Sunday, November 22, 2015

LELETI KHUMALO a.k.a SARAFINA



Leleti Khumalo a.k.a SARAFINA


cover la movie ya Sarafina

Wakati nakua moja ya filamu zilizopata kuvuma utotoni mwangu, ilikuwa filamu ya SARAFINA!
Nilipoiona kwa mara ya kwanza, nilitamani kuwa kama Sarafina, nilitamani kuigiza, kuimba na kucheza kama yeye. 

Nilitamani kuwa mdada jasiri kama Sarafina!... nadhani sikuwa peke yangu katika hili,  Sarafina aliwagusa maelfu ya watoto na  vijana katika namna ya pekee na wapo watu wazima ambao filamu hii ilikuwa bora kwao na kila mtu alikuwa na sababu zake za kuipenda filamu ya Sarafina.

Leo nimemkumbuka mhusika mkuu Leleti khumalo almaarufu kama SARAFINA! Nikaamua tu kudodosa ni wapi alipo, ni nini anafanya, na kitu gani kinaendelea maishani mwake. 
Tiririka nami!

TUMJUE SARAFINA KWA KIFUPI….


Alizaliwa March 30 mwaka 1970 katika mji mdogo ujulikanao kama Kwamashu, kaskazini mwa Durban, nchini Afrika kusini. Mugizaji huyu ana asili ya Zulu. Baba yake Sarafina alifariki wakati Sarafina akiwa na miaka mitatu na kumuachia mama yake mzigo wa kuwatunza Sarafina ndugu zake watatu. 


Mama yake Sarafina alikuwa mtumishi wa ndani ‘Housegirl’ katika nyumba za wazungu.
Sarafina na ndugu zake waliishi katika nyumba chakavu ambayo samani pekee iliyoonekana ndani mwao  ni kitanda. Waligubikwa na umasikini mkubwa kama ilivyokuwa kwa watu wengine weusi kwa kipindi hicho. Pamoja na maisha hayo duni, Sarafina alijipa faraja kupitia muziki, akishiriki dansi mbalimbali za kikabila maeneo ya kwao.

Akiwa na miaka 15, Sarafina alikutana na Mbongeni Ngema, mwigizaji, mwanamuziki na mwandishi wa michezo ya kuigiza. Mbongeni alifika ‘garage’ ambako Sarafina na vijana wenzake walikuwa wakikutana kufanya mazoezi ya dansi zao. 

Mbongeni alipoziona kazi za Sarafina, alimuuliza kama anaweza kuigiza na Sarafina alikubali hapo hapo. Na huo ukawa mwanzo wa safari yake akianzia kuigiza katika filamu ya Sarafina iliyoandikwa na kutayarishwa na Mbongeni Ngema.
Mbongeni Ngema miaka hiyooo


Mbongeni Ngema sasa hivi!

Filamu ya Sarafina ilifungua milango ya umaarufu na mafanikio tele kwa Sarafina, akijipatia heshima kubwa kupitia tuzo mbalimbali alizopata pamoja na mialiko ya kimataifa, achilia mbali kufuatwa na watayarishaji wengine wa filamu. Sarafina pia alicheza filamu ya Yesterday pamoja na Hotel Rwanda (alishiriki kipande kidogo) ambazo zilifanya vyema sokoni.

Mwaka 1992 mwaka mmoja baada ya filamu ya Sarafina kuzinduliwa.  Sarafina aliolewa na Mbongeni Ngema, ikiwa ni ndoa ya tatu  ya Mbongeni. Katika filamu ya Sarafina. Mbengeni ameigiza kama Askari mnoko kibaraka wa wazungu, akitumia jina la Sabela!

MAISHA BAADA YA NDOA
Siku ya harusi yake na Mbongeni

Sarafina alianza kuonekana katika kazi mbalimbali nyingi zikiwa ni kazi zilizoandaliwa na mumewe kama filamu ya Yesterday. Pia  alitoa album ya muziki iliyoitwa ‘Leleti and the Sarafina’ na kufanya kazi nyingine nyingi za sanaa. ila ghafla akapotea lakini Maisha yakaendelea!

Mwaka 2005, Ghafla tu, Sarafina alitangaza kuachana na Mbongeni ikiwa ni baada ya miaka 13 ya ndoa. Leleti alipofanya interview na Nicky Greenwall wa  E.TV katika kipindi chake cha ‘The close up’. Sarafina alisema aliishi maisha ya kuigiza furaha mbele za watu wakati katika uhalisia aliishia maisha ya ajabu sana.

Sarafina aliongeza kuwa alivumilia kwa kipindi kirefu katika ndoa isiyo na furaha na vyombo vya habari havikufahamu hili kwa kuwa aliishi maisha ya usiri mkubwa akijaribu kuuonyesha ulimwengu kuwa ndoa yake ilikuwa PERFECT!

Anasema ndoa yake na Mbongeni ambaye amemzidi Sarafina miaka 15, haikuwafurahisha watu wengi ikiwemo familia yake kwakuwa Mbongeni alikuwa bado katika ndoa yake ya pili baada ya kumtaliki mke wa kwanza. Pamoja na kupingwa  asiolewe na Mbongeni,bado Sarafina aliamua kuolewa kwa kuwa alimpenda jamaa  na aliona Mbongeni yu mapenzi naye kwa dhati. Loooh! 

Siku ya harusi Mke wa  Mbongeni alijaribu kuzuia harusi yao hata hivyo hakufanikiwa na Sarafina  akaolewa. Maisha aliyoishi yalikuwa tofauti na aliyoyatarajia. Alizuiwa kufanya vitu vingi. Alizuia kutoka kwenda popote, alifanyiwa vituko vingi vya ajabu ambavyo alivivumilia kwa miaka 13 (Anakataa kueleza kwa undani matatizo aliyokutana nayo)  na asubuhi moja akaamka na kusema Imetosha!

Sarafina akatengana na Mbongeni ambaye inasemekana pia alikuwa katika mahusiano na mwanamke mwingine. Pamoja na Mbongeni kudai kuwa anaamini Sarafina anampenda na anajua amemuumiza sana katika uhusiano lakini Sarafina atamsamehe na kurudiana naye. Na haikuwa hivyo mwanamke aliondoka kimoja!  Sarafina na Mbongeni hawakujaaliwa kupata mtoto.

BAADA YA TALAKA!

Sarafina alianza kugiza katika tamthiliya maarufu nchini Afrika Kusini iitwayo Generation. Na mwaka 2012 miaka saba baada ya talaka yake na Mbongeni. Sarafina aliolewa tena na mfanyabiashara mkubwa aitwaye Skhuthazo Winston Khanyile.


Harusi yake na Khanyile

Mwaka 2013, Khanyile na Sarafina walipata watoto mapacha.  Sarafina alipata uzao wake wa kwanza akiwa na miaka 43!! To God be the Glory!!
Leleti akiwa na mapacha wake katika jarida la Drum


Kwa sasa Sarafina ni mtangazaji katika kituo cha  redio cha Vuma Fm. 


Anasema hakika maisha anayoishi sasa ndio maisha aliyoyataka, mapenzi na upendo anaoupata sasa ndio upendo alioulilia ndani ya ndoa ya miaka 13 pasipo mabadiliko. Ana furaha na anahisi amebarikiwa!

Huyu ndiye Leleti Khumalo a.k.a Sarafina!!

Mengineyo!
Mwanamke aliyekuja kuolewa na Mbongeni baada ya Sarafina naye  wakati anaingia aliingia kwa mbwembwe akidai mitala ni kitu cha kawaida...ila stress aliyoikuta umo imebidi aokoke tu na sasa anaipa second thought yake LOL!!

Katika Movie ya Sarafina yule Interrogator ni huyu Barker Haines wa Isidingo hahahahaa..
enzi hizo hajawa whitehead kama jina lake.

Tukutane tena wakati mwingineee!! 
UMEJIFUNZA NINI?

Imeandikwa na kutayarishwa na Laura Pettie kwa msaada wa mitandao mbalimbali.

3 comments:

  1. I have been reading story ya Mbongeni na Leleti for so long. Leo nimefurahi kuisoma tena.

    ReplyDelete
  2. I have been reading story ya Mbongeni na Leleti for so long. Leo nimefurahi kuisoma tena.

    ReplyDelete
  3. DAAA NIMEJIFUNZA UJASILI SANA BIG UP SARAFINA

    ReplyDelete



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger