Wednesday, September 24, 2014

UREMBO NA LAURA......TREATMENT YANGU YA NYWELE ZA ASILI

MWANAMKE NYWELE HASA ZIKIWA ZAKO MWENYEWE HAHAHAHAAA!!

Watu wengi wanadhani kuwa na nywele ndefu za asili, nzuri na zinazopendeza ni kitu kisichowezekana kwa mwanamke wa kisasa au kuwa na nywele za asili ni ushamba au kutokuwa mrembo.

Dhana hii ni potofu kabisaaa!... unaweza kuwa na nywele zenye dawa au nywele bandia za kusukia na bado ukashindwa kuzitunza vizuri na ukaondoa mvuto wako.

Sikatai kwamba kuna wakati tunahitaji mambo ya ziada kichwani ili kupendeza lakini pia si vibaya mara kadhaa ukaziachia nywele zako halisi na ukajiletea muonekano tofauti kabisa!!

Kutunza nywele za asili si kazi ndogo na hasa unapotaka ziwe nywele  zenye afya na zinazovutia.  Nywele za asili huleta muonekano wa mwanamke anayejiamini kwelikweli.
Binafsi nina nywele za asili nikimaanisha hazina dawa kabisa…. ingawa pia huwa ninasukia weaving au kuvaa wig pale ninapotaka muonekano tofauti lakini mara nyingi kichwa changu huwa huru. Leo ningependa kushea pamoja nanyi njia mojawapo ninayoitumia kutunza nywele zangu.

1. OSHA NYWELE ZAKO KWA MAJI YA UVUGUVUGU 
kwa shampoo unayotumia… huwa inasaidia kuondoa mafuta mafuta na uchafu unaoshikana na nywele hasa kwa vile huwa tunamaliza hata wiki mbili pasipo kuosha nywele…. Wengine wenye nywele za asili huogopa kuziosha mara kwa mara kwa kuhofia zitasinyaa na kuwa fupi hahahahaaa… hapana ndio unazisafishia njia ziwe ndefu zaidi…. Osha tu mara kwa mara usiogope…. Ukishaosha suka nywele za uzi zinasaidia kunyoosha au tumia hand dryer kukaushia…kariakoo  kuna mpaka Tsh. 35,000/= tu hilo hand dryer….  Kama unanunua nguo ya elfu 40,000/= utashindwa kweli kuwa na hiki kifaa??? Sema tu hujakipa kipaumbele lakini ni kifaa muhimu mwanamke mwenye kuzipenda nywele zake kuwa nacho
Shampoo ya mayai iko smoooooth

2. CHUKUA YAI NA UTOE KIINI PEKEE….

Mimi niliamua kuweka kiini na ute wake… lakini vizuri ukitumia kiini pekee

3. ONGEZA ASALI VIJIKO VITATU VYA CHAKULA


4. VURUGA MCHANGANYIKO WAKO



5. PAKAA NA UVAE KOFIA YA KUFUNIKA
Unaweza tanguliza mfuko wa plastic ile miyeusi kisha ukavaa kofia na kufunga lemba kwa juu ili kupata joto zaidi…. Njia hii ni bora kuliko moto mkali wa saluni.
excuse my nails heheheee!!...


6. KAA NA KOFIA KWA SAA MOJA AU ZAIDI.
7. OSHA NA MAJI YA UVUGU VUGU NA SHAMPOO…  zikitakata zikaushe kwa taulo na paka mafuta ya maji kwanza…. Hii inasaidia kuondoa ukavu wa nywele. Mi natumia Olive oil for hair

unaweza tumia mafuta ya nazi au yoyote ila ya maji ni mazuri baada ya kuosha

Zikishakauka vizuri…paka mafuta kwenye ngozi na umassage kichwa kwa dakika kadhaa…utahisi tu ngozi ya kichwa iko fresha kabisaa.

Mafuta ninayotumia kwa sasa 
nina aina mbili hii aina ya kwanza...ni mazuri sana kwa kweli

Kupata mafuta kwenye ngozi kunasaidia sana kuondoa ukavu kwenye kichwa na hata mba si rahisi kukuvamia. Ukipuuzia ukapata mba kuzitibu mba ni kazi sana na huwa zinazuia ukuaji wa nywele itakiwavyo.

Zilikatika sana pembeni ila now zinarudi faaaasta sana...


Furahia nywele zako na jisikie farahati kurock your natural hair mara moja moja!!... sio kila siku una fake hair kichwani Lol!!.... jiamini unaweza kuzilinda na kuzitunza nywele zako mwenyewe na zikawa na mvuto..
Njia hii pia hata walioweka dawa na nywele ni dhaifu wanaweza kuitumia.
Unaifanya treatment hii mara mbili kwa mwezi inatosha kabisaaa au hata zaidi kulingana na nafasi yako.

Zipo treatment zingine pia  kama ya kutumia mtindi ambayo ni nzuri mnooo imesaidia kunijazia nywele…. Tukutane tu kila jumatano hapa uwanjani!!
natumaini umeambulia kitu... Mwanamke nywele shost!!

No comments:

Post a Comment



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger