Friday, April 29, 2011

SIRI YANGU 2.... na Laura Pettie


Ijapokuwa sasa naanza kuikubali hali hii lakini bado Kelvin anazunguka kichwani pangu na nahisi moyo wangu ukiumia zaidi ninapozitazama picha zake, ninapokumbuka nyakati za furaha tulizokuwa pamoja, nyakati tamu ambazo kwa hakika najua hazitajirudia tena katika anga hili la karima. Muda huo wa jioni ya jumapili hiyo tulivu Nilikuwa ufukweni hapo pamoja na rafiki yangu Iloma aliyekuwa ameambatana na mumewe Jonas. Iloma alikuwa mfanyakazi mwenzangu na rafiki yangu mkubwa wa tangu utotoni. Yeye alikuwa tayari ameshaolewa na kubahatika kupata mtoto wa kiume mwenye umri wa mwaka mmoja. Wakati Iloma na mumewe Jonas wakiogelea pamoja na mtoto wao mimi nilibakia pale ufukweni nikiwatazama namna walivyokuwa wanafurahia maisha yao ya ndoa. Nilihisi nikiwaonea wivu kwa amani na upendo uliokuwepo kati yao. Nilihisi uchungu ambao naweza sema hausemeki mdomoni wala hauandikiki karatasini. Ilikuwa ni mithili ya mvuke wa maji ya moto penye kidonda kibichi.
Nilijiinua taratibu na kuanza kutembea kuelekea upande uliokuwa hauna watu zaidi. Nilizidi kupiga hatua na kutafuta mahali palipokuwa pamefichana na kuketi hapo. Nilihisi upweke, nilihisi uchungu na simanzi zikinikaba na kunifanya nijiinamie na kulia kwa kwikwi.
“ Kelvin…Kelvin why!... Why Kelvin…”
nilipayuka mwenyewe bila kujali kama kuna mtu anayeniona ama kunisikiliza. Niliyainua macho yangu juu na kuzitazama mbingu huku machozi yakizidi kunitiririka kwa fujo. Mikono yangu niliifumbata kifuani na sasa nilishindwa kuhimili uzito wa majonzi niliyokuwa nayo na nikaangua kilio cha nguvu.

Nililia sana nisijue hata cha kufanya pale nilipokuwa nimeketi. Mara zote nilitamani kukurupuka usingizini ili yale yote yageuke kama ndoto, lakini wapi hali iliendelea kuwa halisi na isiyo na hata chembe ya kiini macho!


“ sikustahili hukumu hii Kelvin, sikustahili maumivu haya mimi sasa kwanini umenifanyia hiv?” nilijiuliza pasipo kuwa na uhakika wa kupata jibu toka kwa huyo niliyemkusudia. Nililia kwa dakika kadhaa kisha taratibu nilijaribu kujizuia kulia. Ingawa hisia zilinitawala lakini pia nilijua kuwa kulia vile kusingebadili chochote katika historia chungu aliyoniachia Kelvin.

Nilivuta pumzi mara kadhaa na kuziteremsha kwa nguvu nikijaribu kuacha kulia hata hivyo nilishindwa kabisa kujitawala. Kilio cha chini kwa chini hakikukoma na machozi nayo yalizidi kuteremka kwa mithili ya kijito cha maji kitokacho bondeni..


Nikiwa nimeketi chini, niliikunja miguu yangu na kuyafanya magoti yawe egemeo la kidevu changu na mikono iliikumbatia miguu yangu hali macho yangu yaliyoviringwa na machozi yakiitazama bahari pasipo kuitambua akilini. Nilishtuliwa na mkono uliotua katika bega langu la kushoto. Nilihisi mshtuko usio wa kawaida mara baada ya mguso huo. Niliugeuza uso wangu kwa haraka na kumtazama mgusaji huyo aliyenifanya nihisi hisia Fulani za faraja moyoni mwangu. Alikuwa Jonas mume wa rafiki yangu mpenzi Iloma.



“ mbona umejificha huku Karen….na hupaswi kuwa katika hali hii kila mara” alinisemesha kwa upole hali akichuchumaa na kuzifanya nyuso zetu ziwe mkabala. Alikuwa mwanaume wa kuvutia mpole na mwenye sura nzuri ya kusisimua na mara nyingi watu walipenda kumfananisha na mwanamuziki Robert Kelly, urefu wake wa kadri, weusi wake wenye mvuto na sauti yake ya kiume iliyo nzito na tulivu, kwa hakika viliwafanya watu wa kila rika wazidi kumpenda Jonas.

Mbali na uzuri wa sura yake Jonas alikuwa na haiba ya upole na ucheshi na mara nyingi uso wake ulipambwa na tabasamu pana la kuhangaisha!
“ jonas haya ni maisha yangu ninayoyastahili”

“ hapana Karen, you still have a chance to be happy!” alinijibu akijiweka sawa kwa kuketi pale mchangani kando yangu. Macho yake maangavu yalimetameta na kutoa nuru ya faraja.

“ kwa vipi Jonas na Kelvin ameondoka na furaha yangu…huwezi kukisia hata robo tu ya maumivu niliyonao ndani ya moyo wangu,

kwanini amenifanyia hivi mimi mbona nilijitahidi kuwa mpenzi bora kwake sasa kwanini ameniacha katika hali hii jonas?” niliongea kwa ghadhabu na taratibu nikajiinamia tena kuanza kulia upya. Najua nilimpa Jonas wakati mgumu mno, alijisogeza karibu yangu na kuketi ubavuni pangu kisha taratibu aliupitisha mkono wake wa kuume mgongoni pangu na kunivutia ubavuni pake. Nilijikuta nikiuficha uso wangu kifuani pa Jonas. Nilihisi faraja na kupata ahueni kuwa mikononi mwa mtu kama huyu.

Pasipo kutarajia nikaizungusha mikono yangu kiunoni pa jonas na sasa kila mmoja aliyasikilizia mapigo ya moyo ya mwenzake. Tulitulia hivyo kwa sekunde kadhaa nami nikijitahidi kuzizuia kwikwi za kilio. “huyu ni mume wa rafiki yako Karen!” mawazo hayo yalipita kwa kasi akilini mwangu na nikajikuta najiondosha mikononi mwake ghafla na kusimama mbele yake hali macho yetu yakitazamana sawia. Niligundua sikupaswa kuwa nae pale.

“ u mrembo sana Karen!” alinitamkia kwa sauti ile ile ya kubembeleza. Sikumjibu kitu zaidi ya kuanza kupiga hatua na kumuacha pale alipokuwa ameketi. Nilirudi hadi pale nilipokuwa nimeketi mwanzoni na kumkuta Iloma akimvalisha mtoto wake sweta. Alionekana kukasirishwa na jambo.
“ Karen umemuona wapi Jonas?” Iloma aliniuliza mara tu aliponiona
“ aah!... kwani alikuaga anakwenda wapi?” nilimuuliza nikianza kuhisi kuwa Jonas hakuwa amemuaga mkewe wakati ananifuata kule nilikokuwa nimeketi.
“ hujamuona?” alinitupia tena swali badala ya kujibu swali nililomuuliza. Nilishidwa kumpa jibu la kumridhisha lakini hata hivyo nilizuga kwa kumkaribia na kumchukua mtoto.
“ ni bora tukiondoka sasa naona mtoto anakufa na baridi ya hapa beach” nilijisemeza kukwepa maswali zaidi ya Iloma aliyekuwa anaonekana kuwa na wasiwasi na mahali aliko mumewe.
“ Karen nimeanza kuchoshwa na tabia za Jonas…ni bora kama tutaongea kesho ofisini” iloma aliniambia kwa msisitizo kidogo, macho yake yalionyesha umakini katika kile alichokuwa anataka kunieleza. Nilimtumbulia macho tu pasi kuongea lolote. Niliteremsha pumzi za haraka na kumuuliza
“ Jonas amekufanyia nini Iloma?” nilimuuliza kwa mshangao kidogo
“ nadhani ni tatizo linalokua taratibu na kama sitalitafutia suluhisho mapema jungu bovu litageuka magae Karen” aliongea kwa huzuni.Aliniacha njia panda!
“ Kwani Jonas ame…” sikuweza kuimalizia sentesi yangu kwa vile Jonas alitokea upande wa pili mahali tulipokuwa tumeegesha gari. Iloma alimtazama mumewe kwa hasira kidogo na kuelekea kule alikokuwa amesimama.
“ hata hapa Jonas kwanini unataka kunitia aibu hivi mbele ya rafiki yangu!” nilimsikia Iloma akimfokea Jonas kwa hasira pengine bila kujua kuwa nilikuwa nae huko alikokuwa. Jonas hakumjibu kitu zaidi ya kuzunguka upande wa dereva na kuingia garini. Niliwafuata nikiwa nimempakata mtoto na kuingia garini. Safari nzima ya kuelekea nyumbani ilitawaliwa na ukimya wa ajabu licha ya Jonas kujaribu kumsemesha mkewe lakini Iloma alionekana wazi kuwa na kisirani fulani. Kwa hakika sikuwaelewa wanandoa hawa. Waliniteremsha nyumbani kwetu na wao wakaendelea na safari yao.

Thursday, April 28, 2011

....Me & Zuhura visiting Kita!

Lizbeth a.k.a Kita



Easter Monday niliamua kumtembelea huyu malaika! it was funny kwa kweli, looking at her blue eyes, i just felt like i want to be a mom so soon and yeah Kita made me think twice about having my own angel... praying she could have those amazing eyes as well hahahahaaa...next year inshallaah!


sharing her album



Kita you are so beautiful honey...
OMG! once you carry her hutataka kumuweka chini kabisaaaa



Rafiki yangu Zuhura akipokea baraka za Kita



Me & baba Kita, Mr. Wynjones ...
where is mama Kita jaman?... cant believe hujatokea

Asanteni sana familia ya Wynjones Kinye kwa ukarimu mliotuonyesha..

SIRI YANGU......na Laura Pettie

....Hadithi hii niiandika muda kidogo lakini nimeona si mbaya kama nitaiweka humu kama mwanzo tu wa yale niliyoyaahidi...Ni hadithi inayohusu maisha ya msichana Karen...ilikuwaje mpaka yaliyomo yakabaki kuwa siri yake...lets share!

Karen


Upepo mwanana ulivuma toka pande mmoja kuelekea upande mwingine, upepo huo uliyayumbisha makuti makavu yaliyokuwa yakining’inia minazini na kuleta raha isiyo kifani. Minazi ile nayo iliinamia upande na kuzidi kuleta mandhari ya kuvutia hapa ufukweni mwa bahari. Nilikuwa nimetulizana pembezoni kidogo mwa mgahawa uliopo hapa coco beach. Kopo la soda aina ya cocacola lilikuwa mkononi hali mawazo yangu yakiwa kule baharini ambako watu walionekana kuyafurahia maji bahari.


Ilikuwa kawaida yangu kupumzika mahali kama hapa kila mwisho wa wiki. Yote hii ilikuwa ni kutafuta namna ya kujisahaulisha machungu niliyokumbana nayo miezi miwili iliyopita. Machungu ambayo kwa namna moja ama nyingine yameyabadili maisha yangu na kunifanya niyaone katika yalivyo ndani ya upande mwingine wa shilingi. Katikati ya wiki nilifanya kazi mpaka saa tatu za usiku na niliporejea nyumbani niliishia kulala kwa uchovu mpaka alfajiri ya siku iliyofuata. Nilikuwa mtoto wa tatu na wa mwisho katika familia yetu. Kaka yangu Brian alikuwa daktari katika hospitali moja binafsi. Dada yangu Debby alikuwa anamiliki saluni yake binafsi na mimi kitinda mimba nilikuwa muhasibu. Baba yetu alikuwa mwenye kumiliki biashara mbalimbali hali mama alikuwa msaidizi wa baba katika biashara zake na mara nyingi alikuwa akikaa kwenye duka lililokuwa karibu kabisa na nyumbani. Katika kukua kwangu nilikuja kugundua kuwa baba na mama walikuwa katika mgogoro mzito ambao hawakutaka kuuweka wazi kwetu! Mgogoro huo uliokuwa ukifukuta chini kwa chini uliniacha ndani ya maswali mazito!

Mara nyingi niliposhtuka usingizi usiku niliwasikia wazazi wangu hawa wakizozana kwa sauti za kunong’ona na nilishindwa kuelewa kilichokuwa kinapelekea hali hiyo kati yao. Mara kadhaa baba aliondoka nyumbani na kukaa wiki mbili hadi tatu bila kurejea nyumbani na tulipomuhoji mama alibakia kulia na kutuambia kuwa hakukuwa na kitu kibaya kati yao. Mpaka namaliza chuo na kuajiriwa bado sikuwa naelewa kilichokuwa kinawakosanisha wazazi wangu.

Ukweli ni kuwa sikuipa akili yangu nafasi ya kujua kuwa katika kitu mapenzi zipo raha na karaha na kwa hakika ilikuwa zamu yangu kupambana na kitu karaha ya kuachwa mpweke ndani ya dunia hii ya mapenzi. Sikuwahi kuwaza kuwa mapenzi yanaumiza hivi hususani linapokuja suala la kuachwa bila huruma, bila hatia wala kupewa njia ya kukabiliana na huu mtihani….Inshallah! machozi ya mnyonge Mungu huyalipa na kuyalipia.

Mwaka mmoja uliopita nilivikwa pete ya uchumba na aliyekuwa mchumba wangu wa siku nyingi Dokta Kelvin Nashon. Sherehe hiyo ya kuvishana pete ilifanyikia katika hoteli ya kitalii ya Paradise huko Bagamoyo. Huku tukishuhudiwa na ndugu, jamaa na marafiki mimi na Kelvin tulifikia uamuzi huo mara baada ya uchumba wetu kutimiza mwaka mmoja, mwaka mmoja wa misukosko ya hapa na pale, mwaka mmoja ulioweka hatihati ya kuachana na ndio huo Mwaka mmoja uliojaa kila aina ya mbwembwe za penzi shatashata, kweli kivumacho hakidumu na kikidumu jua kweli kigumu. Nilimpenda Kelvin mno na ndiyo maana licha ya kutokea hayo yaliyouumiza moyo wangu nahisi bado nampenda Kelvin. Niliamini tungefunga ndoa na Kelvin miezi michache tu baada ya kuvikwa pete ile lakini hilo halikutimia. Kelvin amefunga ndoa miezi miwili iliyopita na msichana aliyekuwa kipenzi cha wazazi wake.

Ingawa alishanieleza toka awali kuwa wazazi wake wamemtafutia mchumba toka kwao Bukoba lakini sikufikiria kuwa ingefikia hatua hii yakuachwa solemba na pete yangu kidoleni. Nililia sana lakini pia nilikuja tambua kuwa sitaweza kuibadili historia na kilichobaki ni kuukubali ukweli kuwa mimi Karen nimeachwa na Kelvin mwanaume niliyempenda kuliko kitu chochote hapa duniani. Sijui ni nilidanganywa, sijui nilizuzuka lakini yote kwa yote, alichonitendea Kelvin kilikuwa zaidi ya maumivu na zaidi ya aibu. Waliokuwa wakichukia kupendana kwetu walipata cha kusema, walipata cha kucheka…Kelvin kwanini ulinitendea hivi bila huruma?

Uchungu wa kuachwa na Kelvin ulinirudia mara kwa mara kunifanya niwe mnyonge mno, nilizikumbuka mara kadhaa nyakati tamu na za kusisimua tulizokuwa pamoja, ilikuwa ni kama msomaji anavyofungua ukurasa mmoja baada ya mwingine, yote yamebakia kama kumbukumbu tu. Kelvin si wangu tena!. Licha ya familia yangu kuwa nami kwa kila hali lakini bado jereha la moyo aliloniletea Kelvin lilikuwa bichi kabisa. Ni bora basi asingenivisha pete hii ambayo kila ninapoitazama natokwa na machozi, ni bora basi angeniacha awali kabla sijamuingiza moyoni mwangu!

Kelvin amenitupa, Kelvin amenisaliti na ameniacha kama kipofu katika msitu wenye kiza kinene. Uchangamfu niliokuwa nao ulitoweka kabisa na ilifikia hatua mimi Karen nikakoroga sumu na kujaribu kujiuua ili tu kuiepuka aibu na jitimai iliyonikumba kutokana na mkasa huo! Baba yangu aliyekuwa nchini Kenya kikazi alirejea haraka Tanzania mara tu alipopewa taarifa kuwa nilikuwa hospitali mahututi sijitambui. Kuponea kwangu chupu chupu kuliwafanya wazazi wangu wawe karibu zaidi na mimi ili kunifanya nisijisikie mpweke,

wakasahau kuwa raha kamili ya dunia ni mambo matatu ni yale alowahi kuyataja hayati Shaaban Robert. Kwanza afya ujaliwe kuwa nayo mtu, pili akili upewe umiliki vitu lakini zaidi ya haya upendwe na mtu!.....

ITAENDELEA....

MAMBO 10 AMBAYO PRINCESS KATE HATAWEZA TENA KUYAFANYA BAADA YA NDOA HAPO KESHO

10 Things Kate Middleton Can't Do After the Wedding

kila la kheri Catherine! 29th April, 2011 will be your day to remember!!!

Check out some of the crazy things Kate will have to wave goodbye to:

#1 Her Nickname, Kate
After the wedding, her full title will be ‘Her Royal Highness the Princess William of Wales’. She will only be known by her title, Catherine, or ma'am. No nicknames allowed with the royals!

#2 No 'Monopoly'
You won't find anyone in the House of Windsor passing GO or collecting $200 thanks to Prince Andrew, Duke of York. In 2008 he stated that the Royal Family was not allowed to play Monopoly at home "because it gets too vicious" and the game has been banned ever since.

#3 When the Queen is Finished Eating, So is Kate
As customary in Britain, when the Queen has finished eating everyone else must be prepared to lay down their forks. No one is allowed to continue eating once Queen Elizabeth II has had her last bite.

#4 No Personal Business, No Controversy
As a member of the Royal Family, Kate will not be allowed to cause any sort of controversy or scandal whatsoever. In fact, she cannot speak about any political views, social views, or any other topic that would show her personality.
I guess she won't be hanging out with LiLo anytime soon!

#5 No Work
If you are a Royal, you cannot hold any other job than being a Royal. Kate may have her degree in Art History, but she definitely does not need it anymore.

#6 No Autographs
One day Kate may have to sign some Royal documents as future counsellor of state if hubby William becomes king and that means no signing anything that is not official business. Prince Harry caught hell last year for signing the cast of a young girl who had fractured her arm.

#7 No Eating Shellfish
I hope Kate doesn't have a taste for lobster or oysters! British Royals are never served shellfish in order to avoid poisoning.

#8 No Politics
For obvious reasons, Kate will not be able to run for office.

#9 No Voting
Kate will no longer be able to vote as the Royals are not allowed for the sake of keeping things neutral between the Royals and politics.

#10 No Privacy
Ever since her relationship with Prince William began, Kate has been no stranger to the flashing lights of the paparazzi. After the wedding she will no longer be able to live her life in private. Cameras will be constantly on her with every move she makes and any time she speaks. I probably need not remind anyone the trouble that Prince William's late mother, Princess Diana, had endured with the paparazzi.

Could you live by these rules/expectations?

hahahahaaaa wanayaweza wao...hata kama ndio kuwa princess these regulations are too hard for me!!! what about you?

Tuesday, April 26, 2011

Nimerudi ....kublog kama kawa!

...wadau nilimiss blogging kwa muda sasa, ila ndio nimerudi na ninajiandaa kuwaletea vile vitu nilivyowaahidi wakati nafungasha virago...

haya safari ndio imeanza...achieni breki ili twende sambamba


Laura Pettie


Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger