Monday, July 15, 2013

SINDI....NA LAURA PETTIE (26)

26

Jerry na Pamella waliachana  na kutazamana, nyuso zao zikionyesha wazi hali ya kukumbukana vya kutosha.
‘I  miss you’ Jerry akatamka akiwa ameyakamata mashavu ya Pamella kwa mikono yake yote miwili huku huku wakitazamana machoni.

 Pamella hakujibu chochote wala hakutabasamu kuonyesha kulifurahia lile neno.  Alimtazama Jerry katika namna ya kumjulisha moyo wake ulikuwa na maumivu na lile neno alilotamka halukupooza hata nusu ya vile alivyokuwa anajisikia..



Jerry akamuelewa na alijua kwanini Pamella alikuwa akimtazama vile. Kulikuwa na mkusanyiko wa matukio kati yao tangu walipoonana mara ya mwisho. Kama si kumsikia kwa siri akikiri mapenzi aliyonayo juu yake mbele ya Meddy si ajabu Jerry angeshauliza kwanini alikuwa akitazamwa vile. Kwa wakati ule ukweli alishaujua!

Hakumuhoji kitu, alimuachia na kurudi nyuma hatua moja huku akiendelea kumtazama Pamella usoni. Akamrushia kombora!
‘Naona hujafurahia ujio wangu Pam…niondoke?’ Jerry akauliza kwa utulivu hali akijua wazi ni nini kilichokuwa kikimuumiza Pamella wakati Pmaella mwenyewe alitamani sana Jerry atambue hisia zake, kosa lake na hatimaye atamake neno samahani, ambembeleze kwa hili na lile.

Pamella akaumia na ile hali ya Jerry kutoelewa hisia zake, na mbaya zaidi kutomhoji kuhusu mnuno alioutengeneza wakati ule kama alivyotegemea na alivyozoea. Wivu ukamsosomola kidogo umtie wazimu.
‘Ndio!’ Pamella akajibu kwa hasira kidogo akijua Jerry asingeondoka pamoja na kumjibu vile. Alikosea!

Jerry aliinua mikono juu kama mateka na kisha kuishuha mikono yake, akigeuka taratibu na kuanza kuondoka. Pamella akajawa na bumbuwazi na moyo ukamuuma mara mbili. Hakuwa hivi Jerry, hakuwa hivi alivyo sasa. Nyakati kama hizi angelimuangukia Pamella miguuni na kumuomba msamaha. Imekuwaje?

Jerry akatoka chumbani kwa Pamella asigeuke hata nyuma. Pamella akakabwa na kitu kooni, hasira zilizoungwa kwa wivu zilimvamia ghafla na kumtaabisha. akajikuta tu akinyanyua miguu yake na kutoka mule chumbani kwa kasi akimfuata Jerry nyuma

‘Jerry…Jerry’ Akaita kwa sauti iliyoshindwa kuakisi ghadhabu na lawama kwa wakati mmoja. Jerry akasimama akiwa ameshaufikia mlango wa kutokea nje pale sebuleni. alsimama tu bila kugeuka na Pamella akiwa mita chache nyuma yake.

‘Why are doing this to me?’ Pamella akauliza kwa hamaki, machozi yakimlenga lakini pia akipigana kiume kuonyesha kutoelemewa na hali ile. Jerry akatulia kwanza pengine akimpa Pamella nafasi ya kuunganisha maswali yote aliyotaka lakini hakusikia swali lingine zaidi ya kwikwi za kilio nyuma yake.

Hakugeuka alikishika kitasa cha mlango na kutaka kuufungua
‘Jerry kwanini lakini?’ Pamella akauliza tena na Jerry akatabasamu kidogo akiifurahia ile hali ya Pamella kuhamanika sababu yake. Akakiachia kitasa na kumgeukia Pamella.
Akamtazama kwanza kabla ya kuamua kuzungumza naye

‘Nimefunga safari toka nilikotoka mpaka hapa Pamella… huonyeshi kufurahia ujio wangu….na nakuuliza kama u don’t want me here….unanijibu ndio…then what do you expect me to do Pam?’ Jerry akauliza kwa sauti ya upole tu akiyaweka wazi makosa ya Pamella.

‘I’m Sorry…’ Pamella akajishusha akiomba radhi kwa unyenyekevu na machozi yakimteremka. Jerry akarudi mpaka pale alipokuwa mesimama na Pamella na kumuweka tena kifuani pake.
‘I missed you Jerry mnooo…’ Pamella akalalamika kifuani pa Jerry akimkumbatia zaidi na kufanya Jerry atabasamu tena. tabasamu la ushindi. Kwa mara ya kwanza tangu amjue Pamella alihisi ushindi mkubwa, alihisi kupendwa, alihisi kuwa mwanaume mbele ya Pam lakini zaidi alihisi kumkamata Pam vile alivyotaka!

Walirudi chumbani na kuketi kitandani wakiongea hili na lile na Pamella akajikuta akilalamika kuhusu simu yake kupokelewa na Sindi
‘She is my girl Pam…’ akakiri’
‘What!...that slut!...your girl?’ Pamella akaduwaa
‘Whatever she is….i love her’ Jerry akakiri tena kwa utulivu

‘What about me?....we had a thing Jerry…you love me….what about us?’ Pamella alihamanika sasa akijuta na kuuliza kile akilicholeta yote haya hadharani. Moyo ulimuenda mbio mno.

‘tuzungumzie mambo mengine Pam… you have Patrick na sitaki kuvuruga mahusiano yenu tena…uliniambia nikipata msichana wa class yangu nikwambie…I’m sorry nimechelewa kukwambia ila ndio hivyo it is me and Sindi and not you anymore…happy now?’ Jerry alizidi kuukatakata moyo wa Pamella, akimkumbusha kauli zake mwenyewe.

Pamella akafumba macho akiumeza ule ukweli aliotupiwa. Akahisi kama mtu anayemeza tindikali mbichi. Zaidi ya maumivu! Jerry alijua ni kwa kiasi gani alimuumiza Pamella na na hata yeye aliumia kumuona Pam katika hali ile lakini ilimpasa kumwambia ukweli kupunguza mikanganyiko aliyokuwa nayo. Ilimpasa kuwa wazi ili apate ahueni katika moja ya vitu vilivyokuwa vikimsonga.

Pamella akageuka na kumpa mgongo, akianza kulia kimya kimya na Jerry hakudiriki kumsogelea. Alitulia tu akiyatazama mabega ya Pamella akichezacheza kwa mirindimo ya kilio chake cha kwikwi na asijitolee hata kumfariji. Sio kwamba hakumuhurumia, alijaribu mno kujizuia kumpa Pamella matumaini hewa. Hakuhitaji kuwaweka wanawake wawili moyo wake. Ilimpasa kuchagua na chaguo lake lilimdondokea Sindi Nalela!

Pamella akalia kwanza kisha taratibu akamgeukia Jerry aliyekuwa amejiinamia nyuma yake.
‘So Unabreak up na mimi si ndio?’ akauliza kwa sauti ya majonzi
‘Pamella!...’ Jerry akaita kwa akishusha pumzi kuashiria hakujua hata aanzie wapi kusema alichotaka kusema.
‘Okay!...fine… at least lala hapa lep’ Pamella alitaka kukubali yote ingawa moyo wake ulimgomea

‘No!...lazima nirudi kwa Sindi’ kauli hii ikaufanya moyo wa Pamella ukatike mara mbili zaidi. Thamani ilikuwa ya chini kulinganisha nay a Sindi mbele ya Jerry. Hili lilikuwa tusi zito mno kwake.

‘Kwa hiyo ulifunga safari saa tano usiku kuja kuniambia that slut is your girl blah blah blah or what?’ akauliza kwa ghadhabu

‘Pamella…nina mengi sawa?....nina vurugu nyingi kichwani mwangu…. I cant lie to myself anymore….na sitaki kuvuruga kichwa changu zaidi… nilitaka kuwa wazi kwako… kesho najitokeza kwa baba yangu…. siwezi ishi maisha ya kujificha nikikimbia kivuli cha mtu nisiyemjua’ Jerry aliongea kwa hisia akiwa sasa amesimama akitembea huku na kule

‘Lie to yourself?..... why don’t you tell sindi the truth wewe ni nani?.....kwanini usiwe wazi kwake kwa kila kitu?.... amekusaidia nini maishani mwako?....huna shukrani Jerry… na sikutegemea malipo kama haya baada ya yote niliyokufanyia Jerry…sikutarajia utaniumiza hivi…. Oh Mungu wangu ….get out Jerry…get ouuut…Oh Mungu wangu’ Pamella alichachatika, aliweweseka, alikuwa na zaidi ya maumivu ya moyo. Alihisi mwili ukiwaka moto kwa wakati ule.

Alipayuka kwa hasira akishindwa kujidhibiti na kulia kwa kuhamanika, akajikunja na kujiibamia uku akiushikilia moyo wake kana kwamba ulikaribia kuchomoka na kudondoka.

Jerry akajikuta akihisi kuchanganyikiwa, alimhurumia Pamella alivyokuwa akilia. Akamsogelea na kutaka kumgusa lakini Pamella alisimama na kumshambulia kwa vibao huku akimsukumia nje ya chumba chake. Akaufunga mlango na kuuegemea kwa mgongo. Akiserereka taratibu na kuketi chini akilia.

Jerry alisimama nje ya ule mlango akimuita Pamella, akitaka amsikilize, akimsihi asilie, akijaribu kumuomba msamaha na moyoni akijihisi hatia kwa alichofanya! Ukweli uligonga kichwani mwake na kumuingia moyoni bado alikuwa anampenda Pamella.
888888888888888888888888888

Jua la asubuhi lilishachomoza, upepo ulioiandama siku hiyo ulifanya watu wajivishe masweta na makoti pamoja na lile jua kuwaka. Kulikuwa na dalili mawingu kujikusanya kwa mbali. Fiona Agapela alikuwa ameketi nje ya nyumba ya rafiki yake akimtazama anavyo kja akitokea ndani mwake kuja pale alipokuwa ameketi.

Rafiki wa Fiona aliketi akimtazama Fiona kwa kituo. Ni kama aliigundua hali ya kukosa amani aliyokuwa nayo Fiona.
‘Usinambie umeshaharibu uko?’ akaanzisha mazungumzo
‘Yaani kama ni jumba mbovu basi limeshaniangukia…Jerry yuko hai’ akasema kwa msisitizo uliotembeza macho yake juu chini na kumfanya rafiki yake aukunje uso wake na kumtazama Fiona kana kwamba alikuwa anabadilika rangi.

‘Nini?...Umemuona?’ rafiki akauliza
‘Nimeambiwa…na zaidi nimemsikia Agapela anaonge na nani sijui kuhusu ndoa na matakataka gani sijui kuhusu Jerry….hii yote inamaanisha Jerry yupo na bado anapumua’ Fiona aliongea kwa hasira za waziwazi

‘Kha! sasa wale jamaa uliowakodi ina maana hawakuifanya kazi au?’ rafiki yake akauliza uso ukiunda kicheko ambacho hakikutoka
‘mbuzi wale sijui hata wako wapi….’ akasonya msonyo mrefu wa kupigia mluzi kisha akaachia tusi lingine

‘…na siwapati hata kwenye simu…. hapa hata chooni sijaenda nadhani wiki inatimia kwa wasiwasi nilionao….’ Fiona akao gea tena ka ghadhabu na kumfanya rafiki yake acheke kwanza kwa hali ya kutoamini lakini pia kwa kauli za Fiona alishindwa kujizuia kucheka.

‘Sasa?’ Rafiki yake akauliza akujiweka vizuri lakini jibu hakulipata Fiona alishasimama
‘Ngoja nimtafute yule wakili wa Agapela….ni mwnaaume yule nikimuweka sawa nitajua kipi uturi kipi manukato…baadaye shoga’ akaaga asingoje hata ushauri wa rafiki yake. Kulikuwa na dalili zote za kuchanganganyikiwa.

Wakati Fiona akihaha, Sindi alikuwa nje akifanya usafi chooni kisha ghafla akasimama kama mtu anayewaza, akamkumbuka mama yake, akajikuta akitabasamu. Akamalizia kufagia na kisha akarudi ndani mwake. Akaketi kitandani akitikisa kichwa akiwaza na kuwazua.

Jerry alipoonndoka jana yake alienda wapi na kipi kilichomfanya aondoke kwa ghadhabu vile. Akatoa msonyo mdogo akiachana na ile hali kuwaza na kusimama kama amtu aliyetaka kutoka tena nje lakini akaghairi na kulifuata sanduku alilolebeba na kulileta kitandani.

Wakati akitoa vile vitu sandukuni, Mlango ukafunguliwa na Jerry akaingia akitokea kule anakobadilishia nguo baada ya kulala hotelini na hiyo ilikuwa ni baada ya ugomvi wake na Pamella usiku uliopita. Aliondoka kwa Pamella na kurudi hotelini kulala.

Jerry akaingia na kusimama mlangoni akimtazama Sindi ambaye wala hakujishughulisha kumpokea kama ilivyo kawaida yake. Jerry akanyamaza kimya na kumfuata Sindi pale kitandani. Akimkabidhi kimfuko kidogo cha plastiki.

Sindi akakipokea na kukirushia pembeni asitazame hata kilichokuwa ndani ya mfuko, akaendelea kupangua vilivyokuwemo ndani ya sanduku na kuviweka kitandani.
Jerry akajua Sindi alikuwa amenuna. Akajiketisha mbele yake karibu na lile sanduku na kukishika kidevu cha Sindi kwa mkono wake wa kushoto

‘Umeninunia mama?’ akamuuliza kwa upole huku akitabasamu na Sindi akautoa mkono wa Jerry taratibu pasipo kusema kitu na kuendela na kile alichokuwa anafanya.
‘Nataka kurudi nyumbani’ akainua uso na kuzungumza na Jerry ambaye aliduwaa kwanza

‘Kwanini?’ akamuuliza akinyanyua lile sanduku kama bomu lililotaka kulipuka na kulitupilia mbali na pale, akamsogelea Sindi kwa pupa zaidi
‘Kwanini Sindi?’ akarudia tena akimtolea macho ya kutoamini alichosikia
‘Umeanza visa Jerry…sikuelewi’ Sindi akajibu akionyesha wazi kuumia
‘…. sitaki kuwa mzigo kwako…bora nirudi nyumbani’

Jerry akashusha pumzi ndefu iliyobeba uziro wa ratili moja! Ghafla alihisi uzito kichwani kana kwamba alitupiwa dnia aibebe utosini.
‘Sindi sikiliza…sikiliza mama..’ akaikamata mikono ya sindi na kuikusanya pamoja kwenye viganja vyake. Macho yakipepesuka na asijue aanze na lipi. utulivu uliokuwa usoni pa Sindi ndio ulizidi kumchanganya zaidi

‘…Nimekukosea Sindi…najua….lakini sioni kama nimekuona mzigo au nimekuchoka Sindi….samahani jana sikuwa vizuri’ alijitetea
‘ukalala wapi?’ Sindi akauliza tena kwa utulivu na hili likawa swali la ghafla sana kwa Jerry. Akatumbua macho kwanza akiikimbiza akili yake ifanye haraka kumletea jibu
‘Kwa Meddy’ akajibu baada ya ssekunde kadhaa zilizokaribia kuhitimisha dakika

‘Kwa hiyo tukitibuana hapa namimnitoke nikalale kwa mtu si ndio?’ Sindi akashindilia swaliu lingine lililokaribia kumfanya Jerry apayuke kwa malalamiko lakini akajishtukia na kujaribu kujiweka sawa

‘Nisamehe’ akashuka miguuni pa Sindi ambaye hakumjibu kitu. Jerry akajiinua haraka na kupekua vile vitu vilivyotolewa sandukuni akiutafuta ule mfuko mweusi aliokuja nao. akaupata na kumkabidhi SIndi mikononi.
‘Zawadi yako mke wangu…’ akamuwekea mapajani na Sindi akajikuta akitabasamu kwa mbali kwa kuitwa mke. akaufungua ule mfuko na kutoa simu ya nokia almaarufu kama nokia ya tochi.

Sindi akaachoa lile tabasamu lenye nguvu kuliko vifaru mia.
‘Asantee…nimeipendaa asante jamani’ akaruka kwa furaka na kumkumbatia Jerry akiifurahia ile simu.

‘umebakiwa hata na nauli sasa baada ya kununua simu?’ Sindi akauliza kwa huruma
‘ usijali nitalala hata njaa ili uwe na furaha’ akajibu Jerry na Sindi akajikuta akizisahau hasira zote za jana yake. Maongezi yakapamba moto. akimuonyesha namna ya kuweka laini na kumuacha ahangaike na ile simu yeye Jerry akimtazama na kujiskia raha na amani kubwa moyoni. Alitaani yale ndio yawe maisha yao halisi. Vicheko vikatawala tena ndani mwao

usiku wa siku ile haukuwa mzuri, Baada ya chakula cha usiku na maandalizi ya kuingia kulala Jerry aliingia bafuni kuoga wakati Sindi akiweka sawa kitanda. Simu ya Jerry iliyokuwa kwenye suruali iliyotundikwa kwenye msumari nyuma ya mlango iliita kwa sauti na kumshtua Sindi.

Akaangaza huku na kule akitafuta ulipotokea ule mlio, akapajua na kuifuata suruali. Wakati akiitoa ile simu mpigaji akawa ameamua kukata lakini akiwa bado na ile simu mkononi ujumbe ukaingia na Sindi akairudisha ile simu kwenye suruali na kugeuka kurudi kitandani. Akasita na kuirudia tena ile simu ilipoanza kuita mara ya pili.

‘Pam!’ akalisoma lile jina na akikumbuka kuipokea simu ya huyu mtu na asiongee. Simu ikaita mkononi mwake mpaka ilipokatika. Akaamua kuufungua ujumbe wa maneno.’
‘Jerry pokea simu honey…please talk to me’ akausoma ule ujumbe kimya kimya kisha akaurudia kwa sauti na aliuelewa pamoja na elimu yake ndogo.

Wakati akiwa bado ametaharuki na kujaribu kuutafakari vizuri. Jerry akaingia na Sindi akampatia simu yake ikiwa na ule ujumbe hewani. Jerry aahisi joto ghafla kidogo atamani kukimbia chumba chake bila kujielewa. lile taulo kiunoni aliliona kama  limezengushiwa zege kwa muda ule. lilikuwa zito mno!

Ugomvi ukazuka, Sindi akihoji Pam ni nani, akikumbushia kuipokea simu yake siku moja na asiongee. Ugomvi ukashika kasi zaidi kwa Sindi kukosa majibu ya maana na Jerry akishindwa kumkumbusha kuwa Pam ni Pamella yule msichana aliyekuja kumfuata kijijini.

Sindi akaichukua simu ya yake na kuibamiza sakafuni huku Jerry akishuhudia simu ile mpya ikitawanyika vipande vipande
‘unanidanganya kwa simu huku unawanawake uko nje…. ulinileta unichezee hivi?... ulinileta unifanyie hivi mimi?....’ Sindi alikuwa nalaia kwa hasira sasa akibwata na Jerry akichanganyikiwa.

Simu ya Jerry ikaanza tena kuita na Sindim akampokonya Jerry na kuibamiza sakafuni simu ya Jerry pia. Simu ikafiriki dunia ikimfuata mwenzake.
‘Sindi!’ Jerry akaja juu
‘’Nini?...nini?.... sema nini?’ Sindi alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa kwa hasira na kule kubwatuka kulishawavuta watu akiwemo rafiki yake Jamila aliyeingia bila kukaribishwa

‘Sindi tulia basi…’ akajaribu kumzuia Sindi asizidi kubwatuka na kutoa maneno yaliyoweka wazi wapi walikotoka na Jerry
‘Nimemuacha mwanaume anayenipenda…mwanaume anayenijali….nimefanya nini hiki sasa…nini hiki Jerry?’ Sindi alikuwa analia kwa hasira akiwa mikononi mwa Jamila

‘Shem naomba ukalale kule kwangu au kwa Meddy….muache kwanza atulie ndio mtaelewana’ jamila akatoa angalizo ambalo liliafikiwa na Jerry ambaye aliondoka kwenda kwa Meddy usiku huo. Wakati Sindi akilia huku Pamella naye alikuwa akilia kule kwake. Simu yake ilikuwa haijapokelewa na Jerry. Alihisi kudharauliko mno. laiti tu angejua kilichokuwa kikiendelea wakati huo
888888888888888888

Yote haya yalikuwa upande huo lakini upande huu. Nyanza alikuwa amelala nyumba ya wageni pale ubungo akiingoja asubuhi kwa hamu kubwa. alishamtafuta binamu yake Sakala na alishampata na walishahidiana kuwa angemfuata pale hotelini kesho yake. Alikuwa na amani kubwa na matarajio makubwa moyoni mwake.

Usiku ulikuwa mrefu kwake, akimngoja binamu yake ambaye alikuwa akiuza mitumba pale mwenge stendi. Hakujua mengine yote yaliyokuwa yakiendelea upande mwingine wa dunia.


….. NINI KITAJIRI….TOA MAONI YAKO…..

1 comment:

  1. Nimekuwa nikisoma kimya kimya ila msema kweli mpenzi wa Mungu dada una kipaji maana ni kama naangalia movie vile.

    ReplyDelete



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger