22
Pamella Okello alijikuta akiiachia simu idondokee mapajani
mwake pasipo kujitambua. Mikono ikalala juu ya usukani kiuchovu huku macho yake
yakitembea taratibu mule ndani ya gari na asielewe kila alichokitazama. Mdomo
wake uliokuwa wazi ulidhihirisha bumbuwazi lililomtembelea ghafla kwa wakati
ule.
Taratibu akashusha
pumzi na kufumba macho katika namna ya kuumeza ule ujumbe aliousoma kama mtu
anayemeza kaa la moto. Akatulia hivyo kwa sekunde kadhaa pengine akitaka
kuiweka sawa akili yake ama tu alitaka kupingana na kile kilichosomwa na macho
yake.
Alitaka sana kuishika tena simu na kurudia kuusoma ule
ujumbe, ajiridhishe kuwa haukutoka kwa Jerry lakini moyo ulisita alihisi
kuurudia mara mbili kungeuchana moyo wake vipande viwili. Akashuka garini kama
mtu aliyemriwa na kurudi ofisini kwake.
Dakika mbili mule ndani ya ofisi ilikuwa kama kukalia moto
kwa sekunde mbili tu. Alisimama akakaa, akawasha kiyoyozi na kukizima hapo hapo
akiinyanyua simu yake na kuirudisha mezani pasipo kuitumia. Kiwewe!
888888888888888888
Jerry Agapela alikuwa sofani akisoma gazeti moja la michezo
huku akitazama Luninga nyumbani kwa Meddy Hakim ambaye alikuwa pembeni
akiandika andika mambo kadhaa kwenye laptop yake, kisha akaitua pembeni na kumtazama
Jerry ambaye naye alitupa gazeti pembeni na kushusha pumzi ndefu akionekana
wazi lile gazeti lilikuwa geresha mikononi mwake.
‘Atakutafuta tu’ Meddy akamsemesha akimtazama kwa huruma
‘Sijali….’ Jerry akajibu uso wake ukilisaliti jibu lake
waziwazi
‘unajali Jerry….nimekushauri umjibu hivyo kupima kama kweli
hajali wewe kuwa na mtu mwingine…. uhitaji kuhamanika kama hivi’ Meddy kwa
msisitizo. Aliona dhahiri ushauri aliompa Jerry ulikuwa unamtesa sasa baada ya
kumjibu uongo Pamela ambaye hakumjibu kitu chochote. Hali ile ilimletea Jerry
wasiwasi.
‘Angalau angenipigia kuthibitisha….it shows hanipendi
kweli….nimemjibu vile na bado yuko kimya…hata meseji ya kutaka ukweli hajatuma
let alone kunipigia kabisa…’ Jerry akababaika na kuobnyesha hofu yake waziwazi.
‘She is a smart woman Jerry!.... usitarajie atajiburuza mbele
yako after the whole drama…. leo ni birthday yake…hebu mchunie sasa na usimtamkie
lolote kama nilivyokushauri…jibu ulilompa liwe zawadi kwake….i swear hatamaliza
saa 24 toka sasa hajakutafuta…. na kama atavuka hizo saa 24 move on Jerry she
is not into you for real!’ Meddy akamjibu kwa kirefu, akinyanyuka na kwenda
zake jikoni. Jerry akakipakata kichwa chake kilichoanza kuwa kizito mithili ya
jiwe la mwamba.
Meddy akarejea pale sebuleni akiwa na vinywaji kwenye glasi
mbili. Akamuwekea Jerry mbele yake kwenye kistuli kidogo nay eye kurudi kukeri
pale pale kimtazama Jerry namna alivyokuwa amekipakata kichwa chake.
Akamsikitikia!
Kama mtu aliyekurupushwa Jerry akainua kichwa na kumtazama
Meddy.
‘It is over…I’m done Meddy… nitaumia hivi mpaka lini…lini?’
Jerry akauliza kwa sauti iliyojaa maumivu
‘Now you are talking like a man!....’ Meddy akakolezea
akinyanyua glasi yake hewani kama ishara ya kuunga mkono kauli ya Jerry
‘Baadaye..’ akaaga kwa kunyanyuka ghafla na kutoka mule ndani
pasipo kumuaga Meddy vizuri. Meddy akakunja uso na kumshangaa lakini hakutaka
kumzuia. Akamwacha atoke na kwenda zake. Dakika moja baadaye simu yake iliiita
na mpigaji alikuwa Pamella.
‘Yes mama sema…’ Meddy akaitikia akinyanyuka kwenda kufunga
mlango ulioachwa wazi na Jerry
‘Serena Hotel kuanzia saa moja jioni….my birthday party…don’t
miss it dear’ Pamella akatoa maelezo yake
‘Nakuja mwenyewe au nije na kampani’ Meddy akauliza
akitabasamu na akilisubiria jibu la Pamela kwa hamu kubwa
‘Whatever dear!...ila usikose tu’ Pamela akajibu baada ya
kusita kwa sekunde kadhaa. Wakaagana na Simu zikakatwa. Meddy akacheka peke
yake, akitikisa kichwa pia huku taratibu akiifuata rimoti na kuongeza sauti ya
luninga iliyokuwa inaonyesha wimbo mmoja wa mahadhi ya dancehall. Akaucheza
akwa furaha asijue alichokuwa anakifurahia.
88888888888888888888
Jerry Agapella alielekea hotelini akapumzika na kufanya mambo
yake kwanza kisha akatoka na kurudi garini ambako alielekea anakobadilishia
nguo na kuvaa anavyojua kisha akaliacha gari hapo na kurudi kwa Sindi Nalela.
Jioni hiyo akamkuta Sindi akimalizia kupika chakula cha usiku
kwenye kordo. hawakusalimiana. Baada ya kuingia ndani na kuketi dakika mbili
ndani, Sindi akaingia na kumpita tu bila kumsemesha chochote. alikuwa na
sufuria mkononi alilolishika kwa vitambaa na kwenda kulitua chini karibu na
stuli iliyokuwa na beseni la vyombo kwa juu.
Alipogeuka ili atoke Jerry akamuita, akasimama bila kugeuka
‘Ni jeuri au nini?’ Jerry akamuuliza
‘kwani vipi?’ Sindi naye akamuuliza akiwa kasimama vile vile
pasipo kugeuka
‘nenda kamalize shughuli zako nataka kuongea na wewe’ Jerry
akamhimiza
‘Nimeshamaliza’ akajibu Sindi kimkato na Jerry akajikuta akimshangaa
‘Una ugomvi na mimi?’ akamuuliza na hapo ndipo Sindi
alipogeuka kwa hasira
‘Nyanza anakuja lini?.... uliniahidi nini?.... sioni chochote
ulichotimiza tangu unilete hapa…hii ina maana gani?’ Sindi akauliza kwa hasira
na Jerry akaduwaa kwanza kwani hakutegemea maswali kama yake wakati kama ule.
‘Okay!....ndio maana nimekwambia umalize shughuli zako ili
tuongee’ akajitetea akijua alichomuitia
mwanzo hakikuwa kile alichotaka kuongea sasa. Sindi ahakumjibu alitoka na
kuishia zake nje akimuacha Jerry ametabua uso kwa mshangao.
Wiki ilikuwa imekatika tangu usiku ule aliomgusa Sindi.
Asubuhi yake hawakusemeshana na Sindi alionekana kuwa na hasira za hapa na
pale. Jerry akaondoka na kwenda kwa Meddy ambako alikaa siku sita huku akiwa
amemuaga Sindi kuwa anafuatilia mambo yake mkoani.
Siku sita alizobaki mwenyewe Sindi alipata nafasi ya
kutafakari mengi mno, alikumbuka nyumbani, alimkumbuka Nyanza, aliwakumbuka
rafiki zake na wazazi wake lakini kikubwa alikumbuka ahadi za Jerry tangu
alipokuwa kijijini mpaka alipomleta mjini. Akazihesabu ahadi zilizotimizwa,
hakupata hata moja ya kumtuliza, akawaka hasira, akimsubiri Jerry kwa ghadhabu
na ndio hivyo kajikuta akimnunia tangu alipoingia.
Baada ya pilika pilika zote za jioni hadi giza lilipoingia,
Jerry na Sindi wakakaa mezani kula, huku ukimya ukiwa mheni wako katika kipindi
chote cha mlo. Hakuna aliyemsemsha mwenzake wala aliyedai chumvi imezidi ama
hata kuomba kioande cha limao akolezee kwenye samaki. Walikula kimya kimya.
Wakapisha kuingia maliwatoni na ndio sasa wakaketi mmoja
kitandani mwingine kwenye sofa. Wakitazamana.
‘Nipe muda kidogo Sindi mambo ya hela hayajakaa sawa’ Jerry
akajitetea
‘Sijakataa kuhusu hela ila lini sasa atakuja?’ Sindi
akasisitizia ahadi iwe wazi
‘mwezi ujao nadhani nitakuwa nimepata nauli’ Jerry akajibu tu
kumfurahisha Sindi akijua wazi hakuwa hata na mpango wa kwenda kijijini kule
sababu ya Nyanza.
Nuru ikachomoza usoni pa Sindi baada ya jibu lile, mwenyewe
uzuri wake ukichomoza upya na kule kuoga na kutakata, kula na kutulia ndani.
Sindi alikuwa amenawiri mno. Rangi yake nyeupe ikawiva vizuri, ngozi yake
ikalainika na kung’aa kama ya mtoto mchanga achilia mbali nywele zake za asili
zilizokuwa laini kujaa kichwani na kuuongezea uzuri wa Sindi. Jerry akameza
mate!
Sasa wakaongea mengine mengi na Jerry akamkabidhi Sindi pesa
ya mtaji aliyokuwa anaitaka.
‘Mbona mtaji nimeshapata kwa kusuka…. nimenunua vifaa vya kazi vile pale’ Sindi akamuonyesha Jerry mfuko wa
plastiki uliokuwa na hivyo vitu
‘Basi hiyo ongezea tu’ hakutaka airudishe
‘Hapana, hii tuweke kwenye kibubu, kujazia jazia kodi ya chumba
nami nikipata katika biashara yangu nitakuwa najazia tu…mwisho wa mwezi tuna
kitu cha kulipa kodi, umeme na maji kwa pamoja’ Sindi akatoa mawazo yake na
Jerry akajikuta akiitikia na kukubaliana naye, moyoni akikiri Sindi alikuwa na
akili za maisha.
Wakachangamka kwelikweli na mazungumzoa yakapamba moto. Saa
nne usiku wakatengana kwenye pazia na kuutafuta usingizi. Lakini ni kama usiku
ilikuwa unajirudia. Hawakulala walikodoleana macho kwenye pazia na wasionane.
Jerry akavumilia kidogo na usiku ulipotengamaa akashindwa,
akanyanyuka na kumfuata Sindi kitandani. Kimya kimya Sindi naye akageuka pasipo
kubisha wala kusukumana akampokea Jerry maungni mwake na kumruhusu amguse
alipotaka. Hali ile ikazidi, hakuna aliyetaka kumtoa mwenzake maungoni mwake
Jerry ambaye akili yake ilishahamia sayari nyingine akajiinua
kidogo na kumuuliza Sindi kama kama alikuwa tayari kwa lile tukio alilotaka
kulifanya na Sindi akaitikia kwa kichwa nap engine hakuushirikisha ubongo. kwa
wakati ule hata ungemwambia tukamchinje Nyanza nadhani angeitikia ndio na
asijielewe.
Zikazuka purukushani za hapana na pale na alajiri ya asubuhi
hiyo Jerry Agapela akambikiri Sindi
Nalela. Akili ilipomrejea Sindi alilia mno asubuhi ile kwa majuto na misuto!
ila ndio chenza lilishamenywa!
888888888888888888888
Taa za rangi hafifu ziliongeza nakshi katika sebule hili
kubwa ya kisasa. Muziki wa taratibu wa ala uliokuwa ukisikika toka kwenye spika
kubwa zilizokuwa hapo sebuleni, zilijenga mahadhi ya mahaba yenye kuvutia
zaidi.
Pamela Okello alikuwa amesimama dirishani akitazama nje,
mkono akiwa na glasi yenye mvinyo ambayo aliipeleka mdomoni mara kadhaa mpaka
pale alipoona asingeweza kuipeleka mdomoni tena. Alishusha pumzi na kugeuka,
akapiga hatua chache na kuifikia meza iliyokuwa na vinywaji mbalimbali. Akaitua
ile glasi na kulifuata kochi kubwa
lililokuwa mbele yake.
Pamela akaketi hapo, uso wake mzuri ukionyesha kujawa na
mahangaiko yaliyokisumbua kichwa chake. Akajikunyata kwenye lile kochi
akiitazama sakafu pasipo kuitambua akilini mwake.
‘Jerry..’ akaliita hili jina kwa sauti
‘Nooo…Noooo’ akapaza sauti akiyukla mwenyewe huku akihema kwa
ghadhabu. Akasimama haraka na kuifuata ile glasi yenye mvinyo, akaibugia kwa
mkupuo hali mikono ikimtetemeka
‘Bastard!...’ akapayuka tena na kuibamiza ile glasi sakafuni,
machozi yakimvamia na kumtetemesha. Akalia peke yake kwanza na akionekana wazi
kutaka kupambana ile hali.
‘Ooh Mungu wangu….’ akalalamika akitembea kivivu na kuketi
kwenye sofa dogo. Akaibebesha miguu yake katika sofa na kuikumbatia akizidi
kuhamanika.
‘Simu yake iliyokuwa kwenye mkono wa kochi hilo alilokalia ikaingia
ujumbe na Pamela akaichukua na kuufungua
‘sikufichi kitu Pamela..ni kweli Jerry anatoka na Sindi kama
alikujibu hivyo nadhani alimaanisha….vipi Patrick alikurudisha salama after
party?’ aliusoma ule ujumbe akimalzia kwa kufumba macho kuashiria ujumbe ule ulimuumiza sana.
Meddy alikuwa anaushindilia mkuki moyoni mwake. Alishavumilia
kutokusikia lolote toka kwa Jerry lakini alipoutaka ukweli wa ile meseji
kupitia Meddy Hakim, rafiki mkubwa wa Jerry, jibu alilolipata lilimkata maini,
likamuwewesesha na zaidi likamfanya aukumbuke uwepo wa Sindi na kujaribu
kujilinganisha naye mbele ya Jerry. Isingewezekana aachwe kupapatikiwa kirahisi
rshisi sababu ya Sindi!
Akiwa katika hamaniko lile, kengele ya mlango ikalia,
akasonya akiitazama saa ukutani na siweze hata kukisia ugeni ule ulikuwa wa
nani asubuhi ile. Akatoka chumbani kwake na kuelekea sebuleni ambako,
aliukorokochoa mlango na kuufungua.
akanyoosha shingo yake na kuchungulia nje kupitia mlango wa
chuma uliokuwa umetangulia kabla ya ule wa mbao. Moyo ukapiga mkambi! Alikuwa
Fiona Agapela mama wa kambo wa Jerry. Maswali mia moja yakakimbizana kichwani
mwake kwa kasi ya ajabu kidogo yaubomoe ubongo wake. Hakuwahi kumzoea mwanamke
huyu wala kumkaribisha kwake sembuse kusalimiana naye kwa bashasha sasa ni kipi
kilichokuwa kimemleta asubuhi ile?
Alimtazama Fiona Agapela kwa Mshangao kupitia lile Lango la
chuma hali Fiona akimtazama kwa uso uliojaa mashaka na wasiwasi
uliochanganyikana na hali ya kutia huruma. Pamella akahisi ule haukuwa ujio wa
heri na ndivyo ilivyokuwa!
……. HAYA SASA….. FIONA KAFUATA NINI KWA PAMELA?
No comments:
Post a Comment