Thursday, May 26, 2011

NDOA NDOANO...

Katika maongezi na ndugu yangu mmoja, aliwahi kuniambia
pata MWENZI WA MAISHA MWENYE MAPUNGUFU YOTE ILA SI MWENYE UPUNGUFU KATIKA UAMINIFU…NI ZAIDI YA SHUGHULI!!!

Huyu kijana wa miaka 28 tu, too young jaman, mwenye shahada yake ya uzamili tena aliyoipata mwaka huu mwanzoni, mwenye kazi nzuri kabisa ya uafisa mipango Halmashauri ya Chamwino Dodoma AMEJIUA KWA KUJIPIGA RISASI usiku wa kuamkia May 25.…kisa kikiwa ni kumfumania mkewe na mwanaume mwingine…

unaambiwa ilikuwa heka heka ya vitanda na mikeka kiasi cha kufikia mwanaume kumkimbiza mkewe Vicky mpaka nyumbani kwao kasha kumtandika risasi za mbavu…akafikiri ameua naye akajitungua risasi…inauma na inasikitisha sana kwamba mkewe yu mahututi Hospitalini na yeye ameshalala nyumba ya milele uko kwao Tabora…ila ametuachia funzo kuwa uaminifu katika mahusiano huepusha zaidi ya UKIMWI…

jaman tulio katika mahusiano tujaribu kuwa na hofu kidogo na Mungu itatuepusha na zahama kama hili…. TABIA YA KUWA NA WAPENZI WENGI NI YA KUJIENDEKEZA TU!

UPUMZIKE KWA AMANI FREDY!…

No comments:

Post a Comment



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger