Friday, September 9, 2011

KUSAMEHE....shughuli nzito isiyohitaji mbeleko!


...wahenga walisema hakuna aliyemkamilifu...kwamba binadamu si malaika kuwa kila atakachofanya kimekamilika. mapungufu yapo na ndio hasa yanayotufanya sisi binadamu tuitwe binadamu na si malaika!

katika maisha kuna kukosea na kukosewa na hapo ndipo neno SAMAHANI linapotumika. yapo maudhi ambayo mdau unaweza ukasamehe papo hapo na yapo yale ambayo unaweza kuchukua wiki, miezi au hata miaka mpaka kufikia hatua ya kusamehe.

...kila binadamu ana haiba yake wapo wanaweka vinyongo hata baada ya kusamehe na wapo ambao husamehe na kusahau...yote kwa yote kumsamehe mtu ambaye hajakuomba radhi wala kujutia alilokufanyia ndiyo shughuli nzito isiyohitaji mbeleko...

...Zipo faida nyingi za kusamehe bila kujali kama aliyekukosea amekutaka radhi au la! bila kujali kama ulilkosewa ni kubwa au la! cha msingi ni kumsamehe mtendaji kosa bila kinyongo...

Faida moja wapo ni kuwa unapomsamehe mtu unajihisi kuutua mzigo moyoni ijapokuwa mtu anapokutaka radhi huwa anakusaidia kupunguza uchungu wa kosa ulilotendewa lakini bado wewe mtendewaji unahitaji kujifunza kusamehe toka moyoni bila kujali kama umeombwa radhi au la!


pili, unapomsamehe mtu hata mbingu hufurahi, kwa vile ni kati ya mambo ambayo dini zetu hizi hutufunza na kututaka kusamehe kama ambavyo Mwenyezi Mungu hutupatia msamaha bila kinyongo!

Tatu, amini usiamini, unapokosewa au kutendewa vizivyo nawe ukaumia na kulia, waama ukasononeka sana bila mtendaji kukutaka radhi ingawa anajua kosa lake kisha ukamsamehe...baraka huongezeka maishani mwako! jaribu leo na utaligundua hili...

Mwisho, kusamehe ukupa hali ya utu, hali ya kuthamini, hali ya afya na kukuondolea masononeko, maisha ni mafupi sana kuyatumia kumchukia mtu au kumkasirikia...kumbuka tu kuwa hata wewe ni mara nyingi umewakosea watu aidha kwa kujua au kutojua na pengine huwahi kuwataka radhi lakini leo hii wanakuthamini, wanakupenda na kukujali...na kuna hali ya msuto moyoni mwako!


...ni hayo tu na zaidi nakazia, samehe bila kujiuliza, kisasi kitakuumiza tu! samehe bila mipaka, Mungu atakupa mibaraka, samehe bila kuombwa msamaha, na utaishi maisha ya furaha!
LAURA!!!

Thursday, September 1, 2011

...IT'S BEYONCE....KIMFAACHO MTU CHAKE JAMANI!


Hongera zake....katika kuianza safari ya kuwa mama, wenyewe wanaita lifetime job hakuna likizo wala malipo ya ziada....

wishing them all the Best!

...Back again...Heri ya IDD pili!

i love the song a lot na leo nimeuchezaaaa mpaka baaaasi....dedication to all of you...



huyu kaka anayemalizia malizia hahahaaaaa yaani anaiwakilisha hasa ndombolo ya solo,
.....YAANI NI BURUDANI BARDAAAA...IDD NJEMAAAA


LAURA

Thursday, June 16, 2011

....KUMRADHI WADAU

....Nimepata meseji kadhaa zenye kuulizia hiki na kile kuhusu blog...nakiri nimetoweka kidogo kutokana na majukumu ya hapa na pale ila punde hali itarudi kuwa sawa.

Naheshimu mawazo na mchango wenu hata mkiwa wawili kwangu ni sawa na watu elfu mbili...

Naahidi nitayafanyia kazi maombi yenu ya hadithi na kupost hiki na kile mara kwa mara. ni majukumu tu ndio yanapelekea hali hii, majukumu ya kutafuta pesa ambazo zimeota matairi ukisema uzifukuzie kwa miguu ndio utabaki unasindikiza wenzio...shurti ujitume hasa ukitaka kuzifikia!

alamsiki! tuzidi kuwa pamoja katika maswali na hoja!

Laura

Sunday, June 12, 2011

PERUZI YA ENZI....YOU ARE STILL THE ONE BY SHANIA

..The lovely, romantic and so sweet song to dedicate to the one you love...





have a nice weekend

MSEMO WA LEO....

...ALIYEKUPA WEWE KUMBI NDIYE ALIYENINYIMA MIMI KITI...

..Tunakumbushwa tu kuwa majaaliwa uliyojaaliwa wewe umepewa na na yule aliyemnyima mwingine hayo majaaliwa...usiyaringie..usiyatambie kwa vile mtoaji ni mmoja anaweza kukugeuzia kibao!

na halikadhalika ukipata shukuru ukikosa usikufuru kwani mpaji ni Mola, anagawa kulingana na matakwa yake!

kama aliviumba vidole bila kufanana basi si ajabu nasi kutokufanana kimajaaliwa

Wednesday, June 1, 2011

USICHUKIE UKIKOSOLEWA!

habari zenu wadau, natumaini kwa kudra za mwenyezi Mungu bado mnapomua bila ushuru, hilo pekee ni jambo la kumshukuru Karima mwenye Huruma kwani waliotangulia mbele ya haki si kwamba wao walikuwa wenye dhambi kuliko sisi, basi tu tunapewa nafasi kadhaa turekebishe njia na mapito yetu

Haya ndugu baada ya salam hiyo hebu nirejee katika mada! kusema kweli hakuna binadamu mwenye akili timamu asiyependa sifa tena sifa njema za kutukuka. kila mmoja wetu anapenda kuonekana bora mbele za watu. tunachotofautiana ni namna kila mmoja anavyozipokea hizo sifa.

...wapo wanaozipokea na kuzidisha juhudi bila kubadili mienendo ya tabia zao

...wapo wanaozipokea kwa mikogo na kubadilika na kuanza nyodo

...wapo wanaozipokea na kubweteka wakidhani safari imefika ukingoni kumbe kama ni mlo basi ndio chai ya asubuhi.

Lakini lazima tukumbuke binadamu si malaika kwamba katika safari yake ya kimaisha kila atakalo tenda litakuwa jema na la uhakika. kuna mambo unaweza kuyafanya nawe ukaona uko sahihi kabisa na wanafiki pembeni wakakujaza sifa hewa nawe ukaona umefika unapotaka kumbe uko uendako kuna kuanguka, kuna kuporomoka, kunapotoka, na kuumbuka!

inapofikia hatua hii wanaokupenda na wasiokupenda watakusahihisha iwe kwa njia ya kistaarabu au ya aibu, vyovyote vile watakwambia bila soni kwamba hapa si hivi pale si vile...

hapa sasa ndio pa kuonana wabaya ila mimi binafsi nakukumbusha, usiamini sifa mia za watu ukamdharau mtu mmoja mwenye hoja tofauti. wewe si malaika tulia na utafakari uambiwalo pengine kweli hauko sahihi

siku zote changamoto za maisha huletwa na vitu vilivyo negative, ni kupitia makosa mtu hujifunza kilicho sahihi, ni kupitia kuanguka mtu hujifunza kusimama kwa bidii hivyo usiogope wala usichukie kukosolewa hata kama unaona anayekukosoa hana hoja yenye mashiko msikilize tu! yawezekana akakupa kilicho bora au mawazo mapya kupitia kukosoa kwake!

... sifa pekee hazijengi, believe me! nimexperience hilo na nimegundua makosa yangu katkka safari ya maisha yangu ndio yamenifikisha hapa nilipo, ningekataa kukubali kuwa sikufanya makosa basi si ajabu ningeendelea kukosea mpaka leo.

...Nawatakieni Alhamisi njema yenye baraka tele

...

HAHAHAHAAAA!....OH my!

...NIMESHINDWA KUJIZUA KUCHEKA JAMAN...




CHEKA UONGEZE SIKU ZA KUISHI...

PERUZI YA ENZI...ADIA BY OLIVER NG'OMA

... was one of the best Congolese music...i never tired watching it, never tired shaking my head and tapping my foot just following this melodious beats




wapi unakumbuka?

MSEMO WA LEO...

...Hamadi ni iliyo kibindoni; silaha ni iliyo mkononi...

haya shughuli hiyo!

WARAKA WA MWISHO....3 Na Laura Pettie

Tuliongozana kuelekea garini. Dakika kumi na tano baadaye tulikuwa sinza kwa Remmy nilikokuwa naishi na mchumba wangu Sakina.

Tulimkuta mdogo wangu Edna akiandaa chakula mezani hivyo muda mfupi baadae tulijiunga mezani na kupata chakula cha mchana pamoja na Bonny hali maongezi yakizidi kupamba moto.

“Maisha bwana kitendawili! Hivi ulitegemea kuwa siku moja utakuja kuwa mtu wa kuishi mwenyewe ndani mwako bila sapoti ya washikaji” bonny aliniuliza huku akijimiminia maji ya kunywa katika glasi yake na kugugumia mafunda kadhaa.

“aah! Wapi bwana lakini ndio hali halisi hivi Martin Totoz yuko wapi?” Nilimtupia swali Bonny wakati tukiiacha meza na kurejea sebuleni. Bonny aliachia tabasamu na kumtazama Sakina aliyekuwa hana habari na mazungumzo yetu kisha taratibu akanikonyeza.

Nilimuelewa hakutaka kuzungumzia habari za huyo Martin Totoz tukiwa pale na Sakina karibu. Tuliongea mengi na kukumbushana hili na lile. Mwishowe Bonny aliaga na kushukuru kwa mapokezi tuliyompa. Nilimuomba Sakina aniruhusu nimsindikize Bonny kwa vile usiku ulishaingia naye bila hiyana aliniruhusu.

Sakina, kama kuna siku ambayo nailaani basi ni siku hii uliyonipa ruhusa hii ya kumsindikiza Bonny. Ni huko ndiko kulikotokea chimbuko la mimi na wewe kutengana hivi, naogopa hata kumsingizia shetani kuwa ndiye aliyenipitia .

Tukiwa njiani kuelekea nyumbani kwa Bonny maeneo ya mbezi beach Nilimkumbushia tena Bonny juu ya wapi aliko Martin Totoz ambaye tulimpachika jina la Totoz kutokana na tabia yake ya kupenda wanawake bila kubagua rangi. Umri wala maumbile. Bonny aliachia tena tabasamu na kuniambia

“tunaishi karibu kabisa, yaani kwangu na kwake pua na mdomo”
“wacha bwana!” nilistaajabu
“ tena tupite kwake atakuwa yupo tu, siku hizi katulia kidogo” alisema Bonny
“Martin katulia! Aah! Wapi kwani ameoa?” nilimuuliza hali nikiyahamisha macho yangu toka mbele na kumtazama Bonny kwa mshangao

“Ana kifaa hicho bwana si mchezo! Yaani ni new model ya kisasa automatic baba!” tuliangua kicheko kwa kauli hiyo ya utani na ni wakati huo Bonny alikatiza kicheko na kunionyesha kona moja fupi ilibeba njia iliyoishia katika geti moja jeusi lililokumbatia ukuta wa kadri uliosujudia nyumba ya ghorofa moja.

“Martin anaishi hapa!”Bonny alitamka hayo huku akilikaribia geti la nyumba ile ya vigae na kupiga honi. Punde kijana mmoja alifungua geti na kuja mbio mpaka upande ule alioketi Bonny.
“shikamoo Mzee” alimsabahi kwa heshima kubwa na akionekana wazi kumfahamu Bonny
“Marhaba, mzee yupo?”

“Hapana ametoka kidogo lakini alinipa maagizo kuwa kama mtu akija kumtafuta amngoje”

“sawa kijana!” Bonny aliitikia na kuanza kulielekeza gari kuelekea ndani ya nyumba ile nikajikuta natabasamu baada ya kuona mtu kama Bonny kijana wa miaka thelathini na ushee akiitwa mzee.

Ilikuwa nyumba ya kisasa mno. Bustani kadhaa za maua na miti ya matunda ilileta mandhari tulivu yenye harufu ya kipekee. Kwa vyovyote ungepata jibu la kuwa wanaoishi hapa walikuwa na neema ya maisha haswa! Magari mawili ya kisasa yalikuwa yamepaki upenuni mwa nyumba.

Tuliteremka garini na moja kwa moja Bonny kama mtu aliyepazoea pale alinielekeza mlangoni na sote tukajitoma na kuivamia sebule kubwa iliyotapakaa mapambo ya kila namna. Makochi aghali, zulia la hariri na vitu kadha wa kadha vilivyonifanya nitunduwae tu!

Mwanzo ndio huoooo ITAENDELEA....

Tuesday, May 31, 2011

PERUZI YA ENZI.... MUCHANA BY KANDA BONGOMAN

Jikumbushe tu, Miaka hii wakati kibao hiki kinapanda chati ulikuwa wapi hasa...ni mambo gani unakumbuka...kwangu nakumbuka utoto wangu...na mengi ya kufurahisha na kuhuzunisha!




Zidi kuburudika!

Monday, May 30, 2011

MSEMO WA LEO...

...RANGI RANGILE, ASO HILI HANA LILE...

wakati ukijitapa kuyajua haya kuna wenzio wanayajua yale

kazi kwako!

WARAKA WA MWISHO...2 Na Laura Pettie

Ilikuwa jumapili, jumapili tulivu, jumapili iliyobeba mvua za rasharasha zilizokuja na kutoweka na kuondoa vumbi na hali joto iliyokuwa imelikamata jiji kwa miezi kadhaa.

Kama kawaida ndani ya siku hii waumini mbalimbali wa madhehebu ya kikristo walijumuika na wenzao katika kumwabudu mungu makanisani.

Nami nilikuwa mmoja wao nikiwa na mchumba wangu Sakina Mtanga mwanamke niliyempenda na nitakayempenda kwa dhati mpaka kufa. Mara baada ya misa tulitoka kanisani na kuingia garini tayari kwa kuelekea nyumbani ambako kwa siku hiyo niliamua kupumzika na mchumba wangu huyu kwa minajili ya kupanga hili na lile kuhusiana na ndoa yetu ambayo haikuwa mbali


Wakati nikielekea gari langu nililokuwa nimepaki umbali mfupi toka lilipo geti la kuingilia kanisani nilisikia sauti ya sakina ikiliita jina langu kwa sauti. Nikageuka nyuma na kuangaza angaza katika namna ya kumtafuta ili nipate kujua mahali alipokuwepo.

Nikamuona Sakina akiwa amesimama pembezoni mwa mti kubwa uliokuwa karibu na lango la kuingilia kanisani akiwa pamoja na kijana mmoja ambaye hakuwa mgeni sana machoni pangu ila kwa wakati ule sikumtambua haraka.

Nilichapua hatua za haraka haraka na kuwaelekea kule alikosimama Sakina na kijana yule huku akili akijaribu kupambanua haraka haraka ni wapi hasa nilipata kukutana na yule kijana aliyekuwa amesimama na mchumba wangu Sakina.

Nilipowakaribia nilitumbua macho yangu kwa mshangao hali kiganja changu cha mkono wa kuume kikimbilia kinywani na kuzuia ukelele wa mshangao uliotaka kunitoka ghafla bila ridhaa yangu.

“ Bonny!” niliita kwa sauti hali nikimtazama kijana huyo pasipo kuamini macho yangu. Bonny naye akiwa katika hali ya kustaajabu aliachia kicheko kifupi kisha kwa haraka akaja kunikumbatia kwa furaha. watu wachache waliokuwa wamesimama karibu nasi waligeuka na kututazama kwa mshangao.

Tulikumbatiana kwa sekunde kadhaa kabla ya kuachiana na kuendelelea kutazamana kwa mshangao wa kutoamini kabisa.

“ siamini macho yangu Jimmy, unajua nilipomuona Sakina nikahisi na wewe utakuwa hapahapa” Bonny aliongea kwa furaha
“ kwanini?” nilimuuliza kimtego hali nikijua vema jibu ambalo ningelipata toka kwa Bonny
“ Mlikuwa hamuachani toka Makongo sekondari!” alijibu haraka haraka na wote kwa pamoja tukaangua kicheko cha furaha.
“ uko wapi siku hizi maana toka tuachane makongo mabest wote sina mawasiliano nao”
“ ndio nimerudi toka Japan, sasa hivi niko Kizito construction company”.Bonny aliongea kwa bashasha hali akishindwa kabisa kuizuia furaha isijianike usoni pake.

“Jamani twendeni basi nyumbani mkaulizane vizuri” Sakina aliingilia kati maongezi yetu na sote kwa pamoja tukakubaliana naye.

Tuliongozana kuelekea garini. Dakika kumi na tano baadaye tulikuwa sinza kwa Remmy nilikokuwa naishi na mchumba wangu Sakina.


ITAENDELEA...

KUHANGAIKA NA SIMU YA MWENZA WAKO....

...simu hasa hizi za mkononi zimevunja ndoa, uchumba na mahusiano ambayo pengine hivi leo yangekuwa na matokeo ya kumpendeza Mungu...ni simu hizi hizi ndio zimesababisha watu kutapeliana na kuibiana, watu kuuana na kuchongeana ili mradi tafrani juu ya tafrani...

...Mimi leo nagusia simu ya mwenza wako, mpenzi, mchumba, mume au mke. kuna tabia hii ya kuchungulia simu ya mwenza wako ili kujua hili ama lile.

sikatai jamani simu inaweza kukufunulia mengi haswa! tena makubwa ya kuajabisha hata malaika mbinguni lakini upo utaratibu jamani wa kupekenyua simu ya mwenzio usikurupuke tu kila anapoingia basi we macho kwenye simu, akiisahau popote basi wewe mikono hiyooo kwenye simu utaadhirika kama si mwaminifu polepole utamshika tu!

...kama unahisi kuna dalili ya kusalitiwa ruksa kufanya upelelezi pengine ukianzia na simu, kwa muda acha kabisa kuifuatilia simu yake kisha ghafla mshtukize na kuichukua ama kumuomba uiangalie...akibabaika kuna kitu!

...kumbuka simu pekee haiwezi kukupa majibu ya uaminifu wa mwenzio kwa vile mtu naweza kuwa nalaini zaidi ya moja, simu zaidi ya moja, facebook ndio balaa, na wakati mwingine anayekuzunguka naye anajua fika uhusiano wenu hivyo katika muda hatari hawezi kumpigia au kumtumia meseji.

...Kingine wawili mnapopendana kuna wabaya wenu wanaangaliana. hivyo si ajabu mtu kuamua kumtumia mwenzi wako ujumbe wa mapenzi au kumpigia manane ya usiku ili mradi kukurusha roho...siku hizi hakuna cha mwanaume wala mwanamke wote tumehitimu chuo cha ufitini!

... hivyo kabla hujammuhukumu mwenzio kwa meseji ama simu inayoashiria usaliti fanya uchunguzi kwanza, sio upokee simu ya mwenzio usikie sauti ya kike au ya kiume inamuita dear...ukurupuke tu kumtwanga mwenzio makofi ama kubeba kilichochako na kutimua...utajuta!

... MSIMAMO WANGU:
usijitie opareta wa simu ya mwenzi wako utakufa kwa kihoro kabla ya siku zako, ishi kwa amani ukimuamini kama si mwaminifu atajulikana tu.

Mtangulize Mungu katika masuala ya uhusiano wako, atakusimamia vema kabisa!

usisome meseji wala kujibu kwa niaba ya mpenzi wako bila kibali chake.

usimtukane mtu kwenye simu bila kujua ana mahusiano gani na mpenzi wako.

usiibe namba ya mtu kwenye simu ya mpenzi wako kwa nia ya kumtukana au kumchunguza usifanye vitu holela kuna sheria!

using'ang'anie simu ya mpenzi wako kila mara anapokuwa nawe, mpe uhuru wa kutosha kama ambavyo ungependa kuwa nao

ni hayo tu...una mengine ya nyongeza nifahamishe tu!

PERUZI YA ENZI....LIBERIAN GIRL BY MICHAEL JACKSON

...i love this song a lot, video yake ni zaidi ya ubinifu. but mostly i like this part of verse
Liberian Girl, You Know That You Came
And You Changed My World, Just Like In The Movies,
With Two Lovers In A Scene,
And She Says . . ."Do You Love Me"
And He Says So Endlessly . . ."I Love You, Liberian Girl"



furahia kuperuzi!

MSEMO WA LEO...

...AKUNYIMAYE MBAAZI KAKUEPUSHIA MASHUZI...

Mashuzi ndio kule kushuta ashakum si matusi wenyewe mnasema kujamba!

na mbaazi unapozila shurti zikuchafulie tumbo na hivyo kushuta wajibu sasa unaponyimwa mbaazi shukuru tu umeepushiwa hiyo zahama la kuchafua hewa

Yumkini, maana yake binadamu unapokosa kitu usiumie sana pengine Mungu kakuepusha na mabaya ambayo yangekupata, kuumia kupo ila ndio isiwe kuumia mpaka unakufuru...

Shukrani kwa kila jambo limalotokea maishani mwetu!

WARAKA WA MWISHO 1.... Na Laura Pettie

....Baada ya kumalizana na SIRI YANGU..., nimekuja na kitu waraka wa mwisho, hadithi niliyoitunga mwaka 2009 ikiwa maalumu na dedication mama yangu mdogo Mary Samwel.
Mungu azidi kukupa maisha marefu nizidi kufaidi upendo yako!


Kwako SAKINA

Nakuandikia waraka huu hali nikijua wazi kuwa utakuwa waraka wangu wa mwisho kwako na kwa walimwengu. Nauita waraka wa mwisho kwa vile nimedhamiria kuukimbia ulimwengu uliojaa kila aina ya lila na fila na kwenda kule kusikorudika.


Sitajali walimwengu watanihukumu vipi kwa uamuzi wangu huu kwavile yaliyonikuta yanatosha na aibu niliyoipata pia inatosha acha nikapumzike na masahibu ya dunia.
Sakina, Dunia uwanja wa fujo nikiwa na maana kila mmoja huja na mirindimo yake, Dunia mti mkavu kiumbe usiuelemee lakini zaidi dunia tambara bovu lisolositiri makovu! na haya nimeyashuhudia mimi mwenyewe ndani ya miaka yangu arobaini na mbili niliyovuta pumzi ya bure ya mwenyezi mungu.

Nikisema nimlaumu Karima kwa kumleta kiumbe huyu aliye chanzo cha yote haya yaliyonikumba nitakuwa nakufuru lakini pia nikisema niulaumu ulimwengu kwa kutonipa tahadhari naona kama nitakuwa najikosha kwa vile nilipokanywa sikusikia la mwadhini wala mteka maji msikitini. Wembe nilioulilia sasa umenikata!

Sakina, nimekutendea mengi ya kufurahisha na kuhuzunisha. Nimekutendea yale ambayo kwa hakika kwa binadamu mwingine kamwe asingeliweza kunistahi na kunisamehe lakini wewe sakina uliyafumbia macho na kunipa nafasi kadhaa za kujirekebisha.

Aibu yangu ilikuwa yako vilevile. Sakina nasita hata kukuita mpenzi kwa sababu ya yale ambayo yametokea kati yetu lakini kwa jinsi ninavyojutia sina maneno ya kutosha kuuelezea uchungu wa toba nilio nao. Nakutaka radhi kabla sijaueleza ulimwengu yaliyonikuta!


Sakina, naandika waraka huu hali matone ya machozi yakizidi kuulowanisha waraka huu, najuta, najuta na narudia kusema najuta nikiwa na maana kuwa najuta kuliko neno majuto linavyomaanisha.

wahenga walisema asiyefunzwa na mama hufunzwa na ulimwengu na leo hii nakiri ulimwengu umenishikisha adabu!


Sijui nianzie wapi kusimulia haya yaliyonikuta, niko njia panda nisijue basi la kupanda. Pengine nianze na siku hii iliyozaa mambo yote haya, siku ambayo nitailaumu mpaka naingia kaburini!

ITAENDELEA...

Sunday, May 29, 2011

BARUA YA OPRAH...3

"When I started, not even I imagined that this show would have the depth and the reach that you all have given it. It has been a privilege for me to speak to you here in this studio, in this country and in 150 countries around the world on this platform that is The Oprah Winfrey Show.

You let me into your homes to talk to you every day. This is what you allowed me to do, and I thank you for that. But what I want you to know as this show ends: Each one of you has your own platform. Do not let the trappings here fool you.

Mine is a stage in a studio, yours is wherever you are with your own reach, however small or however large that reach is. Maybe it's 20 people, maybe it's 30 people, 40 people, your family, your friends, your neighbors, your classmates, your classroom, your co-workers. Wherever you are, that is your platform, your stage, your circle of influence. That is your talk show, and that is where your power lies.

In every way, in every day, you are showing people exactly who you are. You're letting your life speak for you. And when you do that, you will receive in direct proportion to how you give in whatever platform you have.


"My great wish for all of you who have allowed me to honor my calling through this show is that you carry whatever you're supposed to be doing, carry that forward and don't waste any more time. Start embracing the life that is calling you and use your life to serve the world."

HAHAHAAAA...EEE BWANA WEE!

...shughuli iko hapa, nimecheka bila kupenda jamani...



enjoy your weekend!

Thursday, May 26, 2011

PERUZI YA ENZI...

...Furahia KUPERUZI ENZI ukiwa nami… hii itakuwa safu ya mistari ama video ya enzi zile wenyewe tunaita zilipendwa… hii yote ni katika kujikumbusha yaliyopita...maana viaja wengi wameshikilia ya leo tu na mpya ya kesho... ya kale dhahabu kukumbushana wajibu!

mwenyewe anamwemwesa
If there's fire stiring in your heart, And you're sure its strong and right
Keep it burning through the cold and dark, It can warm the lonely nights
Oh, You might need somebody, You might need somebody too...

You Mighty Need Somebody - SHOLA AMA


hapo vipi?

Barua ya Oprah...2

"The first week we went national, I remember I got a letter from a woman named Carrie in Ann Arbor, Michigan. Carrie said, 'Oprah, watching you be yourself makes me want to be more of myself.' That was and still remains one of the nicest things I ever heard. What Carrie felt is what I wanted for every single one of you.

I wanted to encourage you to be more of yourself just as you all encouraged me, and you cheered me on and occasionally complained about my outfits, my big hair and earrings the size of napkins. Now I see you had every reason to.
"Soon after I started the show, something shifted for me. It really did. I started the show as a job and was very happy to get the job, but it was not long before I understood that there was something else going on here. More than just job satisfaction.

Something in me connected with each of you in a way that allowed me to see myself in you and you in me. I became your surrogate—to ask the questions, deliver the answers, learn, grow, expand my thinking, challenge my beliefs and the way I looked at the world. I listened and grew, and I know you grew along with me.

"Sometimes I was the teacher, and more often, you taught me. It is no coincidence that I always wanted to be a teacher and I ended up in the world's biggest classroom. And this, my friends, will be our last class from the stage.

"What I knew for sure from this experience with you is that we are all called. Everybody has a calling, and your real job in life is to figure out what that is and get about the business of doing it. Every time we have seen a person on this stage who is a success in their life, they spoke of the job, and they spoke of the juice that they receive from doing what they knew they were meant to be doing.

We saw it in the volunteers who rocked abandoned babies in Atlanta. We saw it with those lovely pie ladies from Cape Cod making those delicious potpies. ... We saw it every time Tina Turner, Celine, Bocelli or Lady Gaga lit up the stage with their passion. Because that is what a calling is.

It lights you up and it lets you know that you are exactly where you're supposed to be, doing exactly what you're supposed to be doing. And that is what I want for all of you and hope that you will take from this show.

To live from the heart of yourself. You have to make a living; I understand that. But you also have to know what sparks the light in you so that you, in your own way, can illuminate the world."

ITAENDELEA...

MSEMO WA LEO...


MTAKA NYINGI NASABA, HUFIKWA NA MWINGI MSIBA!


Kumekucha! Msemo huu ni kama mshika mbili moja humponyoka sasa huyu si mbili tu, atataka hata 10 zote azikamate yeye… yahusu! Usitake nyingi sifa, utakufa!

Na dunia hii iliyojaa sifa za kinafki unalamba mchanga watu wanakusifia nawe kwa kuzitaka nyingi nasaba unaamua kutafuta mpaka kokoto….

hahahahaha! yatakayokukuta utasimulia vizazi vyako vijavyo!

shukrani!

SIRI YANGU 11....Na Laura Pettie

Sikukumbuka kitu mpaka nilipokuja kuzinduka nikiwa hospitali. Nilipofumbua macho nilishuhudia kitanda changu kikiwa kimezungukwa na watu kadhaa. Nilimtambua mama aliyekuwa analia muda wote, nilimtambua dada yangu Debby ambaye naye alikuwa analia, nikamtambua Kelvin aliyekuwa karibu yangu kabisa.

Nilifumba macho tena kuvuta kumbukumbu zangu. ‘jonas amefariki usiku huu kwa ajali ya gari kinondoni’ maneno hayo yalipita ubongoni mwangu na ghafla nilipiga yowe
“ mamaaaa! Mama jonas, jonas jonas mama?... mama jonas yuko wapi?” nililia wa sauti ijapokuwa walijitahidi kunituliza lakini asikudanganye mtu kilio cha kufiwa hakituliziki. Nililia sana mpaka nilijihisi kuchoka na sauti kunikauka.

Kelvin akaniambia nililetwa pale jana usiku na hivyo nilikuwa nimepoteza fahamu kwa muda mrefu. Sikuwa nasikia la mnadi dini wala mteka maji msikitini. Yote yalikuwa kama ndoto ama habari Fulani ya kufikirika isiyo na ukweli hata chembe.
Jioni ya siku hiyo nilitoka hospitali na kwenda kwa jonas.

Nilipouona umati wa watu pale nyumbani ndipo nilipoamini kuwa Jonas alikuwa ameniacha. Ndani vilio vilikuwa vikali mno kukawa hakuna wa kumbembeleza mwenzake. Nilipoingia ndani Iloma aliyekuwa amevikwa nguo nyeupe aliponiona alipiga mayowe na kutaka kunyanyuka ili anifuate. Nilimsogelea na tukakumbatiana kwa nguvu.

Iloma alikuwa analia jamani. Alikuwa analia mno na kwa uchungu hasa! Hivyo ndivyo Jonas alivyoniacha, hivyo ndivyo jonas alivyonipigia simu saa moja kwa kifo chake. Alikuwa ameondoka bila kusubiri kauli yangu. Ningejua ningemwambia yote akiwa hai! Leo amekufa, jonas amelala na sitamuona tena na ina maana yale niliyotaka kumwambia sitamwambia tena!. Inaniuma sana na itaniuma mpaka kesho.

Ajali mbaya ya gari iliyotokea baada ya tairi la gari lake kupata pancha na kuyumba na hatimaye kugonga msingi wa nyumba ndio iliyomuua Jonas. Alizikwa makaburi ya kinondoni na kumuacha mjane iloma akiwa na mzigo wa kumlea mtoto wao wa pekee kim.

Miaka imekatika kama maji katika mkondo wake. Kidonda alichoniachia Jonas hakiponi bali kinazidi kuleta maumivu ambayo hayasimuliki mdomoni wala hayaandikiki kitabuni. Nimekwisha jifungua mtoto wa kiume aitwaye Junior Jon. Mtoto huyu mzuri wa kiume ananiliza kila uchao.

Nimekonda kama uchelewa kwa mawazo na sononeko la moyo. Vikao vya familia vimeshakaa mara kadhaa kujadili suala la kumtambulisha baba wa mtoto lakini nimeendelea kukataa kumtaja kwa kisingizo kuwa yuko nje ya nchi.najua uongo haukidhi haja ya milele na ndio maana nahisi mzigo wa siri hii ukiwa mzito moyoni mwangu hasa ninapomtazama Junior.

“ sasa mwanangu vipi kuhusu huyu mkwe, maana mimba tumekusaidia kulea na mtoto amezaliwa na anakuwa lakini baba yake hatukijui hata kivuli chake” baba alinieleza usiku mmoja mara baada ya chakula

“ atakuja tu baba” nilimjibu nikitegemea angekubaliana nami
“atakuja …atakuja….lini? anaogopa nini kujitokeza hadharani ana uso wa nyani?”
“ hapana baba!”

“ sasa! Kinachomshinda kuja nini ama kinachomshinda kutuma hata mshenga nini?”
“ mpe nafasi ajiandae jamani. Kuja atakuja tu” nililalamika kiasi kwamba baba alishindwa hata la kuendelea kusema

“ sawa mama, sisi tutangoja lakini mwambie afanye hima maana Junior huyu anahitaji kulelewa na wazazi wote wawili!”
“ sawa baba” sikungoja swali, maoni wala hoja ya nyongeza. Nikajiondokea zangu na kwenda kulala
Natamani kuueleza ulimwengu ukweli lakini sijui nianzie wapi jamani. Iloma ambaye tumekuwa naye bega kwa bega tangu afiwe na mumewe sidhani kama atanielewa siku nikiiweka hadharani siri hii na sielewi ataniweka katika kundi la watu wa namna gani wanafiki ama mahayawani! ingawa sasa Iloma ameolewa tena na yupo kwa mumewe mpya Roho inanisuta, roho inaniuma mno kwa vile Junior sasa ananiuliza mama baba yangu yuko wapi!

Nashindwa niseme nini. Maneno ya Jonas yanazunguka kichwani pangu kila uchao. Namkumbuka mno hasa masaa machache kabla kifo chake alipofika ofisini kwangu, aliponipigia simu na kuisikia sauti yake kwa mara ya mwisho. Nakiri nilimpenda na hata sasa nampenda ingawa hayupo nami.

Nawauliza walimwengu! Nisaidieni kupata jibu! Niitunze siri hii mpaka lini? Mwanangu nitakuja kumjibu nini kuhusu baba yake? Je nikiiweka hadharani siri hii jamii itanichukulia vipi, Iloma atanifikiriaje mimi, wazazi wangu watanionaje nanyi walimwengu mtanihukumu vipi?
Ama siri hii ibaki kuwa siri yangu!!!?


Email: queenlauryn5@yahoo.com
Inbox me in facebook: laura Pettie

Wenye majibu mnisaidie, nakaribisha maoni, ushauri n.k, hadithi imeishia hapa, kaeni mkao wa kula na kitu kingine toka kwa yule yule mwandishi wako Laura Pettie!

NDOA NDOANO...

Katika maongezi na ndugu yangu mmoja, aliwahi kuniambia
pata MWENZI WA MAISHA MWENYE MAPUNGUFU YOTE ILA SI MWENYE UPUNGUFU KATIKA UAMINIFU…NI ZAIDI YA SHUGHULI!!!

Huyu kijana wa miaka 28 tu, too young jaman, mwenye shahada yake ya uzamili tena aliyoipata mwaka huu mwanzoni, mwenye kazi nzuri kabisa ya uafisa mipango Halmashauri ya Chamwino Dodoma AMEJIUA KWA KUJIPIGA RISASI usiku wa kuamkia May 25.…kisa kikiwa ni kumfumania mkewe na mwanaume mwingine…

unaambiwa ilikuwa heka heka ya vitanda na mikeka kiasi cha kufikia mwanaume kumkimbiza mkewe Vicky mpaka nyumbani kwao kasha kumtandika risasi za mbavu…akafikiri ameua naye akajitungua risasi…inauma na inasikitisha sana kwamba mkewe yu mahututi Hospitalini na yeye ameshalala nyumba ya milele uko kwao Tabora…ila ametuachia funzo kuwa uaminifu katika mahusiano huepusha zaidi ya UKIMWI…

jaman tulio katika mahusiano tujaribu kuwa na hofu kidogo na Mungu itatuepusha na zahama kama hili…. TABIA YA KUWA NA WAPENZI WENGI NI YA KUJIENDEKEZA TU!

UPUMZIKE KWA AMANI FREDY!…

MSEMO WA LEO...

Wahenga walionya usiwe

...KISEBUSEBU NA ROHO KIPAPO...

wakiwa na maana usiwe mtu wa sitaki nataka utakosa mengi utakimbiwa na wengi!

hutaki shikilia sitaki yako, unataka ng'ang'ania kilicho chako

My best...and...My favorite...! HABIBI Ya Nour El Ain

..ilikuwa sitoki redioni wala mbele ya TV huu wimbo ulipokuwa unaimbwa, sikuwa naelewa chochote lakini uzuri wa video, jumlisha sauti ya Bwana Amr Diab zidisha utamu wa ala kisha ugawanye maana halisi ya huu wimbo...sadaktaaaa! unaweza kusahau jina lako kwa muda ati!

unaambiwa
Habibi, ya nour el ain, My darling, glow in my eyes,
Ya saakin khayali.Who lives in my fantasies.
Aashek bakali sneen,I've adored you for years,
Wala ghayraak fibali.No one else is in my mind.

dedication to my beloved Man! wangu namwambia Habibi Eyounaak ma-ayaa!



Enjoy yourself!

THE OPRAH WINFREY SHOW FINALE...A wonderful letter to you!


After 25 years of history-making, life-changing television, Oprah hosts the finale of The Oprah Winfrey Show.

CHINI NI UJUMBE AMBAO OPRAH UMEUACHA KWETU WAPENZI WA VIPINDI VYAKE...NIMEUPITIA UJUMBE WOTE NA HAKIKA MARA TU NILIPOMALIZA NIMEJIKUTA NIKIGUNDUA MENGI KUHUSU MIMI LAURA, AND WHAT HOLDS ME BACK TO LIVE MY LIFESTYLE DREAM!

NIMEONA SI VIBAYA NIKISHEA NANYI UJUMBE HUU KILA SIKU!
ANAANZA KWA KUSIMULIA ALIPOTOKA... NINGEPENJDA KUJUA KAMA MNAPENDA NITAFSIRI AU TUSHUKE TU NA HII PART YA LUGHA YA WENZETU.....

On September 8, 1986, the first national episode of The Oprah Winfrey Show was broadcast into homes across America. Now, 25 years later, Oprah steps onto the stage for the last time to share her greatest lessons and hopes for her viewers.

"After deliberating for some time, we decided to do what we do best, and that is a show about and with everyday people. This show always allows people, hopefully, to understand the power they have to change their own lives.

If there's one thread running through each show we do, it is the message that you are not alone. Twenty-five years and I'm still saying thank you, America. Thank you so much. There are no words to match this moment. Every word I've ever spoken from this stage of The Oprah Show for 4,561 days of my life is what this moment is all about.
...

"When I came here, I was about to turn 30 years old. I didn't have a vision or a lot of great expectations. Stedman talks about vision all the time, but I didn't have one when I came here. I just wanted to do a good job and cause no harm. ... That first day was a shock to me. There was no audience.

There I am in my best Anne Klein II velour outfit, my guests were a few Chicago football players, New Year's Day, 1984. ... I needed people. I needed to have you to gauge how things were going during the show, if you were responding, if you were laughing, if you were tracking with me. So after that first show, we put up some folding chairs in the audience. We brought in the staff.

Secretaries. Anybody we could find in the building and filled the first rows with staff people and the rest with people off the street that we bribed with doughnuts and coffee, and we'd say, 'Come in.'
...

"Two years later, when we went national, I remember at the time, Roger King told me that one station manager said that he'd rather put a potato in a chair in his market than have a big black girl with a funny name. And in spite of that, from Memphis to Macon, from Pittsburgh to Pensacola, from New York to New Orleans, you all let me in."

ITAENDELEA...

SIRI YANGU 10....Na Laura Pettie

...Saa kumi jioni niliondoka kazini na kurejea nyumbani. Nilimkuta mama anaandaa chakula cha jioni lakini pia akiwa na uso uliosawajika. Nilibadili nguo kisha nikajiunga naye jikoni.

Mama alionekana kuwa mwingi wa mawazo na kila mara alinitazama kwa kituo. Mwisho alitoa dukuduku lake.

“ Karen utanificha mpaka lini mwanangu!” aliacha kukata kata nyanya na kuniuliza

“ juu ya nini” moyo ulipiga mkambi lakini ilinipasa kuuliza kujua kisa. Mama alivuta pumzi na kuziteremsha kwa kasi. Alitikisa kichwa kabla ya kurudia kunitazama kwa kituo na kuniambia

“ wewe mjamzito Karen, mimi ni mama yako nakujua kama ninavyokijua kiganja cha mkono wangu wa kuume, umejitahidi kuficha lakini mwanangu unasahau kuwa mimba haina siri!”
“ mama!” nilishtuka
“ unakataa nini Karen!?” alianza kunijia juu hali akionekana wazi kukerwa na mshangao wangu.

“ kwanini umeniwazia hivyo mama” nilihoji badala ya kujibu huku nikijigeuzia dirishani na kuyatumbua macho yangu kwa woga.

“ sikulazimishi ukiri lakini kumbuka mficha maradhi kilio umuumbua!”

sikujibu kitu kuchelea kubanwa zaidi lakini tayari nilishakaa mguu sawa nikijua ipo siku bomu litalipuka tu lakini pia nilijipa tumaini kuwa Jonas angenioa bila kujali kama ningevunja ndoa ya rafiki yangu Iloma.

Masaa yalikuwa hayaendi hata kidogo. Mara kadhaa niliitazama saa yangu ya mkononi na kuutumbulia macho mshale wa dakika uliokuwa ukienda kwa maringo bila kujua moyo wangu uliokosa subira ulikuwa ukipiga mara mbili ya kawaida.

Saa moja usiku nikiwa chumbani simu yangu ya mkononi iliita. Zilikuwa ni namba ngeni kabisa machoni pangu. Nilihisi jonas alikuwa ameamua kunishangaza.

Nikaipokea kwa mbwembwe lakini baada ya kusikia sauti nyingine tena ya kike nilijiweka sawa na kusikiliza na sasa nikaitambua sauti hiyo kuwa ni sauti ya iloma. Nikajiinusha toka kitandani na kusimama wima sakafuni simu ikiwa sikioni.

Nikatega sikio kwa makini.
“ Karen!... Mungu wangu!...Karen… mdogo wangu… Jonas ameniacha” huku akilia aliyatamka maneno hayo kwa uchungu hasa. Nikahisi bomu la talaka limelipuka. Nami kiherehere cha moyo kikanikumba

“ kakuacha! Sikuelewi Iloma” niliongea kwa sauti ya mshangao huku nikiwa katika hali ya kawaida kabisa kwa vile nilishahisi Jonas amemweleza mkewe juu ya talaka lakini wakati nikiwaza hayo Iloma alitamka maneno ambayo mpaka leo hii ninapoyakumbuka natokwa na machozi ya uchungu.

“ Karen! Jonas amefariki usiku huu kwa ajali ya gari kinondoni” nilihishiwa nguvu, simu ikaniponyoka mkononi na pasipo kujitambua nilianguka chini na kuzirai.

ITAENDELEA....

Tuesday, May 24, 2011

SIRI YANGU 9....Na Laura Pettie

...Aliongea kwa uchungu mno huku mikono ikiwa imelishikilia tumbo lake mithili ya mama mjamzito aliyeshikwa na uchungu wa uzazi. Nilimtazama mama bila kuelewa nimwambie nini cha kumtuliza.

Nilijua alikuwa ananiwazia sivyo! Kelvin hakuwa katika fikra zangu kabisa na wala hakuwa chanzo cha huzuni yangu. Ilikuwa ni siri yangu kuwa kilichotokea kati yangu na Jonas ndicho hasa kilichokuwa kinanimaliza. Sikujua nianzie wapi kuuelezea ulimwengu masahibu haya yaliyonikumba pasi ulimwengu huo kunihukumu vikali!

“…wenzio wanatelekezwa na watoto wewe Kelvin hajakuachia chochote cha kumkumbuka sasa mawazo ya nini, bado u msichana mrembo na najua mungu atakupatia mume bora wa kukufuta machozi yako, cha msingi tulia, jiheshimu na tafakari upya maisha yako” alimeza funda la mate na sasa akaketi pale kochini nilipokuwa nimeketi na kunikumbatia.

“ hupaswi kulia hivi mwanangu!” alinikumbatia zaidi
“ lakini mama…”
“ shh.shhh! najua umeumia moyo mno lakini anza kubadili maisha yako sasa, anza upya Karen, pigania maisha ya furaha karen!” aliniachia na kunitazama usoni hali akionesha wazi kutopendezwa na hali yangu, akaelekea jikoni. Wakati nikiwa nimeketi pale sofani nikitafakari, mlango uligongwa na haraka niliinuka na kwenda kuufungua.

Alikuwa Kelvin! Hakungoja kukaribishwa alinipita mlangoni na kujitoma ndani kwa haraka. Nikaufunga mlango na kugeuka kumtazama. Akili ilikuwa imekimbilia kusikojulikana na kuyaacha macho yangu yakimtumbulia Kelvin bila hata salamu.
“…Karen! Sasa imetosha na unahitaji msaada wangu kwa vyovyote iwe ni kama daktari ama kama Kelvin!” aliketi na kuendela kuongea kwa msisitizo

“hali yako inanitisha Karen mpaka leo ukashindwa kuendelea na misa kanisani Karen, umeshindwa kupiga kinada na kuimba imekuwaje!?” alinionyesha wazi mshangao wake. Machozi yalijaa ndani ya mboni za macho yangu na kilio cha kwikwi kilinikaba kisawasawa.

Kwa haraka alinyanyuka na kuja kunikumbatia pale nilipokuwa nimesimama kama mlingoti wa bendera. Sikumpa pingamizi lolote na hakika alinipa faraja kuwa mikononi mwake kwa dakika kadhaa, harufu ya jasho lake ilinifikia barabara na kuichanganya zaidi akili yangu.


Alinisogeza mbali kidogo na kifua chake kisha nyuso zetu zikapata nafasi ya kutazamana kwa ukaribu zaidi. Macho yake yenye mvuto yalimetameta hali midomo yake ikimwemweseka na kunikumbusha wakati ule alipokuwa sehemu ya maisha yangu.

Mikono yake iliyojaa upole ilipita usoni pangu na kufuta michirizi ya machozi iliyokuwa ikizidi kuweka vijito katika paji la uso wangu!. Nilitamani aendelea kuyafuta machozi hayo milele na milele.

“hustahili huzuni Karen!” alininong’oneza na kunirudisha tena kifuani pake.ilikuwa ni kama mtoto aliyempoteza mama yake kwa miaka kadhaa na sasa mama huyo alikuwa mbele yake na tena mikononi mwake. Tulikumbatiana hivyo kwa muda huku kila mmoja akisikilizia mapigo ya moyo ya mwenzake. Kuwa mikononi mwa Kelvin lilikuwa jambo la faraja mno kwangu.

Hisia zangu kwa Kelvin zilikuwa palepale japo mara kadhaa nilijaribu kuzikana hisia hizi ambazo nalazimika kukiri sijui kma zitatoweka.
Mama aliporejea pale ukumbini alitunduwaa kwa sekunde kadhaa kabla ya kujikohoza ili kutujulisha kuwa alikuwa pale. Kelvin alinitoa maungoni mwake na kugeuka kumtazama mama. Alijiweka sawa na kumsalimia mama ambaye alikuwa akimtazama katika namna isiyoeleweka.

“ umeamua kuja kummaliza kabisa!” mama alimtupia swali
“ hapana mama! Nadhani Karen anahitaji msaada wangu ili arejee katika hali yake”
“ sikiliza Kelvin…” mama aliketi sofani na kumtazama Kelvin kwa macho makali zaidi mithili ya mwanamke aliyetelekezwa kwa miaka mingi na mumewe na sasa mwanaume huyo alikuwa mbele yake akimtaka warudiane.

kisha akaendelea kusema “ kwa vyovyote vile unapaswa kukaa mbali na huyu binti tangu sasa! Na hilo si ombi bali ni amri mwanangu, tangu lini ungo ukaomba msaada wa sinia kupepeta mchele?”
“ mama yaliyopita si ndwele…” Kelvin alitaka kujitetea
“ na ndio tunaganga yajayo hivyo!” mama alidakia kwa dharau
“ nilikosa lakini sitaki Karen ajutie kuwa na mimi maishani mama” alijaribu kumuelewesha
“ ajutie! Karen ajutie mara ngapi? Kelvin nakuheshimu kijana! Na sitaki kukuvunjia heshima yako. Mlango ule pale!” alimuonyesha kwa kidole chake cha shahada! Huku naye akinyanyuka na kwenda kuufungua kabisa.
“ mama… najua nina makosa…mama nipe tu nafasi mama…” Kelvin alishindwa hata kuzipangilia sentensi zake katika mpangilio unaoeleweka lakini ni dhahiri akili yake iliduwazwa na maneno yale ya mama.

Nilitaka kumtetea Kelvin lakini mama aliniwahi na kunitazama kwa jicho kali mno! Kelvin aligeuka na kunitazama. Alishusha pumzi ndefu mara kadhaa na machozi yalionekana kwa mbali yakizinyemelea mboni za macho yake. Hakuamini!

“ Kelvin! Hii iwe safari yako ya mwisho hapa! Iwe kwa kheri au shari Kaa mbali na Karen tafadhali kwa namna yoyote ile” mama alizidi kuupigilia msumari moyo wa Kelvin. Hakumudu hata kupiga hatua moja. Kelvin alifumba macho yake taratibu na kuyaruhusu machozi yatiririke mbele ya mama.

Hata alipoyafumbua alibakia kuyapepesa na kuyafanya yabubujike mithili ya kijito kitokacho mlimani. Midomo yake iliwayawaya isijue hata itamke nini cha kuibadili hali ile. Alishidwa kupigana na hisia zake kabisa.
Nilihisi uchungu mkubwa moyoni mwangu. Sikutaka kumshuhudia Kelvin akizidi kulia mbele zangu. Nilikimbilia chumbani huku nami nikiomboleza. Kelvin aliondoka zake na mama alinifuata chumbani. Aliponikuta nalia aliguna kwa sauti na kuniambia
“ anza upya maisha Karen! Mapenzi ni sehemu tu ya maisha na wala si maisha! Hivyo Kelvin si maisha yako binti!”
“ lakini si Kelvin mama! …”

“ what! Si Kelvin anayekupa wazimu huu?” mama aliniuliza kwa mshangao. Nikazinduka na kutambua kosa! Nilikuwa nimeropoka bila kufikiria. Nilijituliza na kumtazama mama ambaye sasa alinifuata kwa kasi pale kitandani na kuketi!
“ Karen! Ni nini kinakusumbua mpenzi?” aliniuliza kwa upole kana kwamba ndio kwanza alikuwa ananiona katika hali ile ya masononeko.

“ni hisia tu za kumkosa Kelvin lakini si kosa la Kelvin!” niliirekebisha kauli yangu na mama akanisogelea na kunikumbatia. sikumuona tena Kelvin mpaka siku niliyofikishwa hospitali baada ya kuzirai.

Hali yangu haikuwa ya kuridhisha. Ujauzito ulinisumbua sana na hasa kwa vile ulikuwa wa kuficha. Sikujua ningeficha mpaka lini lakini pia sikuwa tayari kuitoa kwa kuhofia kufa na kutenda dhambi ya uuaji wa kiumbe kisicho na hatia. Iloma alisimama nami bega kwa bega huku mara kadhaa akija nyumbani kunipa kampani. Hata yeye hakujua kuwa nilikuwa na ujamzito wa nani.

“ lakini Karen mimba hii ni ya nani?”
“ utamjua tu, kwa sasa yuko nje kibiashara!” nilimjibu kimkato na alikubaliana nami japo kwa shingo upande kwa vile tangu niachane na Kelvin hakuwahi kuniona karibu na mwanaume yeyote.

Siku hiyo nilikuwa ofisini nikimalizia kufunga hesabu za kampuni. Wakati nikiendelea na kazi zangu mlango wa ofisini ulifunguliwa na Jonas akaingia na kuurudishia kisha akasimama mlangoni pale. Kwa vile nilikuwa na kazi nyingi sikuyaondosha macho yangu kwenye kompyuta iliyokuwa mbele yangu zaidi ya kumpa karibu ya mbali mgeni huyo. Baada ya kukamilisha hesabu zangu niliinua uso wangu na kumtazama jonas

“ jonas! Karibu” nilijitutumua kumkaribisha kiti nikichelea kuvuruga taratibu za kazi kwa kuingiza mambo binafsi. Hakujisumbua hata kukitazama kiti zaidi ya kuendelea kunitazama kwa pozi akiwa bado amejisimika pale mlangoni.
“ Karen!” aliniita kwa upole nami sikuitika si kwa kupenda bali kwa kisirani kilichokuwa moyoni mwangu.
“ tunahitaji kumlea mtoto huyo ndani ya ndoa! Tunahitaji kuwa pamoja katika kipindi hiki kigumu”
“ sihitaji msaada wako Jonas!”
“ I’m serious Karen! Nataka kukuoa”
“ what!” nilipayuka kwa sauti bila kutarajia mkono wangu wa kuume ukikimbilia kinywani na kuziba pumzi za mshangao huo wa ghafla..

“ nataka kumpa iloma talaka, sitajali ulimwengu utanihukumu vipi lakini nimetambua nakupenda sana na wewe ndio chaguo langu halisi. Najutia kuchelewa kulitambua hilo lakini sina budi kuwa mkweli mbele za mungu na hata mbele za ulimwengu. Karen, you mean the world to me”

“ sikiliza Jonas! Sijapata kuona mwanaume mpumbavu kama wewe!”
“ Asante mama!” alijibu hali akitabasamu
“ hata kama nitakufa leo hii nakuhakikishia hutanioa! Na tangu sasa…” nilimpa msimamo
“ karen! Kwanini unapigana na hisia zako…unanipenda sawa! Unanipenda Karen lakini hutaki kuwa wazi, just look into my eyes Karen! You love me…you love me Karen!” alinifuata pale mezani. Nikanyuka na kuzunguka upande wa pili nikiwa na nia ya kuuelekea mlango na kumtaka atoke nje lakini hata hivyo aliniwahi na kunivutia kwake kwa nguvu za ajabu.

Mikono yake ilitutumka na kujaa mishipa ya damu, alinibana vema kifuani pake na kuziacha nyuzo zetu zikitazamana. Nilikuwa nahema mithili ya mpiga mbizi ndani ya tope.

Aliiunganisha midomo yetu na kunipa busu moja lililounyong’onyeza mwili wangu! Aliponiachia Jonas aliachia tabasamu, tabasamu lile lile lililokuwa na uwezo na kuiteka akili yangu kwa sekunde tu!

“ fungua kitabu cha moyo wako na usome nini mungu amekuandikia karen! Unajikana mwenyewe kwa kuzikana hisia zako…Karen tunapendana ila tunaogopana kuwa wazi Karen, haitakuwa na maana tukiendelea kuteseka na hisia hizi moyoni!” alizungumza kwa upole nami nikajikuta nazishusha pumzi taratibu na kumtazama Jonas usoni nilikiri kimoyomoyo lakini hali uso ukionyesha utulivu!

“ Karen! Unanipenda?” aliniuliza kwa sauti ndogo ya kubembelezea jibu
“ labda jonas!” nilijikuta nimetamka hilo bila kutarajia. Kwa mara ya kwanza tangu nimfahamu jonas nilimbusu kimahaba kwa hiari yangu, Nilimkumbatia kwa mapenzi yote bila kushurutishwa na kumruhusu anitawale alivyotaka yeye na nilihisi raha ya ajabu kuwa na jonas karibu.

Raha ambayo ilizidi hata kuwa na Kelvin usiku na mchana. Tulipoachiana alinitazama kwa muda kisha akatabasamu na kuniambia “ nimebarikiwa kuwa nawe na nitakuoa tu!” akanikumbatia tena na kunibusu. Aliponiachia nilihisi upweke wa ghafla. Nilitamani aendelee kuwa pale mara zote.

Aliuelekea mlango akaufungua na kusimama kizingitini hali akinitazama katika namna isiyotabirika kabisa. Alirudi ghafla ndani kuja kunikumbatia tena safari hii akilia machozi.
“ Jonas unalia nini?”

“ siamini Karen! Siamini kama umekubali kuwa mke wangu…Karen nakupenda sana mama sana tu” nilitamani kumwambia hata mimi nilikuwa nampenda lakini nilihofu kutamka hilo haraka. Nilitaka kujifikiria mara mbili na sikutaka kuonekana rahisi mno mbele ya Jonas. Aliniachia na sasa akatoka na kuniacha ofisini peke yangu.

Nilijisikia amani na furaha nikisahau kuwa jonas alikuwa mume wa mtu tena mume wa rafiki yangu mpenzi iloma. Nusu saa baadae Jonas alinipigia simu akiwa ofisini kwake.
“ nitakuwa mwanaume mtiifu kwako naahidi…karen unanipenda?” alirudia tena swali lake lakini sikujibu kitu zaidi ya kutabasamu na kuangua cheko simuni
“ nitakujibu leo usiku” nilimwambia kwa upole
“ saa ngapi maana sidhani kama nitalala vema bila kuisikia kauli yako juu yangu”
“ unipigie saa moja usiku na nitakwambia kila kitu”
“ Karen! Wewe ndio ubavu wangu halisi na si Iloma”
“haya kazi njema mpenzi”

“ my god! Unaniitaje! Hebu rudia Karen can’t believe it baby!” aliongea kwa furaha
“ kazi njema mpenzi” nilirudia kusema na wote tulicheka simuni. Baada ya hapo ilikuwa ni ubishani wa nani aanze kukata simu. Ilinibidi nisalimu amri na kukata simu ili niendelee na kazi. Nilipouweka mkonga wa simu chini Iloma alifungua mlango na kuingia ofisini kwangu.

Alishuhudia nikiangua kicheko kirefu cha bashasha.
“ mbona uso umeng’aa na tabasamu vipi kuna mtu kaikuna roho yako nini?”

“ sana tu!” nilimjibu iloma kisha taratibu nikanyanyuka na mafaili yangu na kuelekea ofisini kwa bosi wetu Mr.Tummy nikimuacha iloma ananitazama kwa mshangao wa waziwazi.laiti angejua….

ITAENDELEA....

KUMBE MACHO MAN...MWANAMIELEKA HAYUPO NASI TENA


Kwa wale wapenzi wa mieleka WWE, mwanamieleka mashuhuri Randy Savage a.k.a Macho Man hayupo nasi kufuatia ajali mbaya aliyoipata uko seminole Florida may 20, 2011. inasemekana alipata mshtuko wa moyo wakati akiendesha usafiri wake, hali iliyopelekea kuuvamia mti na kupoteza maisha papo hapo.

Macho Man alikuwa pamoja na mkewe Lynn, wakati ajali hiyo ikitokea lakini mkewe hakuumia sana zaidi ya kupata majeraha kidogo mwilini.

Macho Man atakumbukwa kwa ustadi wake ulingoni na staili yake ya kipekee ya kufunika macho mara zote anapopanda ulingoni au kutokezea katika halaiki...


Akiwa amejitwalia tuzo kadhaa katika medani ya mieleka Macho Man pia alijishughulisha ma muziki, filamu na vipindi kadhaa vya televisheni.

yapo mengi ya kusimulia, vituko ulingoni, kupanda na kushuka kwake na bila kusahau maisha yake binafsi yaliyobeba mikasa mbalimbali ya kusisimua

Macho man amekufa ikiwa ni baada ya siku kumi tu tangu atimize mwaka mmoja wa ndoa yake ya pili. Alizaliwa mnamo November 15, 1952 Columbus, Ohio na kustaafu rasmi mchezo wa mieleka mnamo mwaka 2005.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahala peponi AMEN!

MSEMO WA LEO....

aliyepasua nazi kwa jiwe aligundua

...NAZI HAISHINDANI NA JIWE....

sasa ndio wewe nazi utake kufanya kazi za jiwe utaumbuka!

SIRI YANGU 8...Na Laura Pettie

“ unasemaje Jonas! Ulinibaka ….sikufanya vile kwa hiari yangu yaani pamoja na kuistiri ile aibu leo unaniambiaje?” nilipayuka kwa ghadhabu hali naye akiwa na hasira zake.Ukweli alinitibua hasa!
“mimi ni mume wa mtu Karen!” alinipandishia
“leo ndio mume wa mtu ila siku ile ulikuwa mume wa mbuzi si ndio?” nilimuuliza kwa kejeli.
“kama hutaki kuitoa usinihusishe kwa lolote Karen!”
“sitakuhusisha wewe ila mkeo na viongozi wenzio”
“Shut up! Unadhani ni sifa kuutangaza upuuzi kama huu Karen?”

“ndio unagundua saa hizi kuwa ni upuuzi! Mimba sitoi na kuilea utailea…toka nje upesi shetani mkubwa wewe!” nilimfukuza kwa hasira. Aliuendea mlango na kuufungua kisha akatoka na kuubamiza kwa nguvu. Niliketi chini na kuangua kilio kama mfiwa. Niliomboleza kwa masaa kadhaa pasipo kunyamaza.

Sikujua ningeieleza nini jamii juu ya ujauzito ule. Ningewaeleza nini wazazi wangu na marafiki zangu achilia mbali ndugu na jamaa. Nisingeweza kukiua kiumbe hiki kisicho na hatia. Nililia mpaka usingizi ukanipitia.

Sikuwa na amani moyoni na hasa nilipomtazama Iloma. Nilijitahidi kumkwepa na kukaa mwenyewe nikitafakari hatma yangu. Nyakati zingine niliupitisha usiku huku nikisononeka na kulia, huu ulikuwa ni mtihani mwingine mkubwa kwangu. Siku chache baadae nikiwa katikati ya kazi zangu ofisini. Jonas aliingia ghafla ofisini kwangu. Zilikatika dakika kadhaa tukitazama pasipo kuongea.

“ unataka nini ?” nilimuhoji na kuvunja ukimya
“ Nisamehe Karen! Sikustahili kukujibu vile hata kidogo, nakubali kuilea mimba hiyo kwa moyo mmoja …niliongea yale kwa hasira tu”
“Tafadhali toka ofisini kwangu! Sina haja na msaada wako Jonas, sina shida na wewe…toka nje…tokaaa na tokomee” nilizungumza kwa sauti kiasi Jonas alihisi kama angeendelea kukaa pale si ajabu mambo yangeharibika.

Alitoka nje huku akionekana kusononeka. Nilirudi kuketi mezani pangu huku tayari machozi yakiwa njiani.
Alfajiri ya siku iliyofuata ambayo ilikuwa ni jumapili, niliamka nikiwa sina amani moyoni. Furaha ilikuwa imekimbilia kusikoeleweka. Nilijiandaa kinyonge na kuelekea kanisani. Kila aliyekuwa ananifahamu alinitazama kwa mshangao kidogo.

Uso ulionekana kujaa majonzi ambayo nilishindwa kabisa kuyaficha moyoni mwangu, macho yalikuwa yamejaa mithili ya mtu aliyekesha akitwanga gunia la vitunguu.
Niliingia kanisani na kuketi mbele kabisa wakati mzee wa kanisa alipomkaribisha jonas atoe taarifa ya kamati ya vijana kwa ufupi.

Alinitupia jicho la wizi na kuchapua hatua za haraka haraka kuelekea mbele. Sikummaliza kabisa! Nilihisi hasira hasa nilipokumbuka majibu yake siku ile..
“ bwana yesu asifiwe!” alitamka kwa sauti ndogo iliyokosa uchangamfu
“ Ameeeeeen!” kanisa liliitikia kwa sauti kubwa na furaha kama ilivyokuwa kawaida pale Jonas aliposimama kuongea kila mmoja alimfurahia si tu kwa namna alivyoongea kwa kuvutia bali pia ule muonekano wake wa mtu wa mungu!

“…Kwa baraka zake mwenyezi mungu leo hii tena tumekusanyika hapa katika ibada hii ya kumshukuru mungu. Hatuna budi kumshukuru mungu kwa upendo wake wa ajabu kwetu wanaadamu, Kwa ufupi kamati ya vijana imefanikiwa kukamilisha miradi ifuatayo” alifungua faili lake na kabla ya kutamka chochote alinitupia tena jicho la wizi. Kisha akaendelea

“tumekuwa tukitoa mafunzo ya robo…samahani mafunzo ya kiroho kwa ajili ya vijana wenzetu waliokatika ndoa na hata kwa wale wanaotarajia kufunga ndoa katika juma hili. Kwa hakika tumefanikiwa kwa asilimia sitini…aah! Samahani kwa asilimia tisini kuimarisha roho ya kanisa. Bwana yesu asifiwe sana! Pili ni kwamba mradi wa ukuzaji…samahani usambazaji neno..” alijichanganya kiasi cha kuwafanya waumini watazamane kwa mshangao, haikuwa kawaida kwa Jonas kukosea kosea vile taarifa za kanisa na namna alivyokuwa akiongea kwa sauti ndogo ya kusitasita ndio kabisa kanisa zima ilionekana kumsikiliza kwa mshangao wa waziwazi.

Wakati akiendelea kusoma taarifa hiyo kwa kujikanganya alinishuhudia nikinyanyuka toka pale kitini na kupiga hatua za taratibu kuelekea nje. Asilimia kubwa ya waumini waligeuza shingo zao na kunitazama. Nadhani wengi walitarajia kuniona nikipiga kinanda kanisani na kuimba mara baada ya taarifa ile kama siku zote nifanyavyo.

Nilikuwa mwimbaji mzuri kanisani na wengi walivutiwa na namna nilivyokuwa nikipiga kinanda kanisani na kuimba peke yangu lakini siku hiyo mambo yalikuwa tofauti. sikutaka kabisa kuusikia unafiki wa Jonas mbele ya halaiki ya watu waliofika kuabudu na kumsikiliza yeye kama mtu wa mungu na nilijua fika kuwa ningejichanganya kama Jonas na hivyo kuongeza maswali vichwani mwa watu..

Niliondoka kabisa kanisani na kurudi nyumbani. Niliingia ndani na kujitupa kochini kama gunia la viazi. Pasipo kujielewa nilizama mawazoni na kwa hasira nilizokuwa nazo machozi yaliupamba uso wangu pasi kujitambua akilini.

Wakati wote huo sikuwa nimetazama upande wa pili wa sebule hii ambako mama alikuwa ameketi akinitazama. Nilishtuliwa na sauti ya mama iliyonitoa kabisa mawazoni

“ na sasa unajichongea kaburi Karen, alikupa mapenzi gani mwanangu mpaka ushindwe kumsahau kabisa akilini mwako?...tazama! umekonda Karen uso umechujuka kwa mawazo na umeshindwa kusali sababu ya Kelvin, Kelvin ni nani hata akuharibu hivi mwanangu kwanini hutaki kuukubali ukweli kuwa amekuacha na hutampata tena?” mama alinifokea bila kujali kuwa hatukuwa tumeonana kwa takribani mwezi mzima na wala hatukuwa tumesalimiana.

ITAENDELEA.....

WANAWAKE NA CHUKI....

...Imekuwa kama hulka wanawake kuchukiana migongoni na kuchekeana usoni, hulka hii si kwa wanawake wa kitanzania pekee ila acha niwaguse watanzania wenzangu...

chuki miongoni mwetu imekuwa kama fasheni, mwanamke mwenzetu asifanikiwe, matumbo yanajaa gesi kwa wivu, mwanamke mwenzio akipata matatizo roho inakukwatuka kwa furaha...hiki ni nini jamani?

wanawake wakikaa zaidi ya watatu hawakosi kuyasema mabaya ya mwenzao wa nne, kwani mazuri yake hamyaoni?...chuki nyingine kujiletea kadhia zisizo na msingi. mpende mwanamke mwenzio toka moyoni hupungukiwi kitu mwenzangu.

katika mahusiano ndio balaa, wasisikie mwenzao kwake kunaungua moto, watatamani wafanye hata sherehe, na kama ndio hawasikii ngumi wala makonzi baaasi watatafuta kila njia watakalo litimie na ajabu ya Musa kwa ya firauni wanaokufanyia hivyo ni watu wako wa karibu wanaokujua ndani nje!

usipige hatua moja ya maendeleo, wenye kununa watanuna, wenye kuzusha watazusha ili mradi hakuna jema wanalotaka likufike

tujirekebishe...chuki zako zazidi kumpa baraka mwenzako...apangalo mola huwa hata ukichelewesha miaka kumi lililoandikwa limeshaandikwa... hivyo husda na vijicho na masengenyo juu ya mwenzako ni kupoteza muda wako ambao ungeutumia nawe kutafuta maendeleo yako!

...ni hayo tu! panapo majaaliwa... tuzidi kuombeana kheri

Monday, May 23, 2011

MSEMO WA LEO....

Wenyewe tunawaita wahenga sijui yapi yaliwakuta wakaamua kujipa moyo kuwa

... BANIANI MBAYA KIATU CHAKE DAWA...

haya jembe hilo mwanakwetu ukiamua kulima au kupalilia au hata kuchimbia shimo kazi ni kwako hahahaaaa!

Laura and ma galfriend Zuhura...after kupanga tukaamua kupumzika hapa pamoja!

SIRI YANGU 7......Na Laura Pettie

Muda wote huo nilikuwa nimeshastahimili ile harufu mbaya niliyokuwa ninaisikia na sasa nilishanza kuhisi kichefuchefu! Nikaona nisipoaga mapema nitaweza kutapika mbele ya wenyeji wangu!

Binafsi nilihisi kuna kinyesi cha mtoto kimesahaulika pale ukumbini au choo cha mle ndani hakikuwa safi! Nikashindwa kuelewa kama iloma hakuwa akikerwa na ile harufu au ndio pua zimeshajizoelea kuvuta uvundo wa aina ile!

Niliondoka kwa iloma na kurejea nyumbani. Niliingia nyumbani huku tayari giza likiwalimeshatanda. Ilikuwa saa mbili na robo. Nilimkuta dada yangu Debby akiwa ananingoja wimawima ukumbini hali mama akiwa amelala sofani akitazama televisheni. Niliwasabahi akaitikia mama peke yake. Nikajiweka sawa!
“ Karen! Hivi ni nini kinaivuruga akili yako we mtoto?”
“hata salamu Debby?” nilimkatiza
“Najua u mzima wa afya, lakini huku unakoelekea nadhani utakuwa na matatizo katika akili yako”
Nilishusha pumzi fupi ya kero, nikamtaza Debby kwa hasira .
“ Debby! kaka brian alichanifokea sana asubuhi hivyo inatosha, hakuna mtu anayehoji kilichonikuta, hakuna mtu anayehoji sababu za msingi nilizonazo wote mnaniona hayawani tu! Kama ni kustarehe basi ningeanza siku nyingi na si leo hii nikiwa na kazi na maisha yangu” nilikuja juu na tayari machozi yalisha tengeneza mfereji mashavuni mwangu. Niliwaza juu ya kubakwa kwangu na kulinganisha na lawama ninazopewa nikaona uonevu mkubwa juu yangu!
“ Okey! Nini kilichokufanya ulale nje jana?...brian amenipigia simu akanieleza kuwa umerejea asubuhi ya leo na tena ulilala nje bila hata taarifa kwa mama” Debby sasa alihoji taratibu na kuketi kochini
“ haitabadili akili ya mtu kati yenu! Endeleeni kuniona punguani!” nilimjibu kwa mkato na kutokomea chumbani. Nikajifungia na kuanza kulia. Nililia muda mrefu na hatimaye nikapitiwa na usingizi. Hata mama aliponigongea sikutaka kumfungulia kabisa. Nikalala na njaa mpaka asubuhi.

Asubuhi na mapema niliamkia kujiandaa. Wakati nikijishughulisha kwa hili na lile simu yangu ya mkononi iliita na haraka nikaipokea pasipo hata kuangalia jina la mpigaji. Moyo ukapiga paa! Ilikuwa ni sauti ya Jonas

“ Nimeshindwa kulala kwa amani Karen!...nakupenda sana, sijui niseme nini unielewe Mpenzi…” sikumpa nafasi ya kuendelea kuongea upuuzi wake. Nilikata simu na kuirushia kitandani.

Nilihisi kubanwa na binadamu huyu aliyekuja ghafla katika maisha yangu. Nikatamani kumweleza Iloma ukweli wa kile alichonifanyia mumewe lakini pia sikuwa na ushahidi wa kutosha kumtia hatiani!

Wiki hiyo nzima sikuwa na amani moyoni. Ijapokuwa mama alijitahidi sana kuniweka sawa lakini akili yangu ilikuwa bado inazungukwa na mambo mengi.

Siku hiyo kama kawaida ya jumamosi zingine niliamka mapema na kufanya usafi wa nyumba pamoja na kufua. Mida ya saa nne Iloma alinipigia simu na kuniambia kuwa alikuwa njiani kuja kwangu. Nilimalizia kazi zangu haraka na kujiweka tayari kumngoja iloma.

Sikuwa na shaka kwa vile ilikuwa kawaida yake kunitembelea nyumbani. Saa nne juu ya alama iloma aliingia nyumbani, alionekana mchangamfu na mwenye furaha. Mara baada ya kusabahiana na utani wa hapa pale kupita tuliketi barazani na yeye akawa ananisaidia kumenya baadhi ya viungo vya kupikia.

“…angalau sasa Jonas ametulia Karen” aliniambia kwa bashasha
“ matatizo ni sehemu ya uhusiano” nilimjibu kimkato huku nikishusha pumzi. Masikini Iloma hakujua kuwa katika kipindi hicho Jonas alikuwa akinipigia simu kila usiku kunibembeleza niwe mpenzi wake kwa siri. Nilikuwa nikijitahidi kwa kadri nilivyoweza kumkwepa Jonas!
“ umenisaidia sana Karen nadhani napaswa kukuombea upate mume bora kabisa!”
“ dua imefika…vipi Kim anaendeleaje?” nilibadili mada ili kukwepa kuongelea zaidi masuala ya ndoa.
“alikuwa na anaharisha sana wiki iliyopita lakini sasa hali yake nzuri kiasi” Iloma alitamka taratibu hali akiendelea kumenya vutunguu swaumu vilivyokuwa ndani ya ungo. Nilipepesuka kidogo na haraka nikajishikiza kwenye sinki lililokuwa kando yetu.
“Karen nini?” iloma aliuliza kwa hamaki akiweka ungo chini na kuja kunishikilia
“najisikia vibaya Ilomaa…mama nakufa!” nilipiga ukelele hafifu kabla ya kuanza kuona kizunguzungu, nikajikuta nakosa nguvu. Nilifumba macho na kuyafumbua taratibu lakini uwezo wa kuona ukatoweka ghafla sikuelewa kilichoendelea.

Nilipokuja kuzinduka nilijikuta juu ya kitanda cha hospitali. Niliangaza huku na kule pasipo kumuona yeyote. Nikajituliza tuli hali akili ikianza kutafakari kilichonikuta.

Wakati nikiwaza hili na lile mlango wa wodi ulifunguliwa na kijana mmoja aliyevalia mavazi ya kitabibu aliingia akiwa na faili mkononi. Taratibu nikaiweka shingoyangu sawia na kumkodolea macho yule kijana. Nikatunduwaa alikuwa Kelvin Nashon! Mchumba wangu aliyeniacha nikiuguza madonda ya roho!

“ unaendeleaje Karen!” alinihoji taratibu kwa sauti yake ile ile ya upole iliyojaa kila aina ya ukarimu. Sikumudu kufungua mdomo na kujibu kitu. Nadhani akili ilichanja mbuga na kukiacha kichwa kikiwa kitupu mithili ya mtungi uliotoboka! Macho yalitanuka zaidi na nikawa ninamtazama mwanaume huyu aliyekuwa mbele yangu kama kiumbe cha ajabu toka sayari nyingine.

Nilihisi mkuki moyoni, machozi ya hasira ya kuachwa solemba, machozi ya hasira ya kusalitiwa yalitanda katika mboni za macho yangu na kufanya macho yametemete mithili ya mbalamwezi!

“ ondoka…go away kelvin!” nilimudu kutamka maneno hayo kwa sauti ya kitetemeshi kabla ya kukabiliana na kwikwi nilizoshindwa kuzivumilia, nikaangua kilio cha kugugumia. Sikujali kuwa alikuwa pale kunisaidia kama daktari na wala si kama Kevin Nashon.

“ weka hasira kando Karen… unahitaji kusaidiwa kama mgonjwa” Kelvin alinisemesha taratibu hali akijivuta na kusogea karibu zaidi na pale nilipokuwa nimelala. Nilihisi kuumia kana kwamba nilikuwa nimeachwa jana tu!

“ sitaki Kelvin! Kama ni kufa acha nife Kelvin ungekuwa nia ya kunisaidia usingenitendea vile… ni msaada gani ulio nao wewe… msaada gani Kelvin, wewe! Wewe una msaada gani kwangu?” nilimpayukia kwa hasira tayari nikiwa nimeshaketi kitandani na kumtazama vema Kelvin. Alikiinamisha kichwa chake chini kwa sekunde kadhaa kisha kama ilivyoada yake aliachia tabasamu lake tulivu.

“ Karen! Hayo ni masuala binafsi na hapa niko kazini” alijaribu kunituliza lakini kinyume chake aliwasha moto nyikani. Niliteremka toka pale kitandani huku nikipepesuka na kuangaza huku kule kuangalia kama kuna kitu changu. Nilipotaka kupiga hatua nilihisi uzito kichwani nikayumba na kutaka kudondoka. Kelvin akaniwahi na kunidaka haraka.

“ niache, usiniguse Kelvin…” nikamkemea na kujitoa mikononi mwake huku nikiwa nimejiegemeza kitandani nilimtazama kwa chuki kiasi ambacho hata yeye Kelvin alishindwa kuamua la kufanya juu yangu.

Alionekana wazi kutafuta maneno yatakayotosheleza kuelezea huruma yake kwangu. Akakosa!
“ Karen!...karen” aliniita kwa upole
“ sitaki kusikia na…” sikumalizia kauli yangu kwa vile mlango ulifunguliwa na mama pamoja na Iloma wakaingia. Mama alikuja mbio kunikumbatia.
“ooh! Karen unajisikiaje?” mama alinihoji nami sikushughulika kusikiliza
“ Iloma sitaki kulala hapa ni bora mkinihamishia hospitali nyingine”nilipayuka kwa hasira
“ kwanini?” mama alihoji haraka akiwa amekumbwa na mshangao
“ Iloma umenielewa?” nilisisitiza bila kujali swali la mama
“ lakini Karen …”alitaka kupingama nami
“ hakuna cha lakini kama hakuna kati yenu mwenye uwezo wa kunitoa hapa mpigieni baba yangu simu aje ama kaka yangu Brian” nilizidi kuja juu mno. Mama akamtazama Iloma na kumwambia
“ nenda kalipie kule mapokezi na tumpeleke Marie stopes sasa hivi” alichomoa pochi yake na kutoa pesa alizomkabidhi Iloma. Kabla hata Iloma hajapangua hatua moja Kelvin alimuwahi na kumzuia mlangoni.
“ nitalipia mimi acha tu!”
“ Sina haja na msaada wako Kelvin si umetoka kuniambia sasa hivi kuwa uko kazini na sasa unataka kuyalipia matibabu yangu kama nani?” nilimtupia swali la kebehi lililomfanya Kelvin anitazame kwa mshangao wa waziwazi.
“ sikudhani kuwa ungebeba kisirani kama hiki Karen!” aliniambia kwa sauti ya upole nami nikaangusha cheko fupi la dharau na kumwambia “ sikudhani kuwa ungekuwa mkarimu kiasi hiki Kelvin!” .

Akabaki kunitazama tu asijue aongee nini mbele yangu. Nadhani pia aligundua ni kiasi gani nilikuwa na majibu ya ovyo. Mama alinitoa nje huku akiwa amenishikilia na tukaelekea mapokezi nilikomkuta dada yangu Debby. Moja kwa moja walinipeleka hospitali ya maries topes mwenge.

Daktari aliniambia nilikuwa na malaria pamoja na upungufu kiasi wa damu. Nililala hospitalini pale kwa siku moja na kutoka jioni. Mwezi mmoja baadae hali yangu ilitengamaa lakini nilianza kupata dalili Fulani ambazo zilinipa mashaka. Mwezi wa pili dalili hizo zilionekana wazi nami nikaanza kuhisi kitu kisicho cha kawaida katika mwili wangu.

Ijumaa moja tulivu niliamua kwenda hospitali kupata uhakika wa hisia zangu. Nilichohisi kilikuwa kweli kabisa. Nilikuwa na mimba changa! Pamoja na daktari kunithibitishia kwa vipimo lakini bado sikuamini.

Mimba! Kwa asilimia mia moja na pengine na moja ya ziada mimba hii ilikuwa ya Jonas! Shemeji yangu, mume wa rafiki yangu mpenzi Iloma.
“Dokta una hakika na majibu yako?” nilimuuliza Daktari kwa wasiwasi
“ Huniamini?” naye alinirudishia swali huku akinipatia karatasi iliyokuwa na majibu toka maabara. Niliikodolea macho mara mbilimbili nikitamani majibu yasomeke visivyo. Nikairudisha mezani na kusimama.
“inaonekana hukuitarajia kabisa eeh!...” dokta alinisemesha lakini hakuwa katika mawazo yangu. Nikazidi kuchanganyikiwa nisijue hata nianzie wapi kutatua tatizo hili. Nadhani nilitoka katika chumba cha daktari pasipo hata kumuaga. Nilikatiza kordo mbili tatu na kutokezea mapokezi. Niliketi katika benchi moja lililokuwa kando huku akili ikinizunguka isivyo kawaida “ nitafanyaje sasa?” nilijiuliza kwa sauti bila kujali kama kulikuwa na mtu wa kunipatia jibu la swali hilo.

Nilifikiria kuitoa kwa siri lakini nikaona bora kumshirikisha Jonas ili nijue yeye ana mawazo gani juu ya tatizo hili. Nilikosa raha kabisa, nilikosa amani moyoni kiasi kwamba hata wale walionizoea hawa kuacha kunighasi kwa maswali ya kutaka kujua kilichonisibu.

Haya yalikuwa maji ya shingo na kwa hakika nilimlaani Jonas kwa lugha zote! Baada ya kufikiria sana nilimpigia jonas simu na kutaka kukutana naye nyumbani kwetu kwa vile kwa wakati huo mama alikuwa amemfuata baba Nairobi. Jioni ya siku hiyo Jonas aliwasili nyumbani na baada kupata viburudisha koo, niliamua kumpasulia jonas ukweli.

Alitunduwaa kwa sekunde kadhaa huku macho yakiwa yamemtoka mithili ya mjusi aliyebanwa na mlango. Jasho lisilo rasmi lilimbubujika mwanaume wa watu hali kiyoyozi kilikuwa kikitimiza wajibu wake ipasavyo. Midomo yake ilimwemweseka pasipo kutoa neno lolote. Nilimtazama kwa sekunde kadhaa kisha taratibu nilijitoa kochini na kusimama mbele yake.

“ najua lawama hazijengi jonas lakini huu mzigo si wangu peke yangu!” nikauvunja ukimya uliotutembelea ghafla.

“ hakuna njia Karen inabidi uitoe…mimi ni shemasi Karen, mimi ni kiongozi ndani ya kamati ya vijana kanisani…mimi ni mume wa mtu…unadhani nitasimamaje endapo suala hili litajulikana?” alijitutumua kujibu katika namna ya kupayuka na kuhamanika. Eti kwa wakati huo ndio alikumbuka nyadhifa zake kanisani na kuwa yeye ni mume wa mtu.
“ ungeyafahamu hayo mapema usingenitendea unyama ule jonas na tena nataka ufahamu kuwa mimba hii siitoi ng’o! kuzini uzini na kabla hujajua hata adhabu ya uzinzi unataka ujiongezee dhambi ya kuua, utamjibu nini muumba?”

“ itakuwa juu yako Karen siwezi kuhatarisha ndoa yangu sababu yako!” alinijia juu akizidi kuhamanika vibaya mbele yangu, akinitazama kwa chuki ilichonganyikana na hali ya kutoamini...sikutarajia hali ile na sikutegemea jonas angebadilika vile, nilichoka mara mbili ya mwanzo!


ITAENDELEA.....

SIRI YANGU 6.....Na Laura Pettie

..... “ wewe unashtuka hivi Karen unadhani mimi nilishtuka kiasi gani?”
“ No! unajua… sasa…kwani rafiki yako huyo anamfahamu huyo mwanamke?” nilimtupia swali huku maneno yakigongana gongana na kama Iloma angekuwa makini angehisi kitu katika kauli yangu.
“ anasema hamfahamu lakini kama atakwenda naye tena hapo hotelini basi atammaki sura vizuri”
“ lakini usipende kusikiliza maneno ya watu Iloma”
“ hawezi kunidanganya, jonas amebadilika mno tabia sijui nimfanyeje jamani”
nilishusha pumzi na kutafuta haraka cha kusema nikakosa!
“ naomba leo uje uongee naye mbele yangu nyumbani wewe anakuheshimu na nadhani itasaidia kidogo” iloma alitamka taratibu bila kujua kuwa alikuwa ananiweka katika mtihani mkubwa mno.
“ lakini Iloma kwanini usilipeleke swali hili kwa mshenga wenu?”
“ nitakwenda kama ushauri wako kwake hautasaidia Karen”
nikakwama kabisa. Nilitumbua macho tu nikiwa sinahata la kusema. Nikarejea kitini pangu na kujitupa kwa nguvu.
“ nitajaribu!” nilimpa jibu fupi na tabasamu likachanua usoni pake.
“ nadhani leo baada ya kazi twende wote nyumbani kwangu”
“ hapana shaka!” alisimama na kuja kunikumbatia pale nilipokuwa nimeketi kisha akatoka na kwenda kuendelea na kazi zake.

Alizidi kunichanganya mno. Sikujua ningeongea nini na jonas na wala sikujua usiku wa siku hiyo ningeongea nini mama juu ya inshu ile ya mimi kulala nje bila taarifa.

Niliinamisha kichwa changu mezani na kutafakari moja baada ya jingine pasipo hata kufikia muafaka wa kile nilichokuwa ninawaza. Wakati wa chakula cha mchana nilijiweka ‘busy’ sana ili kukwepa kuwa karibu na Iloma na hivyo sikutoka ofisini. Wakati nikiendelea na kazi simu yangu ya mkononi iliita na mpigaji alikuwa Jonas.

Mapigo ya moyo yalibadili kasi kiasi nikahisi joto la ghafla likiuvaa mwili wangu. Simu iliendelea kuita kwa muda na hatimaye ikakatika yenyewe. Dakika tatu mbele jonas alipiga tena safari hii niliikata na kuzima simu kabisa bila kujali watu wengine muhimu ambao wangenitafuta kwa shida za maana.


Jioni ya siku hiyo tuliondoka wote na Iloma na kuelekea kwake. Siku hiyo iloma alikuja na gari lake ambalo hakuwa akilitumia kwa muda mrefu baada ya kupata ajali. Tuliwahi kufika kwake mapema tu na kwa hakika nilianza kustaajabia mazingira ya nyumba hii ya rafiki yangu Iloma. Ilikuwa imepita muda mrefu tangu nimtembelee kwake kwa mara ya mwisho alipojifungua mtoto wake Kim.

Mara baada ya kukaribishwa ndani nilikumbana na harufu moja mbaya niliyoshindwa kuitabiria ni harufu ya nini. Sebule yake yenye makochi mazito ya kisasa yalikuwa shangala baghala huku baadhi yakionekana kuwa na alama za mikojo ya mtoto! Vitabu na magazeti vilisambaa kila kona na kufuta kabisa mandhari tulivu ya nyumba hii.

Nepi kadhaa zenye kinyesi zilikuwa zimetelekezwa chini na kim mwenyewe alikuwa ameketishwa kwenye kapeti akiwa amevalishwa fulana bila hata nguo ya ndani. Uso mng’aavu wa kim wenye kulandana vema na baba ulikuwa umetapakaa uji uliokauka na kwa hakika fulana aliyokuwa amevaa ilitia kinyaa! Bakuli lenye uji wa mtoto lilikuwa limetelekezwa chini karibu na mlango huku inzi wakilizengea.

Nilichagua sofa moja na kuketi wakati Iloma alijitoma ndani na kuniacha nikikagua mazingira ya jumba lile ambalo kwa hakika lilitakiwa kuwa katika usafi wa hali ya juu. Nilihofia kumpakata hata Kim kwa kuhofia kuchafuliwa na haja kwa vile hakuvalishwa chochote na hivyo kuishia kumpungia mikono na kumsemesha kwa hili na lile.

Dakika chache baadae Iloma alirejea ukumbini akiwa amevalia fulana moja nyeupe na kujifunga khanga kiunoni.

Nilimshangaa zaidi! fulana hiyo sikuelewa kama ilikuwa chafu au rangi yake ndio ilikuwa imefubaa hali kadhalika khanga aliyokuwa ameivaa haikumstahili mwanamke kama yeye tena mke wa mwanaume mtanashati kama Jonas! Hapo ndipo nipoanza kuhisi sababu za Jonas kusaka mwanamke mwingine.
“ Lawama! Wee’ lawama!” alimuita mtumishi wake wa ndani. Pengine nikitegemea kutokea kwa msichana mwenye umri wa kati ikawa sivyo. Msichana mdogo mwenye umri kati ya miaka kumi ama kumi na mbili alikuja mbio pale sebuleni na kusimama mbele yetu. Akapiga goti na kunisalimu. Nikaitikia hali nikimtumbulia macho si tu ya mshangao wa namna alivyokuwa mchafu toka utosini mpaka nyayoni bali pia kwa ule udogo wake! Lawama alimchukua mtoto na kutokomea nae jikoni, nikamgeukia Iloma
“ anaweza nini huyu Iloma?” nilimuuliza kwa hamaki
“ ni bora huyu kuliko kuleta wasichana waliopevuka humu ndani” alinijibu kwa kujiamini kabisa
“ hofu ya nini! humuamini Jonas kiasi cha kuhatarisha maisha ya mtoto wako kwa kuajiri mtoto kama huyu asiye jua hata kuoga!!!” nilishindwa kumuelewa
“ Karen! Mwanaume si mtu wa kumuamini asilimia mia moja! Ni bora kitoto hicho kisichojua kuoga angalau utaishi kwa amani, nashukuru anajua vikazi vidogo vidogo!”
“ sikubaliani nawe Iloma!” nilizidi kuhamaki
“ hutakubaliana nami kwa vile hujui hali halisi.” Alinipa jibu lililonifunga mdomo
ukimya ukapita kati yetu na Lawama akarejea pale ukumbini akiwa na chano chenye glasi ya juisi. Alipoitua ile juisi mezani niliitazama vema ile glasi na kushuhudia madoa ya uchafu yakiwa yameipamba glasi ile hali chano ile iliyobeba glasi ikiwa na nyufa. Sikujisikia kunywa tena ile juisi lakini pia sikutaka kumuonyesha wazi Iloma kuwa glasi yake ilikuwa na kasoro. Nikaamua kuinywa hali nikimuomba mungu aniepushe na maradhi ya tumbo!

Wakati tukiongea hili na lile, honi ilisikika nje na nikajua kuwa Jonas alikuwa amewasili. Punde aliingia ndani na kutukuta pale sofani. Akajenga tabasamu kama ilivyo ada yake na kuja kunisalimu. Hatukutazamana hata machoni kwani nilikiondosha haraka kiganja cha mkono wangu na kujifanya kutafuta kitu katika pochi yangu. Iloma ambaye hakujishughulisha hata kumpokea mumewe aliyeishia chumbani alipaza sauti na kumuita lawama. Mtoto yule akaja tena mbio na kupiga goti mbele yake.

“ una masikio magumu sana Lawama! Nikueleze mara ngapi kuwa baba akija umpokee hiyo briefcase yake na kim ameshaoga?” akamuhoji
“ bado mama!” akajibu haraka lawama hali akijivuta nyuma pengine kujiweka mbali na dhoruba ya kofi kama lingemkumba
“… unataka sasa nitumie fimbo kukukumbusha kila kitu eeeh! Haya upesi potea” akamfukuza Lawama.
Jonas aliporejea sebuleni aliketi sofani na kwa sekunde kadhaa alionekana kuanza kukerwa na harufu ile iliyokuwa kero kwangu pia.
“Mama Kim kuna nini kimeoza humu ndani?” Jonas alimuuliza mkewe
“ Labda ni hizo nepi za mtoto hapo chini” alimuonesha mumewe beseni dogo lililokuwa na nepi chafu kwenye kona ya kuelekea kordoni.
“ sasa huoni kuwa ni kero kwa hii harufu, hebu ziondoe upesi” Jonas alimkaripia Iloma ambaye wala hakujishughulisha kuzitoa zaidi ya kumuita Lawama kwa sauti na alipokuja alimuagiza kutoa zile nepi hali zingine alizichukua chini kando ya sofa. Licha ya nepi zile kuondoshwa lakini bado harufu iliendelea kutawala.
Jioni ya siku hiyo tuliongea mengi na Jonas. Nilijitutumua kumuhoji Jonas sababu za yeye kumfanyia yote yale mkewe ambaye naye alikuwa kando yangu akisapoti maneno yangu.
Jonas hakuongea kitu zaidi ya kunitazama kwa chati na kutikisa kichwa kuonyesha kunielewa pale nilipompa ushauri wa kuwa wazi kwa mkewe na kujaribu kurekebishana pale anapoona tofauti!
Alimtaka radhi mkewe na nikajiona kama mtu aliyetua mzigo mzito baada ya kuongea hayo.

ITAENDELEA....

Saturday, May 7, 2011

MSEMO WA LEO....



...katika kuienzi laugha yangu ka kiswahili nimeona niwe natoa misemo mbali mbali ya lugha ya kiswahili hata wewe mdau unaweza kunitupia msemo wako kupitia email ya. queenlauryn5@yahoo.com nami nikautupia humu.... haya msemo wa leo unasema

...Hubebeki kama chungu cha moto!...

eeeh ndugu yangu ukibebwa bebeka, sio tena umfanye mbebaji akubebe huku ananung'unika! binadamu unasaidiwa katika hili nawe badala ya kuonyesha shukrani ndio kama vile huo msaada unaukatia risiti, utataka utendewe vile unavyotaka wewe wakati yote ni hiyari ya mtenda!

ALAMSIKI

SIRI YANGU 5..... na Laura Pettie

“ sikuelewi jonas… hivi…ina maana …my god!” niliwaya waya tu pasipo kujua la kusema

“ Karen huelewi nini hapo nina maanisha kile nilichokisema”

“ hauko makini na akili zako Jonas! nilikuheshimu sana na sikutarajia kusikia upuuzi kama huu toka kwako na kumbe ndio maana Iloma hana amani moyoni mwake…. sikutarajia ungelikuwa mpumbavu kiasi hiki Jonas. Umenivunjia heshima na umemvunjia Iloma heshima yake”

nilinyanyuka na kujiandaa kuondoka lakini sikumudu hata kupiga hatua moja Jonas aliudaka mkono wangu na kuungandamiza mezani. Nilimtazama tu pasipo hata kumkemea. Mboni za macho yake zilimeremeta na kuyaonyesha dhahiri malengelenge ya machozi yaliyotuama machoni pake.

“ kwanini unanifanyia hivi Karen, kwa vile umegundua kuwa nakupemda sana”
“ sihitaji kusikia upuuzi wako Jonas” nilimfokea
“ narudia kile nilichokisema Karen nakupenda sana na hilo nililitambua siku nyingi Karen, nimekuwa nikihangaika na kuteseka sana juu yako lakini hutaki kuzielewa hisia zangu! Hutaki kunipa nafasi ya kukuonyesha namna ninavyokupenda Karen” machozi yaliteremka taratibu mashavuni pake.

Nikahisi kumuonea huruma Jonas. Kwa namna alivyokuwa akilia nilihisi imani lakini alikuwa mume wa mtu tena mume wa rafiki yangu mpenzi.

“ na Iloma je?... anayonafasi katika maisha yako Jonas” nilirejea kuketi pale kitini na kuuondoa mkono wangu katika kiganja cha mkono wake wa kuume.

“ hilo nalitambua lakini nafasi iliyo ya kipekee ni ile ninayotaka kukupa wewe Karen. Unaisumbua nafsi yangu mno na kama si Iloma kubeba mimba yangu kabla ya ndoa Karen ningekuoa wewe”

Nilishusha pumzi ndefu na kumtazama mwanaume huyu kwa mshangao mkubwa.

“ siwezi kumsaliti Iloma siwezi Jonas nataka ufahamu hilo na…” simu yangu ya mkononi iliita na mpigaji alikuwa mama.

Nilinyanyuka haraka na kwenda kuipokelea kando. Mama alikuwa anataka kujua mahali nilipo kwani muda wa mimi kuwa nyumbani kama kawaida ulikuwa umeshawadia na ikizingatia alikuwa mgonjwa.

Nilimwambia mama avute subira kwani ningekuwa nyumbani muda mfupi baadae. Niliporudi mezani niliimalizia juisi yangu na kumwambia Jonas kuwa nahitajika nyumbani haraka.

Nilikurupuka asubuhi ya saa moja nikiwa mahali ambapo ilinichukua dakika kadhaa kupatambua. Yalikuwa ni mazingira mapya kabisa tofauti na yale niliyoyazoea.
Niliangaza huku na kule pasipo kupatambua mahali pale na hali mwili mzima na hasa kichwa kikiwa na uzito wa ajabu.

Nikiwa ndani ya tafakari hizo mlango wa chumba nilichokuwamo ulifunguliwa na Jonas akaingia akiwa na sinia lililokuwa na staftaha. Niliduwaa!

“Jonas!...umenifanyia nini hiki…mungu wangu…Jonas…nitasema nini …hapa ni wapi sasa?” nilishindwa hata kuzipangilia sentesi zangu katika mpangilio unaoeleweka.

Akili ilianza kufanya kazi na mara moja nilitambua kuwa nilikuwa katika moja ya vyumba vya hoteli ya Lightness.

ITAENDELEA....

Friday, May 6, 2011

SIRI YANGU 4....Laura Pettie

Niliduwaa tu na barua ile mkononi. Nikairudisha bahashani na kuanza kutafakari ujumbe ule. Jonas alikuwa akinitafutia nini mimi au naye alikuwa akimuhisi vibaya iloma na ndio alikuwa anataka anitumie mimi kama mpelelezi. Kwa hakika sikuwaelewa wanandoa hawa hata chembe. Sikuendelea na kazi tena.

Nilitoka na kumpitia Iloma kwa ajili ya kwenda kupata chakula cha mchana. Tuliingia mgahawani city garden na kuchagua mahali pazuri na kuketi. Tuliagiza chakula na ndipo Iloma alipoanza kunisimulia mambo mbalimbali ya Jonas. Alinieleza kuwa Jonas hakuwa akila chakula cha nyumbani pale kwa muda mrefu sasa.
`
Mara nyingi alisingizia kuwa alishakula hotelini na kama haitoshi hata chai Jonas hakunywa nyumbani kwake. Iloma alizidi kunilalamikia kuwa mumewe huyo alionesha wazi kuwa alikuwa amemchoka kwa namna Fulani na yeye hakumvutia tena kwani hata katika hafla mbalimbali Jonas hakutaka kuongozana na mkewe, Alinilalamikia vitu vingi ambavyo vilinifanya nianze kumuona jonas katika muonekano mpya wa mwanaume wa ajabu na mnafiki.

“ nimebadilika nini Karen hata Jonas anione sifai tena jamani” Iloma aliniuliza swali ambalo nililikwepa kwa vile ukweli ni kuwa Iloma alikuwa amebadilika mno kimaumbile na pia kitabia tangu amzae mtoto wake wa kwanza kim. Alikuwa ameongezeka mno na kupata umbile jipya lisilo la kuvutia. Urembo wake uliisha kwani sasa hata nywele zake zilichanwa katika mtindo wa kifagio kila siku na hakujiremba kabisa. Na kama haitoshi hakuvalia kinadhifu kama ilivyokuwa zamani na hivyo kupoteza kabisa mvuto aliokuwa nao.

Niliogopa kumwambia kuwa hakuwa akivutia lakini pia nilijua kuwa Jonas hakustahili kumtendea mkewe mambo ya ajabu eti kwa vile tu hakuvutia tena. Nilipanga akilini kumwambia jonas ajirekebishe katika makutano yetu ya jioni hiyo.

Iloma alikoseshwa raha na tabia za jonas, aliendelea kunilalamikia juu ya Jonas.
“ Karen hata chai!... Chai tu ushindwe kunywa nyumbani kwako hebu niambie anamaanisha nini sasa”
“ kwa kweli sijui nini kimemsibu shemeji, hata hivyo inawapasa kuketi chini na kurekebishana Iloma”
“ wapi! Nimrekebishe Jonas wapi Karen! Nianze kumlazimisha kunywa chai nyumbani kwa fimbo?”
niliangua kicheko kifupi kwa majibu ya Iloma ambaye aliendelea kukiweka akiba kicheko chake, alinitazama bila hata tabasamu na kushuhudia nafsi yake ikipigana na uchungu aliokuwa nao. Machozi yalimlengalenga na haraka aliyafuta na kitambaa chake cha mkononi na kuniambia kwa sauti ya kulalamika

“ Bado mapema mno kufikiria talaka, mtoto wetu ndio kwanza ana mwaka sasa na yeye ameshaanza vituko nitamvumilia mpaka lini na kama haitoshi karen Jonas sasa anarejea nyumbani usiku wa manane kila siku hata kama ni biashara Karen biashara ya saa nane za usiku, biashara gani hizo jamani!”
nilishusha pumzi ya nguvu. Nilipata faraja ya kusikia haya kwa namna moja nilianza kumshukuru mungu kwa kumuweka mbali Kelvin kwa vile pengine tungeoana naye angeniumiza hivi kila uchao.
Nilimfariji na kumpa maneno ya matumaini ya kumbadili Jonas. Angalau aliachia tabasamu na kuipa nafasi roho yake iliyokuwa imesongwa na mawazo mengi mno. Tuliondoka pale mgahawani mara baada ya kumaliza chakula na kurudi ofisini. Niliendelea na kazi zangu huku nikiwa na mawazo mengi lakini pia nilikuwa na hamu ya kuongea na Jonas ili nimsikie naye alikuwa na yapi juu ya Iloma. Sikutaka kuhukumu upande mmoja tu!
Jioni ya saa kumi na moja na nusu nilimaliza kazi zangu na kufunga ofisi. Nilipita ofisini kwa Iloma na kumkuta akimalizia kutunza nyaraka mbalimbali za mle ofisini. Kichwani nilikuwa ninatafuta njia ya kumkimbia Iloma na kwenda kukutana na mumewe. Nilihofu kuwa angeweza kuhisi vibaya endapo ningemweleza ukweli wa kule niendako lakini pia Jonas alikuwa ameniasa kumkwepa Iloma. Binafsi yangu nilihisi msuto ukipita nafsini mwangu kwa kuona kuwa kukutana na Jonas bila idhini ya Iloma lilikuwa ni kosa kubwa.
“ Iloma acha mimi nitangulie kaka yangu Brian alisema atanipitia pale kituoni ili twende wote mahali”
“ oh! Itakuwa vema mkinipa lifti pia si unajua pale posta usafiri ulivyo wa shida na leo sijaja na gari” alinijibu pasipo kunitazama na laiti angelifanya hivyo si ajabu angeliushuhudia wasiwasi uliokuwa juu ya paji la uso wangu.
“ aah! Hatuendi nyumbani na… isitoshe alisema atanipitia kwa taksi ya Dulla” nilibabaika kidogo
“ amepata nyumba ndogo nini maana teksi ya Dulla ndio usafiri wa kwenda kona!” aliniambia kiutani nami nikashusha pumzi na kumshukuru mungu
“ pengine huwezi kujua ati! Na labda anataka kwenda kunitambulisha wifi mdogo” nilizidi kumdanganya rafiki yangu huku nikijifaragua faragua kwa vicheko vya uongo na kweli. Moyoni nilihisi mzigo mzito kumtendea rafiki yangu unafiki kama huu. Tulitoka ofisini mpaka kituoni na baada ya dakika kama kumi teksi ya dulla ilisimama umbali mfupi toka pale tulipokuwa tumesimama na Iloma. Ni yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kuiona na akanishtua
“ haya mama Dulla huyoo … na angalia msifumaniwe huko ukarudi na ngeu” alinitania huku akinionyesha mahali ilipokuwa imepaki teksi ile.
“ tupo makini michapo yote kesho Iloma”
“haya msalimie Brian!”
“salamu zimefika, tutaonana kesho!”
nilimpungia mkono na kuanza kuchapua hatua za haraka kuielekea teksi ile. Vioo vyeusi vya teksi ya Dulla vilimfanya Iloma asimuone mumewe ndani ya gari. Nilifungua mlango wa nyuma na kujitoma ndani ya gari. Jonas alikuwa ameketi kiti cha nyuma.

Tulisabahiana na Dulla akaliondoa gari. Kama mtu alikuwa amepewa maelezo kabla Dulla alitupeleka Lightness Hotel. Tuliingia mle hotelini na kwenda moja kwa moja mapokezi. Cha kushangaza Jonas aliomba funguo za chumba na kupatiwa. N

ilihisi alikiandaa chumba hicho mapema na sikumuelewa kwanini alichukua chumba wakati tulihitaji kuongea mara moja na kuachana. Sikuwa mjinga kiasi cha kuburuzwa na Jonas. Nilisimama nyuma yake na alipogeuka tulikutanisha nyuso zetu sambamba.
“ hii ina maana gani Jonas!?” nilimuuliza kwa hamaki
“ hatuwezi kuongelea pale mgahawani Karen, mimi ni mume wa mtu na mfanyabiashara ninaye julikana sana hapa jijini, wewe ni rafiki wa mke wangu. Kuketi mgahawani pale tukiongea hakutaleta picha nzuri kwa jamii na isitoshe Iloma hajui kama wewe uko na mimi muda huu” alijitetea kwa kadri alivyoweza lakini pia sikuwa mjinga kiasi ambacho alifikiria. Nikampachika swali
“ sasa Jonas kuonekana mgahawani tukiongea na kuonekana tukielekea vyumbani kipi kina unafuu?”
“ okey! Kwahiyo tukakae mgahawani sio?” aliniuliza kwa sauti kali kidogo
“ nadhani ni bora zaidi Jonas” sikungoja maelezo zaidi nilianza kuchapua hatua kuelekea mgahawani. Nikachagua meza moja iliyokuwa kwenye kona na kuketi. Alinifuatia nyuma na kuketi kiti kilichokuwa mbele ya meza iliyokuwa kati yetu. Aliagiza vinywaji na chakula na kwa pamoja tukaanza kula huku maongezi yakichipukia
“ ni bora uniambie kiini cha mwito huu shemeji” nilimrudisha katika mada kuu
“ mbona una haraka Karen kula kwanza mama” alinijibu hali akiachia tabasamu lake zuri la kuvutia
“ halafu ninayo mengi ya kukuuliza Jonas”
“ juu ya nini?” alionesha mshtuko akaacha kula na kunitumbulia macho
“ mbona una haraka kula kwanza shemeji” nilimtania na wote kwa pamoja tukaangua kicheko. Tulipomaliza kula mhudumu aliondoa baadhi ya vyombo na tukabaki tunaburudika na vinywaji.

Ni hapo ndipo Jonas aliponitobolea kiini cha mwito ule, sikupata hata nafsi ya kumsuta Jonas kutokana na yale niliyoyasikia toka kwa mkewe.

Kwa takribani dakika moja na nusu nilibaki nikiwa nimemtumbulia macho jonas pasipo kujitambua akilini. Nilijaribu kushusha pumzi ndefu na kuangaza huku na kule ili japo nitoke ndotoni lakini bado ilibaki dhahiri kuwa sikuwa ndotoni.

Sikuwa naota wala sikuwa nawaza ilikuwa ni kweli kuwa masikio yangu yalikuwa yamesikia kile kilichotoka mdomoni mwa Jonas.

ITAENDELEA....


Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger