Saturday, April 13, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (6)

6
SEHEMU YA SITA
Nyanzambe alitembea kwa mwendo wa kasi akionekana mwenye jazba mno. Sindi alikuwa nyuma akimkimbilia, akajitahidi kumharakia na kumfikia, huku uso ukiwa umesawajika, jasho likimtoka na machozi yakimlenga, Sindi alisimama mbele ya Nyanza akiomba huruma yake
‘Sio hivyo unavyofikiria Nyanza…’ alitaka kujitetea

‘Kumbe ni vipi?....bila soni Sindi unashikwa shikwa na mwanaume mwingine zaidi yangu?...kweli?’ Nyanza aliongea akitetemeka kwa jazba
‘Sikumruhusu aniguse’ Sindi akajitetea tena



‘Unadhani sikuona kila kitu?....unadhani nilimvamia tu bila sababu?.... naona sikufai mama….mimi maskini tu nitakupa nini?….nitakupeleka wapi mimi? kuwa huru tu’ Nyanza aliongea kwa uchungu akijitazama na kumtazama Sindi ambaye alikuwa akitikisa kichwa muda wote kuashiria kutokukubaliana na kauli za Nyanza.  Ile sentensi ya kuwa huru tu ilimfanya Sindi ahamanike. Akamzuia Nyanza kumpita na kumshikilia kama mtoto anayemzuia mama yake kuondoka na kumuacha

‘Una maana gani?’ akamuuliza kwa huzuni
‘Nimekuacha huru….yoyote utakayemtaka mchukue tu…. nimeshapigana vya kutosha sababu yako’ Nyanza alijibu akikwatua mkono na kuondoka tena kwa kasi. Sindi hakumfuata nyuma wala hakutazama kule alikokuwa anaelekea Nyanza. Alitulia akitazama sehemu moja pasipo kupepesa hata macho kwa sekunde kadhaa. Kwa unyonge akashika njia ya kumrejesha kwao akiwa na jitimai ya kumtosha.
888888888888888888888

Mzee Agapela alikuwa ofisini kwake, mbele ya laptop yake alikuwa akiendelea kuchapa kile alichokuwa akikichapa katika laptop yake lakini ghafla aliachana na ile kazi na kuhamishia macho yake katika picha ndogo ya mezani iliyokuwa kando ya laptop.

Picha yake na kijana wake Jerry Agapela. Alitulia kwa sekunde kadhaa akiitazama tu ile picha  mpaka pale alipoamua kuvua miwani yake na kutumia vidole vya kiganja chake cha mkono wa kushoto kuzia machozi yaliyokuwa njiani kumtembelelea. Aliyabinya macho yake kwa sekunde kadhaa akijizuia kulia nap engine akizisikilizia zile hisi a za uchungu zilizomjia moyoni. Alikumkumbuka mtoto wake na kupotea kwake kulimkumbusha marehemu mke wake Sophia, mama mzazi wa Jerry Kristus Agapela, mkewe wa kwanza.

Mzee Agapela alishusha pumzi na kutoka pale kitini, akalifuata dirisha na kusimama hapo kitambo akitazama nje, lakini pia akili yake ikizunguka kupita maelezo. Moyo wake ulijaa wasiwasi, mashaka na sononeko kubwa juu ya kijana wake. Alikuwa wapi?... alikuwa hai?.... alikuwa na hali gani?....nini kilimpata?.....na kwanini?.....na kwa vipi?.... Maswali yaliyokosa majibu yalikimbia mchakamchaka kichwani mwake na kumuongezea sononi.

Alizama mawazoni akitazama kule nje, mawazo yaliyomchota yalimfanya asisikie hata kule kufunguliwa mlango wa ofisi yake wakati mkewe Fiona alipoingia mule ofisini. Kwa hatua za taratibu Fiona alimfuata mumewe na kusimama nyuma yake akimtazama namna alivyokuwa ametopea mawazoni. akamgusa began a kumshtua.

‘unawaza sana mume wangu….’ Fiona alimsemesha Mzee Agapela akimpapasa mgongoni
‘Jerry!....inaniumiza kuliko ninavyoweza kuelezea….inanivuruga sana nadhani it is time niajiri mpelelezi binafsi’ Agapela alijibu akitoka pale dirishani na kuifuata meza iliyokuwa na kahawa. Akajimiminia kidogo na kupiga funda kadhaa wakati Fiona akiwa anamatazama kama mtu aliyetaka kusema jambo lilimponyoka ghafla.

‘Mpelelezi binafsi?..... Come on Darling!.....huliamini jeshi la polisi….Kwanini usi…usi… au….’ alitafura maneno ya kujazia sentensi yake na akakosa
‘Inaelekea wiki ya tatu…siwezi kutulia na kufanya kazi pasipo kujua kijana wangu yu wapi….. no!...nguvu ya ziada inahitajika….siwezi kukaa idle huku sioni la maana linaloendelea….’ Agapela alizungumza akizunguka na kurejea kuketi kochini

‘huo ni uamuzi wako…..and what about the will?’ Fiona akauliza kwa amcho makavu, sura yake ikionyesha wazi kutopendezwa na uamuzi wa mumewe.
‘Sidhani kama huu ni wakati wa kuzungumzia will Fiona!....’ Agapela alikuja juu kidogo
‘ni mrithi wa robo tatu ya mali zako…. hivi huoni kuna haja ya kuchange kitu hapo….’ Fiona alisisitiza akimfuata Agapela pale alipokuwa ameketi

‘Sijaona bado….sijapata uhakika kuwa mwanangu hayuko hai….na zaidi ya yote sijaipa akili yangu nafasi ya kufikiria will….my son is alive and healthy…sijali umeguswa na jambo hili au lah…bado huna haki ya kuulizia chochote kuhusu will…right!?’ alizungumza kwa sauti kali kidogo kiasi cha kumfanya Fiona ajishtukie na kugundua alikuwa amevuka mipaka ya kuhoji alichokuwa akikipigia mahesabu.

‘….. nimeuliza kwa nia njema darling…. nimekuwa nawe kwa kila hali kwa hatua zote… ina maana hujawahi kuniamini kuwa naumizwa na hili tukio…. kweli?....okay!’ Fiona alitoka kwa mwendo wa kasi kidogo akiufuata mlango. Agapela akataka kumuita lakini akaona isingefaa kitu, hakutaka kulumbana na wala hakuwa na nguvu ya kubembeleza mtu kwa wakati ule. Akamuacha atoke na kuubamiza mlango. Akashusha pumzi na kujiinamia tena.

Miaka miwili ya ndoa yake na Fiona, imekuwa miaka ya malumbano na matatizo mengi kuliko alivyotazamia. Mara kadhaa alijikuta akimkumbuka marehemu mkewe Sophia na kutamani hata kuurudisha wakati nyuma na kuzugumza naye machache. Alimkumbuka sana mwaamke huyu sit u kwa uvumilivu wake kwake bali pia kwa uzuri wake wa shani.

Aliumizwa na mengi aliyomfanyia Sophia wakati alipokuwa hai, aliumizwa na namna alivyomtendea Sophia sababu tu ya uwepo wa Fiona pembeni ya ndoa yao.  Alimzika kwa machozi ya uongo na kuoa tena mwezi mmoja tu tangu afiwe. Lakini leo hii alikuwa anamlilia Sophia kwa machozi ya kweli, machozi ya majuto na toba. Kwa kumuoa Fiona aliyeitikisa ndoa yake alikuwa ametema jiwe na kubugia kaa la moto.

Kule nje ya mlango Fiona alisimama akiwaza, ile hali ya kutoitwa hata kubembelezwa haikumfurahisha. Alisimama pale mlangoni akiguna guna mara kadhaa na kuamua kumchungulia mumewe kupitia tundu la mlango. Alimuona vizuri namna alivyokuwa ameketi na kukipakata kichwa chake kwa mikono yake.

Fiona akasimama na kushusha pumzi, akipepesa macho huku na na kuuma kidole chake cha shahada cha mkono wa kushoto, ni kama vile alitembelewa na mchecheto. Haraka akatoka eneo lile na kutokomea. Mali za Agapela zilikuwa zinampeleka asikotarajia na Mzee agapela hakujua nyoka aliyekuwa amemuuma alikuwa anamfuga mwenyewe.
88888888888888888

Siku mbili baada ya ugomvi wa ngumi kati ya Jerry na Nyanzambe. Jerry alikuwa akizungumza na Mama Alma, nesi aliyekuwa akimhudumia na kumtazamia kidonda chake.
‘Hali yako haijawa njema bwana mdogo….sitarajii ujitoneshe kiasi hiki na uone ni jambo dogo’ Mama Alma alimgombeza Jerry wakati akifunga vifaa vyake baada ya kumsafisha kidonda

‘Ilikuwa bahati mbaya mama…’ Jerry alisema akijitutumua kutabasamu katikati ya maumivu aliyokuwa anayasikia
‘Na isijirudie tena…umenielewa?’ Mama Alma alimuuliza uso ukiwa na ile huruma ya kimama. Jerry akaitikia kwa kichwa na akuagana na mama Alma ambaye alitoka na kuishia akimuacha Jerry pale alipokuwa akiuma meno na kujilaza chali.

Akili yake ilikuw ana mengi kwa wakati ule. Alitabasamu alipofikiria sababu za yeye kutoneshwa vile. Mwanamke!
Hakuwa mtu wa kupigana sababu ya mwanamke na mpaka dakika ile hakukuwa na mwanamke mbaye angesimama na kudai Jerry alikuwa mali yake. Wakati akiwaza hili jina la mtu likapita katika akili yake Pamela Okello! Mwanamke mrembo, msomi mwenye maisha yake, rafiki yake wa muda mrefu sana na mwanamke ambaye alikuwa akimpigia misele siku nyingi, akimbembeleza awe wake, akimshawishi na kujitahidi kumvutia kwake bila mafanikio.

Pamela Okello alikuwa amegoma kuwa mpenzi wake, alikuwa amegoma kuvunja urafiki wao sababu ya mapenzi, alimkatalia Jerry katakata akiutetea urafiki wao. Alikuwa akimngoja Pamela maishani mwake lakini ghafla hisia zake zilianza kutekwa na Sindi Nalela ambaye ni kama alimvamia na kuuchukua moyo wake jumla jumla. Jerry alicheka kivivu akikumbuka tukio la yeye kutandikwa ngumi.

Tabasamu lile likafifia taratibu alipoirudisha akili yake katika kile alichokuwa akikiwaza usiku na mchana. Moyo wake uliumia na akajikuta akifumba macho na kuyasikilizia maumivu yale sambamba na hasira zilizomtembelea kila alipofikiria kitu hiki
‘baada ya kumuua mama ameona na mimi animalize….i hate you….i hate you’ alitamka kwa ghadhabu kali alimfikiria baba yake. Alizisikia vema kauli za wale waliomteka na kumburuza kama gunia. Aliwasikia vema wakati wakipokea maelezo ya namna ya kumuua na aliisikia vema mmoja wa wale watu waliomteka akimuarisha mwenzake ampigie simu Agapela.

Moyo ulitikisika kwa ghadhabu…. Aliuma meno na kudumba tena macho safari hii akiyasikilizia maumivu ya moyo na maumivu ya kidonda chake.


.....ILIKUWAJE?..... NA ITAKUWAJE...FUATANA NAMI 

No comments:

Post a Comment



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger