Saturday, July 27, 2013

10 MINUTES WITH GOD:.... SHUKA BWANA BY ABIUDI MISHOLI


.......Yawezekana mpendwa rafiki mihangaiko ya kidunia imekushika kiasi kwamba kile kitabu kitakatifu kiitwacho biblia… umekisahau…kimejaa vumbi… unakiona lakini uvivu wa kukifungua unakupata…. Yawezekana lipo jambo unalomlilia Mungu akutimizie Lakini…. siku, wiki mwezi, miaka inakatika na huoni lolote linalotokea… unamatazama Mungu kwa wasiwasi…. unajiuliza umekosa nini?...kwanini wewe… kwanini hili…kwanini sasa… na hupati majibu. Mungu anaonekana yuko mbali sana na wewe. 


katika kitabu cha ZABURI 145: 17 – 19….. anasema “Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote…..Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote…….Bwana yu karibu na wote wamwitao…..wote wamuitao kwa uaminifu…. atafanyia wamchao matakwa yao….Naye atasikia kilio chao na kuwaokoa” MPENDWA RAFIKI MUITE MUNGU KWA UAMINIFU….KWA UVUMILIVU NAYE ATAKUITIKIA…MUNGU HACHELEWI ….YUPO KWA AJILI YAKO KWA AJILI YANGU KWA AJILI YETU SOTE…. BARIKIWA NA WIMBO HUU…. NIMEKUANDIKIA MAISHA YAKE HAPO CHINI

Nakuhitaji bwana… Nakuhitaji Jehova… wewe ndiwe msaada wangu…. niende wapi
ila kwako…tazama shida zangu…tazama kwanza…Bwana nitazame… sina wa kunisaidia…ila ni wewe… hima bwana shuka…uniokoe


(Shuka bwana shuka…. shuka bwana
Sikuitii hukumu ila shuka
Mbona uko mbali….shuka bwana…bwana mi naomba bwana shuka) X2
(Unisikie bwana
Kulia kwangu…..unitazame baba na macho yako
Unyooshe mkono wako na uniguse…hima bwana shuka uniokoe) X2

Hima bwana shuka uniokoe….  hima bwna shuka nitetee…. hima bwnaa shuka unikomboe …Haleluya!
Ni wewe msaada pekee…uliyebaki…sina cha kutumaini ila wewe bwana… tabu zangu ni nyingi… shida zangu ni nyingi…. nani atakaye nitoa?... nani atakayenisaidia?... sioni!
Ila ni wewe Yehova….bwana shuka…shuka niokoe…. shuka nitazame… shuka niguse… Nionee huruma… ni wewe nakutumainia…Haleluya!

Ona majaribu…yananisonga
Yanijia kwa kasi …kama mabomu
Akili zaniruka…. niyafikiripo
Mbona upo kimya…niokoee
Niende wapi mimi…. kote nasimangwa
Mungu nakutegemea… na ujue
Lakini….hata ukinyamaza… kukupiga siwezi
Maana Mungu ni mkuu….mnooo
(RUDIA PALE UNISIKIE…..)

Nawe pia najua una tabu…Najua una mateso… najua una shida….lakini jipe moyo
Mungu yu pamoja nawe….Ayubu alisema….najua mtetezi wangu yu hai…Hatimaye atasimama juu ya nchi…atanitetea
Hata wewe atakutetea…. Jifunge kiume…endelea mbele… na iko siku… kama sio leo, kesho…. lakini Mungu atakufuta machozi

MUNGU AKUBARIKI SANA!



No comments:

Post a Comment



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger