Friday, March 6, 2015

UREMBO NA LAURA:... JINSI YA KUPAKA WANJA MNENE a.k.a WANJA WA LULU


Asalam Aleykum wasomaji wangu!

Leo nakuletea tena lile somo la kupaka wanja mnene a.k.a wanja wa Lulu!
Tuelewane kwanza....huu wanja waaaala hauchagui, uwe na nyusi msitu uwe na nyusi za kuokoteza, dada kwa wanja huu wote mtafanana na kupendeza! wanja huu haujawahi kumchukiza mtu!

Pili, uwe na wanja wa pencil au wanja wa poda wote mnaweza kuuchora huu wanja. Sasa wenzangu na mimi mnaoona ubahili wa kununua wanja wa elfu 20 ule poda usijisikie unyonge. Huu niliojipaka hapo pichani ni wa elfu mbili tu hahahhaaa shame on me!

Tatu, Wanja huu hautaki mkata tamaa kwenye kujifunza...weka nia tu kuwa mara mbili tatu nitaweza maana kuna akina dada mnajidekeza bwana aah mi siwezi... aah mi siwezi nitakufuata uko na  bakora nikucharaze viboko mpaka uweze...usinitanie! hahahahaaaa

Anyway, hebu tuanze somo letu....
Watu wengi huuliza unatumia vifaa gani kuuchora?.... hapa nitakuwekea vifaa ambavyo mara nyingi hutumika haswa na sisi tunaojitengeneza wenyewe majumbani.... wale wa saluni uko kuna brands za vifaa na vipodozi... ila simple tu ya kama yangu hiyo aaah ndugu yangu vifaa vya malaki havinihusu!

TAFADHALI SOMA MAELEZO VIZURI USIPOELEWA RUDIA!! au  ULIZA!...ULIZA!! ...ULIZA!!
A. MAHITAJI

1. UNAHITAJI WANJA
Wanja wa pencil uwe Black au Brown

hapa nakushauri nunua wanja mkavu uwe mgumu kidogo





Wanja wa Poda uwe Black au Brown


Huu hapa chini ni wa kwangu.

Huu wangu  uko double. Upande mweusi ni wanja

upande huo mwingine ni Concealer (nitaelezea kazi yake chini uko)


2. UNAHITAJI BRUSH MOJAWAPO KATI YA HIZI...
Nasisitiza moja wapo au ukiwa nazo zote sio mbaya pia!



Hizi za chini ni zangu.... ninazo zote!
The funniest Part is nilitafuta brush kama hiyo ya kulia nikakosa

ikatokea tu mtu akataka kuniuzia kwa bei ya nauli Dar to Mwanza hahahahaaa

Nikaona tabu ya nini...nikanunua Mascara tu duka la urembo nikachomoa hicho kidude
nikakioshaaa baaasi nikatimiza haja ya moyo!! 


3. UNAHITAJI  CONCEALER...

Zipo Concealer za muundo tofauti na rangi tofauti....  utachagua muundo wowote upendao cha muhimu...narudia cha muhimu...chukua concealer inayoendana na rangi yako!

Zipo hizi kama Pencil...usichanganye na wanja huu sio wanja

Na ndio kule juu kwenye wanja wangu kuna concealer pia, yaani two in one!


kuna hizi zimekaa kama lipstick  hivi....


kuna aina hii ya kwenye kikopo



Hii hapa chini ndio yangu sasa...!!

4. UNAHITAJI CHA KUPAKIA CONCEALER...

kuna watu wanatumia vidole lakini concealer haitachonga vizuri kingo za wanja wako ukitumia vidole. unahitaji kibrush chake hasa kama unatumia concealer ya kikopo kama hiyo yangu. hizo  concealer za pencil au ctick unaweza  kuchorea tu bila kuhitaji brush kivile... Umeelewa?



Brush yangu  ndio hiyo....


B. NAMNA YA KUUCHORA SASA....

Ukishakuwa mjuzi hutaitaji kanuni hizi zinazoanza nazo hapa...yaani ' automatically' utajichora fasta tu bila kufuata vijikanuni...ila wewe unayejifunza nitakupa hizi kanuni mbili. Ili uelewe vizuri. So usidhani utazifuata kila siku.... hapana zitumie unapojifunza basi, ukishakuwa mzoefu wala hutohitaji!

1. KANUNI YA KWANZA...
Hii ndio kanuni ya kwanza.... 
Unapaswa kujua wanja wako unauchora kuanzia wapi?

Utauinulia wapi?

na utaishia wapi?

Kanuni hii itakusaidia kuchora nyusi zinazofanana
Sio nyusi moja imeinuka mwishoni mwa jicho uko nyingine imeinukia katikati

Utachekesha umati wa Mtume  Wallah! hahahahahaaaa

Tumia kitana au chochote tu kupimia.... na pia hapo palipo inuka kidogo ni uamuzi wako painuke sana au painuke kidogo ni wewe tu mchoraji...
Umeelewa sasa?

2. KANUNI YA PILI....
Chora mstari hivi....



Halafu chorea juu upate kitu kama hiki
Si unaona  kwa juu  kainua ndio kanuni ya kwanza ilipotumika

Sasa wewe utainua kwa kiwango unachopenda wewe juu zaidi au hivi hivi
Yote kheir!!


Tumemalizana na Kanuni... sasa umeshachora hicho kimchoro... twende hatua ya pili



---- Anza kujaza wanja kwenye nafasi katikati ya mchoro wako... usikandike shoga fanya kupaka juu juu. Ujanja hapa ni anzia kujaza mwisho mpaka katikati hivi... huku mwanzoni mwa nyusi utapajazia na kibrush ili pawe pepesi hivi...

---- ukishajaza jaza chukua kibrashi kimojawapo...anza kuparaza nyusi sasa... sawazisha kule nyuma kisha rudi huku mbele napo paraza vizuri.... sababu umeanzia mwisho basi brashi itakuwa imepata wanja so ukiparaza patajaa tu... ukipenda unaweza kutumia wanja wa brown kujazia mbele napo inasaidia kuleta wepesi.

---- Paraza mpaka uone umeenea vizuri na huku mwanzo pamekaa vyema.... paka concealer yako


 Concealer yako itachonga vizuri kingo za nyusi zako
Kama hivi!...sasa kazi ya kibrush cha concealer ndio hii kunyoosha nyusi zako!


unaona Concealer inavyoshepu nyusi zako


Umeona hapo?....
Concealer ina kazi nyingine ya kuficha alama nyeusi usoni
Hiyo sitoizungumzia leo.
Leo ni kujua namna ya kushepu nyusi


NIMEJICHORA MWENYEWE SASA




CHINI hapa nakuwekea na video hii toka Youtube!.... 




KAMA HUJAELEWA BASI NJOO FACEBBOK
Search Laura Pettie
Uliza swali lako

NITAKUJIBU FASTA KABISA!!

Natumaini kuna kitu utakuwa umeambulia kwenye somo la leo


....Nawapenda sana...
Wikendi njeeeema!!


2 comments:



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger