.....huu wimbo umenikaaje leo yaani naurudia rudia tu! it reminds me of something lakini zaidi ni namna nilivyokuwa nauimba before sijajua the real lyrics
Kama ulipata kuwa mpenzi wa tamthiliya hii ya Egoli miaka ya 1995-1997....Characters wafuatao hawatakuwa wageni machoni pako. Nimeweka waliokuwa my favorite wachache tu!! ilawapo weeengi sana.
Egoli imedumu katika seasons 18! kwa miaka 18 ndani ya episodes zaidi ya 2,000! ikishirikisha wasanii wa kimataifa na toka mataifa mbalimbali.
Kwa Tanzania Sauda Simba Kalumanga ndiye aliyepata nafasi ya kuwa muigizaji katika scenes tano za Egoli mwaka 2002. Wengi wao sasa ni watu wazima sana na ujana umewapa mkono lakini kwangu mimi Egoli inabaki kuwa Tamthiliya ya kwanza ya kisouth Africa kuiona na kuipenda since then nimekuwa addictive na South Africa's soap operas kama Isidingo, generation, Scandal, Muvhango, 7de Laan and Jacob's cross
Haya wadau wangu, Mungu katujaalia uzima mpaka muda huu wengine tunaandika wengine mnasoma....hili pekee ni jambo la kumshukuru Mungu, maana kwa maisha sasa kuliona jua la kesho ni majaaliwa.
.......Nisizunguke sana, niende moja kwa moja kwa ninalotaka kulisema barazani hapa!
Kauli ni mali...hasa kama kali hiyo ni njema yenye kuburudisha, kuelimisha na kuleta kila aina ya raha. Kama ilivyo mali, kauli pia ina thamani yake, Mali ukiichezea utakula za uso sawasawa na kauli ukijichanganya utakula za uso.
.....I love Tony, na lile bass lake kwa mbali hahahahaaaa it makes the song more attractive and it reminds me of so many things....my beautiful childhood....i had all the lyrics in one of my exercise book copying them from newspapers
Ni moja ya filamu zilizowahi kunitoa machozi na kunifanya niutumie
usiku wa siku niliyoitazama kuifikiria tena na tena..... ni filamu ya
kuhuzunisha sana,
Kuna wakati nilishindwa kuyazuia machozi na nikajikuta nikiyafuta na kujaribu
kuisimamisha filamu hii kupisha huzuni niliyokuwa ninaisikia…..Sijui kwanini lakini kwangu
ni kati ya filamu zilizopata kunigusa mno!
Ni filamu ya kikanada iliyoandaliwa na kuongozwa
na Denis Villeneuve mwaka 2010, ikiwa
imetolewa katika moja ya simulizi za Wajdi Mouawad. Ikiwa imechezwa kwa umahiri wa hali ya juu na muigizaji wa kiblegiji Lubna Azabal (Niwal Marwan)
Lubna Azabal (Niwal Marwan)
Filamu hii inaanzia pale mapacha wawili Jeanne na Simon Marwan wanapopewa barua
alizoacha mama yaokama
usia, barua zilizojaa utata na vitendawili. Baada ya kusoma barua aliyowaachia
mama yako, Jeanne na Simon wanajikuta katika jukumu la kumtafuta baba yao
waliyedhani amekufa na kaka yao ambayo hawakupata kumsikia ili wawakabidhi
barua alizoacha mama yao na wao wapate kutimiza usia wa mama yao aliouacha
katika barua aliyowaandikia wao..
Jeanne na Simon wakisoma barua waliyoachiwa na mama yao
Jeanne anaonekana kuwa mwepesi mno kuianza kazi, huku akiwa
na shauku ya kujua asili yake pia, anajikuta akizunguka huku na kule akikumbana
na kadhia mbalimbali mpaka pale anapoamua kumuomba kaka yake ajiunge naye
katika jitihada zile huku tayari akiwa na nusu ya taarifa kuhusu historia ya
mama yake
Filamu hii inayaonyesha maisha Nawal Marwan(mama yao)
tangu anapojifungua mtoto wa kiume na kulazimika kwenda kumficha kituo cha
kulele yatima ili asiuawe na wajomba zake (kaka zake Nawal) ambao pia walimuua
mpenzi wake Nawal kwa kuwa tu alikuwa muislamu. bibi yake Nawala anamuunguza
mtoto wa Nawala katika kisigino na kumuachia alama ya doti tatu.
Nawal anaondoka kijijini kwao na kuja mjini kujiendeleza
kielimu akiwa na madhumuni na kujikomboa na kujitegemea ili arudi kumchukua
mtoto wake toka katika kile kituo. lakini kila kitu kinakwenda kinyume na alivyopanga na kutarajia. Utamu unaanzua hapa!!
Niwal akimsaka mtoto wake baada ya vita kuanza
Moja ya matukio yaliyoniumiza ni pale Nawal anapogundua basi alilopanda linakaribia kuchomwa moto baada ya kushambuliwa kwa risasi. Anapoona linamiminiwa petrol Nawala anajisalimisha kwa kunyoosha rozari juu kuwa yeye ni mkristo, wakati anaporuhusiwa kutoka anamtazama mwanamke mwenzake muislamu aliye na binti mdogo mikononi mwake...
Hii scene iliniuma jamani mnooooo
hofu ya kifo kisichoepukika ikijionyesha wazi usoni pake. Nawal anaamua kumnyang'anya yule mtoto na kudai kuwa ni wake ili ajapo amuokoe binti yule mdogo.... hata hivyo yule mtoto asiyeelewa chochote anapiga mayowe kuwa anamtaka mama yake mbaye yuko garini. Wapiganaji wale wanalipua lile basi na kumuua yule mtoto kwa risasi....Aisee! i couldnt take it....niliumia utadhani i was there and i did nothing to save that kid....Vita tusikie kwa jirani tu!!
Abou Tarek Baba na kaka wa Jeanne na Simon
Lubna Azabal ameitendea haki filamu hii kiasi cha yeye binafsi kujizolea tuzo zifuatazo:-
2012,,,,,, Magritte Award - Best Actress for Incendies
2011.,,,,,,Genie Award - Best
Performance by an Actress in a Leading Role for Incendies
2011:,,,,,, Jutra Award - Best Actress for Incendies
2011: ,,,,, Vancouver
Film Critics Circle Award
for Best Actress in a Canadian Film for Incendies
Huku filamu yenyewe ikijizolea tuzo mbalimbali kumi
Best Canadian Film, Toronto
Film Critics Association
Adelaide Film
Festival: 10 awards including Best Feature Film 2011
.....moja ya nyimbo zilizotamba miaka ileeee, nilikuwa naupenda sana na kwa kweli sikuwa najua ni nini hasa kilikuwa kinaimbwa....miaka ikapita na nikaja kujua ni nini hasa kilikuwa kinaimbwa...i was like whaaat! hahahahaaaaa Bobby is a bad news!
Napenda anapoitikia hiki kiitikio, it sounds goooood
If ain't good enough good enough baby
I'll work harder
I'll keep pumpin every minute girl
And baby I'll do you up, do you up baby
And I will not stop till I know your heart
hahahahaaaa!
Enjoy the song and keep the lyrics to yourself *wink*
Katika safari yetu ya maisha hapa duniani, kuna nyakati tunakumbana na matatizo ambayo kwa namna moja ama nyingine yanatufanya tuone Mungu yu mbali nasi.....yanatufanya tuone Mungu ametususa, ametuacha na kamwe hasikilizi maombi yetu....
Ni nyakati kama hizi wengi wetu hukata tamaa, huacha kusali, humgeukia binadamu kama kimbilio (waganga) na wengine huenda mbali kiasi cha kukatisha maisha yao. Wimbo huu wa Ambassadors hunipa faraja, tumaini na subira ya kuwa Mungu ananisikia na atanijibu.
Nimeandika lyrics za wimbo huu, ziwe kama zawadi kwa wale wote wanaopitia nyakati za taabu na mateso. ENJOY!!!
Nataka kusema jambo....likikugusa hili basi utaniwia radhi mwenzangu
Katika maisha binadamu huwezi kuishi tu bila kuhitaji msaada wa mtu mwingine.... Nazungumzia msaada wa aina yoyote. Adamu mwenyewe alipewa msaidizi ndio iwe wewe binadamua wa leo wa kizazi cha ngapi sijui.... Maisha yanapanda, maisha yanashuka huwa hayasimami na yakisimama kwako basi unawalakini. Unayemsaidia leo anaweza kuja kukusaidia kesho kwa msaada mkubwa kuliko huo unaompa.
Nimeamua tu siku moja moja kuwa na mgeni humu
ndani…nimuulize machache, tuongee hiki na kile. Wahenga walisema mgeni baraka
nami ndio nazikaribisha baraka hizo ndani ya blog hii…. Naanza na Annie huyu dada nimependa tu na hulka yake, hana makuu na mtu hana chokochoko na watu...hajui kujivuna wala kupanda seuze ile kujiskia juu wakati aliyejuu ni Maulana peke yake. Nilimuuliza machache naye bila hiyana akanijibu
LAURA: Je una
Nickname yoyote mbali na jina lako?
ANNIE: Hapana sina
LAURA: Heheheee you need one darling! may be nikupe nickname moja Kamamaa*wink*
LAURA:Uko
katika mahusiano?…kama ndio unayaelezeaje mahusiano
yako, kama hapana kwanini hauko katika mahusiano?
ANNIE: Hapana siko kwenye mahusiano yoyote,sababu nimeamua kutulia
kwa muda ili niishi maisha ya peke yangu
LAURA: Time will tell dear, you might need somebody to lean on someday....wish you luck!