Friday, September 9, 2011
KUSAMEHE....shughuli nzito isiyohitaji mbeleko!
...wahenga walisema hakuna aliyemkamilifu...kwamba binadamu si malaika kuwa kila atakachofanya kimekamilika. mapungufu yapo na ndio hasa yanayotufanya sisi binadamu tuitwe binadamu na si malaika!
katika maisha kuna kukosea na kukosewa na hapo ndipo neno SAMAHANI linapotumika. yapo maudhi ambayo mdau unaweza ukasamehe papo hapo na yapo yale ambayo unaweza kuchukua wiki, miezi au hata miaka mpaka kufikia hatua ya kusamehe.
...kila binadamu ana haiba yake wapo wanaweka vinyongo hata baada ya kusamehe na wapo ambao husamehe na kusahau...yote kwa yote kumsamehe mtu ambaye hajakuomba radhi wala kujutia alilokufanyia ndiyo shughuli nzito isiyohitaji mbeleko...
...Zipo faida nyingi za kusamehe bila kujali kama aliyekukosea amekutaka radhi au la! bila kujali kama ulilkosewa ni kubwa au la! cha msingi ni kumsamehe mtendaji kosa bila kinyongo...
Faida moja wapo ni kuwa unapomsamehe mtu unajihisi kuutua mzigo moyoni ijapokuwa mtu anapokutaka radhi huwa anakusaidia kupunguza uchungu wa kosa ulilotendewa lakini bado wewe mtendewaji unahitaji kujifunza kusamehe toka moyoni bila kujali kama umeombwa radhi au la!
pili, unapomsamehe mtu hata mbingu hufurahi, kwa vile ni kati ya mambo ambayo dini zetu hizi hutufunza na kututaka kusamehe kama ambavyo Mwenyezi Mungu hutupatia msamaha bila kinyongo!
Tatu, amini usiamini, unapokosewa au kutendewa vizivyo nawe ukaumia na kulia, waama ukasononeka sana bila mtendaji kukutaka radhi ingawa anajua kosa lake kisha ukamsamehe...baraka huongezeka maishani mwako! jaribu leo na utaligundua hili...
Mwisho, kusamehe ukupa hali ya utu, hali ya kuthamini, hali ya afya na kukuondolea masononeko, maisha ni mafupi sana kuyatumia kumchukia mtu au kumkasirikia...kumbuka tu kuwa hata wewe ni mara nyingi umewakosea watu aidha kwa kujua au kutojua na pengine huwahi kuwataka radhi lakini leo hii wanakuthamini, wanakupenda na kukujali...na kuna hali ya msuto moyoni mwako!
...ni hayo tu na zaidi nakazia, samehe bila kujiuliza, kisasi kitakuumiza tu! samehe bila mipaka, Mungu atakupa mibaraka, samehe bila kuombwa msamaha, na utaishi maisha ya furaha!
LAURA!!!
Thursday, September 1, 2011
...IT'S BEYONCE....KIMFAACHO MTU CHAKE JAMANI!
Hongera zake....katika kuianza safari ya kuwa mama, wenyewe wanaita lifetime job hakuna likizo wala malipo ya ziada....
wishing them all the Best!
...Back again...Heri ya IDD pili!
i love the song a lot na leo nimeuchezaaaa mpaka baaaasi....dedication to all of you...
huyu kaka anayemalizia malizia hahahaaaaa yaani anaiwakilisha hasa ndombolo ya solo,
.....YAANI NI BURUDANI BARDAAAA...IDD NJEMAAAA
LAURA
huyu kaka anayemalizia malizia hahahaaaaa yaani anaiwakilisha hasa ndombolo ya solo,
.....YAANI NI BURUDANI BARDAAAA...IDD NJEMAAAA
LAURA
Thursday, June 16, 2011
....KUMRADHI WADAU
....Nimepata meseji kadhaa zenye kuulizia hiki na kile kuhusu blog...nakiri nimetoweka kidogo kutokana na majukumu ya hapa na pale ila punde hali itarudi kuwa sawa.
Naheshimu mawazo na mchango wenu hata mkiwa wawili kwangu ni sawa na watu elfu mbili...
Naahidi nitayafanyia kazi maombi yenu ya hadithi na kupost hiki na kile mara kwa mara. ni majukumu tu ndio yanapelekea hali hii, majukumu ya kutafuta pesa ambazo zimeota matairi ukisema uzifukuzie kwa miguu ndio utabaki unasindikiza wenzio...shurti ujitume hasa ukitaka kuzifikia!
alamsiki! tuzidi kuwa pamoja katika maswali na hoja!
Laura
Naheshimu mawazo na mchango wenu hata mkiwa wawili kwangu ni sawa na watu elfu mbili...
Naahidi nitayafanyia kazi maombi yenu ya hadithi na kupost hiki na kile mara kwa mara. ni majukumu tu ndio yanapelekea hali hii, majukumu ya kutafuta pesa ambazo zimeota matairi ukisema uzifukuzie kwa miguu ndio utabaki unasindikiza wenzio...shurti ujitume hasa ukitaka kuzifikia!
alamsiki! tuzidi kuwa pamoja katika maswali na hoja!
Laura
Sunday, June 12, 2011
PERUZI YA ENZI....YOU ARE STILL THE ONE BY SHANIA
..The lovely, romantic and so sweet song to dedicate to the one you love...
have a nice weekend
have a nice weekend
MSEMO WA LEO....
...ALIYEKUPA WEWE KUMBI NDIYE ALIYENINYIMA MIMI KITI...
..Tunakumbushwa tu kuwa majaaliwa uliyojaaliwa wewe umepewa na na yule aliyemnyima mwingine hayo majaaliwa...usiyaringie..usiyatambie kwa vile mtoaji ni mmoja anaweza kukugeuzia kibao!
na halikadhalika ukipata shukuru ukikosa usikufuru kwani mpaji ni Mola, anagawa kulingana na matakwa yake!
kama aliviumba vidole bila kufanana basi si ajabu nasi kutokufanana kimajaaliwa
..Tunakumbushwa tu kuwa majaaliwa uliyojaaliwa wewe umepewa na na yule aliyemnyima mwingine hayo majaaliwa...usiyaringie..usiyatambie kwa vile mtoaji ni mmoja anaweza kukugeuzia kibao!
na halikadhalika ukipata shukuru ukikosa usikufuru kwani mpaji ni Mola, anagawa kulingana na matakwa yake!
kama aliviumba vidole bila kufanana basi si ajabu nasi kutokufanana kimajaaliwa
Wednesday, June 1, 2011
USICHUKIE UKIKOSOLEWA!
habari zenu wadau, natumaini kwa kudra za mwenyezi Mungu bado mnapomua bila ushuru, hilo pekee ni jambo la kumshukuru Karima mwenye Huruma kwani waliotangulia mbele ya haki si kwamba wao walikuwa wenye dhambi kuliko sisi, basi tu tunapewa nafasi kadhaa turekebishe njia na mapito yetu
Haya ndugu baada ya salam hiyo hebu nirejee katika mada! kusema kweli hakuna binadamu mwenye akili timamu asiyependa sifa tena sifa njema za kutukuka. kila mmoja wetu anapenda kuonekana bora mbele za watu. tunachotofautiana ni namna kila mmoja anavyozipokea hizo sifa.
...wapo wanaozipokea na kuzidisha juhudi bila kubadili mienendo ya tabia zao
...wapo wanaozipokea kwa mikogo na kubadilika na kuanza nyodo
...wapo wanaozipokea na kubweteka wakidhani safari imefika ukingoni kumbe kama ni mlo basi ndio chai ya asubuhi.
Lakini lazima tukumbuke binadamu si malaika kwamba katika safari yake ya kimaisha kila atakalo tenda litakuwa jema na la uhakika. kuna mambo unaweza kuyafanya nawe ukaona uko sahihi kabisa na wanafiki pembeni wakakujaza sifa hewa nawe ukaona umefika unapotaka kumbe uko uendako kuna kuanguka, kuna kuporomoka, kunapotoka, na kuumbuka!
inapofikia hatua hii wanaokupenda na wasiokupenda watakusahihisha iwe kwa njia ya kistaarabu au ya aibu, vyovyote vile watakwambia bila soni kwamba hapa si hivi pale si vile...
hapa sasa ndio pa kuonana wabaya ila mimi binafsi nakukumbusha, usiamini sifa mia za watu ukamdharau mtu mmoja mwenye hoja tofauti. wewe si malaika tulia na utafakari uambiwalo pengine kweli hauko sahihi
siku zote changamoto za maisha huletwa na vitu vilivyo negative, ni kupitia makosa mtu hujifunza kilicho sahihi, ni kupitia kuanguka mtu hujifunza kusimama kwa bidii hivyo usiogope wala usichukie kukosolewa hata kama unaona anayekukosoa hana hoja yenye mashiko msikilize tu! yawezekana akakupa kilicho bora au mawazo mapya kupitia kukosoa kwake!
... sifa pekee hazijengi, believe me! nimexperience hilo na nimegundua makosa yangu katkka safari ya maisha yangu ndio yamenifikisha hapa nilipo, ningekataa kukubali kuwa sikufanya makosa basi si ajabu ningeendelea kukosea mpaka leo.
...Nawatakieni Alhamisi njema yenye baraka tele
...
Haya ndugu baada ya salam hiyo hebu nirejee katika mada! kusema kweli hakuna binadamu mwenye akili timamu asiyependa sifa tena sifa njema za kutukuka. kila mmoja wetu anapenda kuonekana bora mbele za watu. tunachotofautiana ni namna kila mmoja anavyozipokea hizo sifa.
...wapo wanaozipokea na kuzidisha juhudi bila kubadili mienendo ya tabia zao
...wapo wanaozipokea kwa mikogo na kubadilika na kuanza nyodo
...wapo wanaozipokea na kubweteka wakidhani safari imefika ukingoni kumbe kama ni mlo basi ndio chai ya asubuhi.
Lakini lazima tukumbuke binadamu si malaika kwamba katika safari yake ya kimaisha kila atakalo tenda litakuwa jema na la uhakika. kuna mambo unaweza kuyafanya nawe ukaona uko sahihi kabisa na wanafiki pembeni wakakujaza sifa hewa nawe ukaona umefika unapotaka kumbe uko uendako kuna kuanguka, kuna kuporomoka, kunapotoka, na kuumbuka!
inapofikia hatua hii wanaokupenda na wasiokupenda watakusahihisha iwe kwa njia ya kistaarabu au ya aibu, vyovyote vile watakwambia bila soni kwamba hapa si hivi pale si vile...
hapa sasa ndio pa kuonana wabaya ila mimi binafsi nakukumbusha, usiamini sifa mia za watu ukamdharau mtu mmoja mwenye hoja tofauti. wewe si malaika tulia na utafakari uambiwalo pengine kweli hauko sahihi
siku zote changamoto za maisha huletwa na vitu vilivyo negative, ni kupitia makosa mtu hujifunza kilicho sahihi, ni kupitia kuanguka mtu hujifunza kusimama kwa bidii hivyo usiogope wala usichukie kukosolewa hata kama unaona anayekukosoa hana hoja yenye mashiko msikilize tu! yawezekana akakupa kilicho bora au mawazo mapya kupitia kukosoa kwake!
... sifa pekee hazijengi, believe me! nimexperience hilo na nimegundua makosa yangu katkka safari ya maisha yangu ndio yamenifikisha hapa nilipo, ningekataa kukubali kuwa sikufanya makosa basi si ajabu ningeendelea kukosea mpaka leo.
...Nawatakieni Alhamisi njema yenye baraka tele
...
Subscribe to:
Posts (Atom)



