Tuesday, May 20, 2014

PERUZI YA ENZI.... FROM ME TO YOU BY YVONNE CHAKACHAKA NA LYRICS ZAKE!



I have come to plead receive the love from me
So hard to find someone who’s kind
Now it’s to share to one another show some care
We all need some understanding to survive
Join me everybody to find the love we need

This is from me to you
All we have to do
Live together in our world and find the love we all once knew
This is from me to you
All we have to do
Live together in our world in true harmony

Monday, May 12, 2014

KOREAN DRAMA.... LEE MIN HO a.k.a CITY HUNTER!!



Lee Min Ho 

 Nilikosa tu kazi ya kufanya nikajikuta natamani kuangalia chochote cha kunichangamsha…. Katika harakati za kutafuta kiburudisho nikaletewa CD ya series ya kikorea…. Mimi ni mpenzi mkubwa wa series za kikorea .… kuanzia zile za kihistoria mpaka za kisasa, weka mapenzi na maisha au visasi na vita kwa wakorea hunibandui kwenye kiti!


Safari hii nikakumbana na hii series ya CITY HUNTER!... Wakati naanza kuiangalia kidogo nighairi na kuiweka kando lakini saa moja mbele nikajikuta nang’ang’ania kuiangalia masaa. Sio tu kwa utamu wa hadithi na maudhui yake bali pia kwa waigizaji mahiri walioshiriki hususani muigizaji mkuu LEE MIN HO!!
Aisee!... ni miaka mingi sijakaa kwenye Tv nikatazama kitu kwa usongo na kuvutiwa na muigizaji wa kiume kiasi cha kuhisi nawehuka…ila kwa Lee Min Ho heheheeee I had to rewind and rewind some parts of the series  and guess what….i couldn’t get it enough LOLEST!!
Mkorea Lee Min Ho
Ni ndani ya miezi miwili tangu niitazame Ciy Hunter…. Na tayari nimeshatazama series zake zingine tatu…
kuna hiyo City Hunter …. Hii ni ya kipelelezi, visasi na karate za kutosha, mtoto anaibiwa toka kwa mama yake, aliyemuiba ni rafiki wa marehemu baba wa mtoto. Anamkuza porini uko kama mwanaye kisha amatuma mjini kulipa kisasi… yanayoendelea hapo hadi mtoto kuja kugundua kisasi anacholipisha ni kwa maslahi ya baba mlezi tu… ngoma imeranduka vibaya mno! Piga nikupige zimeshatembea vya kutosha!
Kuna hii Personal taste…. Hii bwana Jamaa mtu wa michoro ya ramani, baada ya mzee wake kudhulumiwa mali akaamua kufungua kampuni yake akihangaikia tenda hapa na pale ili afikie malengo… katika kutafuta namna ya kushinda tenda ambayo anaishindania na kijana mwenzake ambaye baba yake ndiye aliyewadhulumu akina Lee min ho… 
SOMA ZAIDI....


Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger