ANNIE NG'INGO...
 |
| Annie |
Nimeamua tu siku moja moja kuwa na mgeni humu
ndani…nimuulize machache, tuongee hiki na kile. Wahenga walisema mgeni baraka
nami ndio nazikaribisha baraka hizo ndani ya blog hii…. Naanza na Annie huyu dada nimependa tu na hulka yake, hana makuu na mtu hana chokochoko na watu...hajui kujivuna wala kupanda seuze ile kujiskia juu wakati aliyejuu ni Maulana peke yake. Nilimuuliza machache naye bila hiyana akanijibu
LAURA: Je una
Nickname yoyote mbali na jina lako?
ANNIE: Hapana sina
LAURA: Heheheee you need one darling! may be nikupe nickname moja Kamamaa*wink*
LAURA:Uko
katika mahusiano?…kama ndio unayaelezeaje mahusiano
yako, kama hapana kwanini hauko katika mahusiano?
ANNIE: Hapana siko kwenye mahusiano yoyote,sababu nimeamua kutulia
kwa muda ili niishi maisha ya peke yangu
LAURA: Time will tell dear, you might need somebody to lean on someday....wish you luck!