Wednesday, January 21, 2015

MEKONI.... MAPISHI YA SOSEJI NA MAYAI




Huu ni mlo wa chap chap...

MAHITAJI
Soseji idadi unayotaka
mayai 2/3
nyanya 1
kitunguu 1
majani ya mint kiasi
pilipili manga
hoho nusu
chumvi

JINSI YA KUPIKA
1. Pasua mayai yako kwenye bakuli safi yachanganye

2. kwenye hilo hilo bakuli  kata kata soseji zako saizi unayopenda

3. katia hoho kidogo

4. katia vitunguu vyembamba

5. katia nyanya ziepuke mbegu za nyanya

6. nyunyuzia pilipili manga na chumvi

7. dondoshe vijani vichache vya mint

8. vichanganye kwa pamoja

9. weka kikaangio jikoni na mafuta kiasi

10.  mimina mchanganyiko wako

11. ukaushe vizuuuri kama unavyokausha yai

MLO WAKO TAYARI!!

UKIPENDA 
unaweza ukakata kipande ukakiweka katikati ya vipande viwili vya mkate
sukumia na chai ya rangi ya viungo, juisi, chai ya maziwa, soda...etc


TUONANE JUMA LIJALO!!




No comments:

Post a Comment



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger