Muda wote huo nilikuwa nimeshastahimili ile harufu mbaya niliyokuwa ninaisikia na sasa nilishanza kuhisi kichefuchefu! Nikaona nisipoaga mapema nitaweza kutapika mbele ya wenyeji wangu!
Binafsi nilihisi kuna kinyesi cha mtoto kimesahaulika pale ukumbini au choo cha mle ndani hakikuwa safi! Nikashindwa kuelewa kama iloma hakuwa akikerwa na ile harufu au ndio pua zimeshajizoelea kuvuta uvundo wa aina ile!
Niliondoka kwa iloma na kurejea nyumbani. Niliingia nyumbani huku tayari giza likiwalimeshatanda. Ilikuwa saa mbili na robo. Nilimkuta dada yangu Debby akiwa ananingoja wimawima ukumbini hali mama akiwa amelala sofani akitazama televisheni. Niliwasabahi akaitikia mama peke yake. Nikajiweka sawa!
“ Karen! Hivi ni nini kinaivuruga akili yako we mtoto?”
“hata salamu Debby?” nilimkatiza
“Najua u mzima wa afya, lakini huku unakoelekea nadhani utakuwa na matatizo katika akili yako”
Nilishusha pumzi fupi ya kero, nikamtaza Debby kwa hasira .
“ Debby! kaka brian alichanifokea sana asubuhi hivyo inatosha, hakuna mtu anayehoji kilichonikuta, hakuna mtu anayehoji sababu za msingi nilizonazo wote mnaniona hayawani tu! Kama ni kustarehe basi ningeanza siku nyingi na si leo hii nikiwa na kazi na maisha yangu” nilikuja juu na tayari machozi yalisha tengeneza mfereji mashavuni mwangu. Niliwaza juu ya kubakwa kwangu na kulinganisha na lawama ninazopewa nikaona uonevu mkubwa juu yangu!
“ Okey! Nini kilichokufanya ulale nje jana?...brian amenipigia simu akanieleza kuwa umerejea asubuhi ya leo na tena ulilala nje bila hata taarifa kwa mama” Debby sasa alihoji taratibu na kuketi kochini
“ haitabadili akili ya mtu kati yenu! Endeleeni kuniona punguani!” nilimjibu kwa mkato na kutokomea chumbani. Nikajifungia na kuanza kulia. Nililia muda mrefu na hatimaye nikapitiwa na usingizi. Hata mama aliponigongea sikutaka kumfungulia kabisa. Nikalala na njaa mpaka asubuhi.
Asubuhi na mapema niliamkia kujiandaa. Wakati nikijishughulisha kwa hili na lile simu yangu ya mkononi iliita na haraka nikaipokea pasipo hata kuangalia jina la mpigaji. Moyo ukapiga paa! Ilikuwa ni sauti ya Jonas
“ Nimeshindwa kulala kwa amani Karen!...nakupenda sana, sijui niseme nini unielewe Mpenzi…” sikumpa nafasi ya kuendelea kuongea upuuzi wake. Nilikata simu na kuirushia kitandani.
Nilihisi kubanwa na binadamu huyu aliyekuja ghafla katika maisha yangu. Nikatamani kumweleza Iloma ukweli wa kile alichonifanyia mumewe lakini pia sikuwa na ushahidi wa kutosha kumtia hatiani!
Wiki hiyo nzima sikuwa na amani moyoni. Ijapokuwa mama alijitahidi sana kuniweka sawa lakini akili yangu ilikuwa bado inazungukwa na mambo mengi.
Siku hiyo kama kawaida ya jumamosi zingine niliamka mapema na kufanya usafi wa nyumba pamoja na kufua. Mida ya saa nne Iloma alinipigia simu na kuniambia kuwa alikuwa njiani kuja kwangu. Nilimalizia kazi zangu haraka na kujiweka tayari kumngoja iloma.
Sikuwa na shaka kwa vile ilikuwa kawaida yake kunitembelea nyumbani. Saa nne juu ya alama iloma aliingia nyumbani, alionekana mchangamfu na mwenye furaha. Mara baada ya kusabahiana na utani wa hapa pale kupita tuliketi barazani na yeye akawa ananisaidia kumenya baadhi ya viungo vya kupikia.
“…angalau sasa Jonas ametulia Karen” aliniambia kwa bashasha
“ matatizo ni sehemu ya uhusiano” nilimjibu kimkato huku nikishusha pumzi. Masikini Iloma hakujua kuwa katika kipindi hicho Jonas alikuwa akinipigia simu kila usiku kunibembeleza niwe mpenzi wake kwa siri. Nilikuwa nikijitahidi kwa kadri nilivyoweza kumkwepa Jonas!
“ umenisaidia sana Karen nadhani napaswa kukuombea upate mume bora kabisa!”
“ dua imefika…vipi Kim anaendeleaje?” nilibadili mada ili kukwepa kuongelea zaidi masuala ya ndoa.
“alikuwa na anaharisha sana wiki iliyopita lakini sasa hali yake nzuri kiasi” Iloma alitamka taratibu hali akiendelea kumenya vutunguu swaumu vilivyokuwa ndani ya ungo. Nilipepesuka kidogo na haraka nikajishikiza kwenye sinki lililokuwa kando yetu.
“Karen nini?” iloma aliuliza kwa hamaki akiweka ungo chini na kuja kunishikilia
“najisikia vibaya Ilomaa…mama nakufa!” nilipiga ukelele hafifu kabla ya kuanza kuona kizunguzungu, nikajikuta nakosa nguvu. Nilifumba macho na kuyafumbua taratibu lakini uwezo wa kuona ukatoweka ghafla sikuelewa kilichoendelea.
Nilipokuja kuzinduka nilijikuta juu ya kitanda cha hospitali. Niliangaza huku na kule pasipo kumuona yeyote. Nikajituliza tuli hali akili ikianza kutafakari kilichonikuta.
Wakati nikiwaza hili na lile mlango wa wodi ulifunguliwa na kijana mmoja aliyevalia mavazi ya kitabibu aliingia akiwa na faili mkononi. Taratibu nikaiweka shingoyangu sawia na kumkodolea macho yule kijana. Nikatunduwaa alikuwa Kelvin Nashon! Mchumba wangu aliyeniacha nikiuguza madonda ya roho!
“ unaendeleaje Karen!” alinihoji taratibu kwa sauti yake ile ile ya upole iliyojaa kila aina ya ukarimu. Sikumudu kufungua mdomo na kujibu kitu. Nadhani akili ilichanja mbuga na kukiacha kichwa kikiwa kitupu mithili ya mtungi uliotoboka! Macho yalitanuka zaidi na nikawa ninamtazama mwanaume huyu aliyekuwa mbele yangu kama kiumbe cha ajabu toka sayari nyingine.
Nilihisi mkuki moyoni, machozi ya hasira ya kuachwa solemba, machozi ya hasira ya kusalitiwa yalitanda katika mboni za macho yangu na kufanya macho yametemete mithili ya mbalamwezi!
“ ondoka…go away kelvin!” nilimudu kutamka maneno hayo kwa sauti ya kitetemeshi kabla ya kukabiliana na kwikwi nilizoshindwa kuzivumilia, nikaangua kilio cha kugugumia. Sikujali kuwa alikuwa pale kunisaidia kama daktari na wala si kama Kevin Nashon.
“ weka hasira kando Karen… unahitaji kusaidiwa kama mgonjwa” Kelvin alinisemesha taratibu hali akijivuta na kusogea karibu zaidi na pale nilipokuwa nimelala. Nilihisi kuumia kana kwamba nilikuwa nimeachwa jana tu!
“ sitaki Kelvin! Kama ni kufa acha nife Kelvin ungekuwa nia ya kunisaidia usingenitendea vile… ni msaada gani ulio nao wewe… msaada gani Kelvin, wewe! Wewe una msaada gani kwangu?” nilimpayukia kwa hasira tayari nikiwa nimeshaketi kitandani na kumtazama vema Kelvin. Alikiinamisha kichwa chake chini kwa sekunde kadhaa kisha kama ilivyoada yake aliachia tabasamu lake tulivu.
“ Karen! Hayo ni masuala binafsi na hapa niko kazini” alijaribu kunituliza lakini kinyume chake aliwasha moto nyikani. Niliteremka toka pale kitandani huku nikipepesuka na kuangaza huku kule kuangalia kama kuna kitu changu. Nilipotaka kupiga hatua nilihisi uzito kichwani nikayumba na kutaka kudondoka. Kelvin akaniwahi na kunidaka haraka.
“ niache, usiniguse Kelvin…” nikamkemea na kujitoa mikononi mwake huku nikiwa nimejiegemeza kitandani nilimtazama kwa chuki kiasi ambacho hata yeye Kelvin alishindwa kuamua la kufanya juu yangu.
Alionekana wazi kutafuta maneno yatakayotosheleza kuelezea huruma yake kwangu. Akakosa!
“ Karen!...karen” aliniita kwa upole
“ sitaki kusikia na…” sikumalizia kauli yangu kwa vile mlango ulifunguliwa na mama pamoja na Iloma wakaingia. Mama alikuja mbio kunikumbatia.
“ooh! Karen unajisikiaje?” mama alinihoji nami sikushughulika kusikiliza
“ Iloma sitaki kulala hapa ni bora mkinihamishia hospitali nyingine”nilipayuka kwa hasira
“ kwanini?” mama alihoji haraka akiwa amekumbwa na mshangao
“ Iloma umenielewa?” nilisisitiza bila kujali swali la mama
“ lakini Karen …”alitaka kupingama nami
“ hakuna cha lakini kama hakuna kati yenu mwenye uwezo wa kunitoa hapa mpigieni baba yangu simu aje ama kaka yangu Brian” nilizidi kuja juu mno. Mama akamtazama Iloma na kumwambia
“ nenda kalipie kule mapokezi na tumpeleke Marie stopes sasa hivi” alichomoa pochi yake na kutoa pesa alizomkabidhi Iloma. Kabla hata Iloma hajapangua hatua moja Kelvin alimuwahi na kumzuia mlangoni.
“ nitalipia mimi acha tu!”
“ Sina haja na msaada wako Kelvin si umetoka kuniambia sasa hivi kuwa uko kazini na sasa unataka kuyalipia matibabu yangu kama nani?” nilimtupia swali la kebehi lililomfanya Kelvin anitazame kwa mshangao wa waziwazi.
“ sikudhani kuwa ungebeba kisirani kama hiki Karen!” aliniambia kwa sauti ya upole nami nikaangusha cheko fupi la dharau na kumwambia “ sikudhani kuwa ungekuwa mkarimu kiasi hiki Kelvin!” .
Akabaki kunitazama tu asijue aongee nini mbele yangu. Nadhani pia aligundua ni kiasi gani nilikuwa na majibu ya ovyo. Mama alinitoa nje huku akiwa amenishikilia na tukaelekea mapokezi nilikomkuta dada yangu Debby. Moja kwa moja walinipeleka hospitali ya maries topes mwenge.
Daktari aliniambia nilikuwa na malaria pamoja na upungufu kiasi wa damu. Nililala hospitalini pale kwa siku moja na kutoka jioni. Mwezi mmoja baadae hali yangu ilitengamaa lakini nilianza kupata dalili Fulani ambazo zilinipa mashaka. Mwezi wa pili dalili hizo zilionekana wazi nami nikaanza kuhisi kitu kisicho cha kawaida katika mwili wangu.
Ijumaa moja tulivu niliamua kwenda hospitali kupata uhakika wa hisia zangu. Nilichohisi kilikuwa kweli kabisa. Nilikuwa na mimba changa! Pamoja na daktari kunithibitishia kwa vipimo lakini bado sikuamini.
Mimba! Kwa asilimia mia moja na pengine na moja ya ziada mimba hii ilikuwa ya Jonas! Shemeji yangu, mume wa rafiki yangu mpenzi Iloma.
“Dokta una hakika na majibu yako?” nilimuuliza Daktari kwa wasiwasi
“ Huniamini?” naye alinirudishia swali huku akinipatia karatasi iliyokuwa na majibu toka maabara. Niliikodolea macho mara mbilimbili nikitamani majibu yasomeke visivyo. Nikairudisha mezani na kusimama.
“inaonekana hukuitarajia kabisa eeh!...” dokta alinisemesha lakini hakuwa katika mawazo yangu. Nikazidi kuchanganyikiwa nisijue hata nianzie wapi kutatua tatizo hili. Nadhani nilitoka katika chumba cha daktari pasipo hata kumuaga. Nilikatiza kordo mbili tatu na kutokezea mapokezi. Niliketi katika benchi moja lililokuwa kando huku akili ikinizunguka isivyo kawaida “ nitafanyaje sasa?” nilijiuliza kwa sauti bila kujali kama kulikuwa na mtu wa kunipatia jibu la swali hilo.
Nilifikiria kuitoa kwa siri lakini nikaona bora kumshirikisha Jonas ili nijue yeye ana mawazo gani juu ya tatizo hili. Nilikosa raha kabisa, nilikosa amani moyoni kiasi kwamba hata wale walionizoea hawa kuacha kunighasi kwa maswali ya kutaka kujua kilichonisibu.
Haya yalikuwa maji ya shingo na kwa hakika nilimlaani Jonas kwa lugha zote! Baada ya kufikiria sana nilimpigia jonas simu na kutaka kukutana naye nyumbani kwetu kwa vile kwa wakati huo mama alikuwa amemfuata baba Nairobi. Jioni ya siku hiyo Jonas aliwasili nyumbani na baada kupata viburudisha koo, niliamua kumpasulia jonas ukweli.
Alitunduwaa kwa sekunde kadhaa huku macho yakiwa yamemtoka mithili ya mjusi aliyebanwa na mlango. Jasho lisilo rasmi lilimbubujika mwanaume wa watu hali kiyoyozi kilikuwa kikitimiza wajibu wake ipasavyo. Midomo yake ilimwemweseka pasipo kutoa neno lolote. Nilimtazama kwa sekunde kadhaa kisha taratibu nilijitoa kochini na kusimama mbele yake.
“ najua lawama hazijengi jonas lakini huu mzigo si wangu peke yangu!” nikauvunja ukimya uliotutembelea ghafla.
“ hakuna njia Karen inabidi uitoe…mimi ni shemasi Karen, mimi ni kiongozi ndani ya kamati ya vijana kanisani…mimi ni mume wa mtu…unadhani nitasimamaje endapo suala hili litajulikana?” alijitutumua kujibu katika namna ya kupayuka na kuhamanika. Eti kwa wakati huo ndio alikumbuka nyadhifa zake kanisani na kuwa yeye ni mume wa mtu.
“ ungeyafahamu hayo mapema usingenitendea unyama ule jonas na tena nataka ufahamu kuwa mimba hii siitoi ng’o! kuzini uzini na kabla hujajua hata adhabu ya uzinzi unataka ujiongezee dhambi ya kuua, utamjibu nini muumba?”
“ itakuwa juu yako Karen siwezi kuhatarisha ndoa yangu sababu yako!” alinijia juu akizidi kuhamanika vibaya mbele yangu, akinitazama kwa chuki ilichonganyikana na hali ya kutoamini...sikutarajia hali ile na sikutegemea jonas angebadilika vile, nilichoka mara mbili ya mwanzo!
ITAENDELEA.....
Monday, May 23, 2011
SIRI YANGU 6.....Na Laura Pettie
..... “ wewe unashtuka hivi Karen unadhani mimi nilishtuka kiasi gani?”
“ No! unajua… sasa…kwani rafiki yako huyo anamfahamu huyo mwanamke?” nilimtupia swali huku maneno yakigongana gongana na kama Iloma angekuwa makini angehisi kitu katika kauli yangu.
“ anasema hamfahamu lakini kama atakwenda naye tena hapo hotelini basi atammaki sura vizuri”
“ lakini usipende kusikiliza maneno ya watu Iloma”
“ hawezi kunidanganya, jonas amebadilika mno tabia sijui nimfanyeje jamani”
nilishusha pumzi na kutafuta haraka cha kusema nikakosa!
“ naomba leo uje uongee naye mbele yangu nyumbani wewe anakuheshimu na nadhani itasaidia kidogo” iloma alitamka taratibu bila kujua kuwa alikuwa ananiweka katika mtihani mkubwa mno.
“ lakini Iloma kwanini usilipeleke swali hili kwa mshenga wenu?”
“ nitakwenda kama ushauri wako kwake hautasaidia Karen”
nikakwama kabisa. Nilitumbua macho tu nikiwa sinahata la kusema. Nikarejea kitini pangu na kujitupa kwa nguvu.
“ nitajaribu!” nilimpa jibu fupi na tabasamu likachanua usoni pake.
“ nadhani leo baada ya kazi twende wote nyumbani kwangu”
“ hapana shaka!” alisimama na kuja kunikumbatia pale nilipokuwa nimeketi kisha akatoka na kwenda kuendelea na kazi zake.
Alizidi kunichanganya mno. Sikujua ningeongea nini na jonas na wala sikujua usiku wa siku hiyo ningeongea nini mama juu ya inshu ile ya mimi kulala nje bila taarifa.
Niliinamisha kichwa changu mezani na kutafakari moja baada ya jingine pasipo hata kufikia muafaka wa kile nilichokuwa ninawaza. Wakati wa chakula cha mchana nilijiweka ‘busy’ sana ili kukwepa kuwa karibu na Iloma na hivyo sikutoka ofisini. Wakati nikiendelea na kazi simu yangu ya mkononi iliita na mpigaji alikuwa Jonas.
Mapigo ya moyo yalibadili kasi kiasi nikahisi joto la ghafla likiuvaa mwili wangu. Simu iliendelea kuita kwa muda na hatimaye ikakatika yenyewe. Dakika tatu mbele jonas alipiga tena safari hii niliikata na kuzima simu kabisa bila kujali watu wengine muhimu ambao wangenitafuta kwa shida za maana.
Jioni ya siku hiyo tuliondoka wote na Iloma na kuelekea kwake. Siku hiyo iloma alikuja na gari lake ambalo hakuwa akilitumia kwa muda mrefu baada ya kupata ajali. Tuliwahi kufika kwake mapema tu na kwa hakika nilianza kustaajabia mazingira ya nyumba hii ya rafiki yangu Iloma. Ilikuwa imepita muda mrefu tangu nimtembelee kwake kwa mara ya mwisho alipojifungua mtoto wake Kim.
Mara baada ya kukaribishwa ndani nilikumbana na harufu moja mbaya niliyoshindwa kuitabiria ni harufu ya nini. Sebule yake yenye makochi mazito ya kisasa yalikuwa shangala baghala huku baadhi yakionekana kuwa na alama za mikojo ya mtoto! Vitabu na magazeti vilisambaa kila kona na kufuta kabisa mandhari tulivu ya nyumba hii.
Nepi kadhaa zenye kinyesi zilikuwa zimetelekezwa chini na kim mwenyewe alikuwa ameketishwa kwenye kapeti akiwa amevalishwa fulana bila hata nguo ya ndani. Uso mng’aavu wa kim wenye kulandana vema na baba ulikuwa umetapakaa uji uliokauka na kwa hakika fulana aliyokuwa amevaa ilitia kinyaa! Bakuli lenye uji wa mtoto lilikuwa limetelekezwa chini karibu na mlango huku inzi wakilizengea.
Nilichagua sofa moja na kuketi wakati Iloma alijitoma ndani na kuniacha nikikagua mazingira ya jumba lile ambalo kwa hakika lilitakiwa kuwa katika usafi wa hali ya juu. Nilihofia kumpakata hata Kim kwa kuhofia kuchafuliwa na haja kwa vile hakuvalishwa chochote na hivyo kuishia kumpungia mikono na kumsemesha kwa hili na lile.
Dakika chache baadae Iloma alirejea ukumbini akiwa amevalia fulana moja nyeupe na kujifunga khanga kiunoni.
Nilimshangaa zaidi! fulana hiyo sikuelewa kama ilikuwa chafu au rangi yake ndio ilikuwa imefubaa hali kadhalika khanga aliyokuwa ameivaa haikumstahili mwanamke kama yeye tena mke wa mwanaume mtanashati kama Jonas! Hapo ndipo nipoanza kuhisi sababu za Jonas kusaka mwanamke mwingine.
“ Lawama! Wee’ lawama!” alimuita mtumishi wake wa ndani. Pengine nikitegemea kutokea kwa msichana mwenye umri wa kati ikawa sivyo. Msichana mdogo mwenye umri kati ya miaka kumi ama kumi na mbili alikuja mbio pale sebuleni na kusimama mbele yetu. Akapiga goti na kunisalimu. Nikaitikia hali nikimtumbulia macho si tu ya mshangao wa namna alivyokuwa mchafu toka utosini mpaka nyayoni bali pia kwa ule udogo wake! Lawama alimchukua mtoto na kutokomea nae jikoni, nikamgeukia Iloma
“ anaweza nini huyu Iloma?” nilimuuliza kwa hamaki
“ ni bora huyu kuliko kuleta wasichana waliopevuka humu ndani” alinijibu kwa kujiamini kabisa
“ hofu ya nini! humuamini Jonas kiasi cha kuhatarisha maisha ya mtoto wako kwa kuajiri mtoto kama huyu asiye jua hata kuoga!!!” nilishindwa kumuelewa
“ Karen! Mwanaume si mtu wa kumuamini asilimia mia moja! Ni bora kitoto hicho kisichojua kuoga angalau utaishi kwa amani, nashukuru anajua vikazi vidogo vidogo!”
“ sikubaliani nawe Iloma!” nilizidi kuhamaki
“ hutakubaliana nami kwa vile hujui hali halisi.” Alinipa jibu lililonifunga mdomo
ukimya ukapita kati yetu na Lawama akarejea pale ukumbini akiwa na chano chenye glasi ya juisi. Alipoitua ile juisi mezani niliitazama vema ile glasi na kushuhudia madoa ya uchafu yakiwa yameipamba glasi ile hali chano ile iliyobeba glasi ikiwa na nyufa. Sikujisikia kunywa tena ile juisi lakini pia sikutaka kumuonyesha wazi Iloma kuwa glasi yake ilikuwa na kasoro. Nikaamua kuinywa hali nikimuomba mungu aniepushe na maradhi ya tumbo!
Wakati tukiongea hili na lile, honi ilisikika nje na nikajua kuwa Jonas alikuwa amewasili. Punde aliingia ndani na kutukuta pale sofani. Akajenga tabasamu kama ilivyo ada yake na kuja kunisalimu. Hatukutazamana hata machoni kwani nilikiondosha haraka kiganja cha mkono wangu na kujifanya kutafuta kitu katika pochi yangu. Iloma ambaye hakujishughulisha hata kumpokea mumewe aliyeishia chumbani alipaza sauti na kumuita lawama. Mtoto yule akaja tena mbio na kupiga goti mbele yake.
“ una masikio magumu sana Lawama! Nikueleze mara ngapi kuwa baba akija umpokee hiyo briefcase yake na kim ameshaoga?” akamuhoji
“ bado mama!” akajibu haraka lawama hali akijivuta nyuma pengine kujiweka mbali na dhoruba ya kofi kama lingemkumba
“… unataka sasa nitumie fimbo kukukumbusha kila kitu eeeh! Haya upesi potea” akamfukuza Lawama.
Jonas aliporejea sebuleni aliketi sofani na kwa sekunde kadhaa alionekana kuanza kukerwa na harufu ile iliyokuwa kero kwangu pia.
“Mama Kim kuna nini kimeoza humu ndani?” Jonas alimuuliza mkewe
“ Labda ni hizo nepi za mtoto hapo chini” alimuonesha mumewe beseni dogo lililokuwa na nepi chafu kwenye kona ya kuelekea kordoni.
“ sasa huoni kuwa ni kero kwa hii harufu, hebu ziondoe upesi” Jonas alimkaripia Iloma ambaye wala hakujishughulisha kuzitoa zaidi ya kumuita Lawama kwa sauti na alipokuja alimuagiza kutoa zile nepi hali zingine alizichukua chini kando ya sofa. Licha ya nepi zile kuondoshwa lakini bado harufu iliendelea kutawala.
Jioni ya siku hiyo tuliongea mengi na Jonas. Nilijitutumua kumuhoji Jonas sababu za yeye kumfanyia yote yale mkewe ambaye naye alikuwa kando yangu akisapoti maneno yangu.
Jonas hakuongea kitu zaidi ya kunitazama kwa chati na kutikisa kichwa kuonyesha kunielewa pale nilipompa ushauri wa kuwa wazi kwa mkewe na kujaribu kurekebishana pale anapoona tofauti!
Alimtaka radhi mkewe na nikajiona kama mtu aliyetua mzigo mzito baada ya kuongea hayo.
ITAENDELEA....
“ No! unajua… sasa…kwani rafiki yako huyo anamfahamu huyo mwanamke?” nilimtupia swali huku maneno yakigongana gongana na kama Iloma angekuwa makini angehisi kitu katika kauli yangu.
“ anasema hamfahamu lakini kama atakwenda naye tena hapo hotelini basi atammaki sura vizuri”
“ lakini usipende kusikiliza maneno ya watu Iloma”
“ hawezi kunidanganya, jonas amebadilika mno tabia sijui nimfanyeje jamani”
nilishusha pumzi na kutafuta haraka cha kusema nikakosa!
“ naomba leo uje uongee naye mbele yangu nyumbani wewe anakuheshimu na nadhani itasaidia kidogo” iloma alitamka taratibu bila kujua kuwa alikuwa ananiweka katika mtihani mkubwa mno.
“ lakini Iloma kwanini usilipeleke swali hili kwa mshenga wenu?”
“ nitakwenda kama ushauri wako kwake hautasaidia Karen”
nikakwama kabisa. Nilitumbua macho tu nikiwa sinahata la kusema. Nikarejea kitini pangu na kujitupa kwa nguvu.
“ nitajaribu!” nilimpa jibu fupi na tabasamu likachanua usoni pake.
“ nadhani leo baada ya kazi twende wote nyumbani kwangu”
“ hapana shaka!” alisimama na kuja kunikumbatia pale nilipokuwa nimeketi kisha akatoka na kwenda kuendelea na kazi zake.
Alizidi kunichanganya mno. Sikujua ningeongea nini na jonas na wala sikujua usiku wa siku hiyo ningeongea nini mama juu ya inshu ile ya mimi kulala nje bila taarifa.
Niliinamisha kichwa changu mezani na kutafakari moja baada ya jingine pasipo hata kufikia muafaka wa kile nilichokuwa ninawaza. Wakati wa chakula cha mchana nilijiweka ‘busy’ sana ili kukwepa kuwa karibu na Iloma na hivyo sikutoka ofisini. Wakati nikiendelea na kazi simu yangu ya mkononi iliita na mpigaji alikuwa Jonas.
Mapigo ya moyo yalibadili kasi kiasi nikahisi joto la ghafla likiuvaa mwili wangu. Simu iliendelea kuita kwa muda na hatimaye ikakatika yenyewe. Dakika tatu mbele jonas alipiga tena safari hii niliikata na kuzima simu kabisa bila kujali watu wengine muhimu ambao wangenitafuta kwa shida za maana.
Jioni ya siku hiyo tuliondoka wote na Iloma na kuelekea kwake. Siku hiyo iloma alikuja na gari lake ambalo hakuwa akilitumia kwa muda mrefu baada ya kupata ajali. Tuliwahi kufika kwake mapema tu na kwa hakika nilianza kustaajabia mazingira ya nyumba hii ya rafiki yangu Iloma. Ilikuwa imepita muda mrefu tangu nimtembelee kwake kwa mara ya mwisho alipojifungua mtoto wake Kim.
Mara baada ya kukaribishwa ndani nilikumbana na harufu moja mbaya niliyoshindwa kuitabiria ni harufu ya nini. Sebule yake yenye makochi mazito ya kisasa yalikuwa shangala baghala huku baadhi yakionekana kuwa na alama za mikojo ya mtoto! Vitabu na magazeti vilisambaa kila kona na kufuta kabisa mandhari tulivu ya nyumba hii.
Nepi kadhaa zenye kinyesi zilikuwa zimetelekezwa chini na kim mwenyewe alikuwa ameketishwa kwenye kapeti akiwa amevalishwa fulana bila hata nguo ya ndani. Uso mng’aavu wa kim wenye kulandana vema na baba ulikuwa umetapakaa uji uliokauka na kwa hakika fulana aliyokuwa amevaa ilitia kinyaa! Bakuli lenye uji wa mtoto lilikuwa limetelekezwa chini karibu na mlango huku inzi wakilizengea.
Nilichagua sofa moja na kuketi wakati Iloma alijitoma ndani na kuniacha nikikagua mazingira ya jumba lile ambalo kwa hakika lilitakiwa kuwa katika usafi wa hali ya juu. Nilihofia kumpakata hata Kim kwa kuhofia kuchafuliwa na haja kwa vile hakuvalishwa chochote na hivyo kuishia kumpungia mikono na kumsemesha kwa hili na lile.
Dakika chache baadae Iloma alirejea ukumbini akiwa amevalia fulana moja nyeupe na kujifunga khanga kiunoni.
Nilimshangaa zaidi! fulana hiyo sikuelewa kama ilikuwa chafu au rangi yake ndio ilikuwa imefubaa hali kadhalika khanga aliyokuwa ameivaa haikumstahili mwanamke kama yeye tena mke wa mwanaume mtanashati kama Jonas! Hapo ndipo nipoanza kuhisi sababu za Jonas kusaka mwanamke mwingine.
“ Lawama! Wee’ lawama!” alimuita mtumishi wake wa ndani. Pengine nikitegemea kutokea kwa msichana mwenye umri wa kati ikawa sivyo. Msichana mdogo mwenye umri kati ya miaka kumi ama kumi na mbili alikuja mbio pale sebuleni na kusimama mbele yetu. Akapiga goti na kunisalimu. Nikaitikia hali nikimtumbulia macho si tu ya mshangao wa namna alivyokuwa mchafu toka utosini mpaka nyayoni bali pia kwa ule udogo wake! Lawama alimchukua mtoto na kutokomea nae jikoni, nikamgeukia Iloma
“ anaweza nini huyu Iloma?” nilimuuliza kwa hamaki
“ ni bora huyu kuliko kuleta wasichana waliopevuka humu ndani” alinijibu kwa kujiamini kabisa
“ hofu ya nini! humuamini Jonas kiasi cha kuhatarisha maisha ya mtoto wako kwa kuajiri mtoto kama huyu asiye jua hata kuoga!!!” nilishindwa kumuelewa
“ Karen! Mwanaume si mtu wa kumuamini asilimia mia moja! Ni bora kitoto hicho kisichojua kuoga angalau utaishi kwa amani, nashukuru anajua vikazi vidogo vidogo!”
“ sikubaliani nawe Iloma!” nilizidi kuhamaki
“ hutakubaliana nami kwa vile hujui hali halisi.” Alinipa jibu lililonifunga mdomo
ukimya ukapita kati yetu na Lawama akarejea pale ukumbini akiwa na chano chenye glasi ya juisi. Alipoitua ile juisi mezani niliitazama vema ile glasi na kushuhudia madoa ya uchafu yakiwa yameipamba glasi ile hali chano ile iliyobeba glasi ikiwa na nyufa. Sikujisikia kunywa tena ile juisi lakini pia sikutaka kumuonyesha wazi Iloma kuwa glasi yake ilikuwa na kasoro. Nikaamua kuinywa hali nikimuomba mungu aniepushe na maradhi ya tumbo!
Wakati tukiongea hili na lile, honi ilisikika nje na nikajua kuwa Jonas alikuwa amewasili. Punde aliingia ndani na kutukuta pale sofani. Akajenga tabasamu kama ilivyo ada yake na kuja kunisalimu. Hatukutazamana hata machoni kwani nilikiondosha haraka kiganja cha mkono wangu na kujifanya kutafuta kitu katika pochi yangu. Iloma ambaye hakujishughulisha hata kumpokea mumewe aliyeishia chumbani alipaza sauti na kumuita lawama. Mtoto yule akaja tena mbio na kupiga goti mbele yake.
“ una masikio magumu sana Lawama! Nikueleze mara ngapi kuwa baba akija umpokee hiyo briefcase yake na kim ameshaoga?” akamuhoji
“ bado mama!” akajibu haraka lawama hali akijivuta nyuma pengine kujiweka mbali na dhoruba ya kofi kama lingemkumba
“… unataka sasa nitumie fimbo kukukumbusha kila kitu eeeh! Haya upesi potea” akamfukuza Lawama.
Jonas aliporejea sebuleni aliketi sofani na kwa sekunde kadhaa alionekana kuanza kukerwa na harufu ile iliyokuwa kero kwangu pia.
“Mama Kim kuna nini kimeoza humu ndani?” Jonas alimuuliza mkewe
“ Labda ni hizo nepi za mtoto hapo chini” alimuonesha mumewe beseni dogo lililokuwa na nepi chafu kwenye kona ya kuelekea kordoni.
“ sasa huoni kuwa ni kero kwa hii harufu, hebu ziondoe upesi” Jonas alimkaripia Iloma ambaye wala hakujishughulisha kuzitoa zaidi ya kumuita Lawama kwa sauti na alipokuja alimuagiza kutoa zile nepi hali zingine alizichukua chini kando ya sofa. Licha ya nepi zile kuondoshwa lakini bado harufu iliendelea kutawala.
Jioni ya siku hiyo tuliongea mengi na Jonas. Nilijitutumua kumuhoji Jonas sababu za yeye kumfanyia yote yale mkewe ambaye naye alikuwa kando yangu akisapoti maneno yangu.
Jonas hakuongea kitu zaidi ya kunitazama kwa chati na kutikisa kichwa kuonyesha kunielewa pale nilipompa ushauri wa kuwa wazi kwa mkewe na kujaribu kurekebishana pale anapoona tofauti!
Alimtaka radhi mkewe na nikajiona kama mtu aliyetua mzigo mzito baada ya kuongea hayo.
ITAENDELEA....
Saturday, May 7, 2011
MSEMO WA LEO....
...katika kuienzi laugha yangu ka kiswahili nimeona niwe natoa misemo mbali mbali ya lugha ya kiswahili hata wewe mdau unaweza kunitupia msemo wako kupitia email ya. queenlauryn5@yahoo.com nami nikautupia humu.... haya msemo wa leo unasema
...Hubebeki kama chungu cha moto!...
eeeh ndugu yangu ukibebwa bebeka, sio tena umfanye mbebaji akubebe huku ananung'unika! binadamu unasaidiwa katika hili nawe badala ya kuonyesha shukrani ndio kama vile huo msaada unaukatia risiti, utataka utendewe vile unavyotaka wewe wakati yote ni hiyari ya mtenda!
ALAMSIKI
SIRI YANGU 5..... na Laura Pettie
“ sikuelewi jonas… hivi…ina maana …my god!” niliwaya waya tu pasipo kujua la kusema
“ Karen huelewi nini hapo nina maanisha kile nilichokisema”
“ hauko makini na akili zako Jonas! nilikuheshimu sana na sikutarajia kusikia upuuzi kama huu toka kwako na kumbe ndio maana Iloma hana amani moyoni mwake…. sikutarajia ungelikuwa mpumbavu kiasi hiki Jonas. Umenivunjia heshima na umemvunjia Iloma heshima yake”
nilinyanyuka na kujiandaa kuondoka lakini sikumudu hata kupiga hatua moja Jonas aliudaka mkono wangu na kuungandamiza mezani. Nilimtazama tu pasipo hata kumkemea. Mboni za macho yake zilimeremeta na kuyaonyesha dhahiri malengelenge ya machozi yaliyotuama machoni pake.
“ kwanini unanifanyia hivi Karen, kwa vile umegundua kuwa nakupemda sana”
“ sihitaji kusikia upuuzi wako Jonas” nilimfokea
“ narudia kile nilichokisema Karen nakupenda sana na hilo nililitambua siku nyingi Karen, nimekuwa nikihangaika na kuteseka sana juu yako lakini hutaki kuzielewa hisia zangu! Hutaki kunipa nafasi ya kukuonyesha namna ninavyokupenda Karen” machozi yaliteremka taratibu mashavuni pake.
Nikahisi kumuonea huruma Jonas. Kwa namna alivyokuwa akilia nilihisi imani lakini alikuwa mume wa mtu tena mume wa rafiki yangu mpenzi.
“ na Iloma je?... anayonafasi katika maisha yako Jonas” nilirejea kuketi pale kitini na kuuondoa mkono wangu katika kiganja cha mkono wake wa kuume.
“ hilo nalitambua lakini nafasi iliyo ya kipekee ni ile ninayotaka kukupa wewe Karen. Unaisumbua nafsi yangu mno na kama si Iloma kubeba mimba yangu kabla ya ndoa Karen ningekuoa wewe”
Nilishusha pumzi ndefu na kumtazama mwanaume huyu kwa mshangao mkubwa.
“ siwezi kumsaliti Iloma siwezi Jonas nataka ufahamu hilo na…” simu yangu ya mkononi iliita na mpigaji alikuwa mama.
Nilinyanyuka haraka na kwenda kuipokelea kando. Mama alikuwa anataka kujua mahali nilipo kwani muda wa mimi kuwa nyumbani kama kawaida ulikuwa umeshawadia na ikizingatia alikuwa mgonjwa.
Nilimwambia mama avute subira kwani ningekuwa nyumbani muda mfupi baadae. Niliporudi mezani niliimalizia juisi yangu na kumwambia Jonas kuwa nahitajika nyumbani haraka.
Nilikurupuka asubuhi ya saa moja nikiwa mahali ambapo ilinichukua dakika kadhaa kupatambua. Yalikuwa ni mazingira mapya kabisa tofauti na yale niliyoyazoea.
Niliangaza huku na kule pasipo kupatambua mahali pale na hali mwili mzima na hasa kichwa kikiwa na uzito wa ajabu.
Nikiwa ndani ya tafakari hizo mlango wa chumba nilichokuwamo ulifunguliwa na Jonas akaingia akiwa na sinia lililokuwa na staftaha. Niliduwaa!
“Jonas!...umenifanyia nini hiki…mungu wangu…Jonas…nitasema nini …hapa ni wapi sasa?” nilishindwa hata kuzipangilia sentesi zangu katika mpangilio unaoeleweka.
Akili ilianza kufanya kazi na mara moja nilitambua kuwa nilikuwa katika moja ya vyumba vya hoteli ya Lightness.
ITAENDELEA....
“ Karen huelewi nini hapo nina maanisha kile nilichokisema”
“ hauko makini na akili zako Jonas! nilikuheshimu sana na sikutarajia kusikia upuuzi kama huu toka kwako na kumbe ndio maana Iloma hana amani moyoni mwake…. sikutarajia ungelikuwa mpumbavu kiasi hiki Jonas. Umenivunjia heshima na umemvunjia Iloma heshima yake”
nilinyanyuka na kujiandaa kuondoka lakini sikumudu hata kupiga hatua moja Jonas aliudaka mkono wangu na kuungandamiza mezani. Nilimtazama tu pasipo hata kumkemea. Mboni za macho yake zilimeremeta na kuyaonyesha dhahiri malengelenge ya machozi yaliyotuama machoni pake.
“ kwanini unanifanyia hivi Karen, kwa vile umegundua kuwa nakupemda sana”
“ sihitaji kusikia upuuzi wako Jonas” nilimfokea
“ narudia kile nilichokisema Karen nakupenda sana na hilo nililitambua siku nyingi Karen, nimekuwa nikihangaika na kuteseka sana juu yako lakini hutaki kuzielewa hisia zangu! Hutaki kunipa nafasi ya kukuonyesha namna ninavyokupenda Karen” machozi yaliteremka taratibu mashavuni pake.
Nikahisi kumuonea huruma Jonas. Kwa namna alivyokuwa akilia nilihisi imani lakini alikuwa mume wa mtu tena mume wa rafiki yangu mpenzi.
“ na Iloma je?... anayonafasi katika maisha yako Jonas” nilirejea kuketi pale kitini na kuuondoa mkono wangu katika kiganja cha mkono wake wa kuume.
“ hilo nalitambua lakini nafasi iliyo ya kipekee ni ile ninayotaka kukupa wewe Karen. Unaisumbua nafsi yangu mno na kama si Iloma kubeba mimba yangu kabla ya ndoa Karen ningekuoa wewe”
Nilishusha pumzi ndefu na kumtazama mwanaume huyu kwa mshangao mkubwa.
“ siwezi kumsaliti Iloma siwezi Jonas nataka ufahamu hilo na…” simu yangu ya mkononi iliita na mpigaji alikuwa mama.
Nilinyanyuka haraka na kwenda kuipokelea kando. Mama alikuwa anataka kujua mahali nilipo kwani muda wa mimi kuwa nyumbani kama kawaida ulikuwa umeshawadia na ikizingatia alikuwa mgonjwa.
Nilimwambia mama avute subira kwani ningekuwa nyumbani muda mfupi baadae. Niliporudi mezani niliimalizia juisi yangu na kumwambia Jonas kuwa nahitajika nyumbani haraka.
Nilikurupuka asubuhi ya saa moja nikiwa mahali ambapo ilinichukua dakika kadhaa kupatambua. Yalikuwa ni mazingira mapya kabisa tofauti na yale niliyoyazoea.
Niliangaza huku na kule pasipo kupatambua mahali pale na hali mwili mzima na hasa kichwa kikiwa na uzito wa ajabu.
Nikiwa ndani ya tafakari hizo mlango wa chumba nilichokuwamo ulifunguliwa na Jonas akaingia akiwa na sinia lililokuwa na staftaha. Niliduwaa!
“Jonas!...umenifanyia nini hiki…mungu wangu…Jonas…nitasema nini …hapa ni wapi sasa?” nilishindwa hata kuzipangilia sentesi zangu katika mpangilio unaoeleweka.
Akili ilianza kufanya kazi na mara moja nilitambua kuwa nilikuwa katika moja ya vyumba vya hoteli ya Lightness.
ITAENDELEA....
Friday, May 6, 2011
SIRI YANGU 4....Laura Pettie
Niliduwaa tu na barua ile mkononi. Nikairudisha bahashani na kuanza kutafakari ujumbe ule. Jonas alikuwa akinitafutia nini mimi au naye alikuwa akimuhisi vibaya iloma na ndio alikuwa anataka anitumie mimi kama mpelelezi. Kwa hakika sikuwaelewa wanandoa hawa hata chembe. Sikuendelea na kazi tena.
Nilitoka na kumpitia Iloma kwa ajili ya kwenda kupata chakula cha mchana. Tuliingia mgahawani city garden na kuchagua mahali pazuri na kuketi. Tuliagiza chakula na ndipo Iloma alipoanza kunisimulia mambo mbalimbali ya Jonas. Alinieleza kuwa Jonas hakuwa akila chakula cha nyumbani pale kwa muda mrefu sasa.
`
Mara nyingi alisingizia kuwa alishakula hotelini na kama haitoshi hata chai Jonas hakunywa nyumbani kwake. Iloma alizidi kunilalamikia kuwa mumewe huyo alionesha wazi kuwa alikuwa amemchoka kwa namna Fulani na yeye hakumvutia tena kwani hata katika hafla mbalimbali Jonas hakutaka kuongozana na mkewe, Alinilalamikia vitu vingi ambavyo vilinifanya nianze kumuona jonas katika muonekano mpya wa mwanaume wa ajabu na mnafiki.
“ nimebadilika nini Karen hata Jonas anione sifai tena jamani” Iloma aliniuliza swali ambalo nililikwepa kwa vile ukweli ni kuwa Iloma alikuwa amebadilika mno kimaumbile na pia kitabia tangu amzae mtoto wake wa kwanza kim. Alikuwa ameongezeka mno na kupata umbile jipya lisilo la kuvutia. Urembo wake uliisha kwani sasa hata nywele zake zilichanwa katika mtindo wa kifagio kila siku na hakujiremba kabisa. Na kama haitoshi hakuvalia kinadhifu kama ilivyokuwa zamani na hivyo kupoteza kabisa mvuto aliokuwa nao.
Niliogopa kumwambia kuwa hakuwa akivutia lakini pia nilijua kuwa Jonas hakustahili kumtendea mkewe mambo ya ajabu eti kwa vile tu hakuvutia tena. Nilipanga akilini kumwambia jonas ajirekebishe katika makutano yetu ya jioni hiyo.
Iloma alikoseshwa raha na tabia za jonas, aliendelea kunilalamikia juu ya Jonas.
“ Karen hata chai!... Chai tu ushindwe kunywa nyumbani kwako hebu niambie anamaanisha nini sasa”
“ kwa kweli sijui nini kimemsibu shemeji, hata hivyo inawapasa kuketi chini na kurekebishana Iloma”
“ wapi! Nimrekebishe Jonas wapi Karen! Nianze kumlazimisha kunywa chai nyumbani kwa fimbo?”
niliangua kicheko kifupi kwa majibu ya Iloma ambaye aliendelea kukiweka akiba kicheko chake, alinitazama bila hata tabasamu na kushuhudia nafsi yake ikipigana na uchungu aliokuwa nao. Machozi yalimlengalenga na haraka aliyafuta na kitambaa chake cha mkononi na kuniambia kwa sauti ya kulalamika
“ Bado mapema mno kufikiria talaka, mtoto wetu ndio kwanza ana mwaka sasa na yeye ameshaanza vituko nitamvumilia mpaka lini na kama haitoshi karen Jonas sasa anarejea nyumbani usiku wa manane kila siku hata kama ni biashara Karen biashara ya saa nane za usiku, biashara gani hizo jamani!”
nilishusha pumzi ya nguvu. Nilipata faraja ya kusikia haya kwa namna moja nilianza kumshukuru mungu kwa kumuweka mbali Kelvin kwa vile pengine tungeoana naye angeniumiza hivi kila uchao.
Nilimfariji na kumpa maneno ya matumaini ya kumbadili Jonas. Angalau aliachia tabasamu na kuipa nafasi roho yake iliyokuwa imesongwa na mawazo mengi mno. Tuliondoka pale mgahawani mara baada ya kumaliza chakula na kurudi ofisini. Niliendelea na kazi zangu huku nikiwa na mawazo mengi lakini pia nilikuwa na hamu ya kuongea na Jonas ili nimsikie naye alikuwa na yapi juu ya Iloma. Sikutaka kuhukumu upande mmoja tu!
Jioni ya saa kumi na moja na nusu nilimaliza kazi zangu na kufunga ofisi. Nilipita ofisini kwa Iloma na kumkuta akimalizia kutunza nyaraka mbalimbali za mle ofisini. Kichwani nilikuwa ninatafuta njia ya kumkimbia Iloma na kwenda kukutana na mumewe. Nilihofu kuwa angeweza kuhisi vibaya endapo ningemweleza ukweli wa kule niendako lakini pia Jonas alikuwa ameniasa kumkwepa Iloma. Binafsi yangu nilihisi msuto ukipita nafsini mwangu kwa kuona kuwa kukutana na Jonas bila idhini ya Iloma lilikuwa ni kosa kubwa.
“ Iloma acha mimi nitangulie kaka yangu Brian alisema atanipitia pale kituoni ili twende wote mahali”
“ oh! Itakuwa vema mkinipa lifti pia si unajua pale posta usafiri ulivyo wa shida na leo sijaja na gari” alinijibu pasipo kunitazama na laiti angelifanya hivyo si ajabu angeliushuhudia wasiwasi uliokuwa juu ya paji la uso wangu.
“ aah! Hatuendi nyumbani na… isitoshe alisema atanipitia kwa taksi ya Dulla” nilibabaika kidogo
“ amepata nyumba ndogo nini maana teksi ya Dulla ndio usafiri wa kwenda kona!” aliniambia kiutani nami nikashusha pumzi na kumshukuru mungu
“ pengine huwezi kujua ati! Na labda anataka kwenda kunitambulisha wifi mdogo” nilizidi kumdanganya rafiki yangu huku nikijifaragua faragua kwa vicheko vya uongo na kweli. Moyoni nilihisi mzigo mzito kumtendea rafiki yangu unafiki kama huu. Tulitoka ofisini mpaka kituoni na baada ya dakika kama kumi teksi ya dulla ilisimama umbali mfupi toka pale tulipokuwa tumesimama na Iloma. Ni yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kuiona na akanishtua
“ haya mama Dulla huyoo … na angalia msifumaniwe huko ukarudi na ngeu” alinitania huku akinionyesha mahali ilipokuwa imepaki teksi ile.
“ tupo makini michapo yote kesho Iloma”
“haya msalimie Brian!”
“salamu zimefika, tutaonana kesho!”
nilimpungia mkono na kuanza kuchapua hatua za haraka kuielekea teksi ile. Vioo vyeusi vya teksi ya Dulla vilimfanya Iloma asimuone mumewe ndani ya gari. Nilifungua mlango wa nyuma na kujitoma ndani ya gari. Jonas alikuwa ameketi kiti cha nyuma.
Tulisabahiana na Dulla akaliondoa gari. Kama mtu alikuwa amepewa maelezo kabla Dulla alitupeleka Lightness Hotel. Tuliingia mle hotelini na kwenda moja kwa moja mapokezi. Cha kushangaza Jonas aliomba funguo za chumba na kupatiwa. N
ilihisi alikiandaa chumba hicho mapema na sikumuelewa kwanini alichukua chumba wakati tulihitaji kuongea mara moja na kuachana. Sikuwa mjinga kiasi cha kuburuzwa na Jonas. Nilisimama nyuma yake na alipogeuka tulikutanisha nyuso zetu sambamba.
“ hii ina maana gani Jonas!?” nilimuuliza kwa hamaki
“ hatuwezi kuongelea pale mgahawani Karen, mimi ni mume wa mtu na mfanyabiashara ninaye julikana sana hapa jijini, wewe ni rafiki wa mke wangu. Kuketi mgahawani pale tukiongea hakutaleta picha nzuri kwa jamii na isitoshe Iloma hajui kama wewe uko na mimi muda huu” alijitetea kwa kadri alivyoweza lakini pia sikuwa mjinga kiasi ambacho alifikiria. Nikampachika swali
“ sasa Jonas kuonekana mgahawani tukiongea na kuonekana tukielekea vyumbani kipi kina unafuu?”
“ okey! Kwahiyo tukakae mgahawani sio?” aliniuliza kwa sauti kali kidogo
“ nadhani ni bora zaidi Jonas” sikungoja maelezo zaidi nilianza kuchapua hatua kuelekea mgahawani. Nikachagua meza moja iliyokuwa kwenye kona na kuketi. Alinifuatia nyuma na kuketi kiti kilichokuwa mbele ya meza iliyokuwa kati yetu. Aliagiza vinywaji na chakula na kwa pamoja tukaanza kula huku maongezi yakichipukia
“ ni bora uniambie kiini cha mwito huu shemeji” nilimrudisha katika mada kuu
“ mbona una haraka Karen kula kwanza mama” alinijibu hali akiachia tabasamu lake zuri la kuvutia
“ halafu ninayo mengi ya kukuuliza Jonas”
“ juu ya nini?” alionesha mshtuko akaacha kula na kunitumbulia macho
“ mbona una haraka kula kwanza shemeji” nilimtania na wote kwa pamoja tukaangua kicheko. Tulipomaliza kula mhudumu aliondoa baadhi ya vyombo na tukabaki tunaburudika na vinywaji.
Ni hapo ndipo Jonas aliponitobolea kiini cha mwito ule, sikupata hata nafsi ya kumsuta Jonas kutokana na yale niliyoyasikia toka kwa mkewe.
Kwa takribani dakika moja na nusu nilibaki nikiwa nimemtumbulia macho jonas pasipo kujitambua akilini. Nilijaribu kushusha pumzi ndefu na kuangaza huku na kule ili japo nitoke ndotoni lakini bado ilibaki dhahiri kuwa sikuwa ndotoni.
Sikuwa naota wala sikuwa nawaza ilikuwa ni kweli kuwa masikio yangu yalikuwa yamesikia kile kilichotoka mdomoni mwa Jonas.
ITAENDELEA....
Nilitoka na kumpitia Iloma kwa ajili ya kwenda kupata chakula cha mchana. Tuliingia mgahawani city garden na kuchagua mahali pazuri na kuketi. Tuliagiza chakula na ndipo Iloma alipoanza kunisimulia mambo mbalimbali ya Jonas. Alinieleza kuwa Jonas hakuwa akila chakula cha nyumbani pale kwa muda mrefu sasa.
`
Mara nyingi alisingizia kuwa alishakula hotelini na kama haitoshi hata chai Jonas hakunywa nyumbani kwake. Iloma alizidi kunilalamikia kuwa mumewe huyo alionesha wazi kuwa alikuwa amemchoka kwa namna Fulani na yeye hakumvutia tena kwani hata katika hafla mbalimbali Jonas hakutaka kuongozana na mkewe, Alinilalamikia vitu vingi ambavyo vilinifanya nianze kumuona jonas katika muonekano mpya wa mwanaume wa ajabu na mnafiki.
“ nimebadilika nini Karen hata Jonas anione sifai tena jamani” Iloma aliniuliza swali ambalo nililikwepa kwa vile ukweli ni kuwa Iloma alikuwa amebadilika mno kimaumbile na pia kitabia tangu amzae mtoto wake wa kwanza kim. Alikuwa ameongezeka mno na kupata umbile jipya lisilo la kuvutia. Urembo wake uliisha kwani sasa hata nywele zake zilichanwa katika mtindo wa kifagio kila siku na hakujiremba kabisa. Na kama haitoshi hakuvalia kinadhifu kama ilivyokuwa zamani na hivyo kupoteza kabisa mvuto aliokuwa nao.
Niliogopa kumwambia kuwa hakuwa akivutia lakini pia nilijua kuwa Jonas hakustahili kumtendea mkewe mambo ya ajabu eti kwa vile tu hakuvutia tena. Nilipanga akilini kumwambia jonas ajirekebishe katika makutano yetu ya jioni hiyo.
Iloma alikoseshwa raha na tabia za jonas, aliendelea kunilalamikia juu ya Jonas.
“ Karen hata chai!... Chai tu ushindwe kunywa nyumbani kwako hebu niambie anamaanisha nini sasa”
“ kwa kweli sijui nini kimemsibu shemeji, hata hivyo inawapasa kuketi chini na kurekebishana Iloma”
“ wapi! Nimrekebishe Jonas wapi Karen! Nianze kumlazimisha kunywa chai nyumbani kwa fimbo?”
niliangua kicheko kifupi kwa majibu ya Iloma ambaye aliendelea kukiweka akiba kicheko chake, alinitazama bila hata tabasamu na kushuhudia nafsi yake ikipigana na uchungu aliokuwa nao. Machozi yalimlengalenga na haraka aliyafuta na kitambaa chake cha mkononi na kuniambia kwa sauti ya kulalamika
“ Bado mapema mno kufikiria talaka, mtoto wetu ndio kwanza ana mwaka sasa na yeye ameshaanza vituko nitamvumilia mpaka lini na kama haitoshi karen Jonas sasa anarejea nyumbani usiku wa manane kila siku hata kama ni biashara Karen biashara ya saa nane za usiku, biashara gani hizo jamani!”
nilishusha pumzi ya nguvu. Nilipata faraja ya kusikia haya kwa namna moja nilianza kumshukuru mungu kwa kumuweka mbali Kelvin kwa vile pengine tungeoana naye angeniumiza hivi kila uchao.
Nilimfariji na kumpa maneno ya matumaini ya kumbadili Jonas. Angalau aliachia tabasamu na kuipa nafasi roho yake iliyokuwa imesongwa na mawazo mengi mno. Tuliondoka pale mgahawani mara baada ya kumaliza chakula na kurudi ofisini. Niliendelea na kazi zangu huku nikiwa na mawazo mengi lakini pia nilikuwa na hamu ya kuongea na Jonas ili nimsikie naye alikuwa na yapi juu ya Iloma. Sikutaka kuhukumu upande mmoja tu!
Jioni ya saa kumi na moja na nusu nilimaliza kazi zangu na kufunga ofisi. Nilipita ofisini kwa Iloma na kumkuta akimalizia kutunza nyaraka mbalimbali za mle ofisini. Kichwani nilikuwa ninatafuta njia ya kumkimbia Iloma na kwenda kukutana na mumewe. Nilihofu kuwa angeweza kuhisi vibaya endapo ningemweleza ukweli wa kule niendako lakini pia Jonas alikuwa ameniasa kumkwepa Iloma. Binafsi yangu nilihisi msuto ukipita nafsini mwangu kwa kuona kuwa kukutana na Jonas bila idhini ya Iloma lilikuwa ni kosa kubwa.
“ Iloma acha mimi nitangulie kaka yangu Brian alisema atanipitia pale kituoni ili twende wote mahali”
“ oh! Itakuwa vema mkinipa lifti pia si unajua pale posta usafiri ulivyo wa shida na leo sijaja na gari” alinijibu pasipo kunitazama na laiti angelifanya hivyo si ajabu angeliushuhudia wasiwasi uliokuwa juu ya paji la uso wangu.
“ aah! Hatuendi nyumbani na… isitoshe alisema atanipitia kwa taksi ya Dulla” nilibabaika kidogo
“ amepata nyumba ndogo nini maana teksi ya Dulla ndio usafiri wa kwenda kona!” aliniambia kiutani nami nikashusha pumzi na kumshukuru mungu
“ pengine huwezi kujua ati! Na labda anataka kwenda kunitambulisha wifi mdogo” nilizidi kumdanganya rafiki yangu huku nikijifaragua faragua kwa vicheko vya uongo na kweli. Moyoni nilihisi mzigo mzito kumtendea rafiki yangu unafiki kama huu. Tulitoka ofisini mpaka kituoni na baada ya dakika kama kumi teksi ya dulla ilisimama umbali mfupi toka pale tulipokuwa tumesimama na Iloma. Ni yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kuiona na akanishtua
“ haya mama Dulla huyoo … na angalia msifumaniwe huko ukarudi na ngeu” alinitania huku akinionyesha mahali ilipokuwa imepaki teksi ile.
“ tupo makini michapo yote kesho Iloma”
“haya msalimie Brian!”
“salamu zimefika, tutaonana kesho!”
nilimpungia mkono na kuanza kuchapua hatua za haraka kuielekea teksi ile. Vioo vyeusi vya teksi ya Dulla vilimfanya Iloma asimuone mumewe ndani ya gari. Nilifungua mlango wa nyuma na kujitoma ndani ya gari. Jonas alikuwa ameketi kiti cha nyuma.
Tulisabahiana na Dulla akaliondoa gari. Kama mtu alikuwa amepewa maelezo kabla Dulla alitupeleka Lightness Hotel. Tuliingia mle hotelini na kwenda moja kwa moja mapokezi. Cha kushangaza Jonas aliomba funguo za chumba na kupatiwa. N
ilihisi alikiandaa chumba hicho mapema na sikumuelewa kwanini alichukua chumba wakati tulihitaji kuongea mara moja na kuachana. Sikuwa mjinga kiasi cha kuburuzwa na Jonas. Nilisimama nyuma yake na alipogeuka tulikutanisha nyuso zetu sambamba.
“ hii ina maana gani Jonas!?” nilimuuliza kwa hamaki
“ hatuwezi kuongelea pale mgahawani Karen, mimi ni mume wa mtu na mfanyabiashara ninaye julikana sana hapa jijini, wewe ni rafiki wa mke wangu. Kuketi mgahawani pale tukiongea hakutaleta picha nzuri kwa jamii na isitoshe Iloma hajui kama wewe uko na mimi muda huu” alijitetea kwa kadri alivyoweza lakini pia sikuwa mjinga kiasi ambacho alifikiria. Nikampachika swali
“ sasa Jonas kuonekana mgahawani tukiongea na kuonekana tukielekea vyumbani kipi kina unafuu?”
“ okey! Kwahiyo tukakae mgahawani sio?” aliniuliza kwa sauti kali kidogo
“ nadhani ni bora zaidi Jonas” sikungoja maelezo zaidi nilianza kuchapua hatua kuelekea mgahawani. Nikachagua meza moja iliyokuwa kwenye kona na kuketi. Alinifuatia nyuma na kuketi kiti kilichokuwa mbele ya meza iliyokuwa kati yetu. Aliagiza vinywaji na chakula na kwa pamoja tukaanza kula huku maongezi yakichipukia
“ ni bora uniambie kiini cha mwito huu shemeji” nilimrudisha katika mada kuu
“ mbona una haraka Karen kula kwanza mama” alinijibu hali akiachia tabasamu lake zuri la kuvutia
“ halafu ninayo mengi ya kukuuliza Jonas”
“ juu ya nini?” alionesha mshtuko akaacha kula na kunitumbulia macho
“ mbona una haraka kula kwanza shemeji” nilimtania na wote kwa pamoja tukaangua kicheko. Tulipomaliza kula mhudumu aliondoa baadhi ya vyombo na tukabaki tunaburudika na vinywaji.
Ni hapo ndipo Jonas aliponitobolea kiini cha mwito ule, sikupata hata nafsi ya kumsuta Jonas kutokana na yale niliyoyasikia toka kwa mkewe.
Kwa takribani dakika moja na nusu nilibaki nikiwa nimemtumbulia macho jonas pasipo kujitambua akilini. Nilijaribu kushusha pumzi ndefu na kuangaza huku na kule ili japo nitoke ndotoni lakini bado ilibaki dhahiri kuwa sikuwa ndotoni.
Sikuwa naota wala sikuwa nawaza ilikuwa ni kweli kuwa masikio yangu yalikuwa yamesikia kile kilichotoka mdomoni mwa Jonas.
ITAENDELEA....
Thursday, May 5, 2011
CHA KUSIKIA SI CHA KUONA.....
...Maneno hubomoa na kujenga, maneno huuma na kupuliza lakini yote kwa yote maneno ndio salaha isiyoshikika mikononi lakini ndio silaha inayoweza kuwekea maumivu moyoni maishani...
jaman cha kusikia si cha kuona! mara moja unapoletewa maneno ya kuumiza usikimbilie kutaharuki...usikimbilie kuchukua hatua ukiwa na hizo taharuki...utatenda ya kutenda mwisho wa siku ujutie ulichotenda, jipe nafasi angalau uwe na hakika na kile ulichoambiwa...
mathalani umeambiwa kuna mtu fulani anakusema hivi au vile, usitoke tu kwenda kumkunja mwenzio shati na kumtandika makonde, waama ndio ukashika simu na kumpigia au kumtumia ujumbe wa kumtishia pengine na kumlaania ukoo wake...utavuliwa joho la uungwana!
pima ulichoambiwa kama kina tija na hoja za kukujaza jazba, Kabla ya kufanya maamuzi yako au kujijazia masononeko ya bure.
Umeambiwa mpenzi wako ana mpnzi zaidi yako usikimbilie kuhukumu bila ushahidi. mwambie aliyekuletea maneno akupe ushahidi uufanyie kazi na katika kipindi hicho usimuonyeshe umetaharuki ama kuumizwa na taarifa zake kwa vile bunadamu wa sasa raha yao kubwa ni kukuona ukisononeka, ukishindwa kufika unapotaka!
Kamwe usijipe sononeko kwa kitu usichokuwa na uhakika nacho...maisha mafupi sana kuyaishi katika mawazo, maumivu na majuto ya vitu usivyo na uhakika navyo
ALAMSIKI!
SIRI YANGU 3....NA Laura Pettie
...Niliingia ndani nikiwa na mambo mengi kichwani lakini zaidi nilisumbuliwa na kitu moyoni mwangu. Kitu kipya kabisa ambacho hata mimi mwenyewe sikukielewa vema. Zilikuwa ni hisia ambazo nilihisi ni mpya kabisa katika mfumo wa mishipa ya fahamu zangu. Niliishia chumbani ambako baada ya kujitupa kitandani nilipitiwa na usingizi mzito. Nilikuja kushtuliwa na mama yangu aliyekuja kuniamsha kwa ajili ya kupata mlo wa usiku
“ kulala gani huku Karen!” mama alinilalamikia
“ nimechoka mama na hata chakula sijisikii kula kabisa”
“ acha upuuzi Karen! Ina maana bado Kelvin amejaa akili mwako!...sasa sikiliza binti mapenzi yanasumbua mno na kama utayapa nafasi yakuendeshe basi jua utakuwa mtu wa kuishi kwa maji na mkate”
“ ni bora na hivyo mama mimi sijisikii kula hata huo mkate, unadhani hiki alichonifanyia Kelvin ni kitu cha kusahaulika kwa miezi miwili tu, itachukua miaka mama”
alinitazama kwa muda kisha akasogea na kuketi kitandani pangu. Alinikumbatia kisha taratibu akaniachia na kutabasamu. Ilikuwa kawaida yake na nilizidi kumpenda kwa tabia yake hii. Alionekana wazi kutafuta maneno ambayo yangenifanya nimuelewe vema
“ Karen binti yangu! Maisha yamejaa uchaguzi na unayo haki ya kuchagua maisha unayotaka wewe. Kelvin ni nani hata ayatawale maisha yako….ni nani hata atoweke na furaha yako kwanini hutaki kumwambia mungu asante kwa kumuondoa Kelvin maishani mwako kwa vile hujui amekuepusha na nini na amekuandalia nini hapo mbele Karen”
“ nilimpenda Kelvin mama…nilimpenda sana” nilinung’unika kwa huzuni
“ I know baby! Najua hilo lakini yote ni maisha. Wengine wanafiwa na waume zao wiki tu baada ya kuoana Karen na bado wanaishi na wengine wameolewa tena wamezaa na pengine kusahau yaliyopita” nilimtazama mama kwa muda kisha nikamkumbatia tena Si kwamba nilifarijika na maneno yake bali nilitaka tu afarijike na hali yangu. Usiku huo ulipita nikiwa na mawazo mengi mno. Sikuweza hata kupitisha kijiko kimoja cha chakula na cha maana kilichoingia tumboni ni juisi tu ya passion.
Asubuhi ya jumatatu niliamkia kazini kama kawaida. Bosi wetu Mr.Tummy aliniita ofisini kwake mara tu nilipoingia ofisini. Nilipitia mafaili kadhaa na kuangalia ratiba ya siku hiyo kisha nikaelekea ofisini kwa Mr. Tummy. Niligonga kisha nikakinyonga kitasa na kuusukuma mlango kwenda mbele. Niliingia ndani na kumkuta Mr. Tummy ameketi kitini pake akijizungusha kwa madaha hali akizungumza na simu yake ya mkononi. Alinipa ishara ya kuketi katika kiti kilichokuwa mbele ya meza yake. Nikaketi kwa adabu na kumsubiri amalize kuongea katika simu yake. Dakika mbili baadae aliiweka simu yake mezani na kuachia tabasamu
“ shikamoo Mr. Tummy” nilimsabahi kwa heshima kwa vile alikaribiana kiumri na baba yangu Mzazi.
“ marhabaa Karen habari za weekend, habari za mapumziko, habari za kujirusha eeh!” alinisemesha huku akitafuta tafuta kitu katika faili lililokuwa mbele yake. Niliachia kicheko kwa vile ambavyo alikuwa akinihoji kana kwamba alikuwa kijana wa rika langu.
“ nadhani mambo safi! au siyo?” alinitupia jicho la pembeni huku akitabasamu.
“ bila shaka ndio bosi” nilimjibu nikilikatiza tabasamu langu
“ sasa binti kuna kazi moja ya kufunga yale mahesabu ya mapato ya kampuni. Ingawa ni mapema kidogo lakini ni bora yakiandaliwa mapema ili tujue ni kiasi gani kitakwenda benki na kiasi gani kitatumika kununulia gari la kampuni” alinipa maelezo
“ sawa bosi nitakamilisha kazi hiyo mara moja… kuna lingine?”
“ aaah! Hapana binti waweza kwenda kuanza kazi mara moja” aliniruhusu kuondoka nami kwa adabu nilikiachia kiti na kurudi ofisini kwangu. Nilipita mapokezi alikokuwa Iloma na kumsabahi lakini hata hivyo hakuonesha uchangamfu hata kidogo. Nilihisi Iloma alikuwa na matatizo makubwa katika ndoa yake. Nilimkaribia zaidi na kumuuliza
“ Iloma ni nini kinakusumbua siku hizi!” nilitaka kujua zaidi kwa vile kama ni suala lake na mumewe bado sikuona tatizo na hilo lingekuwa kwa watu wengi.
Jonas alikuwa akifahamika kama mfanyabiashara maarufu mwenye pesa na utu kati ya watu. Mwanaume mwenye kujihesimu na kamwe hakuwahi kupatwa na kashfa yoyote ya ajabu na kama haitoshi Jonas alikuwa na uongozi ndani ya kanisa tulilokuwa tukisali na mara zote alionekana kama mfano kwa vijana wenzake wenye ndoa changa. Sikutaka kulipa uzito suala la Iloma kuwa mnyonge sababu ya mumewe Jonas. Iloma aliacha kazi aliyokuwa akiifanya mbele ya kompyuta na kunitazama.
“ Karen tutaongea wakati wa lunch maana sasa nafikiria mengi mno” aliniambia kwa sauti hafifu iliyoonesha hasira za ndani kwa ndani, macho yake makubwa ya mviringo yalikuwa yakipepeseka huku na kule katika hali ya kushindana na hisia fulani. Sikutaka kumdadisi zaidi nikarejea ofisini kwangu na kuanza kuchapa kazi. Mara kadhaa Jonas alifika pale ofisini kwetu kikazi na nilikuwa nimemzoea kwa kiasi Fulani.
Alikuwa mpole na muungwana sana na sasa alikuwa amemtibua Iloma kwa lipi? Wakati nikiendelea na kazi zangu mida ya saa sita na robo alifika mayasa mhudumu wetu pale ofisini, aliingia ofisini kwangu na kujisimamisha mbele yangu akiwa na bahasha mkononi
“ haya mama vipi tena?” nilimuuliza nikijiandaa kucheka kwa vile siku zote mayasa alikuwa mwanamke mwenye maneno mengi yaliyojaa utani. Alijizungusha na kunesanesa kwa madaha kisha akaanza kuniimbia.
“ mesenja kaleta balaa nyumbani kwa meneja bila kufahamuuuu” aliniimbia kibwagizo hicho na kunifanya niangue kicheko. Akanikabidhi bahasha ile iliyokuwa mkononi mwake na kuniambia kwa sauti ya kunong’ ona “ ukila na kipofu usimshike mkono Karen na utamu wa nanasi ulile kwa nafasi!”
sikumuelewa anamaanisha nini. Niliitua mezani ile bahasha iliyokuwa haina hata anuani wala muhuri wa huko itokako zaidi ya jina langu tena moja tu. Nikamtazama Mayasa kwa kituo wakati akigeuka na kuanza kupiga hatua za maringo kuelekea mlangoni, nikakumbuka kumuuliza kitu
“ mayasa!” nilimuita haraka kabla hajakifikia kitasa akageuka na kunitazama
“ nani amekupa barua hii?” nilimuuliza
“utamjua tu ukiifungua lakini mwenzio nimeshakamata elfu kumi kwa kuileta tu hapa hivyo usifikiri aliyenituma kibarua hicho ni sakala kama mimi” alinijibu na kutokomea kabisa. Nikabaki nimeduwaa nikiikodolea macho ile bahasha. Sikutaka kuwazia kuwa pengine imetoka kwa Kelvin kwa vile binadamu huyu alikuwa nchini Botswana alikokwenda mara baada ya kufunga ndoa na isitoshe aliponipigia simu nilimjibu vibaya mno na kumtaka asinitafute kwa vyovyote vile naye akanijibu kwa hasira kuwa hatojisumbua kwa lolote juu yangu. Ingawa niliumia kwa jibu hilo lakini sikuhitaji kumnyenyekea tena Kelvin!
Niliacha kazi zangu zote na kuyahamishia mawazo yangu katika ile bahasha. Taratibu niliifungua na kutoa karatasi iliyokuwemo ndani mwake. Ilikuwa ni barua fupi tu iliyoandikwa hivi
‘ tafadhali tuonane mara baada ya saa za kazi. Nitakupitia hapo jioni na teksi ya Dulla na tafadhali uwe peke yako na fanya maarifa Iloma asijue kuwa nimekupitia mimi. Nina maongezi muhimu sana na wewe
Mr. Jonas’
ITAENDELEA
“ kulala gani huku Karen!” mama alinilalamikia
“ nimechoka mama na hata chakula sijisikii kula kabisa”
“ acha upuuzi Karen! Ina maana bado Kelvin amejaa akili mwako!...sasa sikiliza binti mapenzi yanasumbua mno na kama utayapa nafasi yakuendeshe basi jua utakuwa mtu wa kuishi kwa maji na mkate”
“ ni bora na hivyo mama mimi sijisikii kula hata huo mkate, unadhani hiki alichonifanyia Kelvin ni kitu cha kusahaulika kwa miezi miwili tu, itachukua miaka mama”
alinitazama kwa muda kisha akasogea na kuketi kitandani pangu. Alinikumbatia kisha taratibu akaniachia na kutabasamu. Ilikuwa kawaida yake na nilizidi kumpenda kwa tabia yake hii. Alionekana wazi kutafuta maneno ambayo yangenifanya nimuelewe vema
“ Karen binti yangu! Maisha yamejaa uchaguzi na unayo haki ya kuchagua maisha unayotaka wewe. Kelvin ni nani hata ayatawale maisha yako….ni nani hata atoweke na furaha yako kwanini hutaki kumwambia mungu asante kwa kumuondoa Kelvin maishani mwako kwa vile hujui amekuepusha na nini na amekuandalia nini hapo mbele Karen”
“ nilimpenda Kelvin mama…nilimpenda sana” nilinung’unika kwa huzuni
“ I know baby! Najua hilo lakini yote ni maisha. Wengine wanafiwa na waume zao wiki tu baada ya kuoana Karen na bado wanaishi na wengine wameolewa tena wamezaa na pengine kusahau yaliyopita” nilimtazama mama kwa muda kisha nikamkumbatia tena Si kwamba nilifarijika na maneno yake bali nilitaka tu afarijike na hali yangu. Usiku huo ulipita nikiwa na mawazo mengi mno. Sikuweza hata kupitisha kijiko kimoja cha chakula na cha maana kilichoingia tumboni ni juisi tu ya passion.
Asubuhi ya jumatatu niliamkia kazini kama kawaida. Bosi wetu Mr.Tummy aliniita ofisini kwake mara tu nilipoingia ofisini. Nilipitia mafaili kadhaa na kuangalia ratiba ya siku hiyo kisha nikaelekea ofisini kwa Mr. Tummy. Niligonga kisha nikakinyonga kitasa na kuusukuma mlango kwenda mbele. Niliingia ndani na kumkuta Mr. Tummy ameketi kitini pake akijizungusha kwa madaha hali akizungumza na simu yake ya mkononi. Alinipa ishara ya kuketi katika kiti kilichokuwa mbele ya meza yake. Nikaketi kwa adabu na kumsubiri amalize kuongea katika simu yake. Dakika mbili baadae aliiweka simu yake mezani na kuachia tabasamu
“ shikamoo Mr. Tummy” nilimsabahi kwa heshima kwa vile alikaribiana kiumri na baba yangu Mzazi.
“ marhabaa Karen habari za weekend, habari za mapumziko, habari za kujirusha eeh!” alinisemesha huku akitafuta tafuta kitu katika faili lililokuwa mbele yake. Niliachia kicheko kwa vile ambavyo alikuwa akinihoji kana kwamba alikuwa kijana wa rika langu.
“ nadhani mambo safi! au siyo?” alinitupia jicho la pembeni huku akitabasamu.
“ bila shaka ndio bosi” nilimjibu nikilikatiza tabasamu langu
“ sasa binti kuna kazi moja ya kufunga yale mahesabu ya mapato ya kampuni. Ingawa ni mapema kidogo lakini ni bora yakiandaliwa mapema ili tujue ni kiasi gani kitakwenda benki na kiasi gani kitatumika kununulia gari la kampuni” alinipa maelezo
“ sawa bosi nitakamilisha kazi hiyo mara moja… kuna lingine?”
“ aaah! Hapana binti waweza kwenda kuanza kazi mara moja” aliniruhusu kuondoka nami kwa adabu nilikiachia kiti na kurudi ofisini kwangu. Nilipita mapokezi alikokuwa Iloma na kumsabahi lakini hata hivyo hakuonesha uchangamfu hata kidogo. Nilihisi Iloma alikuwa na matatizo makubwa katika ndoa yake. Nilimkaribia zaidi na kumuuliza
“ Iloma ni nini kinakusumbua siku hizi!” nilitaka kujua zaidi kwa vile kama ni suala lake na mumewe bado sikuona tatizo na hilo lingekuwa kwa watu wengi.
Jonas alikuwa akifahamika kama mfanyabiashara maarufu mwenye pesa na utu kati ya watu. Mwanaume mwenye kujihesimu na kamwe hakuwahi kupatwa na kashfa yoyote ya ajabu na kama haitoshi Jonas alikuwa na uongozi ndani ya kanisa tulilokuwa tukisali na mara zote alionekana kama mfano kwa vijana wenzake wenye ndoa changa. Sikutaka kulipa uzito suala la Iloma kuwa mnyonge sababu ya mumewe Jonas. Iloma aliacha kazi aliyokuwa akiifanya mbele ya kompyuta na kunitazama.
“ Karen tutaongea wakati wa lunch maana sasa nafikiria mengi mno” aliniambia kwa sauti hafifu iliyoonesha hasira za ndani kwa ndani, macho yake makubwa ya mviringo yalikuwa yakipepeseka huku na kule katika hali ya kushindana na hisia fulani. Sikutaka kumdadisi zaidi nikarejea ofisini kwangu na kuanza kuchapa kazi. Mara kadhaa Jonas alifika pale ofisini kwetu kikazi na nilikuwa nimemzoea kwa kiasi Fulani.
Alikuwa mpole na muungwana sana na sasa alikuwa amemtibua Iloma kwa lipi? Wakati nikiendelea na kazi zangu mida ya saa sita na robo alifika mayasa mhudumu wetu pale ofisini, aliingia ofisini kwangu na kujisimamisha mbele yangu akiwa na bahasha mkononi
“ haya mama vipi tena?” nilimuuliza nikijiandaa kucheka kwa vile siku zote mayasa alikuwa mwanamke mwenye maneno mengi yaliyojaa utani. Alijizungusha na kunesanesa kwa madaha kisha akaanza kuniimbia.
“ mesenja kaleta balaa nyumbani kwa meneja bila kufahamuuuu” aliniimbia kibwagizo hicho na kunifanya niangue kicheko. Akanikabidhi bahasha ile iliyokuwa mkononi mwake na kuniambia kwa sauti ya kunong’ ona “ ukila na kipofu usimshike mkono Karen na utamu wa nanasi ulile kwa nafasi!”
sikumuelewa anamaanisha nini. Niliitua mezani ile bahasha iliyokuwa haina hata anuani wala muhuri wa huko itokako zaidi ya jina langu tena moja tu. Nikamtazama Mayasa kwa kituo wakati akigeuka na kuanza kupiga hatua za maringo kuelekea mlangoni, nikakumbuka kumuuliza kitu
“ mayasa!” nilimuita haraka kabla hajakifikia kitasa akageuka na kunitazama
“ nani amekupa barua hii?” nilimuuliza
“utamjua tu ukiifungua lakini mwenzio nimeshakamata elfu kumi kwa kuileta tu hapa hivyo usifikiri aliyenituma kibarua hicho ni sakala kama mimi” alinijibu na kutokomea kabisa. Nikabaki nimeduwaa nikiikodolea macho ile bahasha. Sikutaka kuwazia kuwa pengine imetoka kwa Kelvin kwa vile binadamu huyu alikuwa nchini Botswana alikokwenda mara baada ya kufunga ndoa na isitoshe aliponipigia simu nilimjibu vibaya mno na kumtaka asinitafute kwa vyovyote vile naye akanijibu kwa hasira kuwa hatojisumbua kwa lolote juu yangu. Ingawa niliumia kwa jibu hilo lakini sikuhitaji kumnyenyekea tena Kelvin!
Niliacha kazi zangu zote na kuyahamishia mawazo yangu katika ile bahasha. Taratibu niliifungua na kutoa karatasi iliyokuwemo ndani mwake. Ilikuwa ni barua fupi tu iliyoandikwa hivi
‘ tafadhali tuonane mara baada ya saa za kazi. Nitakupitia hapo jioni na teksi ya Dulla na tafadhali uwe peke yako na fanya maarifa Iloma asijue kuwa nimekupitia mimi. Nina maongezi muhimu sana na wewe
Mr. Jonas’
ITAENDELEA
Subscribe to:
Posts (Atom)








