Thursday, July 25, 2013

SINDI.....NA LAURA PETTIE (30)

30


Jenifa akamuachia kaka yake na kumtazama kuanzia utosini hadi unyayoni. akajikuta akicheka
‘Na huyu ndio Jerry sio yule wa jana usiku…’ Jenifa akamtania kaka yake ambaye akili yake haikuonekana kuyazingatia maneno ya Jenifa. Alikuwa anatazamana na Fiona huku wote wawili wakitabasamu. Chuki ilisomeka mioyoni huku upendo ukionekana usoni!


‘Mzee amenituma kitu ofisini kwake hapo….bahasha ya njano ila ina mhuri wa kwa juu’ Jerry akamuagiza mdogo wake ambaye alitoka kuelekea huko iliko ofisi ya baba yao Mzee Agapela. Jerry akapiga hatua mbili tatu mbele huku akimkazia macho Fiona na lile tabasamu likijirudia
‘Mama!’ akaita akiendelea kutabasamu na lile neno mama likitoka na mwangi wa dhihaka kwa mbali. Fiona naye akatabasamu zaidi
‘Happy to see you my son’ akajibu akijichetusha zaidi kwa kumkaribia Jerry

Wakawa wamesimama sambamba wakiachana upenyo mdogo katikati yao, Macho yao yalitazamana kana kwamba kila mmoja alikuwa akiyasoma mawazo ya mwenzake. Jerry akainamisha kichwa chake chini karibu na sikio la Fiona
‘…Thank you for everything’ akatamka kwa sauti ya kunong’ona kirudisha kichwa chake usawa wa shavu la Fiona na kumbusu shavuni. Fiona akaduwaa! Macho yakamtoka hali uso ukikunja ndita kadhaa na mwili ukihisi ganzi hadi mifupani.

Jerry akampita Fiona na kumfuata Jenifa kule ofisini kwa baba yao. Fiona Agapela akajikaza na kumeza mate kwa bidii kubwa kiasi cha kulifanya koo lake lididimie ndani kwa nguvu na mishipa ya shingo kumsimama. Aliweweseka!

Wakati akiwa bado ametahayari vile, Jerry na Jenifa wakatokea kwenye kordo ile huku Jerry akiwa na ile bahasha aliyoihitaji mkononi. Akatabasamu tena wakati akiagana na Fiona.
‘Mama tutaonana baadaye…Jeni take care !’ akawaaga na Jenifa akamsindikiza mpaka mlangoni na kisha kumgeukia Fiona ambaye nguvu za kusimama zilishaanza kumuishia na akajikuta akishika kichwa na kujiinamia
‘Mama nini?’ Jenifa akamuwahi na kumshika huku akimsogeza kwenye kochi ili aketi
‘Mama imekuwaje?’ Jenifa alizidi kuhoji baada ya kuona Fiona anazidi kukamata kichwa kama mtu mwenye maumivu makali huku akihema kwa nguvu kidogo.

‘Niko sawa’  akajitutumua kujibu huku akimeza mate kwa taabu na kule kuhema kukimzidia. Jenifa akasimama na kumtazama Fiona kwa mshangao uliogandana na wasiwasi. Hakumuelewa! na hakujua hofu iliyomtembelea Fiona ilimzidi uwezo.
88888888888888888888888

‘Maandazi yameisha…kunaa…’ mhudumu akageuka kutazama kabati la vitafunio na kuwatajia Nyanza na Sakala vitafunio vilivyokuwepo hapo mgahawani muda huo waliokuwa wakistaftahi.
‘Basi niletee vitumbua vitatu’ Nyanza akajibu akimtazama mhudumu
‘Mi niletee chapatti mbili’ Sakala akatoa oda yake na mhudumu akaondoka.
‘Enhe sasa ikawaje?’ Sakala akajiweka sawa akionekana kunogewa na stori aliyokuwa akipewa na Nyanza.

‘Nikamzika mama…nikiwa siamini kabisa kilichotokea binamu…. yaani niliweweseka wiki nzima nikiwa bado siamini mama amekwenda na msichana amekwenda…’ Nyanza akawa anasimulia kwa hisia
‘Na hukupata hata mawasiliano yake’ Sakala akauliza akinyanyua mkono wa kushoto kupisha sahani ya chapatti  iliyoletwa na mhudumu. Wakaacha stori na kusemezana na mhudumu hiki na kile kisha mlo ukaanza. Nyanza akamega kitumbua na kukisukumia na chai, akatafuna kwa juhudi na kukimeza kisha akendelea

‘Sikupata kabisa… na nina amini nitampata mke wangu iwe isiwe…ni mimi na jiji hili na biashara hizi mpaka nimpate mke wangu Sindi’ Nyanza akasema akitabasamu
‘Umefanya nitamani kumuona huyo Sindi Nalela maana….mpaka kakufungisha safari ukahama na makazi basi sio mtoto wa kike wa kawaida atakuwa kifaa kwelikweli…’ Sakala akakolezea akicheka na kufanya Nyanza naye acheke.

Stori zikahamia kwenye mambo ya biashara, wakala huku wakiongea mpaka pale Sakala alipomuona Jamila akiingia mpaka mgahawani nay eye kumpigia mluzi wa kumuita. Jamila akageuka baada ya kuguswa na mteja mwingine kumuonyesha anakoitwa. Jamila aligeuka na alipomuona Sakala akatabasamu na kumfuata haraka.

‘Uoe sasa uache kula magengeni kha!’ akamtania sakala huku akimpa mkono  Nyanza na kumsalimia
‘Binamu yangu huyo’ Sakala akadakia wakati Nyanza na Jamila wakipeana mikono
‘Nilijua mna undugu…mnafanana urefu huo…’ Jamila akatania akicheka kwa sauti na kugonga mkono na Sakala sasa.

‘Unatoka wapi?’ Sakala akaacha kucheka na kumuuliza Jamila
‘Umeanza maswali ya jela….’ Jamila akajibu akitabasamu
‘sasa vipi yule dada wa kule kwenu maana hata jina umekataa kuniambia’ Sakala akalalamika
‘Mke wa mtu yule Sakala eeeh…. utakatwa mdomo huo ushindwe kunadi mitumba….’ Jamila akatania tena na safari alimfanya hata nyanza acheke kwa sauti.

‘Mshauri ndugu yako huyu….akakazana na mke wa mtu balaaa…’ Jamila akamnanga Sakala mbele ya Nyanza na asijue huyo mke wa mtu ndiye Sindi Nalela wa Nyanza.
‘mke wa mtu kitugani kwani mimi mbuzi?’ Sakala akang’ang’ania’
haya uje ubebe mitumba yako ulete pale umtafute uongee naye mwenyewe…somo la ukuwadi nilifeli vibaya…jamani baadaye kuna mtu namsubiri kulee’ Jamila akaonyesha anapotaka kwenda kukaa

‘Shemeji nini?’ Sakala anye hakumuachia
‘Nikwambie halafu uzimie hapa…’ Jamila akamrudishia utani uliofanya wote wacheke. Jamila akaaga na kwenda kuketi alikotaka kuketi.
‘unacheki mtoto huyo?’ Sakala akachombezea na Nyanza akatikisa kichwa kuashiria kukataa kuwa hakutikiswa na Jamila
‘Sindi ni kitu kingine Sakala…ukimuona ndio utajua kwanini nimemfungia safari…na mji wenu huu sijaona bado’ Nyanza akahitimisha kauli yake na kumfanya Sakala apige mluzi mdogo
‘aiseee!’ akakomea hapo. Wakanyanyuka na kutoka mgahawani
8888888888888888888888

Fiona Agapela alishuka kwenye gari lake kama mwehu akitembea haraka haraka na kujikwaa mara kadhaa wakati akilifuata geti la nyumba ya rafiki yake Iloma. Akagonga kama mtu anayekimbizwa, hakungoja hata ile hodi ya kwanza iitikiwe. Aligonga tena mfululizo mpaka Iloma alipofungua mlango nay eye kujitoma ndani kwa kasi
‘Vipi?’ Iloma akamuuliza kwa wasiwasi akichungulia nje ya geti kuhakikisha mwenzake hakuwa akikimbizwa.

‘Nahisi anajua…atakuwa anajua ni mimi….yawezekana’ Fiona aliongea kwa hofu akimtolea macho iloma ambaye hakuelewa hata moja. Akapiga makofi kwa kupokezana mara tatu na kumtazama Fiona kwa wasiwasi
‘Fi unakoelekea sasa utageuka mwehu….nani anajua…na anajua nini?’ Iloma akauliza akiwa bado anashangaa

Fiona akaona kama hakuelewek makusudi, akatembea hatua chache kumfuata Iloma kisha akasita na kurudi alikokuwa amesimama
‘Jerry is back’ akatamka kwa wasiwasi akimuangalia kwa huruma Iloma kana kwamba angelimsaidia kuutua ule mzigo wa wasiwasi. Iloma akashangaa, maneno aliyotaka kuongea yakampotea ghafla, akajikuta akikunja uso na kuukunjua mara kadhaa, akitikisa kichwa kana kwamba alitaka kuung’uta ule mshangao umtoke kichwani.

‘Jerry?!” akauliza swali lenye jibu, hakuamini! na sasa akajua ule wehu wa Fiona ulitaka kumuingia yeye
‘Hebu njoo kwanza…’ akamfuata Fiona na kumshika kama mgonjwa akimuongoza ndani taratibu. alishajua kwanini Fiona alikuwa katika taharuki ile, na alijua kwanini alimwambia simuni kuwa alilazwa kwa mshtuko. Wakaingia ndani na Iloma akamketisha chini Fiona, akampatia glasi ya maji na kuanza kumhoji vizuri.

Fiona akamuelezea japo katika mpangilio usiopangika ukaeleweka.
‘and what is next?’ Iloma akamuuliza naye taharuki zikimnyemelea
‘Nitawaondoa wote duniani kabla hawajaungana kuniondoa’ akajibu akiiweka glasi ya maji chini sakafuni

‘Uwaue baba na mwana??...kisa???’ Iloma sasa alinyanyuka kabisa
‘Nifanyeje sasa?....’ Fiona aliuliza kwa hasira zenye mashaka tele
‘Huwezi kushindwa hiki ukaamua kufanya kile ndani ya muda mfupi na usishtukiwe…. kwanini usirelax Fiona….muda upite uusome mchezo upya… hivi ni nini unataka Fiona unahangaika hivi kutaka kuua?’ iloma akamuuliza kwa kumshangaa mwenzake

‘Nilishaua Iloma….i killed my best friend…I killed her…oh lord…’ Fiona akahamanika, akaweweseka na iloma akakosa maneno ya kutosha kumfariji. alimtizazama kwa woga kana kwamba muda ule  Fiona angenyanyuka na kumuua hata yeye. Baada ya kujishauri cha kumfanya akaamua kumsogelea na kuketi kando yake. Akamkumbatia Fiona ambaye akilia kwa hofu, akilia kwa kuweweseka na kuelemewa na mzigo moyoni mwake.
8888888888888888888888

Wakati Fiona akiweweseka kupitiliza, Jerry na baba yake walikuwa wodini. Mzee Agapela akiwa ameketi sasa na kuonekana mwenye nafuu kubwa. Daktari alikuwa pembeni akimpima presha na kisha nesi kunakili katika faili.
‘nadhani jioni ya leo unaweza kutoka…’ akampa taarifa Mzee Agapela aliyeziitikia zile taarifa kwa furaha na kutikisa kichwa. Dokta akaongea nao mawili matatu na kuwaaga.

‘What happened Jerry?’ baba yake alimuuliza kwa haraka mara tu Dokta alipofunga mlango
‘Hatuwezi kuongelea hili ukiwa na hali hii…. mpigie simu inspekta na umwambie nimerudi na sitaki kesi yoyote….’ Jerry akatoa maagizo
‘But why…lazima waliokutendea hivi watafutwe’ baba yake alitaka kupingana naye
‘I know what I am doing Dad…please!’ akamkata kauli baba yake na akajikuta akikubaliana naye

‘Ungependa kuongea na Inspekta?’ baba yake akamuuliza
‘No…’ akajibu akitikisa kichwa pia wakati huo mlngo ukifunguliwa na Meddy akaibgia akiwa na gazeti mkononi
‘umelipata?’ Mzee akamuuliza wakati akitembea kuja pale kitandani
‘Ndio Mzee…hili hapa’ Meddy akamkabidhi Mzee Agapela lile gazeti. Mzee akalikunjua na kuangaza kutafuta mahali kilipo kifaa cha kutunzia miwani yake.

Jerry akaifuata bahasha ile ya njano na kukitoa kifaa hicho akampatia mzee wake.
‘Tuko mgahawani…kabla ya kuondoka tutapita kukuaga’ Jerry akamuaga baba yake.
‘Take care son…. kuna bodyguard atawasili kesho asubuhi kwa ajili ya ulinzi wako binafsi’ Mzee akajibu na sijue ni kiasi gani alimshtua Jerry

‘Mlinzi?...for what Dad?’ Jerry akauliza kwa kushangaa na kukereka pia. akili yake ilimrudisha mbio kwa Sindi. Angeendaje kule kama angekubali kulindwa msaa 24?. Mzee Agapela akatabasamu na kuinamia gazeti lake na Jerry akajua baba yake hakutaka kujadiliana naye kuhusu hilo. Wakatoka!

Kule mgahawani, Jerry na Meddy waliketi kupata chakula cha mchana huku wakiongea.
‘Sidhani kama ni mjamzito….the girl is rude sijapata ona….na harsh worda mno….’ Jerry alimuelezea Sindi.
‘…na ndio nakwambia huyo tayari kama huamini mpeleke akapime au mpime mwenyewe home’ Meddy akashikilia msimamo wake
‘Unaanzaje kumwambia unachohisi….salamu hapokei, hagusiki yaani ndani maelewano hakuna kabisa’ Jerry akalalamika zaidi na Meddy akajikuta anacheka

‘Kwa hiyo kila ukienda unatolewa knock out…hujamgusa kabisa?’ Meddy akzidi kucheka alipouliza hili kiasi cha kufanya Jerry naye acheke kichinichini
‘Hola!’ akajibu sasa akionekana kujiona mjinga kwa kituko kile

‘ we mwanaume bwana unashindwaje kumdhibiti mtoto wa kike …ulimmenya mwenyewe….’ Meddy akatania zaidi na
‘sio rahisi aisee…kwanza hata uje unatabasamu tangu kituoni anakupokea kwa shari….kila analofanya anakushushua basi dah!...na hivi nimenyoa nywele  nimejisopsop sijui atahoji nini..’ Jerry akaongea akimalizia na kupiga funda kadhaa za maji ya kunywa yaliyokuwa kwenye chupa

Meddy akamtulizia macho Jerry kiasi cha kumshtua.
‘nini?’ akauliza Jerry akimtumbulia macho meddy
‘utani kando…hivi kama Sindi ana mimba kweli are you ready kuwa baba?....tayari kuingia katika majukumu ya kulea mke na mtoto?’ Meddy akamuuliza taratibu na Jerry akaonyesha dalili zote za kutotaka kulijibu lile swali
‘…Sijui….na sijajiaminisha kuwa nimempachika mtu mimba…sitaki kuwaza hayo sasa’ Jerry akajibu asiweke numakini hata chembe.

‘haya bwana!’ Meddy akaona aishie hapo lakini alimtazama rafiki yake na kuona mengi yaliyojaa mkanganyiko kwenye maisha ya huyu rafiki yake. Akanyamaza na kushughulikia chakula chake
88888888888888888888888888888
Saa tatu usiku Jerry alikuwa kwake kitandani. Aliogopa kumfuata Sindi na akiwa hapo kitandani, alitulia akisoma kitabu cha hadithib ya Dira ya moyo kilichoandikwa na mwandishi Laura Pettie. Alikisoma taratibu akijua kingemletea usingizi lakini haikuwa hivyo, akajikuta akifunua ukurasa baada ya ukurasa na asilale.

Simulizi ile ilimkumbusha mtu, ilimkumbusha Pamella Okello. Akakiweka kitabu chini na kuitazama dari. alikuwa amemkumbuka mno msichana huyu. Akaiangalia simu iliyokuwa kando yake na kujishauri endapo ampigie au lah.

Akaishiska simu yake mpya iliyokuwa na laini yake nyingine ambayo hakuitumia sana. Akajifikiria sana kumpigia simu pamella siku huo. Akaamua kuipiga ile namba ya Pamela na simu ikaita. Akasubiri ipokelewe kwa shauku kubwa lakini shauku yake ilikatwa na sauti ya kiume iliyopokea simu ile. Sauti ya Patrick!

Jerry akakata simu na kushusha pumzi, akiirudisha simu kitandani sasa kutazama ukutani ambako kulikuwa na picha kubwa ya Pamella. Ilikuwa picha iliyotundikwa hapo kwa mwaka mzima. Alilala na kuamka akiitazama na kujiaminisha mwanamke yule angemkubalia ombi lake simu moja.

Aliitazama picha hii na kugundua tangu alipoingia ndani mwake hakuwa ameitazama kabisa. Kichwa chake kilichotwa na Sindi mno. Kwa dakika zile alizoitazama ile picha alihisi msukumo wa kumuona Sindi nap engine kuyasikia makelele yake tena. Akaamka na kuvaa nguo zake za kuendea kwa Sindi na kutoka

Alikodi taksi mpaka kwa Sindi na muda ule wa saa tano kasoro Sindi alishalala na nyumba nzima ilikuwa katika utulivu mkubwa. Akamgongea Sindi ambaye baada ya kujiridhisha alikuwa Jerry alimka na kumfungulia.

Akatembea kivivu na kujitupa kitandani tena akionekana kuelemewa na usingizi. Jerry akafunga mlango na kuvua zile nguo alizokuwa amevaa, akazima taa. Akavaa bukta yake na kujitupa kitandani alikolala Sindi. alimchungulia usoni na kugundua mwenzake alikuwa ameshapotelea usingizini. Akageukia upande wake na kulala. Hakulala kwa kutulia alitaka kumgusa Sindi akageuka na kumpapasa mkononi na huku akilivuta bega ili ageuke. Sindi akageuka, usingizi ukionekana kumchota mno.
‘Sindi…’ Jerry akaita kwa sauti ya chini akiifuata midomo wa Sindi na kuibusu.

Sindi akafumbua macho yake na kumtazmaa Jerry usoni. Walitazamana tu bila kuongea kitu kwa sekunde kadhaa.
‘Nakupenda…’ Jerry akatamka polepole kwa sauti ya kubembeleza. mwanga wa mbala mwezi ukimgonga Sindi usoni na kuzidisha nuru ya uzuri wake
‘Nakupenda pia…’ Sindi akajibu akitabasamu. almanusura Jerry ahisi moyo ulitaka kuchomoka kwa furaha aliyoihisi.

Akamsogelea zaidi na kumkumbatia kwa upendo na Sindi akiuachoa mwili wake kwa Jerry.
‘umebeba roho yangu Sindi…’ Jerry aliongea taratibu aki papasa Sindi na kuiondoa ile khanga moja iliyokuwa maungoni mwa Sindi na wakati huo Sindi akimtazam Jerry usoni na sura ya upendo ikimpelekea ujumbe wa shurani Jerry. akaiondoa ile khanga na kukiacha wazi kufua cha Sindi. Damu ikiongeza kasi kwenye mishipa yake…

Simu iliyokuwa kwenye suruali yake iliita kwa kwa sauti kubwa. Jerry akafumba macho na kuusikilizia ule mlio akijua wazi a;likuwa amefanya kosa kubwa kuibeba ile simu kwa kujisahau.

Pamella alikuwa amesimama bafuni akimpigia simu Jerry huku mara kadhaa akinyata na kuchungulia kitandani ambako Patrick alikuwa amelala. Wakati ule Jerry alipopiga alikuwa bafuni na Patrick akamweleza kuhusu simu iliyopigwa na mpigaji kutoongea. Pamella alipozitazama zile namba alizitambuanni za Jerry ingawa hakuzisave simuni.

muda huo Patrick alipolala aliamua kumpigia simu Jerry asijue naye alikuwa na Sindi kitandani. Simu iliiita tena na tena na Jerry mwili ulimfa ganzi akiomba Mungu mpigaji akate. Haikuwa hivyo Simu ilikatika na kuanza tena kuita….
…..HAYA SASA…..

1 comment:

  1. jerry nae mbona hana msim
    amo!!! pamela wa nini tena jamanii

    ReplyDelete



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger