Friday, July 24, 2015

UREMBO NA LAURA:.....MATUMIZI YA NAPKINS MEZANI..

NAPKIN

 Baada ya kuwa kimya muda mrefu kwenye kona hii sasa nimerejea! Twende kazi

Wengi wetu nadhani tunajua ni kitu gani. Kwa maelezo ya juu juu ni karatasi au kitambaa kinachokaa mezani kwa ajili ya kufutia pembe za  mdomo na vidole wakati wa kula au baada ya kumaliza kula. 

Kinaweza kuwa kitambaa cha material yoyote ile ila cotton  inapendeza zaidi kwa kuwa ni rahisi kuikunja kwa staili mbalimbali za kupendeza kuliko kitambaa laini.

Kitambaa hiki unaweza ukakikuta mezani hotelini, nyumbani kwa mtu au kwenye sherehe.  Hata wewe unaweza kuandaa msosi wako mzuri nyumbani na kualika wageni wako  kisha ukakitumia kuongeza umaridadi mezani pako. Si unakumbuka charger plates!!

Kuwa Classic ndio habari ya mjini my dear!.... mumeo kaalika watu wa kazini kwake, hebu fanya kitu cha kuwafanya wakitoka hapo waone mwenzao ana mtu anayependa vitu vizuri. Simple table setting ya uhakika!! Hakuna kuomba omba tishu heheheeee!

Zipo staili mbali mbali za namna ya kuiweka napkin mezani. Kuna wengine hufunga kama kipepeo, kuna wengine huikunja pembe tatu na kuiweka juu ya sahani yaani staili za kuifunga ni nyingi sana,  ni wewe tu na uamuzi wako.

NAPKIN HUKAA WAPI?

Kama ni mlo wa kawaida na si ule rasmi wa shughuli maalumu Napkin inakaa popote kulingana na nafasi kwenye meza yako. Ila kwenye shughuli kubwa utaikuta napkin mezani juu ya sahani.

UMEIKUTA NAPKIN KWENYE MTOKO WAKO…UFANYEJE?

Umealikwa mahali mwenzangu, sehemu yenye mchanganyiko wa watu. Nadhani hutotaka kuonekana mshamba saaana au kushindwa kujua ustaarabu wa matumizi ya Napkins au sio? Hahahahaaaa!!

1. Ukifika mezani usikimbilie kuchukua napkin haraka haraka…ngoja watu wawili watatu wakae…na kama mko wawili ngoja mwenzio naye akae!

2. Chukua napkin yako iweke mapajani. Napkin inakaa mapajani kamwe usiweke napkin shingoni. That is not a bib jamani. Bib ni kile kidude tunafungiaga watoto shingoni wakati wa kula, kwa Kiswahili sijui kinaitwaje. Bibs are for babies not adults!! Labda kama unafanya comedy.


3. Ukishaiweka mapajani anza kupata mlo wako kama kawaida. Unapofuta midomo ikunje upate ncha hivi na kufuta kando ya midomo yako. Usitumie napkins kufuta lips za midomo yako. Hahahahahaa na utafutaje mdomo mzima mwenzangu kwani unakulaje kwa mfano?



4. Labda katikati ya mlo umelazimika kunyanyuka na kwenda maliwatoni, nje kupokea simu au vyovyote lakini ndio umelazimika kutoka mezani. USIWEKE NAPKIN MEZANI!!....iweke kwenye siti yako, pale ulipokuwa umekaa. Usiondoke nayo wala usiitundike kwenye mkono wa kiti yakhe! Kuiweka mezani kunamaanisha umemaliza kula na hurejei mezani!

5. ukirudi irudishe mapajani mwako na uendelee na mlo wako! Utakapomaliza kula usiweke napkin juu ya sahani uliyotumia. Iweke pembeni ya sahani kistaarabu. Mwenyeji wako atajua umemaliza kula hata kama kwenye sahani yako kuna chakula. Kutoa napkin mapajani na kuiweka mezani kunamaanisha umeshiba au umemaliza kula.

NINI USIFANYE KWA KUTUMIA NAPKIN
1. Usiitumie kama handkerchief! Labda kupengea kamasi ama kufutia jasho

2. Usifutie midomo yote kama unanawa vile

3. Usiikunjekunje kama mpira au fundo

4. Usiitemee chakula kama kipande cha nyama kigumu hivi… vitu kama hivi huwekwa kwenye charger plate

5. Mwisho ndio kama hivyo ukiondoka katikati ya mlo usiiweke mezani na ukimaliza kula usiiache kwenye kiti… utaratibu nimekupa hapo juu.

Haya kazi kwenu waungwana! Usiwe kama jiwe kutotaka kusogea wala kujifunza…. Maisha ndio haya haya mwenzangu…. Na mambo ya kujifunza ndio haya haya…usiwe mgumuuuuu khaaaa!! Ukang’ang’ana na mambo ya kizamaaani  LOL

 Natumaini umejifunza kitu eeh!!



No comments:

Post a Comment



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger