Monday, March 11, 2013

IT IS MY BIRTHDAY.... 11TH MARCH, 2013

Nimshukuru Mungu kwa majaaliwa aliyonijaalia.....
Niwashukuru wazazi wangu kwa mapenzi na malezi mema waliyonipatia
Niwashukuru ndugu zangu na familia yangu kwa upendo na ushirikiano wanaonipatia
Niwashukuru Marafiki zangu wakiongozwa na Pascalina na Zuhura kwa urafiki mwema walionizawadia
Niwashukuru nyie wasomaji wangu, msiochoka kuingia humu kujua lipi limejiri!



Kwangu siku hii ni siku kama  nyingine ila tu inakuwa ya kipekee kwa vile inahitimisha mwaka mmoja kwenda mwingine, kwangu mimi hii ndio siku ya mwaka mpya. Mengi mno nimepitia ya furaha na huzuni.... mapito na majaribu mengi yamenipata tangu ningali kinda, msichana mdogo mwenye ndoto kubwa mpaka sasa nikiwa mwanamke!...katika yote haya Mungu alinipitisha kwa makusudi maalumu na leo hii ninapotazama nyuma nagundua kuna mazito yalinikuta ili niwe hivi nilivyo leo.

Sina cha kumlalamikia Mungu.... zaidi ya kumshukuru kwa afya, kipaji, maisha na bahati ya kuwa nanyi mlionizunguka.

Napenda pia kuchukua nafasi hii kuwashukuru wote mliokuwa nami mkifuatilia hadithi ya KARATA TATU...ingawa feedback ya maneno ni ndogo but natumaini wengi mlivutiwa nayo na mkaifuatilia mpaka mwisho. Chombezo la kiroba cheusi imekatikia kati kwa vile file lililotumika kuitunza lilikuwa corrupted na ikwa nje ya uwezo wangu kuirecover....hivyo nalazimika kuanza upya kuliandika

pia nimekuwa nikipokea maswali mengi tu kuhusu mimi binafsi na wengine kuhusu Hadithi. Nashindwa kuyajibu kwa wakati kwa vile nafungua email mara chache....ningependa mtumie inbox ya fb na majibu yatakuwa kwa wakati muafaka

ASANTENI SANA SANA SANA KWA UPENDO WENU KWANGU

........HAPPY BITHDAY TO ME......



No comments:

Post a Comment



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger