… ninayo machache tu ya kusema na wewe ndugu msomaji…

Yawezekana wewe ni mwanamke…. una kazi nzuri yenye kukuingizia kipato… una afya njema tu inayokupa nafasi ya kuzunguka huku na kule…. una marafiki wanaoifanya siku yako iishe katika namna ya kupendeza…. lakini huna mume pengine huna hata boyfriend ama unaye lakini maumivu anayokupatia katika uhusiano uliopo unajihisi kama mtu mpweke sana. Pengine unavyo vyote hivi lakini huna mtoto na unaona kama dunia inakuonea, Mungu amekutupa!

Friday, October 18, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (43)

43


Siku hii ilijaaliwa mawingu mazito yaliyofifisha ukali wa jua na kuleta  hali ya ubaridi iliyokuja na kutoweka. Ndani ya saluni kubwa ya kisasa ya wanawake iitwayo Marino kulikuwa na pilika pilika za hapa na pale. Huyu akioshwa nywele, yule akisuguliwa kucha hapa wakiwekana rolazi na kule wakitindana nyusi, mradi kulikuwa na hekaheka za hapa na pale.

Tuesday, October 8, 2013

SINDI.... NA LAURA PETTIE (42)

42

....Fiona Agapella aliendesha gari lake mpaka nyumbani kwa rafiki yake Iloma. akaingia ndani kwa mbwembwe akicheka kwa furaha na chupa ya mvinyo mkononi. Akaitua mezani na kukimbilia jikoni. Akarudi na glasi mbili na kuziweka mezani karibu na chupa ya ule mvinyo. Iloma, rafiki yake akiwa bado na butwaa lililomfanya shindwe hata kuufunga mlango itakiwavyo.



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger