Saturday, March 30, 2013

SINDI.......NA LAURA PETTIE (4)

4
Sehemu ya nne
Njia nzima Sindi na Jerry walibishana hiki na kile, wakaelezana haya na yale. Kwa muda mfupi tu waliozungumza njiani Jerry aligundua Sindi Nalela alikuwa na upeo mkubwa tofauti na elimu yake ya shule ya msingi aliyokuwa nayo.

Pasipo kujua Nyanza alikuwa akiwafuatilia nyuma, walisimama na kubishana, wakisontana kwa vidole na mara kadhaa Jerry akikwepa vibao vya Sindi pale alipomtania na kumcheka. Nyanza aliyaona yote haya na aliyafuatilia kwa umakini mkubwa mpaka pale alipohisi asingeweza kuwafuatilia tena baada ya Sindi na Jerry kuagana na kila mmoja kushika njia yake. 



Uso wa Nyanza uliojaa makunyanzi ya wivu uliochanganyikana na kutokuuelewa ule karibu kati ya Sindi na Jerry.

Kwa hatua za kinyonge alitembea kurudi kule alikotokea, akiwa na hali ya kutaka kujiuliza maswali kwa sauti na hapo hapo akighairi na kujaribu kuimezea hali ile. Aliumia!

Sindi Nalela aliingia katika uwanja wa nyumba yao na kusimama kwanza akichungulia upenuni mwa nyumba yao ambako mama yake alikuwa akitwanga mpunga kwenye kinu kikubwa. Akaamua kuingia ndani kwanza kupeleka vifaa vyake vya kufundishia na kisha akatoka akiwa amejifunga upande wa khanga kiunoni na kubadili viatu.

Alizunguka kule alikokuwa mama yake  na kumsalimia, akibonyea mpaka chini kama ilivyo desturi. Mama yake hakujibu, alimtupia jicho kali sana kisha akaendelea kutwanga mpunga wake. Uso wake tu ulitosha kumfanya Sindi ajue kuna kitu kilikuwa kimemkera mama yake.

‘kuna nini mama?’  aliuliza kwa upole
‘Sina roho ya chuma wala sura ya bati kuweza kustahimili unayoyafanya Sindi…’ mama aliacha kutwanga na kuongea kwa jazba

‘ nimefanya nini mama!?….’ swali lenye ladha ya mshangao lilimtoka Sindi na hapo hapo akimsogelea mama yake na kumtazama kwa udadisi.

Ni kama vile Mama Sindi alitaka kumtesa binti yake kwa maswali ya kichwa. Hakulijibu swali lake, akaamua kuinua mche wa kutwangia na kuendelea kutwanga. Sindi akatulia kwanza akimtazama mama yake pasipo kujua ni nini hasa kilikuwa kimemkwanza. Taratibu akapiga hatua na kuanza kuondoka pale karibu na mama yake. Hatua zile zilimfamfanya Mama Sindi asimamishe shughuli yake na kumtazama Sindi kwa jicho kali, jicho lililoshiria mkusanyiko wa hasira moyoni mwake.

‘Unayoyafanya uko yote analetwa hapa…we jitie umajinuni wakati mahari imeshapokelewa’ akamnanga Sindi ambaye alimsikiliza mama yake kwa unyonge
‘Sasa mama nimeuliza nililokosea…hutaki kuniambia…unanisemea mafumbo tu… haya basi litakalonikuta ni langu..nitalibeba mwenyewe’ akajikuta akimjibu mama yake kwa jazba na kuondoka kwa kazi kuelekea ndani.

Sindi alikimbilia chumbani, akasimama katikati ya chumba akihema kwa hasira zilizomvaa ghafla lakini pia kwa wasiwasi usio rasmi ukimtembelea. Akaamua kuvua ile blauzi aliyokuwa amevaa na kuipandisha kifuani khanga aliyokuwa  ameifunga kiunoni. Wakati akiikaza ile khanga mama yake aliingia na kusimama karibu na kizingiti cha mlango.
‘Ndio amekupa jeuri ya kuja kunijibu unavyojua?’ mama hakuwa na mzaha
‘Mama jamani…. kwanini usiseme tatizo ni nini?’ Sindi aliongea kwa sauti ya kukereka akitupa mabega juu chini na kumtazama mama yake kwa kituo.

‘ wanakuona uko ukizunguka na yule mwanaume….’ mama akasema dukuduku lake
‘yupi?’ Sindi akadakia haraka sana, vinyweleo vikimsimama
‘Mi namjua?.....yule mlimuokota porini uko sijui wapi…. watu wanakuona naye mawio kwa machweo….tukueleweje?’ akamshikia kiuno binti yake na uso sasa ukimkunjuka kiasi baada ya kusema dukuduku lake.

Sindi akashusha pumzi kama mtu aliyeshtukizwa na taarifa ile, macho ya wasiwasi yalimcheza lakini moyoni alijua haikuwa vile watu walivyofikiria
‘kwa hiyo nisiongozane na watu?’ akauliza kwa unyonge
‘alipokuwa hayupo uliongozana na nani?.... watu hapa wanamjua Nyanza na hivi tunangoja kumfuta huyo Nyanza…..umeanza kunyooshewa kidole juu ya mtu asiyehusika kwa ndewe wala sikio…. mahari kipande imeshaliwa usitake tuozwe wote humu kwa mtu mmoja….’ Mama alimpasulia ukweli na akitoka pasipo kumpa nafasi ya kujitetea.

Sindi akaketi kitandani kwa kujipweteka. Alifumba macho taratibu na kuyasikilizia maneno ya mama yake. Yalimuuma kuliko kidonda kilichotoneshwa. Ile kauli tu ya kumfuta Nyanza ilimuumiza sana. Mpaka dakika ile alikuwa hajamwambia Nyanza chochote kuhusu yeye kutolewa mahar na Mzee Dunia.  Alikaa vile akiwa amefumba macho kwa sekunde kadhaa kabla ya kushusha pumzi ndefu zilizomfanya akinyanyue na kukishusha kifua chache chenye matiti mateketeke yaliyokuwa yamesitiriwa na ile khanga kifuani.

Alifumbua macho na kuytatembeza mule chumbani kana kwamba alikuwa akitafuta kitu ambacho kingempa faraja muda ule. Hakuona! Akayatuliza macho yake kwenye kikapu cha nguo kilichokuwa umbali mfupi toka pale, akikitazama pasipo kukitambua akilini. Alikuwa na mtihani mkubwa mbele yake, mtihani ambao hakutaka kujipa hata nusu ya sekunde kuufikiria hali akijua kutokuufikiria  kusingesaidia.
888888888888888888

Baada ya chakula cha usiku Sindi aliingia kulala pamoja na wadogo zake. Wakati wao wakitandika kitanda na kuweka sawa mazingira ya kulala. Sindi alikuwa akinyoosha nguo kwa pasi ya mkaa huku akimulikwa na mshumaa uliokuwa unawaka juu ya kigoda kilichokuwa mbele yake.

Walikuwa wakiongea na kucheka, wakikumbushana matukio ya kufurahisha ya siku hiyo. Vicheko vyao vilitulia ghafla walipohisi dirisha lao la mbao likitikisika. Wakasikilizia kidogo na kwa mara nyingtine dirisha lilitikisika tena na wote wakatazamana, ni kama vile waliijua ile ishara ilimaanisha nini. Sindi akanyanyuka haraka na kukimbilia dirishani na wakati huo huo wadogo zake wakimfuata na kumsaidia kuchungulia. Nyanza aliyekuwa chini ya mti alipunga mkono na wasichana hawa wakaomuona. huku wakicheka kichinichini walimsaidia Sindi kutoka nje kupitia pale dirishani kisha wakafunga dirisha na kurejea haraka ndani, wakikimbilia kitandani na kuunganisha mito. Walifanya haraka haraka kwa kuifunika ile mito mithili ya mtu aliyelala.

Kule nje Sindi alitembea kwa kunyata mpaka alipomfikia Nyanza aliyekuwa amesimama kwenye giza kidogo. Sindi akataka kumkumbatia Nyanza lakini mikono yake ilipanguliwa kwa kasi na kumfanya Sindi amtazame Nyanza kwa mshangao
‘nini tena?’ Sindi aliuliza akizidi kumsogelea Nyanza

‘ameanza kuwa wa maana sana kuliko mimi?’ Nyanza aliongea kwa ghadhabu
‘Nani?’ Sindi akauliza akitupa mikono yake yote miwili hewani
‘Jerry!’ kwa sauti ya kiume iliyojaa wivu, Nyanza alilitamka jina la Jerry na kumfanya Sindi ashushe pumzi tena. Jioni ile alikuwa amegombana mama yake kuhusiana na Jerry na sasa Nyanza alikuwa amemkasirikia sababu ya Jerry. Kichwani mwake hakuona sababu ya watu hawa wawili kumhofia Jerry ambaye kwake alikuwa kama mwanakijiji mwingine yoyote yule, achilia mbali ugeni wake kijijini.

‘Amekuwaje?’ Sindi aliuliza kwa ukali kidogo na kuzidi kumpandishia Nyanza hisia za wivu
‘ina maana hujui unachofanya au umeamua kunidharau?’ Nyanza alizidi kuja juu
‘Nimefanya nini?.... kuongoza naye ndio kumezua ugomvi au ni nini?’ Sindi sasa alionyesha kukereka zaidi

‘ona unavyonijibu kwa jeuri….kwa vile mimi maskini eeh…. kwa vile sina kazi ya maana Sindi….’ Nyanza alikuwa akilalamika na Sindi alimkatiza
‘Nyanza kama utarudia tena hizi kauli zako za mimi maskini sijui sina kazi….nakuapia tutatengana vibaya zaidi unavyowaza…. kwani hao wenye kazi siwaoni au unadhani hao wenye pesa siwaoni…..unadhani kwanini mpaka dakika hii nimetoroka kwetu kuja hapa?.... na kama mwito huu ni wa shari…usiku mwema’ Sindi aliongea kwa jazba akitaka kugeuka na kuondoka. Nyanza alimdaka na kumzuia asiondoke

‘nimekuona naye jioni ya leo…naumia Sindi mwanaume mwingine anapokusogelea vile’ Nyanza sasa sauti ilikuwa ya kulalamika
‘Wivu nyanza!....huu wivu ulionao ndio unafanya tunagombana kila siku….Jerry hajanitongoza na ni mtu mwenye heshima zake na sidhani kama anawazia unavyowaza wewe’ Sindi alijitetea
‘Mimi ni mwanaume mpenzi wangu…. najua inavyokuwa na nakuhakikishia Sindi…Jerry atatutenganisha usipokuwa makini’ Nyanza alizidi kushusha malalamiko mikono  yake ukimvutia Sindi kwake

‘Una uhakika gani?.... ananichukulia kama dada yake na si zaidi ya hapo…. hebu tuachane na hayo kwanza….’ Sindi aliyakatisha mabishano yao na kujisogeza kwa Nyanza zaidi kiasi cha kuwa sambamba pua kwa pua
‘Nimevumilia mwaka sasa…. niahidi nitakubikiri mimi Sindi’ Nyanza alisema kwa sauti yenye mihemo ya mahaba wakati akizipapasa chuchu za Sindi kwa matamanio ya hali ya juu
‘Mimi ni wako jamani…’ Sindi alijibu akijaribu kuutoa mkono wa Nyanza uliotaka kuzama ndani ya blauzi yake nyepesi aliyokuwa amevaa

Wakapapasana, wakichezeana na Sindi alipogundua Nyanza alikuwa katika hali mbaya, alicheka akiitazama suruali yake iliyokuwa imetutumka eneo la mbele. Akajitoa mikononi mwa Nyanza na kumrushia busu akianza kurudi mbio kule dirishani. Nyanza aligugumia maumivu  ya msisimko alioupata. Alikuwa akiingoja kwa hamu siku ambayo angeliupokea usichana na wa Sindi. Aliiota siku hii, aliitamani mno na sasa alitaka ifike kwa namna yoyote ile akihofia kuzidiwa kete na huyu mgeni asiyejua alikotokea.

Wakati Sindi na Nyanza wakimjadili Jerry Agapela, yeye alikuwa kitandani katika moja ya vyumba nyumbani kwa mwenyekiti. Chumbani alimokuwemo, kulikuwa na kijana wa mwenyekiti aliyekuwa anagundisha viatu vyake. Umeme uliokuwa katika nyumba ya mwenyekiti ulimsaidia Jerry kusoma kitabu alichokuwa nacho mkononi lakini mara kadhaa akikitua na kuzungumza na yule mtoto wa mwenyekiti aitwaye Chidi.

‘nani Sindi?....hahahahaaaa yule kwanza kumpata inahitaji nguvu ya ziada’ Chidi alizungumza akicheka wakati wakimjadili Sindi
‘Kwanini?’ Jerry aliuliza kwa pozi kidogo akiwa amelala chali, mkono mmoja ukiwa kisogoni na mwingine ukiwa na kitabu kilichokuwa kimelala kifuanim pake
‘She is smart aisee…. kuna jamaa anaitwa Nyanza ndio kashika makali pale….ila nasikia anasotea mwaka mzima hajala mzigo’ Chidi alisema akijiandaa kucheka
‘What! mwaka?…kwanini’ Jerry aliuliza kishabiki akijiinua kidogo na kulala kiubavu
‘Ohooo!.... Sindi hajaguswa yule…. anapangua mitego so kitoto’ Chidi alijibu na kumfanya Jerry alitoe macho kwa mshangao

‘Kwamba ni bado bikra au?’ alikuwa bado hajaamini
‘ndio maana yake’ Chidi akajibu akinyanyuka na kwenda kuviweka viatu vyake sehemu yenye upepo wakati huo Jerry akiwa anaonekana kutoamini alichosikia.

Akaliita jina la Sindi mara kadhaa na kumfanya chidi acheke na kutikisa kichwa…..


MAMBO YALIANZA HIVI..... USIKOSE KUJUA KILICHOJIRI

No comments:

Post a Comment



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger