Tuesday, October 8, 2013

SINDI.... NA LAURA PETTIE (42)

42

....Fiona Agapella aliendesha gari lake mpaka nyumbani kwa rafiki yake Iloma. akaingia ndani kwa mbwembwe akicheka kwa furaha na chupa ya mvinyo mkononi. Akaitua mezani na kukimbilia jikoni. Akarudi na glasi mbili na kuziweka mezani karibu na chupa ya ule mvinyo. Iloma, rafiki yake akiwa bado na butwaa lililomfanya shindwe hata kuufunga mlango itakiwavyo.


‘The deal is done!’ akapayuka kwa furaha akijipweteka katika kochi na kumtazama Iloma kwa sura ya furaha iliyojaa ushindi. Tabasamu lile halikuweza kuondoa hali ya mshangao aliyokuwa nayo Iloma zaidi ilimuongezea shauku ya kujua kulikoni!

Akajiondoa karibu na ule mlango pasipo kuufunga na kumfuata Fiona pale kochini.
‘Haya vipi tena?’ akauliza akijilazimisha kuondoa hali yake ya mshangao lakini bado ilikuwa imemganda kupitiliza, alihisi alichotarajia kusikia kingemletea ukakasi masikioni. Siku zote habari njema za Fiona zilimaanisha majanga!

Fiona akaimung’unya midomo yake akijitahidi kuizuia furaha yake isimfanye awehuke zaidi.
‘Nimeshamtupa kule’ akajibu akiivuta chupa ya mvinyo na kuanza kuifungua
‘Nani?’ Iloma sasa akatoa macho
‘Kristus!’ akajibu kwa mbwembwe zote akikazana kuifungua ile chupa iliyoonekana kumshinda kidogo.

Iloma akaganda kama sanamu kwa sekunde kadhaa, macho yakiwa yamemtoka, lakini ghafla akakurupuka na kuufuata ule mlango uliokuwa wazi. Akaufunga kwa funguo na kurejea kuketi pale alipokuwa ameketi kwa mwendo wa kunyata.

Fiona akacheka! aliucheka ule woga uliomvaa Iloma ndani ya sekunde zile chache
‘Umesema?’ akauliza kwa sauti ya kunong’ona, kope za macho yakipepesuka kwa kasi ya ajabu.
‘Kazi imeisha’ Fiona akageuza kichwa na kumjibu shoga yake pasipo hata chembe ya wasiwasi, kisha akarejea kuihangaikia ile chupa ambayo sasa ilikuwa imekubali kufunguka.

‘Mungu wangu!... umeua tena?’ Iloma aliuliza kwa mashaka, akishusha sauti chini pengine akitaka hata shetani mwenyewe  asimsikie. Sauti yake ilijaa hamaki!
Fiona akaangua kicheko kana kwamba alichoulizwa kilimaaniha kumsifu na kumtukuza.
‘Nangoja tu kuvaa nguo nyeusi, kulia na kuzimia, miwani machoni, kamera za waandishi kisha 40 days more niko huru na pesa na kila kitu’ akaongea kwa kujiamini akimimina ule mvinyo katika glasi.

‘Lets toast!’ akaiweka chupa mezani na kunyanyua zile glasi. Moja akimpatia Iloma na nyingine akibaki nayo mkononi. Iloma akaipokea ile glasi lakini akashindwa hata kuinyanyua juu achilia mbali kuigongesha na ya rafiki yake. akaitua mezani haraka, mwili ukimcheza cheza! Hata yeye alimuogopa Fiona ghafla!
888888888888888888888

Jerry Agapella anatoka bafuni haraka baada ya kusikia mlio wa kengele. Analikaza taulo lake kiunoni na kukwanyua kizibao kilichokuwa kitandani, akakivaa haraka akionekana kutaka kumuwahi huyo mtu aliyekuwa akibonyeza kengele kana kwamba alikuwa akikimbizwa na kundi la wananchi wenye hasira kali.

Alipoufikia mlango wa sebuleni, mbonyeza kengele akabonyeza tena na kumfanya Jerry atikise kichwa kulia na kushoto, akishindwa kuelewa kilichomkosesha uvumilivu huyo mgongaji. Akaufungua mlango na Pamella Okello akajitosa kwa haraka kiasi cha kumpamia Jerry begani.

‘So unajua kila kitu kuhusu wanachopanga wazazi wetu si ndio’ akamdaka Jerry kwa jazba
‘kuhusu nini?’ Jerry naye akamuuliza akiufunga mlango na kumgeukia Pamela sasa
‘Ndoa!’ akajibu kwa shari kidogo huku mwenzake akionekana kutohamaki hata chembe.

Jerry hakumjibu, alimpita na kuanza kuelekea chumbani kwake na Pamella akamfuata nyuma akimsemesha hiki na kile kuhusiana na hilo suala na Jerry akitabasamu tu hadi alipoufikia mlango wa chumbani kwake. Akageuka na kumtazama Pamella

‘Nahitaji kuvaa’ akafanya kumzuia Pamella asimfuate mpaka chumbani
‘kuna nini cha kunificha hapo…’ Pamella naye akamuuliza akijitia wenyeji zaidi na kumsogeza Jerry pembeni kisha akaufungua mlango na kutangulia kuingia chumbani.

Akasimama ghafla! akaguna, kisha akamgeukia Jerry aliyekuwa amesimama mlangoni, akionekana wazi kuishiwa nguvu. alichotaka kuficha kilikuwa wazi machoni pa Pamella. Picha kubwa ya Pamella iliyozoeleka kuwa chumbani hapo ilikuwa imeondolewa na nafasi yake kujazwa na picha ya kuchora iliyoandikwa ‘I miss you Sindi ’. Ilikuwa picha nzuri ya kuvutia, maneno yale yalikuwa yamezungukwa na maua ya waridi yaliyochorwa kwa ustadi mkubwa. ukubwa wa picha ulifanya maneno yale yasomeke vizuri hata kwa mtu aliye umbali wa mita tano.

Pamella akameza mate na kutaka kujifanya kuyapotezea yale mabadiliko lakini roho ilimuuma mno. Ile jazba ya madeko aliyokuja nayo ilitoweka ghafla na akajikuta tu akishambuliwa na virusi vya wivu uliotokea kusikojulikana. Alifika pale kumtaka Jerry afanye juu chini wazuie ndoa baina yao ingawa moyoni alitamani japo Jerry ambembeleze hapa na pale ili akubali kuolewa naye  lakini kwa kukuta tayari mwenzake ameshamuweka mwingine chumbani na yeye kuondolewa. Akili ilimkaa sawa!

Jerry akafunga mlango na kukifuata kitanda, naye akijaribu kuupotezea ule mshtuko wa Pamella. Ukimya ukapita kati yao. Jerry alitaka kujieleza lakini alingoja kuulizwa na Pamella alitaka kuuliza lakini alingoja Jerry ajieleze. Wakategeana kwa dakika kadhaa kisha Pamella akavunja ukimya

‘We need to talk!’ akazungumza akikaza koo lake na Jerry akainua uso aliokuwa aameuinamisha chini na kumtazama.
‘Nakusikiliza’ akajibu taratibu asijue ni kiasi gani alimuumiza Pamella kwa kutotoa maelezo kuhusu picha ile.
‘Nakusubiri sebuleni’ akajibu Pamella akianza kuondoka chumbani mule. Kiranga chote kilimshuka! Pengine akitarajia Jerry angelimzuia na kumtaka waongelee palepale, haikuwa hivyo. Alimuacha aondoke tu na Pamella akatoka na kusimama nje ya mlango. Akiuma midomo yake na kujizuia kulia! Koo lilimkakamaa, mishipa ikimsimama wakati akizuia hisia zake zisimletee machozi muda ule. Akajikaza kisabuni!

Kule ndani Jerry aliendelea kusimama kama bwege  Fulani na asijue ni nini alitaka kufanya. Akashusha pumzi na kuifuata suruali yake kabatini. Akavaa pamoja na shati kisha akatoka na kumfuata Pamella sebuleni.

Alimkuta ameketi kwenye sofa akiwa amejiinamia, akaketi sofa la mbali kidogo na kukunja nne.
‘Yes…’ akamtoa katika lindi la mawazo akimpa nafasi ya kueleza alichotaka kuongea
Pamella akainua uso wake na kumtazama Jerry kwa jicho la huzuni
‘Umeshasikia kuhusu ndoa inayopangwa kati yetu?’ akamuuliza Jerry kwa sauti ya chini kabisa
‘Yeah..’ Jerry akajibu akitikisa kichwa juu chini mara kadhaa

‘Una maamuzi gani?’ Pamella akamuuliza akiendelea kumtazama kwa huzuni na Jerry akatabasamu tu kwanza. Ukimya ukapita kati yao, Jerry akitazama pembeni na Pamella akimtazama Jerry. Aliumia sana kuona Jerry hakuwa katika hisia zozote na yeye. Kule kukaa mbali naye kulitosha kumfikishia ujumbe kuwa hakuwa moyoni mwake.

‘…Pam!...’ akaita Jerry akisita kidogo kuleta umakini na akitafuta cha kuongea
‘Najua unampenda Patrick… najua akili yako iko kwa Patrick… siwezi kulazimisha kitu kisichokuwepo moyoni mwako…I promise hatutaleta mahari kwenu…so… relax… and…’ akaishiwa maneno na akaduwaa pia kwa kuona macho ya Pamella yakijaa machozi

‘nina swali?...’ Pamella akajitutumua kuongea akiyawahi machozi yasiteremke mashavuni mwake.
‘Uliza tu’ Jerry akajibu kwa upole
‘Unanipenda?’ Pamella akauliza akivuta kamasi nyepesi zilizokuja na tule tumachozi. Jerry hakujibu, alitabasamu tena, ni wazi alijaribu kupotezea lile swali kimtindo.

‘Pamella…’ akaita akishusha na pumzi kwa sauti
‘Nijibu Jerry…just answer my question…do you love me?’ Pamella akasisitiza akipayuka. Jerry akababaika ni dhahiri hakuwa tayari kusema ndio au hapana.

‘kwanini unauliza?... kuna mtu anakupenda tayari…Patrick is there for you…’ Jerry alikwepesha jibu na kuzidi kumuumiza Pamella
‘Jerry!...Jerry! ni kwamba huwezi sema kama unanipenda au lah au kitu gani?....’ Pamella alikuja juu kidogo na Jerry akashindwa kumuelewa

‘Siko katika mood ya kujibizana Pam!... nimekuhakikishia sitaleta mahari kwenu… nimekuhakikishia sitavunja uhusiano wako na Patrick hivi visirani vingine unavyonifanyia… it is not fair’ Jerry akajitetea na Pamella akajiinamia na kufunga macho kwa nguvu zote, akipambana na uchungu aliokuwa akiusikia moyoni mwake.

Ukimya wa safari hii ukakatishwa na kengele iliyolia muda ule. Jerry akaitikia na mlango ukafunguliwa. Meddy, rafiki yake akaingia na kuwakuta wameketi sebuleni pale na Pamella akiwa bado amejiinamia. Akamsabahi Jerry kwa uchangamfu naye akajibu kwa uchangamfu tu lakini kwa Pamella ikawa tofauti. alinyanyuka na kutoka nje pasipo kumuaga yoyote kati yao. Akatoka na kuubamiza mlango!

‘umemfanyaje tena?’ Meddy akashangaa huku akiketi kochi alilokuwa ameketi Pamella
‘Sitakaa niwaelewe wanawake Meddy… I swear!...’ Jerry akaongea akisikitika
‘Why?’ Meddy akauliza kishauku
‘Aisee!... yaani hizi inshu za mahusiano… nina F ya mwisho kabisa… just imagine amekuja na hasira za kulazimishwa kuolewa na mimi… then amekuta nimeondoa picha yake chumbani… akabadilika… anahoji kama nampenda… honestly, sijui kama bado nampenda kimapenzi … akili yangu inamuwaza Sindi sasa… anataka kulia… ananijia juu… what exactly does she want?!’ Jerry akaongea kwa hisia kidogo akionekana kweli kutomuelewa Pamella.

Meddy akacheka kwa sauti kwanza kisha taratibu akamtumbulia macho rafiki yake
‘Viumbe hawa Mungu tu ndio anawaelewa… ninachohisi ni kuwa anakupenda sana ila na Patrick ndiye mwanaume anayetaka kuwa naye kwa sababu anazojua mwenyewe… ila anataka  na wewe uendelee kuwepo ukimbembeleza na kumuonyesha unamhitaji… sasa unapojiwithdraw halafu unamuonyesha moyo wako unaupeleka kwa mwingine inamuumiza sana…’ Meddy akajitahidi kufafanua

‘Kwa hiyo?... niendelee kumlilia wakati najua yuko na mwanaume mwingine?...’ Jerry akauliza kwa mshangao
‘Mbona umeshamlilia miaka miwili huku ukijua yuko na Patrick..’ Meddy akamshushua akicheka
‘That is before I met Sindi Nalela… Siwaelewi wanawake kwa kweli… hata Sindi sikuwa namuelewa… she was there for me nakupenda kibao… lakini tukitibuana kidogo analeta inshu za jamaa yake wa kijijini kana kwamba ndiye aliye moyoni mwake… aaarg! bwana we’ inahitaji akili ya ziada kumuelewa na mwanamke…’ Jerry akalalamika na rafiki yake akacheka zaidi
88888888888888888888888888888

Sindi Nalela anaangaza huku na kule akitazama chumba hiki alichokuwemo asubuhi hii mara baada ya kuletwa na yule mama aliyempokea toka kwa Mzee Rajabu. Kilikuwa chumba kizuri mno kulinganisha na kule alikolala kwa yule mama. Kulikuwa na kitanda kizuri mno, luninga, kabati, meza, sofa, friji ndogo na bafu la ndani. Alikaa kwa mtindo wa kujikunyata akimngoja mwenzake aliyekuwa anaoga ndani ya hilo bafu la ndani.

Alikuwa amechagua kazi za ndani, na ndio alikuwa ameletwa kwa huyo tajiri yake na hapo alimkuta msichana mwenzake aliyemfahamu kwa jina la Nadina. Alionekana kuwa mgeni kama yeye. Wakachukuliwa damu na mkojo na Sindi alijua wazi alihitaji kuficha mimba yake ili apate pesa kujikimu kwa muda. Aliiba mkojo wa Nadina na kuugawa kidogo katika chupa yake na wakati huu alikuwa akizitazama zile chupa za mkojo zilizokuwa mbele yake.

Mlango ukafunguliwa na yule mwenyeji wake akamuomba zile chupa zilizokuwa na majina yao. Sindi akanyanyuka na kumpatia, kisha akarejea kuketi kitandani. Akiwaza huu utaratibu wa kupima afya kama alivyoambiwa. hakuwahi kusikia lakini pia alijiaminisha kuwa pengine ndio ulikuwa utaratibu wa kutumikia nyumba za matajiri.

Mwenzake aliyekuwa anaoga akatoka akionekana kuyafurahia maji mno.
‘Maji ya motooo’ akayasifia akipiga hatua kumfuata Sindi
‘Vipi wameshachukua mkojo?’ akauliza Nadina baada ya kuona meza ikiwa tupu. Sindi akatabasamu na kuitikia kwa kichwa.

‘Sasa umekojoa wapi jamani…si ungegonga utumie bafu’ Nadina akamsemesha akianza kujifuta maji mwilini
‘Nimekojoa kidogo tu kwenye chupa’ Sindi akajibu akizidi kutabasamu naye akinyanyuka na kuanza kujiandaa kwenda kuoga.

Kule sebuleni yule mama aliyempokea Sindi aliziweka zile chupa za mkojo kwenye kimfuko na kumkabidhi mwanamke mwenzake aliyekuwa ameketi kwenye sofa lingine akionekana ndiye mwenye nyumba.

‘Huyu mwingine mkimya kimya umemtoa wapi?’ mwenye nyumba aliyejulikana kama Adella aliuliza akiwa amebebesha mguu mmoja juu ya mwingine, vazi refu la kinaijeria likiwa likiwa linamfanya aonekane kama mke wa chifu toka Lagos!
‘Nimemuokota uko Kigogo… huyu ni biashara nzuri sana… ile kumuona tu nilijua utamnunua kwa malaki wallah… ni mzuri mnooo… mpigie yule pedeshee mzimbabwe aje amuone hutokosa dola za kutosha hapo…’

‘Na mie nimewaza hilo alipoigia tu… tukimtengeneza huyu aisee… tutapanga matajiri hapa mpaka basi… hivi kwanza umehakikisha hawajaona wamefikaje hapa?... si unajua wakiingia ndio wameingia hakuna kutoka…’ adella akauliza kitahadhari

‘Hakuna aliyeona wala anayejua yuko wapi… we nipe mshiko wangu nikazuge zuge tena uko nikutafutie mali…’ mwenyeji wa Sindi aliongea akitabasamu huku Adella akivuta droo moja iliyokuwa kwenye meza kubwa kando ya sofa aliloketi Adella na kutoa bahasha. Akanyoosha mkono na kumkabidhi yule mama

‘Laki nane keshi!... tano za huyu Sindi  na tatu za Nadina… una lingine?’ Adella akauliza
‘Hakuna!...’ akaitikia yule mama huku akijilamba midomo
‘Yaani namuwazia huyu mtoto sijui nimpeleke saluni gani wamesugue hasa… nataka yule mzimbabwe aache mamilioni hapa… kama yule mzungu alivyodata na Shamsa… Malaya yule akajakutoroshwa na wahuni wavuta bangi…’ akalaani adella akisonya

‘hivi Shamsa aliishia wapi?... alikuwa mzuri yule mtoto jamani kha!’ yule mwenyeji wa Sindi aliuliza kishabiki
‘… mpumbavu yule mabwana walikuwa wanamvutisha unga chumbani uko halafu hasemi… nilipogundua nikambadilishia wateja lakini ndio unga ulishamkomalia nikamrudisha kwa mateja wale…ndio mmoja sijui alimtoresha vipi bwege yule…. nasikia yuko sewa Buguruni nyakanyaka… alinikosesha hela za maana kwa ujinga wake…afie tu uko’ Adella aliongea kwa hasira kidogo

Mwenyeji wa Sindi akacheka kishambenga akigongesha mkono na Adella.
kama ni kazi, basi Sindi ndio hii aliyoipata Sindi. Mwenyewe akiwaza chumbani uko mshahara wa laki na ishirini aliohaidiwa kwa kazi za ndani. Akiwaza atavyozitunza na kujituma kwa bidii ili kumfurahisha bosi wake japo amuongezee mshahara hapo baadaye kama alivyomuahidi endapo atachapa kazi.

Sindi alikuwa akioga huku akishukuru Mungu kwa bahati aliyoipata ya kufanya kazi za ndani kwa mshahara kama ule ndani ya amzingira mazuri kama yale!
88888888888888888888888

Asubuhi hii haikuwa na pilikapilika kwa akina sindi peke yao, kwa Mzee Agapella. Fiona alikurupuka asubuhi ile akiwa na maumivu ya kichwa kutokana na ulevi aliutandika usiku uliopita. alikurupuka toka chumbani kwake na kuteremsha ngazi kwa kasi mpaka sebuleni. akamkuta Jenifa anatazama luninga bila wasiwasi.

Akaguna! hakuielewa ile hali ya utulivu iliyokuwemo mule ndani. akafinya uso kwa kufumba macho kwa nguvu, akitaka kuiweka sawa akili yake. Alitaka kujihakikishia kuw alichofanya usiku uliopita na maongezi yake na Iloma hayakuwa ndoto!

akafumbua macho na kumkuta Jenifa akimtazama kwa mshangao
‘Vipi mama?’ akaulizwa na akabaki ameduwaa kwanza. Akaenda mpaka dirishani na kuchungulia nje. Kulikuwa na utulivu mkubwa kama kawaida
‘Baba yako anaendeleaje?’ akamuuliza Jenifa akionekana kama mtu anayedadisi

‘Mama!...’ Jenifa akamshangaa
‘Umemuota?’ akamtundika na swali zaidi lakini Fiona hakujibu. isingewezekana taarifa za kifo chake zisiwe hewani mpaka muda ule hata kwa familia yake tu! alihisi kama yu ndotoni.

‘…Hujaongea na Jerry?’ akamuuliza tena Jenifa ambaye sasa alishindwa kumuelewa mama yake wa kambo
‘No!’ Jenifa akajibu akitikisa kichwa kulia na kushoto
‘Mmh!...wait hebu mpigie kwanza umuulize anaendeleaje?’ moyo wa Fiona ulikuwa unaenda mbio kupitiliza. Jenifa naye akaguna na kuicukua simu yake. Akampigia Jerry lakini simu ilikuwa inaita tu bila kupokelewa. Akakata na kumgeukia mama yake wa kambo

‘Hapokei’ akamjibu akirudisha simu chini ‘… kama kungekuwa na tatizo sidhani kama Jerry angekuwa kimya mpaka muda huu kwa vile yeye ndiye anayemuona kila siku… na mimi nimemuona jana mchana…alikuwa mzima kabisa… kuna kitu umesikia?’ Jenifa akahoji na asijue mama yake ahakuwa hata akimsikiliza muda ule.

Fiona akageuza na kupandisha ngazi haraka kurejea chumbani. Akapekua huku na kule akitafuta simu yake na kuipata. Akabonyeza namba za simu alizoonekana kuzishika kichwani. Akazipiga na punde tu ikapokelewa

‘una uhakika na ulichofanya jana?....’ akamdaka aliyempigia kwa jazba kali
‘Hakuna taarifa zozote mpaka sasa…. na haiwezekani… are you sure?’ akahoji kutaka uhakika kwa sauti ya juu asijali kama kungekuwa na mtu anamsikiliza. Alishachanganyikiwa! akakata simu na kuketi kitandani kwake uso ukiwa na bumbuwazi, macho yakiwa yamemtoka, mikono ikimtetemeka. Hakujielewa sembuse kuwaelewa aliokuwa akiongea nao asubuhi ile!
8888888888888888888888

Pamella Okello alishuka garini katika eneo la maegesho, akachapua hatua kulifuata jengo lililokuwa na ofisi ya mama yake aliyekuwa anasimamia miradi ya familia yao. Wakati akipandisha ngazi kuelekea lango kuu la kuingilia mapokezi. Simu yake ikaitika na mpigaji alikuwa baba yake.

Akasimama kwanza ili kuongea naye
‘… ndio naelekea ofisi kumcheki mama… Dad kwanini usisubiri mpaka urudi ndio tuongelee inshu za hii ndoa… fine!’ akakata simu akionekana kukerwa na maongezi kati yake na baba yake. akaendelea na safari yake na kuingia mapokezi. Hakumsalimia mtu yoyote wala kuhitaji ruhusa yoyote. Sekretari akampigia kelele kumsimamisha akamgeukia na kumtazama sekretari

‘Samahani kuna mtu ofisini naomba usubi…’ sekretari akaktwa jicho kali kabla ya kukatizwa alichokuwa anazungumza
‘It is my mom’s office…’ akamjibu kwa jeuri na kuendelea na safari yake. Sekretari akanyanyua simu na kumpigia Rebecca kumfahamisha ujio wa binti wake uko ofisini kama ilivyo desturi kuwa hakutakiwa kuruhusu mtu endapo kulikuwa na mtu ndani.

Simu ikaita tu, na Rebecca aliyekuwa mikononi mwa Dennis Mzimbwe wakinyonyana ndimi akaipuuza ile simu kwanza lakini hakuweza kuupuuza mlango uliofunguliwa na binti yake nay eye kusimama katika kizingiti cha mlango akiwakodolea macho wawili hawa waliokuwa wamegandana kama ruba!

Pamella akaduwaa! hakutarajia kuikuta hali ile wala kumkutya mtu yule kama mazingira kama yale na mama yake mzazi. Pamella akapiga hatua moja nyuma akiwa amechama mdomo wake wazi kana kwamba alichoona kilikuwa kinamfuata kummaliza.

‘Pam…!’ mama yake akaita kwa mshtuko akijitahidi kuhifadhi kifua chake vizuri kwa kuifunga blauzi yake iliyokuwa wazi na Dennis akiwa ameinamisha kichwa chini. Pamella alikuwa anahema kwa nguvu mno kiasi cha kuyavuta mabega yake juu na kuyateremsha kwa nguvu.

Alitaka kuongea kitu kilichokwambia kooni, midomo ilimtetemeka wakati mama yake alipomfuata pale mlangoni na kumshika mkono kumvutia ndani.
‘mama..’ akamudu kutamka neno hili
‘I can explain darling…’ mama yake alimrai
‘kuexplain nini?.... kwamba hutaki niolewe na Patrick kwa vile unatoka na kaka yake?... mom!’ Pamella alipaza sauti wakati akitamka neno lake la mwisho

‘…ooh Lord!... ooh Mungu wangu’ Pamella alihamanika akiiondoa mikono ya mama yake mwilini mwake ‘….mama unaingilia mapenzi yangu kwa kuamua kutembea na kaka wa mchumba wangu?... mama??....’ akalalamika akitetemeka na machozi yakimanza kumtembelea akamtazama Dennis

‘Bastard!...nilidhani you are the smartest guy Mr. Mazimbwe  kumbe no!....no…noooo… Oh my God’ akashindwa kupangilia sentensi zake na kutoka mbio akiwaacha Rebecca na Dennis wakitazamana katika namna ya kutoamini kilichotokea.


…ITAKUWAJE?.....

1 comment:

  1. jitahidi kuandika basi jamani maana unachukua week nzima mpz unatuangushaa

    ReplyDelete



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger