Friday, January 2, 2015

DARASA:....TUJIFUNZE KIFARANSA na Laura Pettie


Heri ya mwaka mpya msomaji!

Haya sasa Mwaka mapya na mambo mapya. Laura Pettie Blog sasa itakuletea kipengele cha darasa kila siku ya ijumaa. Lengo la kipengele hiki ni kujifunza mengi kuhusu Lugha na tamaduni za wenzetu. 

Kama ambavyo Motto wa blog yetu  ni ‘KUISHI NI KUJIFUNZA’….  Hivyo tunakuletea darasa la utu uzimani ili upate kupanua upeo zaidi na ujifunze zaidi…  Mnasemaje wadau? LIWEPO AU LISIWEPO? Mkiona halifai tutaliacha hakuna tatizo!

KWA KUANZA DARASA LEO. TUNAANZA NA LUGHA YA KIFARANSA…

Tutajifunza salamu na maneno machache ya kuanzia… ukitoka hapa lazima uwe nusu mfaransa hahahahaa. Kifaransa ni lugha ya mahaba. Raha sana ukiijulia na ukitaka kuifurahia basi upate bahati ya kuwasikia watangazaji wanaotumia kifaransa wakibubujisha maneno yao haraka haraka… utawapenda! moja kati ya watu walionivutia nijifunze kifaransa ni mwanadada Angelique Kidjo! wakati ule akitangaza tuzo za Kora...

Utasema wana mafua hivi, halafu kama wanabembeleza kisha kama wanakazia maneno halafu haoooo wanateleza tena. Ni lugha inayokadiriwa kuzungumzwa na watu karibu milioni 338 ulimwenguni!... wanasema ni lugha ya tatu barani ulaya baada ya kiingereza na kifaransa.

Kifaransa ni lugha rasmi Katika baadhi ya nchi za Afrika na hivi dunia imekuwa kama kijiji kimoja. Si haba ukijua lugha tofauti tofauti. Wala huitaji kuwa mtaalamu kile  cha kuombea maji kinatosha kabisaaa!

Tunanze na salamu kwanza na maneno madogo madogo...kisha nitakuwekea na namna ya kutamka ili kukuwezesha kujifunza matamshi wewe mwenyewe. twende kazi.



TUNASALIMIANA....
1. BONJOUR.... 
    Hello, Good morning 
    Habari za asubuhi!


2. BON APRES MIDI... 
    Good afternoon
    Habari za mchana!


3. BONSOIR
    Good evening/night
    Habari za usiku!


4. SALUT!.... hii ni salamu informal ikitumiwa zaidi na watu wa rika moja au vijana zaidi.
    Hi!
    Mambo!


5. BIENVENUE!
    Welcome
     Karibu!


TUNAAGANA!

6. BONNE journée ...
    Good day
    Siku njema!


7. BONNE soirée
    Good evening/ night
    Jioni njema/ usiku mwema!

8. BONNE nuit
    Good night
    Usiku mwema!

9. AU REVOIR
    Goodbye
    Kwaheri!

10. À BIENTÔT
      See you soon! see you later
      Tutaonana karibuni/ baadaye!


TUNASHUKURU

11. MERCI
      thank you
      Asante!   
ukiongeza neno 'Beaucoup' inakuwa Merci beaucoup, hii ina maana thank you so much...   Asante sana!

TUNAPONGEZA

12. FELICITATIONS
      Congratulations
      Hongera!

13. BONNE CHANCE
     Good luck
     kila la kheri!

SOMO LINAENDELEA....
Kumbuka ukimsalimia mtu Bonjour naye atakujibu Bonjour!... vivyo hivyo kwa salamu zingine pia.
mfano. LAURA: Bonjour Ndimaso
             NDIMASO: Bonjour Laura!

umeelewa hapo!...sijasomea ualimu hivyo kama hujaelewa ndio ujue sio fani yangu hii LOL!

Sasa.... katika salamu kuna zile title za watu. huyu ni Mr. yule ni Miss na kadhalika. hebu tuone inakuwaje.

Mr. / Bwana..... inakuwa MONSIEUR
Miss/ Bi...... inakuwa MADEMOISELLE usiogope utaweza tu kuitamka ni rahisi tu!
Madam.... inakuwa MADAME!

mfano, LAURA: Bonjour Monsieur Ndimaso!
            NDIMASO: Bonjour Madame/ Mademoiselle Laura

umeona hapo! umeelewa eeh! haya tuendelee.
sasa umesalimia bonjour ukajibiwa bonjour. Kiswahili tunakuja na ile hujambo, mnaendeleje na kadhalika...

COMMENT ÇA VA? ... ni kama how is it? how are you?... 
na wewe  unajibu 'ÇA VA' na kama ni mambo uko poa saaana unajibu ÇA VA TRES BIEN! ... wakati mwingine kwa mtu wa roka moja hivi unakuwa informal tu kwa kumuuliza ÇA VA?   naye anajibu ca va... au ca va tres bien!




au nauliza COMMENT VAS-TU?... nikiwa na how is it going? how are you? au  unaendeleaje?

ukiulizwa hivi unajibu ...JE VAIS BIEN ...  kama unaendelea poa sana basi unatupia Je vais tres bien.... UPO? lakini pia unaweza jibu Ça va!

Mfano:
LAURA: Bonjour Monsieur Ndimaso!

NDIMASO: Bonjour Madame/ Mademoiselle Laura

LAURA: Comment  Ça va?


NDIMASO: Ça va!/ .....Ça va tres bien!

upooooo? umeelewa kidogo? au bado?...wapi hujaelewa sasa?


sasa ngoja nikupe matamshi! tufunge siku ya leo. 

JEDWALI LA KWANZA......hapa kuna vowels na consonants!




JEDWALI LA PILI.... hizi ni nasal vowel. ukizitamka ni kama unazitamkia puani vile!




Mfano. BONSOIR.... ile salamu ya jioni/ usiku

UTAITAMKA BON-SWA na bon utaitamkia puani kidogo
 kwasababu

1. kwenye Bon kuna 'on' ambayo ni nasal vowel...cheki jedwali la pili mstari wa chini!
2. kwenye soir kuna oi ambayo inatamkwa WA.... cheki jedwali la kwanza mstari wa pili mwishoni.
umeona?.... so umepata namna ya kutamka BONSOIR!


natumaini kuna kitu umeambulia kwenye somo la leo. kama hujaelewa kabisa basi niwie radhi ni ile mimi sio mwalimu na sina kipaji cha ualimu basi tu najaribu kukuletea kile ninachokijua au nilichokijua ili tujifunze pamoja.

i stand to be corrected...

AU REVOIR MES AMIES!!


     
      
      
       
     
       
     
      
    
    
   

4 comments:

  1. Hongera madame, kweli kuishi ni kujifunza.
    Maana hii ni ya muda ila leo imekuwa msaada kwangu.

    Merci Beaucoup

    ReplyDelete
  2. Merci beaucoup madame et mei je peux parler français

    ReplyDelete



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger