Sunday, December 20, 2015

KUHUSU HADITHI YA SINDI

....Wapenzi wasomaji wangu

Nasikitika sana kuwa imebidi niikatishe kutokana na feedback kuwa ya kuvunja moyo.
Siku zote kwa Mwandishi, feedback ni kitu kinachomuhamasisha kufanya kazi kwa bidii zaidi lakini pia ni kitu kinachompa mwongozo wa kujitathmini.

kwa hadithi ya Sindi, nimesikitika sana kuwa pamoja na kazi kubwa ya kuwaburudisha. Feedback yake haikuwa ya kuvutia hata chembe. Kuandika page 15 na mtu akazisoma na kupita kimya kimya  hata comment hata kushare au hata like inaamisha hakuvutika na ulichoandika, hivyo basi badala ya kuendelea kupoteza nguvu zaidi nikaona niirudishe kabatini mpaka hapo nitakapoona kuna mabadiliko.

Kwa sasa, nimeileta NAHIYARI MAUTI kama zawadi ya kufungia mwaka wa wasomaji.
Sijui Feedback ya hii ila kwa kuwa ni zawadi sina neno..

Poleni sana kwa wale wachache mno waliojaribu kunisupport waziwazi ila ndio hivyo imenipasa kuchukua hatua hii.


Niwatakie usomaji mwema!

Laura Pettie!

Tuesday, December 1, 2015

HAPPY NEW MONTH…MAMBO 6 NINAYOKUKUMBUSHA!


Mpenzi msomaji!

Tunauanza mwezi mpya… mwezi wa mwisho wa mwaka…mwezi wa  likizo kwa wengi na mwezi unaojulikana kama mwezi wa sikukuu. Christmas na Mwaka mpya  ni wiki chache zijazo. Ni jambo la kumshukuru Mungu sana kuwa mimi na wewe mpaka dakika hii tupo hai na kwamba pamoja na changamoto zote za kidunia na kiimani bado tungali hai tukipewa nafasi nyingine ya kunyoosha njia zetu na kurekebisha hapa na pale. Tunasema Asante Mungu!

Kama ilivyo ada tunapouanza mwaka, wengi wetu huwa tuna zile New Year’s  Resolutions!.... mipango ya mwaka  mpya kwa mwaka mzima. Na sasa tunapoelekea kuumaliza mwaka tunapaswa kukaa chini na kutazama ni yapi tumeweza kuyatimiza na yapi yamekwama na kwa sababu zipi. Kwa ujumla ni wakati wa kujitathmini kwa kina na kujiandaa kumalizia yaliyokwama na pengine kupanga mengine mapya.

Yawezekana yapo tuliyoyapanga  lakini kutokana na sababu za maana na zisizo za maana kama uzembe na kukata tamaa basi tumeshindwa kuyatimiza. Si busara kuyatupa mbali na kutafuta mapya, ni vema tujitathmini ni kwa vipi mambo haya hayakutimia ili kuyajua kwa undani madhaifu yetu na kuyafanyia kazi.

Kwa kuuanza mwezi nina neno kwako msomaji! Mambo haya SITA  nimeona ni mazuri tukiyafanyia kazi wakati tunapoelekea kuumaliza mwaka.

Friday, November 27, 2015

UREMBO NA LAURA... TUZUNGUMZIE SCRUB!!


Tuzungumzie SCRUB!
Scrubbing ni njia mojawapo ya kusafisha ngozi kwa mtindo wa kusugua kwa kutumia mikono au vifaa maalumu ukiwa umepaka aina yoyote ya scrub uipendayo na inayoendana na ngozi yako.

Scrubbing ni nzuri na muhimu kwa ngozi aina zote na kwa watu wote, wanawake na wanaume! Mambo ya wanaume kuwa na ngozi mvurugo imechoka kama ngozi ya goti na michunusi hujui hata ubusu wapi it is  so 90’s!.... mwanaume usafi na kujijali bwana anhaaa! Uso unaonekana uso hata  Bae anaona raha kukuweka kwenye wallet jamani  hahahahahaaa!! Joke!

Tukija kwa wanawake, usafi wa uso sio kuung’ang’aniza uso  uwe mweupe. Nope!..kwa hiyo hiyo rangi uliyonayo ufanye uso uwe na rangi moja tulivu. No madoa, no chunusi,  no harara. Uso hata ukifuta vipodozi bado utajiamini kuwa una uso msafiiii!!

Yote haya haya hayaji bila kushughulikia uso wako!!.... Kwenye meza yako kusikosekane Scrub au wale wa mabafu ya peke yao. Scrub isikosekane kando ya sabuni. Ni kitu muhimu hiki sio cha kukosa kwa watu wanaojijali.

Kuna watu ni waoga wa kuscrub kwa kuhofia kuwa kuscrub kunachubua ngozi. Nataka nikutoe hofu kuwa,  Kuscrub hakuchubui ngozi isipokuwa aina ya scrub unayotumia ndio inayoweza kukufanya ujichubue. Ni kama mafuta au losheni, ukitaka ya kukubadilisha rangi yapo na ukitaka ya kukuacha na rangi yako yapo. Chaguo ni lako!

Zipo scrub za kisasa na scrub za kutengeneza nyumbani
Zipo Scrub za uso na scrub za mwili au vyote kwa pamoja

FAIDA ZA KUSCRUB

Sunday, November 22, 2015

LELETI KHUMALO a.k.a SARAFINA



Leleti Khumalo a.k.a SARAFINA


cover la movie ya Sarafina

Wakati nakua moja ya filamu zilizopata kuvuma utotoni mwangu, ilikuwa filamu ya SARAFINA!
Nilipoiona kwa mara ya kwanza, nilitamani kuwa kama Sarafina, nilitamani kuigiza, kuimba na kucheza kama yeye. 

Nilitamani kuwa mdada jasiri kama Sarafina!... nadhani sikuwa peke yangu katika hili,  Sarafina aliwagusa maelfu ya watoto na  vijana katika namna ya pekee na wapo watu wazima ambao filamu hii ilikuwa bora kwao na kila mtu alikuwa na sababu zake za kuipenda filamu ya Sarafina.

Leo nimemkumbuka mhusika mkuu Leleti khumalo almaarufu kama SARAFINA! Nikaamua tu kudodosa ni wapi alipo, ni nini anafanya, na kitu gani kinaendelea maishani mwake. 
Tiririka nami!

TUMJUE SARAFINA KWA KIFUPI….


Alizaliwa March 30 mwaka 1970 katika mji mdogo ujulikanao kama Kwamashu, kaskazini mwa Durban, nchini Afrika kusini. Mugizaji huyu ana asili ya Zulu. Baba yake Sarafina alifariki wakati Sarafina akiwa na miaka mitatu na kumuachia mama yake mzigo wa kuwatunza Sarafina ndugu zake watatu. 

Sunday, November 1, 2015

IJUE HALLOWEEN NI NINI NA IMETOKA WAPI....


Chimbuko la Haloween na Laura Pettie.
Kwanza niwatakie heri ya mwezi mpya wa Novemba! nimerudi kublogua kwa kudonyoa donyoa tu. Tuendelee!!

Ni sherehe inayofanyika usiku wa Oktoba 31 kila mwaka! Unapoitafuta maana halisi ya sherehe hii utakutana na maana nyingi zikiwa na mrengo tofauti tofauti.

Kubwa ni  kuwa chimbuko la Halloween ni sherehe ya kipagani iliyokuwa ikifanywa na watu waitwao wacelts miaka 2000 iliyopita. Wacelts kwa miaka ya leo wanatajwa kuwa ni watu wa Ireland, Scotland, Brittany, Wales na kadhalika kwa kuwa chimbuko la lugha ya celts iko ndani ya mataifa haya.

Saturday, September 12, 2015

UREMBO NA LAURA: .....J4 - JIPENDE, JITHAMINI, JIAMINI, JIVUNIE WEUSI WAKO!!!!


Haya jamani mpo wana kona ya urembo na Laura?

Kama umepata nafasi ya kujumuika nasi hapa, ukaisoma makala hii,  basi tuna kila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu!

Leo nataka kuongea na akina dada weusi… weusi tiiii kama mimi ambao bado hawajajikwangua au ndio wanafikiria kujikwangua. Anti wewe ni mzuri tu, …..na weusi wako huo ulionao…..unaweza kuendelea kuwa mzuri hivyo hivyo ulivyo!

Kuna watu wanadhani kuwa mweupe ndio kuwa mzuri, ndio kuwa mrembo, ndio kuwa mlimbwende! HAPANA!!.... si kweli! Hata ukiwa na weusi wako huo huo ulionao bado unaweza kuamua kujiweka katika namna ya kuvutia na ukavutia. Siku zote vile utakavyosimama mbele za watu ndivyo watu watakavyokuchukulia…. Ukijiamini watu  nao watakuamini pia!!

Nimepaka wanja na Lip Balm tu!.... 
usoni hata poda ya kawaida  haijapita

Katika pitapita zangu mitandaoni, hivi karibuni nimegundua kumekuwa na ongezeko la bidhaa za kujichubua. Tena wauzaji wakisifia kabisa kuwa unakuwa mweupee, unatakata, unakuwa na rangi f’lani amazing n.k kana kwamba kuwa mweusi ni laana au uchafu!

Huwa nasikitika sana ninapoona feedback ya bidhaa hizi kwenye picha ambapo  mtu aliyekuwa na weusi wake mzuri tu amekuwa mweupe na ndio anasifiwa kuwa amependeza na amekuwa mzuri.

Uzuri ni vile unavyowaza wewe na unavyojichukulia! Miaka  fulani nikiwa mtoto  mdogo nilikuwa na rafiki yangu aliyekuwa mweupe sana……. Namna alivyojipenda na kujisifia kila mara  kuhusu rangi yake alikaribia kunifanya niamini mimi sikuwa na rangi nzuri hata kidogo hata hivyo kila nilipojitazama niliipenda rangi yangu pia.
Ni mweusi lakini mzuri tu!!

Nilitaka kuanza kuamini weupe ni uzuri mpaka siku moja tukiwa wawili mbele ya watu fulani, mtu mmoja akasema kwa sauti…Laura usije ukajichubua baadaye baki hivyo hivyo una rangi nzuri sana! Rangi adimu! Mweusi anaweza kuwa mweupe lakini mweupe hawezi kuwa mweusi!

Kumsikia mtu akiisifia ngozi yangu kulinipa kujiamini sana, na sasa ndio nikagundua watu wengi wanasikia watu wakisifia weupe wanadhani weupe ndio uzuri  (kama mimi nilivyokuwa nasikia rafiki yangu akijisifia sana)…..kwa kuwa ni nadra kwao kusikia mtu akiwasifia kwa ngozi zao nyeusi (kama mimi nilivyosifiwa)….


Wakati naingia usichana, mama yangu aliniambia kila mara usije ukajichubua baki hivyo hivyo huoni mimi nilivyo mzuri tu (mama yangu ni mweusi pia)… kumsikia mama akisema hivi kulinijaza ujasiri zaidi na leo naweza kumwambia mtu yoyote mweusi BAKI HIVYO HIVYO ULIVYO HUONI MIMI NILIVYO MZURI TU HAHAHAHAAAAA!!
Ni mweusi Ti! na bado ni mzuri tu
na anajikubali mpaka weupe tumemkubali!

Yaani unakuta mtu kajichubua ana sugu balaaa, mwingine mashavu yameungua….mwingine mpaka ndevu zimemtoka… mkorogo umembabua miguu yaani unamtazama unamhurumia maana badala ya kuwa mrembo anakuwa kituko kwelikweli…. Mwingine mweupe kama karatasi yaani mpaka unajiuliza yote haya juu ya nini jamani?

Anyway, unawezaje kutunza  ngozi yako nyeusi na ikavutia?
MAMBO 10 YA KUZINGATIA


1. KUNYWA MAJI MENGI…. Kunywa maji kadiri uwezavyo, Uvivu wa kunywa maji unachakaza ngozi na badala ya kuitibu watu hukimbilia makemikali kuing’arisha kinguvu wakati kumbe maji ni dawa nzuri sana!.... najitahidi lita 1 hadi mbili kila siku! ukiona hayana ladha weka vionjo kama limao kwa mbali au ndimu.

2. Safisha ngozi yako kwa vitu visivyo na kemikali, pendelea vitu natural hata kama ni vya kizungu ila vyenye ingredients natural…. Mfano usoni napenda sabuni ya Liwa, zile natural kabisa au zile zinazofungwa kwenye cover ya kahawia zimeandikwa sandwool soap bee and flower!

3. Tumia vipodozi vinavyoendana na ngozi yako…. Poda, foundation etc viwe vya ngozi yako vitakupa muonekano mzuri sana.

4. Kula chakula bora hususani matunda na mbogamboga usisubiri uandikiwe na daktari

Thursday, September 3, 2015

UREMBO NA LAURA:......LIP SCRUB YA SUKARI NA VASELINE!



Jamani mpooooo!!
Leo tunaongelea utunzaji wa lips zetu ukizingatia kipindi cha baridi ndio hiki.... Haipendezi mwanamke kuwa na lips kaavu, zina mipasuko,  sio soft yaani not smooth not kissable hahahahahaa!

Yaani kuna watu asipopata lipshine dakika tu hutotamani lips zake kwa namna zilizopauka pasuka
au unakuta mdomo una zagamba anafanya kuzing'ata kwa meno, ukiuliza ooh baridi oooh upepo...ooh leo sijapaka lipshine...sasa ndugu yangu hata ukitaka kumkiss babe utakuwa unawahi lipshine kwanza?

Hebu uko!...

Kama unavyotunza uso wako, Lips pia zina matunzo yake tena mepesiiii
Hata dakika tano humalizi!! unabaki na lipsi flani laini ukiongeza na lipshine yako mashallaaaaah! 
Uhitaji nguvu nyingi kuonekana mrembo!
Maaaana

Lips ni kiungo kingine kinachoongeza urembo usoni mwa mwanamke yeyote
Hapa nakuletea namna ya kuscrub lips zako kwa sukari na mafuta ya Vaseline


Lips zangu hizo bila chochote.... na kibaridi hiki na upepo  sijapaka chochooooote kwa masaa kadhaa
ndio hivyo unaona zimeweka michirizi kwa mbaaaali.

FAIDA ZA KUSCRUB LIPS

Thursday, August 27, 2015

UREMBO NA LAURA:.... PRE - POO USHUHUDA WANGU BINAFSI!!


Pre - Poo inasimama badala ya Pre-shampoo
Hii kitu unafanya kabla ya kuosha nywele zako.

Sitaki kuongea maneno matupu ila nataka nikupe mfano mwenyewe kwa kutumia picha.
Ni treatment inayofaa zaidi watu wenye nywele za asili ila hata wenye dawa wanaweza fanya.

inakupa nywele safiiii... hakuna cha mba wala harara kichwani.... inazuia kukatika kwa nywele yaani ile ukichana mpaka unaogopa kutazama chanuo hahahaaa

Inakuza na kujaza Nywele!

 cheki hii picha hapa chini

Friday, July 24, 2015

UREMBO NA LAURA:.....MATUMIZI YA NAPKINS MEZANI..

NAPKIN

 Baada ya kuwa kimya muda mrefu kwenye kona hii sasa nimerejea! Twende kazi

Wengi wetu nadhani tunajua ni kitu gani. Kwa maelezo ya juu juu ni karatasi au kitambaa kinachokaa mezani kwa ajili ya kufutia pembe za  mdomo na vidole wakati wa kula au baada ya kumaliza kula. 

Kinaweza kuwa kitambaa cha material yoyote ile ila cotton  inapendeza zaidi kwa kuwa ni rahisi kuikunja kwa staili mbalimbali za kupendeza kuliko kitambaa laini.

Kitambaa hiki unaweza ukakikuta mezani hotelini, nyumbani kwa mtu au kwenye sherehe.  Hata wewe unaweza kuandaa msosi wako mzuri nyumbani na kualika wageni wako  kisha ukakitumia kuongeza umaridadi mezani pako. Si unakumbuka charger plates!!

Kuwa Classic ndio habari ya mjini my dear!.... mumeo kaalika watu wa kazini kwake, hebu fanya kitu cha kuwafanya wakitoka hapo waone mwenzao ana mtu anayependa vitu vizuri. Simple table setting ya uhakika!! Hakuna kuomba omba tishu heheheeee!

Zipo staili mbali mbali za namna ya kuiweka napkin mezani. Kuna wengine hufunga kama kipepeo, kuna wengine huikunja pembe tatu na kuiweka juu ya sahani yaani staili za kuifunga ni nyingi sana,  ni wewe tu na uamuzi wako.

NAPKIN HUKAA WAPI?

Kama ni mlo wa kawaida na si ule rasmi wa shughuli maalumu Napkin inakaa popote kulingana na nafasi kwenye meza yako. Ila kwenye shughuli kubwa utaikuta napkin mezani juu ya sahani.

UMEIKUTA NAPKIN KWENYE MTOKO WAKO…UFANYEJE?

Umealikwa mahali mwenzangu, sehemu yenye mchanganyiko wa watu. Nadhani hutotaka kuonekana mshamba saaana au kushindwa kujua ustaarabu wa matumizi ya Napkins au sio? Hahahahaaaa!!

1. Ukifika mezani usikimbilie kuchukua napkin haraka haraka…ngoja watu wawili watatu wakae…na kama mko wawili ngoja mwenzio naye akae!

2. Chukua napkin yako iweke mapajani. Napkin inakaa mapajani kamwe usiweke napkin shingoni. That is not a bib jamani. Bib ni kile kidude tunafungiaga watoto shingoni wakati wa kula, kwa Kiswahili sijui kinaitwaje. Bibs are for babies not adults!! Labda kama unafanya comedy.


3. Ukishaiweka mapajani anza kupata mlo wako kama kawaida. Unapofuta midomo ikunje upate ncha hivi na kufuta kando ya midomo yako. Usitumie napkins kufuta lips za midomo yako. Hahahahahaa na utafutaje mdomo mzima mwenzangu kwani unakulaje kwa mfano?


Saturday, July 18, 2015

10 MINUTES WITH GOD!....AMETENDA MAAJABU BY FANUEL SEDEKIA



I'M IN LOVE WITH THIS SONG!

Nimejikuta nausikiliza mara mbili tatu nne tano.... and i was like mmmh kwanini nisishee na nyie 
Ninapofanya shughuli zangu mara nyingi tu huwa nasikiliza muziki
na nyimbo za dini ni sehemu ya muziki ninaosikiliza sana!

R.I.P Fanuel .... 

Friday, July 17, 2015

EID MUBARAK


 KWA WASOMAJI WANGU WOOOOOTE POPOTE MLIPO DUNIANI!!

NAWAPENDA!!

Thursday, April 9, 2015

TBT:.... YA JEAN BY MADILU SYSTEM na lyrics zake



Moja ya nyimbo za kilingala nilizopata kuzipenda saaana
Wimbo huu unanikumbusha safari ya Mwanza to Dar via Kenya kwa basi la Scandinavia
yaani nahisi kulengwa na machozi kwa kweli
Nakumbuka mbaali sana.... mengi mno!
Kweli maisha safari!!

Manu Lima, ko tumbola ngai te.
Ah! Elekaka na yango eh.
Le Grand Ninja.

Ah ngai oh, ngai oh, ngai oh.
Ah ngai og, ngai oh, mawa.

Ah ngai oh, ngai oh, ngai oh.
Ah ngai og, ngai oh, mawa.

Ya Jean aboyi nga tina te oh.
Na sengi ye palado.
Nazangi soutient na vie na ngai oh.
Po a bundela ngai.

Mobali aboyi nga na se ya ndoto.
Aloti na zweli ye mbanda.
Na tongo alamuki au lieu atuna nga.
Akamati decision.

Instrumental
An ngai oh, ngai oh, ngai oh.
Ah ngai og, ngai oh, mawa.

An ngai oh, ngai oh, ngai oh.
Ah ngai og, ngai oh, mawa.

Ya Jean aboyi nga tina te oh.
Na sengi ye palado.

Friday, March 20, 2015

UREMBO NA LAURA:...JINSI YA KUCHORA SIMPLE EYELINER!!

Make up by Laura! 
and the eyeliner too heheheee!


Nimejaribu nilivyoweza.....

Mpo wadau?!

Natumaini mu wazima na mambo yanakwenda vizuri na palipo na mushkeli baaasi Mungu aingilie kati!

Haya leo tuna kitu kinaitwa  Eyeliner…  kusema ukweli miaka miwili nyuma au niseme mwaka mmoja nyuma  ungeniuliza masuala ya eyeliner ningekukodolea macho tu kama si kugoogle ama kutafuta dictionary!... mambo ya kujipamba yalikuwa mbali sana na mimi yaani mbali mnoooo! Urembo pekee ulikuwa kushonea weaving na kutinda nyusi baaasi…make up  sijui mazagazaga gani nilikuwa naona vitu viguuuumu sana…


 Lakini sasa  hivi karibuni tu katika kutafuta hobby mpya nikajikuta nakuwa interested  na masuala ya urembo wa makeup  kwa ujumla… si kwa kutaka kuwa mpambaji basi tu nimejitafutia hobby mpya na ninaifurahia kila ninapopata nafasi na kuifanyia majaribio!


It feels good mnooo unapojaribu kitu kipya na ukaona matokeo…yawe mazuri kidogo au mazuri sana…cha muhimu umejaribu, maisha mafupi kuishi kwa mazoea na kukariri routines!
Sometimes jitazame na ujitafute muonekano mpya…  

YOU ONLY LIVE ONCE DEAR!!!

Eyeliner ni hako kamchoro kwenye macho
ni aina fulani ya urembo inayofanya hata uso wako uonekane tofauti
Kuna dizaini tofauti tofauti za uchoraji macho.

Yaani zipo nyiiingi mno!
Mimi kwa vile si mpambaji na ni mwanafunzi nikachagua simple style tu

Ili kuchora eyeline  unahitaji Eyeliner gel au  eyeliner pencil au eyeliner marker pen


hizi hapa ni aina mbili Eyeliner Marker pen na Eyeliner Pencil

Ninayotumia mimi ni hii hapa!!

Thursday, March 12, 2015

11TH MARCH WAS MY BIRTHDAY!!


 Jana ilikuwa siku yangu ya kuzaliwa
kuna mengi ya kufurahisha yakatokea
lakini...

kubwa lililofanya nitafakari ni ajali iliyotokea Mufindi!
ningeweza kuwa mimi lakini Mungu bado ana mpango na mimi.

Nashukuru ndugu jamaa na marafiki ikiwemo familia yangu kwa kila kitu
Nimeongeza mwaka mmoja... na Birthday ya mwaka huu nimeifurahia kuliko birthday zooote!
sababu naisherehekea nikiwa na status moja mpya maishani mwangu!

Namshukuru Mungu, na natumaini mwaka niliouanza utakuwa mwema kama ulioisha.
Na nitaendelea kuwaburudisha kama kawa!

Asanteni sana!

Saturday, March 7, 2015

HAPPY WOMEN'S DAY



HAPPY WOMEN’S DAY 2015!!
KWAKO…

1. Wewe mwanamke uliyejikubali ulivyo! hii iende kwa wanawake wote weusi tiii kama mimi Waliosema no to mkorogo just to impress somebody! Maana kujichubua sasa ni janga la kitaifa…..Wanawake wenye figa nene za afya sio kupitiliza; pamoja na kudhihakiwa na unene wetu mradi tuna afya njema TUMEJIKUBALI!!

2. Wewe mwanamke unayejithamini! Hii iende kwa wanawake wote waliokataa  unyanyasaji wa aina yoyote toka popote kwasababu zozote!... Mwanaume ni kiumbe kama wewe, anazaliwa na kufa kama wewe, anapenda na kuchoka kama wewe. Ukipendwa pendeka ukichokwa nyanyuka tokaaa!! huko ndiko KUJITHAMINI!! Kung’ang’ania mtu it is so 90’s women! learn to move on shaaa! Uvumilivu wa manyanyaso hauna tuzo dada si peponi si motoni!!

3. Wewe mwanamke unayejituma kutafuta kipato chako!... Hii iende kwa wanawake wote ambao hawamuabudu mwanaume kwa shilingi yake! Hawadhalilishi utu wao kwa pesa! Wanapigana hata kwa kuuza maji ya viroba ili kujisitiri! ….kuhudumiwa ni haki yako….narudia ni haki yako mwaya kama uhudumiwi weka viulizo, mkato, alama ya kushangaa na mwisho fanya magazijuto hicho ni kimeo kubali kataa!!.... ila isikufanye ubweteke kukinga mkono kila siku, kila saa, kila wiki…wanaume wenyewe hawa wa siku hizi hawatabiriki awe mume wa ndoa au mpenzi wanafanana kama ugali wa jana tofauti yao majina! JITUME!!

4. Wewe mwanamke unayejitambua!... matusi si lugha yako, chuki za chini chini si sifa yako, wivu wa kijinga si hulka yako na unyonge si silika yako. Chukua dole gumba! Ama sivyo unahitaji mabadiliko haraka sana. Mwanamke anayejitambua hatukani anatoa facts, hachukii anakupa za uso, ana wivu wa maendeleo sio kwa kuumiza roho  na si mnyonge abadani!!

5. Mwisho kwa Wanawake wote wanaotambua wajibu wao….Mbele za Mungu, kwa waume, kwa wapenzi, kwa mchumba, kwa mchepuko (kwani uongo?) kwa watoto, kwa majirani na kwa  jamii na jamii yenyewe hususani kupendana, kuinuana na kuheshimiana na wanawake wenzao!!...ukiona mwanamke anachekelea madhila ya mwanamke mwenzake ujue HAJITAMBUI na HATAMBUI WAJIBU WAKE!!... kama una wifi humpendi, sijui ma mkwe  sijui nani huwapendi ndugu hii inakuhusu pia!

HAPPY WOMEN’S DAY WANAWAKE WENZANGU!!

BILA SISI DUNIA INGEBOA KUSEMA UKWELI…

Friday, March 6, 2015

UREMBO NA LAURA:... JINSI YA KUPAKA WANJA MNENE a.k.a WANJA WA LULU


Asalam Aleykum wasomaji wangu!

Leo nakuletea tena lile somo la kupaka wanja mnene a.k.a wanja wa Lulu!
Tuelewane kwanza....huu wanja waaaala hauchagui, uwe na nyusi msitu uwe na nyusi za kuokoteza, dada kwa wanja huu wote mtafanana na kupendeza! wanja huu haujawahi kumchukiza mtu!

Pili, uwe na wanja wa pencil au wanja wa poda wote mnaweza kuuchora huu wanja. Sasa wenzangu na mimi mnaoona ubahili wa kununua wanja wa elfu 20 ule poda usijisikie unyonge. Huu niliojipaka hapo pichani ni wa elfu mbili tu hahahhaaa shame on me!

Tatu, Wanja huu hautaki mkata tamaa kwenye kujifunza...weka nia tu kuwa mara mbili tatu nitaweza maana kuna akina dada mnajidekeza bwana aah mi siwezi... aah mi siwezi nitakufuata uko na  bakora nikucharaze viboko mpaka uweze...usinitanie! hahahahaaaa

Anyway, hebu tuanze somo letu....
Watu wengi huuliza unatumia vifaa gani kuuchora?.... hapa nitakuwekea vifaa ambavyo mara nyingi hutumika haswa na sisi tunaojitengeneza wenyewe majumbani.... wale wa saluni uko kuna brands za vifaa na vipodozi... ila simple tu ya kama yangu hiyo aaah ndugu yangu vifaa vya malaki havinihusu!

TAFADHALI SOMA MAELEZO VIZURI USIPOELEWA RUDIA!! au  ULIZA!...ULIZA!! ...ULIZA!!
A. MAHITAJI

1. UNAHITAJI WANJA
Wanja wa pencil uwe Black au Brown

hapa nakushauri nunua wanja mkavu uwe mgumu kidogo


Thursday, January 22, 2015

UREMBO NA LAURA... PEDICURE AT HOME !!


Kama nilivyoahidi kuleta njia ya namna ya kusafisha miguu nyumbani na ndio hii hapa nakuletea leo
Wapo wanaokwenda saluni kuosha miguu na wapo ambao kwa namna moja ama nyingine wanashindwa kwenda kupanga foleni saluni kusubiri kuosha miguu.

Leo nakuletea njia ya kuosha miguu nyumbani mara mbili kwa mwezi, kwamba unaosha wiki hii unasubiri wiki nyingine inapita... kisha unaosha tena kwa staili hii.

Hii si kwa wanawake tu, hata wanaume wanaweza kufanyiwa haya na wenzi wao kama sehemu ya kuimarisha mahusiano yao. Usione tabu kumfanyia mwenzio pedicure home mbona sio kazi sana!

Sasa hebu tuangalie nini cha kufanya

1. ONDOA RANGI KWENYE KUCHA ZAKO...



Nail polish remover na pamba vinahusika hapa. ondoa rangi yote uache kucha chako zikiwa safi. Kama unazikata kucha zako zikate na ulinganishe kulingana na urefu unaotaka. ondoa vinyama nyama kando kando ya kucha kwa kifaa maalumu nadhani unavijua au wembe safi na mpya...toa uchafu chini ya kucha na kama kucha zimefubaa sana zisugue na ule msasa

Wednesday, January 21, 2015

MEKONI.... MAPISHI YA SOSEJI NA MAYAI




Huu ni mlo wa chap chap...

MAHITAJI
Soseji idadi unayotaka
mayai 2/3
nyanya 1
kitunguu 1
majani ya mint kiasi
pilipili manga
hoho nusu
chumvi

JINSI YA KUPIKA
1. Pasua mayai yako kwenye bakuli safi yachanganye

2. kwenye hilo hilo bakuli  kata kata soseji zako saizi unayopenda

3. katia hoho kidogo

4. katia vitunguu vyembamba

5. katia nyanya ziepuke mbegu za nyanya

6. nyunyuzia pilipili manga na chumvi

7. dondoshe vijani vichache vya mint

8. vichanganye kwa pamoja

9. weka kikaangio jikoni na mafuta kiasi

10.  mimina mchanganyiko wako

11. ukaushe vizuuuri kama unavyokausha yai

MLO WAKO TAYARI!!

UKIPENDA 
unaweza ukakata kipande ukakiweka katikati ya vipande viwili vya mkate
sukumia na chai ya rangi ya viungo, juisi, chai ya maziwa, soda...etc


TUONANE JUMA LIJALO!!




Thursday, January 15, 2015

UREMBO NA LAURA....USAFI WA MWILI WA MWANAMKE....




Kama ilivyokuwa mwaka jana kila alhamisi tuna makala ya urembo hapa… na kabla ya yote hebu tumshukuru Mungu kwa wema wake kwanza kwa kutuumba wanawake na kisha akatuweka hai mpaka sasa halafu akatupa nafasi ya kusoma hata hii makala unayoisoma.

Nakuita mwanamke!...nakuita binti…nakuita hapa tuelezane machache kuhusu usafi wetu kwa ujumla. Wanasema usafi ni hulka ya mtu ni kweli lakini ukiamua kuwa msafi hushindwi…na kwanini ushindwe! Nitagusia mambo 15 ambayo kuhusu usafi wa miili yetu maana urembo na usafi ni kama kobe na jumba lake haviachani!

Hebu tuanze…

1. USAFI WA NYWELE

Utatia aibu kama utasukia weaving lako wiki mbili hadi nne na usiwe umepitisha maji kichwani… haijalishi uko wapi ila kukaa na nywele wiki nne pasi kuosha ni UCHAFU bibi!!... toa nywele bandia hizo…au fumua mzigo wa yebo yebo huo uoshe kichwa kama huwezi kuosha zikiwa kichwani…watu wanaweza wasikwambie ukweli ila pembeni ukapewa cheo cha yule dada mchafu maana huwa zinanuuuuka acha!!


Wednesday, January 14, 2015

HEBU PITA ZAWADI SALON... HAPO KINONDONI MANYANYA


Haya wenzangu wapenda mambo mazuri mazuri kwa gharama nafuu kabisaaaa na unapata huduma stahiki na hela yako nakuletea hii sehemu ambayo ukikosa kwenda na ukalalamika urembo gharama basi hujitendei haki mwenzangu.

ZAWADI SALON...ipo kinondoni manyanya barabarani kabisaaaa yaani ukishuka kituoni uhitaji bodaboda wala bajaji na kama una usafiri wako basi ni kutoka nje ya njia kuu na utakuwa umefika...unaona raha hiyoooo!!

Kama unatokea Moroko basi unamwambia konda akushusha kituo cha manyanya....unavuka barabara utaona yadi ya magari mwisho wa ukuta wa yadi utaona frame zimepangana....fremu ya pili ndio ilipo Zawadi Salon!

Kama unatokea kariakoo badi upande huo huo ndio ilipo Saluni....


KWANINI UCHAGUE ZAWADI SALON....
1. Mmiliki ndio mhudumu wako akisaidiana na mtu mwingine hivyo tegemea huduma safi kabisaaa maana bosi ndio anakuhudumia.

2. Dada ni mkarimu mnoooo...yaani anavyokupokea utajisikia huru sana...sio unaingia saluni wahudumu wanakunyali na senti zako kama wanakuhudumia bure!...na biashara huria hii ya nini manyanyaso kwa hela yako!

3. Bei zako ni affordable mnoooo kulingana na huduma zake.... rasta za elfu 25 au 40 unajiangalia unatamani kumuongezea pesa!

4. Ukimpigia simu kuuliza kitu au kuweka miadi unampata haraka sana na atakujibu vizuri...hana nyodo dada wa watu.... yupo kwa ajili yako.... tena ukimtafuta mwambie ulipotoa contact zake ni  kwenye blog ya Laura Pettie....na punguzo utapata!

5. Rasta, weaving zipo hapo hapo saluni kwa bei nafuu mnoooo.... maana anajua anahudumia pia watu wa kipato cha kati....unaenda na pesa zako unachagua rasta zako au weaving... unalipia unasukwa!

6. Ana mkono mwepesi sana!...yeye na mhudumu wake.... unakaa kitini hata sugu za  makalio hazijaanza kuuma mwenzio yuko robo tatu ya kichwa!

7. Yupo wazi siku zote.... unaweza ukapigia ukaongea naye kuhusu kuweka miadi ya kusuka kama utamuhitaji akufuate basi utaongezea gharama kidogo.... na anakuhudumia!!

Mwisho!..... anapamba MAHARUSI... anapamba hata watu wenye mitoko ya hapa na pale.... inahusu kwenda harusini na uso ule ule unaokwenda nao kazini...mmmmmh! kwa ubahili gani sasa unashindwa kupendeza siku moja moja kwa maisha haya haya bwanaaaa!...bei zake zinashikika kabisa kama mimi naziweza wewe utashindwa nini jamani hahahahaaa... hebu tumuunge mwanamke mwenzetu!!


Tena unakuwa huru kumwambia hapa hivi hapa vile na anakusikiliza vizuri... unatoka saluni roho kwatuuuuu na umependeza!!


BAADHI YA KAZI ZAKE NDIO HIZI......

HEBU ZICHEKI....!


MEKONI....UGALI, DAGAA MCHELE ZA NAZI KWA TEMBELE



Kama ilivyo ada…leo tena tuko mekoni. Na wala tusipoteze muda.
Mlo wetu wa leo ni UGALI, DAGAA  MCHELE  za nazi na TEMBELE. Hapo penye ugali unaweza ukaweka wali au hata ndizi za kupika wewe tu upendacho.

TUANDAE UGALI…
Japo najua wengi tunajua kuusonga ugali ila huwezi jua labda wapo wasiojua kuusonga ugali. Acha tuelekezane tu.

-          Bandika sufuria lako la maji ya ugali yachemke

-          Koroga unga mimina kwenye maji…usikoroge mwepesi sana wala mzito sana

-          Sasa uji uchemke, wengine stage hii wanaisha tu basi para para nguna hilo mezani
-          Uji ukichemka vizuri hata ugali utatoka poa

-          Anza kusonga sasa polepole ukiongeza unga… kama sio mjita au msukuma (hahahahaaaa samahani lakini) lazima utataka ugali mwepesi hivyo usimimine unga mwiiingi utashaa!

-          Songa ugali wako mpaka uone unga umepotea na ugali umeshikamana au nati nati sana
-          Usiwaishe kutoa jamani…songa hata dakika tano hivi huku ukiuacha acha jikoni uive. Aibu ukitenga ugali mbichi mezani au ukute unakula mbichi kila siku ila hujui tu
-          Mwisho ipua na utenge kwenye chombo chako.

-          Wengine hunyunyuzia chumvi wakati wa kukoroga uji wa ugali ili kuupa ladha kidogo… kama nakuona ulivyoshangaa hahahahaa
-          Ugali tayari


TUANDAE DAGAA MCHELE

Mara nyingi hawa huwa tunawanunu wameshakaangwa
Wanauzwa kwa mafungu, ni dagaa fulani wana nyama nyama na ukubwa wake unazidi dagaa wale wa mwanza.... 
sehemu wanazouza samaki wa kukaanga mara nyingi utakuta pia wanauza hawa dagaa mchele.

MAHITAJI
- Kitunguu
- Kitunguu swaumu
- karoti
-nyanya za kawaida
-Nyanya ya kopo/ pakti
- binzari masala/ royco/ curry powder/ Onga  au chochote unachotumia
- pilipili manga
- Iliki
- Nazi
-Chumvi
- Hoho...hii ni ukipenda
na dagaa zako

Friday, January 9, 2015

DARASA...TUJIFUNZE KIFARANSA - 2

Ijumaa nyingine tena...tunarudi darasani tena au sio!

Kwanza Bonjour!.... itikia......
Comment ca va?.... itikia....

Haahahaaa i hope hujasahau kitu Lol...
haya leo tujifunze namba....
kama somo lolote lile, kifaransa nacho kinahitaji wepesi wa kukariri...huwezi jua lugha bila kukariri baadhi ya mambo. kuna baadhi ya watu hujiaminisha kuwa ni wazee sasa au watu wazima na hakuna haja ya kujifunza kitu kipya.... hii si sahihi hata kidogo!

una kila haki ya kujua mambo mapya na ukayafurahia bila kujali umri wako. umri usikuzuie kuichangamsha akili yako jamani na kukuza upeo wako... utajisikiaje anakuja mtu anayeongea kifaransa ofisini kwako angalau unaweza kumwambia Bonjour Monsieur naye akajibu bonjour...ukamjulia hali akasema ca va bien!.... urafiki unaanzia hapo na kuna maksi unajiongezea kwa kujua salamu za mataifa mbalimbali... usibaki nyuma nyuma saaana LOL!


kukurahisishia kazi
Hili hapa chini ni jedwali la namba na namba zinavyoandikwa na kutamkwa
0
zéro
[zay-ro]
1
un
[uh]
2
deux
[duhr]
3
trois
[twa]
4
quatre
[katr]
5
cinq
[sank]
6
six
[sees]
7
sept
[set]
8
huit
[weet]
9
neuf
[nurf]
10
dix
[dees]
11
onze
[onz]
12
douze
[dooz]
13
treize
[trez]
14
quatorze
[katorz]
15
quinze
[kanz]
16
seize
[sez]
17
dix-sept
[dee-set]
18
dix-huit
[dees-weet]
19
dix-neuf
[dees-nurf]
20
vingt
[van]
21
vingt et un
[vant-ay-uh]
22
vingt-deux
[van-duhr]
23
vingt-trois
[van-twa]
24
vingt-quatre
[van-katr]
25
vingt-cinq
[van-sank]
26
vingt-six
[van-sees]
27
vingt-sept
[van-set]
28
vingt-huit
[van-weet]
29
vingt-neuf
[van-nurf]
30
trente
[tront]
31
Trente et un
[tront ay-uh]
32
Trente-deux
[tront-durh)
33
Trente-trois
[tront-twa)
34
Trente-quatre
[tront-katr)
35
Trente-cinq
[tront-sank)
36
Trente-six
[tront-sees)
37
Trente-sept
[tront-set)
38
Trente-huit
[tront-weet)
39
Trente-neuf
[tront-nurf)
40
quarante
[karont]
41
quarante et un
[karont-ay-uh]
42
quarante-deux
[karont-deux]
43
quarante-trois
[karont-twa]
44
quarante-quatre
[karont-katr]
45
quarante-cinq
[karont-sank]
46
quarante-six
[karont-sees]
47
quarante-sept
[karont-set]
48
quarante-huit
[karont-weet]
49
quarante-neuf
[karont-nurf]
50
cinquante
[sank-ont]
51
cinquante et un
[sank-ont-ay-uh]
52
cinquante-deux
[sank-ont-deux]
53
cinquante-trois
[sank-ont-twa]
54
cinquante-quatre
[sank-ont-katr]
55
cinquante-cinq
[sank-ont-sank]
56
cinquante-six
[sank-ont-sees]
57
cinquante-sept
[sank-ont-set]
58
cinquante-huit
[sank-ont-weet]
59
cinquante-neuf
[sank-ont-nurf]
60
soixante
[swa-sont]
61
soixante et un
[swa-sont-ay-un]
62
soixante-deux
[swa-sont-dur]
63
soixante-trois
[swa-sont-twa]
64
soixante-quatre
[swa-sont-katr]
65
soixante-cinq
[swa-sont-sank]
66
soixante-six
[swa-sont-sees]
67
soixante-sept
[swa-sont-set]
68
soixante-huit
[swa-sont-weet]
69
soixante-neuf
[swa-sont-nurf]
70
soixante-dix
[swa-sont-dees]
71
soixante-et-onze
[swa-sont-ay-onz]
72
soixante-douze
[swa-sont-dooz]
73
soixante-treize
[swa-sont-trez]
74
soixante-quatorze
[swa-sont-katorz]
75
soixante-quinze
[swa-sont-kanz]
76
soixante-seize
[swa-sont-sez]
77
soixante-dix-sept
[swa-sont-dee-set]
78
soixante-dix-huit
[swa-sont-dees-weet]
79
soixante-dix-neuf
[swa-sont-dees-nurf]
80
quatre-vingts
[kat-ra-van]
81
quatre-vingt-un
[kat-ra-vant-uh]
82
quatre-vingt-deux
[kat-ra-van-dur]
83
quatre-vingt-trois
[kat-ra-van-twa]
84
quatre-vingt-quatre
[kat-ra-van-katr]
85
quatre-vingt-cinq
[kat-ra-van-sank]
86
quatre-vingt-six
[kat-ra-van-sees]
87
quatre-vingt-sept
[kat-ra-van-set]
88
quatre-vingt-huit
[kat-ra-van-weet]
89
quatre-vingt-neuf
[kat-ra-van-nurf]
90
quatre-vingt-dix
[kat-ra-van-dees]
91
quatre-vingt-onze
[kat-ra-van-onz]
92
quatre-vingt-douze
[kat-ra-van-dooz]
93
quatre-vingt-treize
[kat-ra-van- trez]
94
quatre-vingt-quatorze
[kat-ra-van-katorz]
95
quatre-vingt-quinze
[kat-ra-van- kanz]
96
quatre-vingt-seize
[kat-ra-van- sez]
97
quatre-vingt-dix-sept
[kat-ra-van- dee-set]
98
quatre-vingt-dix-huit
[kat-ra-van- dees-weet]
99
quatre-vingt-dix-neuf
[kat-ra-van- dees-nurf]
100
cent
[son]

1000 - Mille
10,000 - Dix Mille
100,000 - Cent Mille
1,000,000 - Un Million
1,000,000,000 - Un Milliard




Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger