Monday, May 30, 2011

MSEMO WA LEO...

...AKUNYIMAYE MBAAZI KAKUEPUSHIA MASHUZI...

Mashuzi ndio kule kushuta ashakum si matusi wenyewe mnasema kujamba!

na mbaazi unapozila shurti zikuchafulie tumbo na hivyo kushuta wajibu sasa unaponyimwa mbaazi shukuru tu umeepushiwa hiyo zahama la kuchafua hewa

Yumkini, maana yake binadamu unapokosa kitu usiumie sana pengine Mungu kakuepusha na mabaya ambayo yangekupata, kuumia kupo ila ndio isiwe kuumia mpaka unakufuru...

Shukrani kwa kila jambo limalotokea maishani mwetu!

No comments:

Post a Comment



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger