Thursday, May 5, 2011

CHA KUSIKIA SI CHA KUONA.....


...Maneno hubomoa na kujenga, maneno huuma na kupuliza lakini yote kwa yote maneno ndio salaha isiyoshikika mikononi lakini ndio silaha inayoweza kuwekea maumivu moyoni maishani...

jaman cha kusikia si cha kuona! mara moja unapoletewa maneno ya kuumiza usikimbilie kutaharuki...usikimbilie kuchukua hatua ukiwa na hizo taharuki...utatenda ya kutenda mwisho wa siku ujutie ulichotenda, jipe nafasi angalau uwe na hakika na kile ulichoambiwa...

mathalani umeambiwa kuna mtu fulani anakusema hivi au vile, usitoke tu kwenda kumkunja mwenzio shati na kumtandika makonde, waama ndio ukashika simu na kumpigia au kumtumia ujumbe wa kumtishia pengine na kumlaania ukoo wake...utavuliwa joho la uungwana!

pima ulichoambiwa kama kina tija na hoja za kukujaza jazba, Kabla ya kufanya maamuzi yako au kujijazia masononeko ya bure.

Umeambiwa mpenzi wako ana mpnzi zaidi yako usikimbilie kuhukumu bila ushahidi. mwambie aliyekuletea maneno akupe ushahidi uufanyie kazi na katika kipindi hicho usimuonyeshe umetaharuki ama kuumizwa na taarifa zake kwa vile bunadamu wa sasa raha yao kubwa ni kukuona ukisononeka, ukishindwa kufika unapotaka!

Kamwe usijipe sononeko kwa kitu usichokuwa na uhakika nacho...maisha mafupi sana kuyaishi katika mawazo, maumivu na majuto ya vitu usivyo na uhakika navyo

ALAMSIKI!

2 comments:

  1. Greetings from Finland. This blog is a fun, through access to other countries, people, culture and nature. Come see Teuvo pictures on my blog. Tell your friends why he must visit Teuvo pictures on my blog. Therefore, to obtain your country's flag rise higher Teuvo blog pictures of the flag collection. Have a wonderful week Teuvo Vehkalahti Finland

    ReplyDelete
  2. thanks Teuvo, i really appreciate your concern, am visiting your blog right now. keep in touch

    ReplyDelete



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger