Thursday, October 30, 2014

UREMBO NA LAURA:....MAFUTA YA MCHAICHAI (LEMONGRASS OIL)

Ya kwangu hayoooo mkononi

yenye majina ya kizungu hayoooo!!...na mmea wake huo hapo nyuma

Nadhani niihamishie alhamisi hii makala ya Urembo na Laura. Maana naona Jumatano huwa inakuwa na mambo mengi mno.

Yote kwa yote, natumaini kwa uwezo na kudra za mwenyezi  Mungu mu wazima. Tuendelee sasa!

Leo nakuletea Mafuta ya mchaichai. Sidhani kama huufahamu huu mmea wa mchaichai. Wengi wetu tunautumia kuungia chai. Na Majani yake si mageni kwetu. Ni mmea wenye harufu na ladha nzuri sana. Wakati mwingine hutumika kama kiungo kwenye chakula na kwenye mapishi, tumia kumarinate kuku kabla hujamchoma au kumkaanga utapenda na roho yako!

Sasa haya ndio  mafuta yake pia. Ni mafuta mazuri mno na kwa mtu yoyote anayejipenda, haya mafuta ni wajibu kuwa nayo. Ni mafuta yenye matumizi mengi kwa wakati mmoja

1. KUKUZA NYWELE ZILIZOKATIKA

Thursday, October 23, 2014

UREMBO NA LAURA:.... JINSI YA KUPAKA WANJA WA KISASA!!


Nyusi ni sehemu ya urembo wa mwanamke... namna unavyozitengeneza nyusi zako unaweza pata muonekano wa kuvutia au ukawa kichekesho pia. Maana unakutana na mtu nyusi zimekaa rafu mpaka basi au ndio vile zimechongwa kipashkuna mno hahahaha... ama ndio uso unakuwa kama anazomea hivi...mradi hekaheka tu!

Unaweza kumpa pole mtu ukijua ana huzuni kumbe walaaa nyusi zimekupa wrong infomesheni!!

Sasa kabla hatujapakana wanja hebu tuone vitu muhimu vya kuwana navyo au kufanya. Hii ni kwa hohehahe wenzangu wanaotaka kupendeza ila ndio wanaona kuna vitu havikamatiki!... unaweza punguza bajeti ya mboga nyumbani hivi hivi...lakini sio sababu usiwe mrembo jamani. tubanane tu humu humu!

1. Tinda nyusi zako unavyotaka wewe.... binafsi sijui ni mazoea au ni nini...huwa nazichana nyusi kurudi chini... kiasi kwamba sasa hivi zinaota kueleke chini LOL!...so nazitrim mwenyewe kwa chini... vyovyote utakavyotinda au kutindwa mradi ziwe kwenye shepu fulani ya kueleweka

2. Kuwa na vifaa !.... wanja sasa hivi unauzwa kila mahali kuanzia 10,000 mpaka 25,000 kulingana na aina ya wanja, quality, brand etc!
kwa wale wenzangu na mimi ambao we cant just use tarakimu 5 za hela  kwa ajili ya wanja tu... basi nunua wanja wa kawaida tu!

WANJA.... 
unaweza kuwa na huu wa penseli au mwingine
Bei yake hata 5,000 haifiki!

Sunday, October 19, 2014

10 MINUTES WITH GOD... LULU BY MTONI EVANGELICAL CHOIR!!




Yesu nipeleke kule kwa baba nikaishi naye kule mbinguni kwenye mji wa lulu na milango ya dhahabu
Yesu nipeleke kule kwa baba nikaishi naye kule mbinguni kwenye mji wa lulu na milango ya dhahabu
Oooooh.. Oooooh lulu..
Ooooh... Ooooh lulu
Ooooh Lulu...
Iko mbinguni
Ooooooh.... mmmmm...
Kweli ndani ya Yesu, Kuna raha ya ajabu isiyo na mwisho
kweli jamani mmmmmmm!
Yesu nakuomba nipe nguvu nikutumikie humu ulimwenguni kabla ya siku zangu hazijaisha..
Yesu nakuomba nipe nguvu nikutumikie humu ulimwenguni kabla ya siku zangu hazijaisha..
Oooooh... Ooooooh Lulu...
Ooooh... Oooooh Lulu
Oooooh Lulu...
iko mbinguni  
Ooooooh.... mmmmm...
Kweli ndani ya Yesu, Kuna raha ya ajabu isiyo na mwisho
kweli jamani mmmmmmm!

ENJOY!!

Wednesday, October 15, 2014

UREMBO NA LAURA:...NAMNA YA KUJIFUNZA 'GELE'... LEMBA LA KINAIJA!! (PICHA NA VIDEO)

Wengi wetu tumeona namna fasheni inakoelekea!
kufunga gele kumeshika chati sana japo fasheni ilikuwepo kitambo tu.
Leo ngoja nikupe hatua kwa hatua za namna kulifunga GELE 

unaweza kukosea hapa na pale lakini nakuhakikishia ukitulia unaweza kugeuka mtaalamu hivi hivi hahahahaa.... ni wewe tu na utundu wako katika kujifunza

HATUA YA 1

kunja kitambaa chako kwa staili hii... vitambaa vya kufungia gele shurti kiwe kikavu kidogo
kikunje hivi ili ule mwanzo kwa lemba uwe smooth pale mbele.  au pia unaweza kunja ikaribie nusu ya kitambaa chako

HATUA YA 2
linganisha pande zile za mwisho zilingane... yaani ukikiweka kichwani sio huku kurefu kule kufupi
Ni kulingane...kwamba ukianza kufunga mstari unaogawa katikati uwe katikati ya uso...sijui umenielewa heheheee...ualimu wito ujue!

Monday, October 6, 2014

SHOUT OUT TO WYNJONES KINYE!!- ASUBUHI ITAFIKA!!



Kuna muziki wa midundo...na kuna muziki wa maneno!
Kivipi?.... ni mara ngapi umesikiliza nyimbo za kikongo ukajikuta unajitikisa tu pasi kujua ni nini kinaimbwa!.... ni mara ngapi umesikiliza wimbo ukajikuta unabonyeza kitufe kurudisha nyuma kidogo ili upate kufaidi ubeti fulani wa wimbo huo?

This is what am talking about!.... Asubuhi itafika ni wimbo wa maneno... Kinye is talented...kuanzia sauti mpaka mpangilio wa tungo zake... ni kati wale vijana wachache wanaofanya muziki kama sehemu ya hobby lakini naamini akiamua kukaza ndula huyu anakwenda sawa na AY!!

Mjini hapa promo tu ila tukisema tufuate talent... kuna talent nyingi sana kama hizi na moja wapo ikiwa hii.... huu sio wimbo wake wa kwanza anazo kadha wa kadha....

kwa leo hebu tulia kidogo ujipe nafasi ya kumsikilia Kinye!... 
Hapo ulipo kama kuna kikwazo unapitia...kama kuna mtihani unakuelemea msikilize Kinye anavyokwambia Asubuhi itafika!!

Hongera sana Kwa kazi nzuri kama hii.... Maaaaan ! una sauti mwana! unayo haswaaaa!! endelea KUITIMIKIA SAUTI YAKO!!


Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger