Thursday, January 30, 2014

PERUZI YA ENZI.... KUKUPENDA ISIWE TABU BY COASTAL MODERN TAARABU




Ni wana Coastal Morden Taarabu... wakidondoka na kitu Kukupenda isiwe tabu!

Kwa wale wapenzi wa Taarabu basi mtakuwa mnamjua Maua Tego...sauti mashallah... kinanda burudani... maneno kuntu... una lingine la kungoja? waaaala!!

Msikie pale...nasikia rahaaa naona utamu nasikia rahaaa naona utamu hahahaa

ENJOY!!

SINDI....na LAURA PETTIE (55)

55

Aliendelea kuketi pale chini akititirikwa na machozi, Alimtazama Tima pale alipokuwa amelala chali akimtazama. ilikuwa kama vile Tima alikuwa amemkodolea macho nap engine muda mfupi tu baadaye angelinyanyuka na kuanguka kile ckiheko chake kirefu. Pengine angelimzomea Nadina kidogo na kumwambie alitaka tu kumshtua. Akasubiri hilo litokee na halikutokea. Tima alilala vile vile akimtazama vile vile pasipo kujitikisa wala kupepesa macho. Ukweli ukaanza kumuingia Nadina kuwa Tima alikuwa marehemu!

Wednesday, January 22, 2014

SINDI.... na LAURA PETTIE (54)

54

Miale ya jua la asubuhi ile ilipenya kwa kasi kupitia dirishani na kugonga barabara usoni pa Sindi Nalela. Alikunja uso kidogo na kuhangaika kufumbua macho  yake, na hata alipoyafumbua yalibaki katika udogo uliomzuia kuona vizuri kilichokuwa mbele yake. Aliyafumba tena na kutulia huku lile jua likimfanya akunje uso maradufu ya mwanzo, akaunyanyua mkono wake wa kushoto ili kujikinga na ule mwanga wa jua. Lahaula!

Tuesday, January 21, 2014

MGENI WETU:.... NIKO NA SABINA NABIGAMBO!! MTANGAZAJI WA rfi


Sabina akiwa tayari kurusha matangazo... rfi

Sauti ya kike inapanda na kushuka katika mirindimo ya kuvutia… natega sikio kwa vile si sauti ngeni masikioni mwangu… nalazimika kupata uhakika zaidi toka kwa mwenzangu kando yangu. ‘Huyu sio Sabina?’ nauliza kwa shauku nikiongeza sauti ya redio na mwenzangu ananihakikishia kuwa aliye hewani ni SABINA NABIGAMBO!!... Naachia yowe la mshangao… ni lini amehamia redio ya kimataifa ya RFI akitokea redio Mlimani?.... 

....naongeza sauti tena sasa nikishindwa kuwa makini na ujumbe unaorushwa hewani kwa vile akili inalazimika kunasa mawimbi na kuuridhisha moyo kuwa ninayemsikia ni Sabina Nabigambo!!...my collage mate!!... so smart… so charming… so kiiiiind…. na leo hii nimepata nafasi ya kuongea mawili matatu kwenye blog yangu… HEBU PITIA MAHOJIANO YETU HAPA….

LAURA: Najisikia furaha sana kukuweka mtu kati leo kama ambavyo umezoea kuhoji wengine… upo tayari?
SABINA: (Anacheka kwanza… this is what I like about her… kicheko chake ni ukaribisho unaompa yeyote mbele yake nafasi ya kujua anayezungumza naye ni mtu mkarimu mnoooo)… Kabisaaaa jisikie huru tu

Thursday, January 16, 2014

USALITI...TALAKA...MAUAJI... NDANI YA MAISHA YA BETTY NA DANIEL BRODERICK



Walipouawa Daniel na Linda Broderick

.....Pengine waliamka asubuhi hii wakiwa na mipango mingi ya kutimiza.. au labda walizungumza mengi na kupanga hili na lile lakini kwa siku hiyo ya  Novemba 5, 1989 Daniel T. Broderick (44) na mkewe  wa miezi nane tu Linda Kolkena Brodreck (28) hawakujua kuwa asubuhi ya siku hiyo ingekuwa ni siku ya mwisho ya uhai wao.

TUANZIE MWANZO KWANZA… PAUKWAAA… PAKAWAAA!
 MUUAJI Elisabeth Anne Bisceglia... 
'Betty' Broderick Mtalaka wa Daniel

Mnamo November 7, 1947 Elisabeth Anne Bisceglia alizaliwa kwenye familia ya Frank Bisceglia na mkewe Marita, akiwa mtoto wa tatu kati ya watoto sita wa familia hiyo. Elisabeth au Betty kama anavyojulikana zaidi alikuwa binti wa kawaida, asiye na purukushani za kwenda na wakati na mwenye ndoto za kuwa mke wa mtu na mama wa nyumbani mwenye kuijali familia yake. Alikuwa ametoka katika familia yenye kipato kizuri tu.

Wednesday, January 15, 2014

PERUZI YA ENZI... ISLAND IN THE STREAM BY KENNY ROGERS & DOLLY




I like country music... i like Kenny Rogers
He is the one who made me fall in love with country music... 
the first time i listened to his song... i knew my favorite music is Country and he has been my favorite singer of all the time!

Nimekuweke hapa lyrics za mwanzo ili twende sambamba
Dolly is amazing!
Baby, when I met you
There was peace unknown
I set out to get you
With a fine tooth comb
I was soft inside
There was something going on

SINDI.....na LAURA PETTIE (53)

53

Mwanga wa jua ulizidi kupungua kadiri sekunde zilivyotengeneza dakika. Hatimaye giza likabisha hodi na kuleta utusitusi eneo kubwa la msitu ule waliokuwa wakiukatisha kwa msaada wa mwanga wa tochi moja na mbalamwezi iliyosafiri pamoja nao.

Sunday, January 12, 2014

USIKARIRI KITENGE MWENZAKE UKWENI.... CHEKI MITINDO HII!!

Hii ni baadhi tu ya mishono ya vitenge....
Kwa vitenge vya uhakika, original toka CONGO, BENIN NA NIGERIA kwa bei nafuu kabisaaaa
hebu tutafutane kwanza....

0713446543 / 0767446543





BONYEZA 'MORE' KUONA ZAIDI....

Friday, January 10, 2014

SINDI .....NA LAURA PETTIE (52)

52

Fiona Agapella akaweka ndita kadhaa usoni na akili yake ikilikumbuka tukio moja lililotokea hivi karibuni, ingawa hakulipa uzito tukio hilo kwa wakati ule lakini kwa sekunde hizi mbili tatu tukio lile lilikuja na uzito wa tani za kutosha kutikisi mbuyu.!

Thursday, January 9, 2014

PERUZI YA ENZI... BIBALA BALA BY AWILO LONGOMBA




One of the best... i like congelese Music saaaana!
na leo nimeamka na bibala bala bibala bala bibala bala yoyooo hahahahaaaa
The are so many memories ndani ya huu wimbo! mamabo ya ikibinda nkoi... ikibinda eee... ikibinda nkoi lolest!

hakikisha hakuna watu karibu kabla ya kubonyeza play!... i swear you are gonna stand up and move your body... kama sio kichwa basi hata bega... sijasema kiuno lol


ENJOY!

VITENGE ORIGINAL NARUDIA ORIGINALE HASA! TOKA CONGO, NIGERIA NA BENIN!!

Haya wapenzi kuna vitenge vyenye ubora wa hali ya juu... vitenge originale kabisaaa 
Kama unavyojua African prints ndio habari ya Mujini...
Sasa usiende ukaharibu shono lako la kisasa kwa vitenge vya kichina... ukifua mara moja unaogopa hata kushindia Lol!

Hapa tuna vitenge vya CONGO.... NIGERIA... na BENIN
Bei ni ya kutupa... yaani sawa na bure ukilinganisha na ubora wa kitenge chenyewe

Jisikie huru kuwasiliana nasi kwa simu hizi hapa chini

0713446543 ...... 0767446543
















TUNAKUVALISHA.... TUNAKUPENDEZESHA!!

Monday, January 6, 2014

SINDI....NA LAURA PETTIE (51)

51

Maneno yaliyokimbizana toka kichwani mwake yaliishia kusikojulikana, kinywa kilibaki wazi wakati macho yakiongezeka ukubwa kwa kadiri alivyoyatumbua, ile mikono aliyoifumbata kifuani ilitetemeka kiasi cha kuonekana dhahiri ikitingishika, Kwa wakati ule kichwa chake hakikufanya kazi sawa sawa, hakuna alililofikiri kwa muda ule, fuvu lilibaki tupu tu kama mtungi uliotoboka. Wahaka juu ya wahaka!

Wednesday, January 1, 2014

HAPPY NEW YEAR... 2014!!


WAPENDWA WASOMAJI WANGU...
...pengine nimechelewa kidogo kuwatakia kila la kheir lakini wanasema bora kuchelewa kuliko kutokufika kabisa!. Nawatakia mwaka mwenye mafanikio, wenye kila unaloomba kulipata na wenye kumjua Mungu na kumkaribia. 

2013 ndio huoo umeingia kwenye historia na kila lililokuletea machozi ya huzuni, sononeko na jitimai acha liwe historia.

kesho nitawawekea tena mambo 10 ninayofikiria, ninayokushauri kuyatilizia mkazo mwaka huu!

ENJOY RESPONSIBLY!!





Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger