Thursday, October 30, 2014

UREMBO NA LAURA:....MAFUTA YA MCHAICHAI (LEMONGRASS OIL)

Ya kwangu hayoooo mkononi

yenye majina ya kizungu hayoooo!!...na mmea wake huo hapo nyuma

Nadhani niihamishie alhamisi hii makala ya Urembo na Laura. Maana naona Jumatano huwa inakuwa na mambo mengi mno.

Yote kwa yote, natumaini kwa uwezo na kudra za mwenyezi  Mungu mu wazima. Tuendelee sasa!

Leo nakuletea Mafuta ya mchaichai. Sidhani kama huufahamu huu mmea wa mchaichai. Wengi wetu tunautumia kuungia chai. Na Majani yake si mageni kwetu. Ni mmea wenye harufu na ladha nzuri sana. Wakati mwingine hutumika kama kiungo kwenye chakula na kwenye mapishi, tumia kumarinate kuku kabla hujamchoma au kumkaanga utapenda na roho yako!

Sasa haya ndio  mafuta yake pia. Ni mafuta mazuri mno na kwa mtu yoyote anayejipenda, haya mafuta ni wajibu kuwa nayo. Ni mafuta yenye matumizi mengi kwa wakati mmoja

1. KUKUZA NYWELE ZILIZOKATIKA



Kuna wakati unaweza ukajikuta ukitumia hiki na kile tena kwa gharama kubwa saaaana ili kuzuia  kukatika kwa nywele au kuhangaika kuzikuza. Mafuta ya mchaichai ukiyachanganya na mafuta ya nazi (coconut oil) au mafuta ya Mzaituni (Olive Oil). Nakuhakikishia ni treatment nzuri sana ya nywele zako.

Unachotakiwa kufanya ni kumimina mchanganyiko wako kiganjani na kusugua kichwani kwa muda wa dakika mbili hadi tano. Kisha funika kichwa kwa kofia yako au funga mfuko wa plastic. Kaa nayo nusu saa hadi saa nzima. Kisha osha na shampoo yako.

Kwenye shampoo napo wengi tunakosea, tunatumia shampoo za nywele kavu wakati nywele zenyewe kavu basi ukitoka kuosha unywele umekakamaa wenyewe tunadhani ndio zimetakata kumbe ndio tunakaribisha kukatika kwa nywele.

Wakati mwingine, ongeza matone kadhaa katika conditioner yako unapotaka kusteam nywele. Matokeo utaniambia!

2. KUFANYIA  MASSAGE

Kuna watu wakisikia massage wanadhani ni kazi moja ngumu saaana kama kupasua miamba Lol!... massage ni kuchua… inawezekana unajisikia maumivu mahali, uchovu nk.. mafuta haya ni mazuri kwa shughuli hiyo. Kwa aina dada wenye waume na wapenzi haya ni moja kati ya mafuta unayopaswa kuwa nayo ndani mwako. 

Usiyapake peke yake yachanganye na mafuta ya Olive au nazi pia yapo mafuta ya massage hii topic nyingine sasa. hapa chukua  vijiko vinne vya mafuta ya nazi, weka kimoja cha mafuta ya Mchaichai

Weekend nzima mara uko vikoba, sijui wapi mara wapi na wapi…hupati hata siku moja na au muda ukamfanyia mwenzio hata message ya miguu jamani?.... aaah! Shoga, maisha ndio haya haya usimpet pet mzee leo mkiwa na furaha unangoja mpaka mkishachokana  au?... 

hivi ndio vionjo vyenyewe sasa na yalivyo na harufu nzuri…. Wallah asiposhukuru basi ana roho ya jiwe ukilikalia yallaaah! ukilibeba yallaaah!! Na si yeye tu unaweza kumuomba hata yeye akufanyie massage!... usione massage centre zinaibuka tu kama uyoga kuna raha uko weee hahahahaaa!

Na uzuri wake ni kwamba husaidia kuondoa maumivu ya misuli, kwa hili hata mimi shahidi ya haya mafuta. baada kukaa kwenye foleni wiki nzima...kupandia daladala dirishani... kukaa ofisini masaa... kusimama kituoni masaa...aaaah! massage muhimu bwanaaa!

3. KWENYE MAMBO YETU YALE
Hapa nashindwa kufunga vizuri maana ni Public lakini mchaichai ni moja ya mafuta ambayo huamsha ashki, huondoa harufu mbaya hasa kipindi umemaliza maliza kusindikiza wageni wenye makoti mekundu, namna ya kufanya siwezi andika hapa hahahahahaaaa.... haya na  huku chini pia huponya fangasi na kurutu kurutu vamizi za hapa na pale. 

Hata ukishafagia barazani kwako ili kuepuka vipele na nini na nini unachovya pamba kwenye mafuta, kidogo tu kisha  unasugulia sehemu fagio lilikopita. Unabaki msafiiii, unanukiaaa, mlainiiii yaani utajipenda mpaka ushangae.


4. KWENYE NGOZI.


Humu yamo pia… una losheni yako au cream yako unapaka mwili, basi unafanya kumix hivi kidogo tu. Kama umewahi kusikia kitu kinaitwa moisturizer kwenye vipodozi basi mafuta ya mchaichai ni moisturizer ya asili kabisaaa. Na hayatoi jasho.

AU Maji ya uvuguvugu, dondoshea matone ya mafuta halafu  loweka miguu yako humo dakika 45. Kisha sugua gaga lako sasa. Kama una harufu mbaya, ama fangasi, au magaga ndio yanaanza lazima utoke softiiii!...kama ndio mzee wako aiii huwezi pata kashfa babe yake anuka miguu ati hahahaaa!

5. KWENYE MAGONJWA

Mapunye, fangasi nk. Mafuta ya mchaichai ni dawa. kuna wakati watoyo wanakuja na mapunye toka shule uko, wakati mwingine minyoo tu inakuletea fangasi au ndio mambo ya kujaribisha mitumba… unatoka na ugonjwa wa ngozi hapo au utangotango…. Basi hii Unasugua kwenye tatizo kila siku, na baada ya wiki lazima uwe umepona labda kama tatizo ni kubwa la kuhitaji vipimo vikubwa. Lakini hizi fangasi za kawaida tu…. Hii mwisho wa matatizo!

MATUMIZI YAKE NI MENGI MNO
HAYA NI MACHACHE TU!


NB: Cha kukumbuka sasa ni kwamba haya mafuta usipopewa feki, hayo niliyokwambia hapo juu yanatekelezeka na  utagundua unayahitaji tu hapa na pale. 
  Kikubwa kumbuka ni makali kidogo hivyo kuna watu wachache ambao wana ngozi sensitive yaani wale ambao akipaka kitu chochote kigeni  rashes zinamtoka… 

kama wewe ni mmoja wapo: fanya hivi chukua paka shingoni, mkononi, au kwenye hairline (mstari wa mbele wa nywele) kaa nayo kwa saa 14…unaweza paka asb jioni ujicheki…kama hakuna chochote kilichotokea basi na ngozi poa na utayatumia bila shida yoyote

NATUMAINI NIMEKUONGEZEA UJUZI FULANI!!


6 comments:

  1. yaani we dada jamani unaelezea vizuriiiii mpaka nimecheka. asante sana nimepata kitu cha maana kweli. niliyaona mahari nikawa sijui matumizi yake

    ReplyDelete
  2. We call it miracle oil!!! Thank you for sharing.

    ReplyDelete
  3. Asante Sana kwa kweli nimepata faida kubwa ya mafuta ya mchaichai Mungu akubariki.

    ReplyDelete
  4. Nasikia yanaondoa visunzua ni kweli?

    ReplyDelete
  5. Samahani kipenz mafuta ya mchai chai nayapataje

    ReplyDelete



Snowfall Widget for Blogger


Snowfall Widget for Blogger