Tuesday, April 30, 2013

SINDI.....NA LAURA PETTIE (11)

11

Pazia jepesi lililojaa matundu yaliyotosha kuigeuza pazia ile kuwa kama nyavu ya kuvulia samaki, ilipepea dirishani na kuruhusu hewa safi iliyosukumwa na upepo ipenye kwa mapana na kumfikia Sindi Nalela pale kitandani alipokuwa amejilaza chali, akili yake ikiwa imekimbilia kusikojulikana na kukiacha kichwa chake wazi mithili ya mtungi uliotoboka.

Macho yake yaliitazama  dari huku yakifumba na kufumbuka taratibu mithili ya mtu aliyekuwa akinyemelewa na usingizi. Alikuwa ametopea mawazoni kiasi cha kutojielewa sawasawa kwa wakati ule.


Friday, April 26, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (10)

10
SEHEMU YA 10


Asubuhi ya Siku iliyofuata Pamela Okello aliondoka na gari lake alilokuwa amekodi mahali uko Shinyanga mjini, akiwa amemuachia Jerry Agapela pesa za kutosha pamoja na simu ya mawasiliano. Wakati anaondoka pale kijijini alimkumbuka Nyanzambe Mugilagila, kijana aliyeonana naye jana yake na kumnasua toka katika zahma la kukwama matopeni.

Moyo wake ulitaka kumuona tena kijana huyu, alitaka tena kuisikia ile lafudhi nzito ya kiume iliyomchangamsha jana yake, alitaka tena kukiona kiumbe hiki na nafsi yake haikumpa hata nafasi ya kuipuuzia hamu yake ya kumtia machoni. Akaegesha gari palepale alipoegesha jana yake na kuteremka.

Monday, April 22, 2013

PERUZI YA ENZI.....LADY BY KENNY ROGERS




NEED I SAY MORE?,,,,, I LOVE KENNY ROGERS.....I LOVE COUNTRY MUSIC AND I LOVE THIS SONG MNOOOOOO....WISH SOMEOJE COULD SING THIS SONG FOR MEEEE

Lady, I'm your knight in shining armor and I love you 
You have made me what I am and I am yours My love,
 there's so many ways I want to say I love you 
Let me hold you in my arms forever more 

 You have gone and made me such a fool 
I'm so lost in your love And oh, we belong together 
Won't you believe in my song? Lady, for so many years 
I thought I'd never find you 

You have come into my life and made me whole Forever 
let me wake to see you each and every morning 
Let me hear you whisper softly in my ear In my eyes
 I see no one else but you 
There's no other love like our love And yes, oh yes, 
I'll always want you near me
 I've waited for you for so long Lady, 
your love's the only love 
I need And beside me is where
 I want you to be 'Cause, my love, there's something
 I want you to know You're the love of my life, you're my lady!


ENJOY!!

SINDI......NA LAURA PETTIE (9)

9
SEHEMU YA TISA
Kule ndani ya gari yule binti alikuwa kitetemeka kiasi kwamba alishindwa kuiokota simu iliyokuwa imengukia miguuni pake huku ikiita. Wakati akiitazama taswira ya uso wa mtu uliokuwa ukimchungulia kwenye kioo cha dirisha, ghafla tu akayahamisha macho yake na kutazama kioo cha mbele cha gari, akamuona mwanaume wa rika la kati akiteremsha kimpando kidogo kilichokuwa kikishuka kuelekea pale alipokuwa, alimtazama mwanaume huyu aliyekuwa na jembe begani na moyo wake ukaingia amani toka kusikojulikana. Alihisi ahueni ikimjia!


Thursday, April 18, 2013

PERUZI YA ENZI: LIKE A PRAYER BY MADONNA




THOSE DAYS WHEN MADONNA WAS THE REAL MADONNA!
Huu wimbo nilikuwa naupenda sana.... nakumbuka baba alileta zile video cassette kama mikate hahahahahaaaa

i loved the video though i found it a bit scary.... the black  Jesus hehehehee
Enjoy the video...enjoy the lyrics...mimi hiki kipande hapo chini ndio nimekikariri vizuuuri and it takes me back to those old days lol!


 When you call my name it's like a little prayer 
 I'm down on my knees, I wanna take you there
 In the midnight hour I can feel your power 
 Just like a prayer you know I'll take you there

 I hear your voice, it's like an angel sighing
 I have no choice, I hear your voice Feels like flying 
 I close my eyes, oh God I think I'm falling 
 Out of the sky, I close my eyes 
 Heaven help meeeee

SINDI....NA LAURA PETTIE(8)

8

SEHEMU YA NANE

Sauti ya kilio ilisikika ndani ya nyumba hii sambamba na sauti ya mkanda uliokuwa unatua juu ya mwili wa huyo aliyekuwa akipiga mayowe. Mama Sindi alikuwa amesimama nje akihaha huku mikono ikiwa kichwani. 

Wanawe mapacha nao walikuwa wakizunguka zunguka huku na kule na  mara chache wakiukaribia mlango na kuchungulia kwa tahadhari kisha kutoka hapo na kukung’uta kung’uta viganja vyao mithili ya mtu aliyeungua na moto. kichapo kiliendelea ndani!

Monday, April 15, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (7)

7
SEHEMU YA SABA
Siku mbili baada ya ugomvi wa ngumi kati ya Jerry na Nyanzambe. Jerry alikuwa akizungumza na Mama Alma, nesi aliyekuwa akimhudumia na kumtazamia kidonda chake.

‘Hali yako haijawa njema bwana mdogo….sitarajii ujitoneshe kiasi hiki na uone ni jambo dogo’ Mama Alma alimgombeza Jerry wakati akifunga vifaa vyake baada ya kumsafisha kidonda

Saturday, April 13, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (6)

6
SEHEMU YA SITA
Nyanzambe alitembea kwa mwendo wa kasi akionekana mwenye jazba mno. Sindi alikuwa nyuma akimkimbilia, akajitahidi kumharakia na kumfikia, huku uso ukiwa umesawajika, jasho likimtoka na machozi yakimlenga, Sindi alisimama mbele ya Nyanza akiomba huruma yake
‘Sio hivyo unavyofikiria Nyanza…’ alitaka kujitetea

‘Kumbe ni vipi?....bila soni Sindi unashikwa shikwa na mwanaume mwingine zaidi yangu?...kweli?’ Nyanza aliongea akitetemeka kwa jazba
‘Sikumruhusu aniguse’ Sindi akajitetea tena

Wednesday, April 10, 2013

HAPPY BIRTHDAY MY DADDY.....




HE IS MY HERO.......HE IS MY DADDY
Daddy...
I don't have money to but you an expensive gift..... and even if i had some, i would never find something more expensive and valuable compared to your presence in my life. You are the best Daddy ever not because you are my dad but because you are a caring father, a loving husband to our mom and a terrific human being!

I have always been your little girl no matter how old I am now; i have never felt grown up when you are around. You are my strength in life, without you, it is tough to survive. Thanks for being there for me...for showing me the way.....for being patient with me even when I made it difficult  for you...for believing in me & encouraging me to dream, to try and never to give up even when things seem to be impossible!

You never gave up on me…Never!....in spite of all the troubles and obstacles…Daddy you are still here with me, supporting me  like you did few years ago when I was a little girl. Apart from mom who would have done that to me?.... I’m so proud to be your daughter…..

Nawaza usiku na mchana nije  nikufanyie kitu gani baba yangu kama shukrani yangu kwako. kila ninaloliwaza naliona dogo kulinganisha na upendo, malezi mema na huduma zote kama mzazi.

Nakosa maneno ya kutosha kukueleza ni kiasi gani ninakupenda baba….ni kiasi gani nafurahi kukuona kila uchao….ni kiasi gani watoto wako tunakuombea afya njema kila siku.

Leo ni siku yako! Birthday yako…..Na ningependa kuchukua nafasi hii kumwambia WEWE NI BABA BORA DUNIANI….NA KAMA NITATAKIWA LEO HII KUCHAGUA UPYA BABA NINAYEMTAKA….KWA HAKIKA NITAKUCHAGUA WEWE.

Mungu akulinde, akupe maisha marefu baba…akupe afya na amani…. watoto wako tuzidi kuufurahia baraka hii ya kuwa na baba kama wewe.

HAPPY BIRTHDAY DADDY!!

Binti yako mpendwa

Laura

SINDI.... NA LAURA PETTIE(5)

5

SEHEMU YA TANO

Jua la asubuhi lilichomoza taratibu kwa miale hafifu huku  miale hiyo ikisindikizwa na mvua za rasharasha zilizoanza alfajiri ya siku hiyo. Upepo mdogo uliokuwa ukivuma kwa mbwembwe uliiyumbisha miti iliyotapakaa kijijini hapo. 

Watu wachache walionekana wakikimbia huku na kule wakikatisha katika ile mvua ya rasharasha na  wanakijiji wengi walijifungia ndani kwanza kuipisha ile mvua huku wachache wengine waliojihimu mashambani wakiendelea na kilimo kama kawaida.



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger